MKASA: Hadi Lini?

MKASA: Hadi Lini?

HADI LINI! 15

Na Bishop Hiluka


Hata mzigo wa majukumu juu ya wazazi wake na wadogo zake ungemuelemea sana Pamela kama angeamua kuondoka kwa Ibrahim, ni afadhali basi angekuwa anafanya kazi mahali walau angeweza kupata faranga mbili tatu ambazo zingeweza kukidhi mahitaji yake na ya wazazi wake, lakini wakati ule hakuwa na kazi, mume wake alikuwa hajamruhusu kufanya kazi kwa kauli ya kwamba yeye alikuwa anao uwezo wa kumhudumia kwa kila kitu. Na kama mume amesema hivyo, je, mke angebisha nini?
Hali ilipozidi kuwa mbaya zaidi Pamela aliamua kupigania haki yake, kwanza kwa kumkabili Ibrahim na kumtaka wakae, wayazungumze na kutatua matatizo ya ndoa yao, lakini Ibrahim alimpuuza. Kuona hivyo Pamela akaamua kwenda kuitafuta haki yake kwenye taasisi mbalimbali za watetezi wa jinsia na hata katika taasisi za kisheria lakini kote huko ilishindikana kwa sababu Ibrahim alidharau mwito kutoka katika taasisi hizo, alipata jeuri kwa sababu ya nafasi yake iliyomfanya kukutana na wakubwa wa nchi.
Pamela alipoona kote huko imeshindikana, ndipo akafikia uamuzi kuwa “liwalo na liwe!” maana alijiuliza, je, angeendelea kuvumilia mateso yale hadi lini? Ndiyo maana aliamua kukata mzizi wa fitina kwa kuwaita wazazi wa pande zote ili sasa aweke wazi kuhusu msimamo wake juu ya ndoa yake na Ibrahim. Kama noma na iwe noma!
Na sasa Ibrahim alikuwa amesimama akimtazama mkewe katika ule usiku usiosahaulika kamwe kwenye kumbukumbu zake, ulikuwa usiku wa kizaazaa! Ibrahim aliendelsa kumkodolea macho Pamela ambaye alikuwa chumbani kwake akiwa kasimama kwenye kibaraza cha ghorofa (balcony) akiangalia mbingu kwa unyonge.
Kilikuwa chumba kikubwa na chenye nafasi ya kutosha ambacho upande wa kulia na wa mbele wa kile chumba kulikuwa na madirisha mapana yenye vioo yaliyokuwa yamefunikwa kwa mapazia marefu na mepesi. Dirisha moja lilikuwa limeungana na mlango uliokuwa unatokea kwenye balcony, sehemu alipokuwa amesimama Pamela.
Upande wa kushoto ukutani kulikuwa na kabati kubwa la nguo la ukutani na kando ya kabati lile kulikuwa na meza nzuri nyeusi ya kioo. Juu ya meza hiyo kulikuwa na seti moja ya runinga kubwa Flat screen katikati ya spika mbili za sistimu ya muziki wa Home threatre.
Katikati ya chumba kulikuwa na kitanda kikubwa cha futi sita kwa sita chenye nakshi nzuri za kupendeza, upande wa kulia wa chumba. Upande huo wa kulia kulikuwa na mlango mwingine wa chumba kidogo cha maliwato.
Upande wa kushoto wa chumba kulikuwa na seti moja ya makochi ya sofa nadhifu na ya kisasa juu ya zulia zuri lenye rangi za ngozi ya Pundamilia. Katikati ya makochi hayo kulikuwa na meza ndogo ya mbao iliyokuwa na umbo la nusu duara. Juu ya ile meza kulikuwa na kibakuli kidogo cha majivu ya sigara, kibiriti kimoja cha gesi, kasha tupu la miwani ya macho na simu ya mezani.
Dirishani kwenye balcony kulikuwa na ua kubwa zuri kwenye chungu cha udongo na kando ya ua hilo kulikuwa na kiti kimoja cha kupumzikia kilichokuwa kinatazama nje. Pembeni ya kile kiti kulikuwa na meza fupi ya mbao yenye droo mbili.
Ibrahim alimtazama Pamela kwa makini na kushusha pumzi za ndani kwa ndani kisha akaachia tabasamu la kebehi.
“Naona unatazama juu kama vile unatarajia Mungu akushushie mume mwingine zaidi yangu!”
Pamoja na kutambua uwepo wa Ibrahim mle chumbani lakini Pamela hakugeuka kumtazama bali aliendelea kutazama kule juu bila kuonesha dalili yoyote ya kumsikia mumewe.
Ibrahim alionesha kukerwa mno, akaiweka briefcase yake sakafuni na simu zake akaziweka juu ya meza ndogo ya mbao yenye umbo la nusu duara, kisha akaanza kupiga hatua kumfuata Pamela. Alimfikia na kusimama nyuma yake huku akimwangalia kwa hasira iliyokuwa imechanganyika na jeuri.
“Mapokezi gani haya, halafu eti mwanamke anataka apendwe!” Ibrahim alisema huku akimtazama Pamela kwa dharau.
Pamela aligeuza shingo yake kumtazama Ibrahim kupitia juu ya bega lake bila kuonesha hisia zozote za kumjali, kisha akageuzia shingo yake upande mwingine akionekana kumpuuza. Ibrahim akapandwa zaidi na hasira na kushika mabega ya Pamela, akamgeuza kwa nguvu.
“Naona wewe na hao wazee sasa mnanitafuta kwa jambo, nasema hamtaniweza!” Ibrahim alibwata kwa hasira huku akimkazia machp Pamela.
Pamela alimkazia Ibrahim kwa chuki kubwa na kukunja sura yake, akaitoa mikono ya Ibrahim kwenye mabega yake na kurudi nyuma hatua moja akiwa bado kakunja sura yake.
“Nitashukuru iwapo utauacha moyo wangu utulie, tafadhali sana niache!” Pamela alisema huku akimtazama Ibrahim kwa makini.
Ibrahim alimsogelea tena na kumshika mabegani kisha akaanza kumtingisha kwa nguvu akionekana kupandwa zaidi na hasira. “Unanifanyia kiburi siyo? Nitakupiga sasa hivi au unadhani nawaogopa hao wazee?” Ibrahim alizidi kubwata huku akimtazama Pamela kwa hasira.
“Ni heri uniue kabisa maana nimechoshwa na maisha haya. Nitaishi hivi hadi lini?” Pamela alisema huku akiitoa tena mikono ya Ibrahim mabegani kwake. Ibrahim alimkazia macho akimtazama kwa makini na kucheka kwa dharau huku akitingisha kichwa.
“Huna lolote, najua ni wivu tu unakusumbua, tena wivu wa kijinga,” Ibrahim alisema huku akishusha pumzi.
“Sikuolewa nikuonee wivu bali nikupende na kukutumikia, na wala si kugeuzwa kijakazi wa mahaba!” Pamela alisema huku akimwangalia Ibrahim kwa makini na kutingisha kichwa chake kwa huzuni. Kisha alipiga hatua taratibu kujitenga na Ibrahim, akasimama hatua chache na kumwangalia kwa makini kuanzia chini hadi juu, kisha anaangua kicheko hafifu kilichokuwa kimebeba uchungu.
“Eti wivu! Utoke wapi katika unyumba duni kama huu!” Pamela alisema huku akiendelea kucheka kwa uchungu.
Kauli ile ikaonesha kumchukiza zaidi Ibrahim, alimsogelea Pamela kwa hasira na kunyanyua mkono wake akitaka kumzaba kibao, lakini Pamela alikinga mkono wake kwa ujasiri aakionesha kutomuogopa mumewe. Ibrahim akamwangalia Pamela kwa hasira na kusonya.
“Kama unyumba wangu ni duni, unangoja nini basi nyumbani mwangu? Si uondoke ukatafute anayeona anakutosheleza!” Ibrahim alisema huku akimtazama kwa hasira.
“Nangoja talaka! na itapendeza zaidi ikiwa ni kifo!” Pamela alijibu kwa dharau. Ibrahim alimkazia macho Pamela na kuachia kicheko cha dharau, kisha anasonya.
“Yaani ufedhuli wako ndiyo unanifanya nikuone kinyaa siku hizi,” Ibrahim alisema huku akishushas pumzi za ndani kwa ndani.

ITAENDELEA...
 
HADI LINI! 16

Na Bishop Hiluka


“Ulitaraji nini wakati una msururu mrefu wa mahawara, unadhani mke nyumbani atakuwa na thamani gani?” Pamela alisema na kumfanya Ibrahim akunje sura yake akimkazia macho Pamela.
“Thibitisha kama una ushahidi juu ya madai yako,” Ibrahim alisema huku akimsogelea Pamela, lakini Pamela alirudi nyuma akimkwepa mumewe.
“Ushahidi uliopo machoni kwa Mungu unanitosha, na ninaamini atanilipia.”
Ibrahim alitaka kusema neno lakini hatia ikamkaba koo, akabaki kushangaa akimtumbulia macho Pamela. Muda ule mlango wa chumba chao ukagongwa taratibu mara mbili. Ibrahim aligeuka kuutazama ule mlango akionekana kujishauri, kisha alipiga hatua na kwenda kuufungua kisha akachungulia nje, akamuona Nduwimana akiwa amesimama nje ya mlango wa kile chumba akiwa na wasiwasi.
“Unasemaje? Kwanini hujalala hadi wakati huu?” Ibrahim alimuuliza Nduwimana huku akiwangalia kwa makini.
“Ni mtoto gani mwenye mapenzi na baba yake atalala kabla ya kumuona? Lakini kwa wanangu imekuwa bure kabisa kuwa na baba asiyependeka!” Pamela alidakia kwa uchungu.
Ibrahim aligeuka kumtazama Pamela huku akionekana kukerwa mno na maneno yake.
“Siongei na wewe tafadhali, niache niongee na mwanangu, na naomba usiingilie!” alimwambia Pamela kwa hasira, kisha akageuka kumtazama Nduwimana na kuachia tabasamu. “Enhe, unasemaje mwanangu?”
“Babu anakuita!” Nduwimana alimjibu baba yake huku akiwa anamtazama kwa wasiwasi.
“Haya nakwenda sasa hivi, na wewe nenda ukalale ili kesho usichelewe shule.”
“Kesho ni Jumapili, hakuna shule.”
“Ooh! Hata kama hakuna shule ulitakiwa uwe umelala saa hizi. Sikuwaambia muwe mnalala mapema?”
Nduwimana alibaki kimya akiwa hana la kusema, alimtazama baba yake kwa wasiwasi, akataka kusema neno lakini akasita na kuondoka taratibu. Ibrahim aliamtazama kwa makini huku akimsindikiza kwa macho hadi alipofika kwenye mlango wa chumba chake.
Kisha Nduwimana alishika kitasa cha mlango na kugeuka kumwangalia baba yake kwa wasiwasi, akalazimisha tabasamu na kumpungia mkono kisha akaingia chumbani kwake.
Ibrahim aliachia tabasamu na kupunga mkono wake kisha akaufunga ule mlango wa chumba chake na kumgeukia Pamela, alimtazama kwa muda kisha akatingisha kichwa.
“Umekwisha wajaza maneno ya uzushi wazee na sasa wanataka kunijia juu. Sijui kwa kufanya hivyo ndiyo utapata faida gani?”
“Hata kama wangelikuwa vipofu wasingeshindwa kubaini maisha na mateso ya nyumba hii!”
“Mateso gani, kwani huli ama kulala humu ndani?”
“Nitaupataje usingizi, unyumba si kula na kulala tu!”
“Kumbe kuna nini cha zaidi?”
“Nenda kaonane na wazazi wako pengine watakueleza.”
Ibrahim alimtazama Pamela kwa muda bila kusema chochote, kisha aligeuka na kufungua mlango taratibu. Akataka kutoka lakini akasita na kugeuka kumtazama Pamela kwa hasira.
* * * * *
Kwenye ile sebule, Mzee Bigirimana alikuwa kasimama akiwa anatingisha kichwa chake kwa huzuni, alisonya huku akimkazia macho mke wake, kisha akageuza shingo yake kuwatazama Mzee Tugiramahoro na mke wake walioonekana kuzama katika mazungumzo wakiongea kwa sauti ya chini.
Mzee Bigirimana alishusha pumzi za ndani kwa ndani na kugeuza tena shingo yake kumtazama mke wake. “Hivi ni mtoto gani huyu umenizalia?” alimuuliza mkewe kwa hasira.
“Si ulitaka mtoto wa kiume, sasa?” Mama Bigirimana alijibu huku akionekana kushangaa kidogo.
“Lakini si mtoto fedhuli kama huyu!”
“Alaa, leo amekuwa fedhuli, siyo?”
“Inamaana wewe huoni kama anatuaibisha sana?”
“Hivi toka lini mwembe ukazaa parachichi au umesahau ulivyokuwa zama zako! Anayoyafanya mwanao ndiyo hayo hayo uliyokuwa unayafanya wewe enzi hizo!”
“Lakini hiyo ilikuwa kijijini na wewe ulikuwa mshamba tu si kama mkweo ambaye amesoma na ana madigirii yake!”
“Mwanamke ni mwanamke tu popote pale alipo na katika mazingira yoyote yale anastahili kuthaminiwa na kuheshimiwa,” Mama Bigirimana alijibu akionekana kukerwa sana na ile kauli ya Mzee Bigirimana.
“Lakini si kama anavyofanya mwanao kwa mtoto wa watu,” Mzee Bigirimana alisisitiza kwa sauti ya chini.
“Ni kweli, lakini pilipili za kale hazitofautiani na za leo!”
Mzee Bigirimana alitaka kusema neno lakini akasita na kumtazama mke wake kwa makini, ni dhahiri alionesha kuchukizwa, akamnyooshea kidole katika hali ya kumuonya. Hata hivyo alishindwa kuvumilia kutokana na hasira iliyoanza kuchemka ndani kwa ndani na kujikuta akipandisha sauti yake kwa ukali.
“Kwa hiyo unataka kusema nini sasa, usiache nikakutia vibao saa hizi!”
“Mwenzangu umenipiga vibao vingapi ndiyo nishangae leo! We piga tu ili roho yako iridhike!” Mama Bigirimana alisema huku akimtazama mumewe kwa makini.
Mzee Bigirimana alitaka kusema neno lakini akasita na kugeuka kuwaangalia Mzee Tugiramahoro na Mama Ninziza Bernice kwa wasiwasi.
Wakati huo wale wazee walionesha kushtuka na kugeuka kuwatazama wazee wenzao kwa mshangao. Mzee Bigirimana akajibaraguza huku akilazimisha tabasamu.
Mzee Tugiramahoro alishusha pumzi na kugeuka kumtazama mke wake kwa mshangao, kisha akatingisha kichwa chake kwa masikitiko makubwa akiendelea kumkazia macho mke wake.
“Naujutia sana unyumba wa binti yangu kwa kweli,” Mzee Tugiramahoro alimwambia mke wake kwa sauti ya chini iliyojaa masikitiko.
Mama Ninziza Bernice alimtazama kwa makini na kuonekana kukerwa, alimwangalia mumewe kwa makini na kutingisha kichwa. “Hata sijui unajuta nini wakati mahari uliyapokea kwa mbwembwe na fahari kubwa!”
Mzee Tugiramahoro alikunja sura yake kwa hasira na kumkazia macho mkewe. “Lakini sikumuoza binti yangu ili afanywe hivi!”
“Basi mwelezeni kijana wenu, hii si karne ile ya unyonge wa mwanamke, sijui mnadhani mwanamke ataendelea kufanywa hivi hadi lini?”
Mzee Tugiramahoro alifikiria kidogo na kuinamisha kichwa chake chini, wakati huo mkewe alimtupia jicho Mzee Bigirimana ambaye muda wote alikuwa anarandaranda pale sebuleni huku akiwa anatazama upande zilipokuwa ngazi za kuelekea juu.
Mzee Tugiramahoro anainua na kumuona Mzee Bigirimana akiwa anarandaranda sebuleni, yeye na Mama Ninziza Bernice wanabaki kumtazama Mzee Bigirimana kwa mshangao.
“Hatukuja hapa kuoneshwa ufedhuli wa namna hii!” Mzee Bigirimana alikuwa anaongea kwa hasira kisha aligeuka kuelekeza kidole chake kwa Mzee Tugiramahoro, “Siku nilipopeleka mahari kwa rafiki yangu nilitambua kuwa atakuwa kapata mkwe bora na siyo mkwe duni kama mwanangu.”
“Sasa wewe zungumza na mwanao vizuri na mimi wacha nimfuate mkwe wangu huko juu nikamtulize ili mambo haya yaishe,” Mama Bigirimana alisema na kuinuka bila kusubiri, akaanza kutembea taratibu na kuzikwea ngazi kuelekea juu. Pale kwenye ngazi akapishana na Ibrahim aliyekuwa anashuka ngazi na kumtazama kwa wasiwasi.

ITAENDELEA...
 
HADI LINI! 17

Na Bishop Hiluka


Ibrahim alisimama akitaka kuongea na mama yake lakini yule mama alimpita pasipo kusimama wala kumtazama. Ibrahim akabetua mabega yake na kushusha pumzi kisha akaanza kushuka ngazi taratibu.
Mama Bigirimana aligeuka kumtazama Ibrahim kwa makini na kutingisha kichwa chake kwa masikitiko huku akiendelea kuzikwea ngazi haraka.
Ibrahim alipofika pale sebuleni alisimama na kumwangalia baba yake kwa wasiwasi, kisha akageuza shingo yake kuwatazama wakwe zake huku akionesha uso wa mashaka kidogo.
“Nasikia unaniita!” Ibrahim alimkabili baba yake akiwa bado ana uso wenye mashaka.
“Kwani nilisemaje? Sikukwambia kuwa nina mazungumzo na wewe usiku huu huu?” Mzee Bigirimana alisema huku akionesha kukerwa kidogo na lile swali la Ibrahim, kisha akageuza shingo yake kuwatazama Mzee Tugiramahoro na mkewe, akashusha pumzi ndefu na kumtazama tena Ibrahim.
“Naomba twende faragha hapo nje tukaongee kidogo.”
Ibrahim alisita kidogo, hofu ilikuwa inamtambaa mwilini na muda ulr alihisi kijasho chembamba kikimtoka. Alimtazama baba yake kwa makini na kuminya midomo yake, kisha akatoka nje.
“Mzazi mwenzangu, ukimaliza mazungumzo na mwanao na mimi nitahitaji kuzungumza na wewe,” Mzee Tugiramahoro alimwambia Mzee Bigirimana alipomuona akijiandaa kutoka nje kumfuata Ibrahim.
Mzee Bigirimana aligeuka kumtazama mzee mwenzie kwa uso wenye mashaka kidogo, akaminya midomo yake kutafakari kidogo, kisha akabetua kichwa chake kukubali.
“Sawa, mzazi mwenzangu,” alisema na kutoka nje haraka. Mzee
* * * * *
Mama Bigirimana alipofika kule juu alisimama kwenye mlango wa chumba cha Pamela, akaonesha kusita sana huku akitazama huku na huko, kisha akabisha hodi mlangoni akiwa na uso wenye wasiwasi kidogo. Alisubiri kwa kitambo kifupi na kugonga tena, lakini alipokuwa akianza kugonga mara ya pili mlango ukafunguliwa na kumfanya kushtuka sana.
Pamela alitoa kichwa chake nje kuchungulia, akamuona Mama Bigirimana na kuachia tabasamu la makaribisho. “Karibu mama,” Pamela alisema huku akimtazama yule mama kwa makini.
“Mwanangu, naomba tuzungumze kidogo, nafahamu kuwa usiku umekwenda mno na ungependa kupumzika,” Mama Bigirimana alimwambia Pamela kwa sauti tulivu huku akimtazama kwa wasiwasi.
“Usijali mama, haya niliyo nayo kwa kweli yanafanya usingizi kwangu kuwa sawa na kijiji cha mbali sana ambacho siwezi kukifikia kwa urahisi.”
“Basi naomba tukazungumzie huko chumbani kwetu kwani huku kwenu si haki niingie.”
“Mama, naheshimu sana mila na desturi za Kiafrika lakini katika mazingira kama haya si vibaya tukazungumzia huku huku chumbani kwetu,” Pamela alisema na kumsisitiza yule mama huku akimpisha aingie ndani.
Mama Bigirimana alionekana kusita sana, akainamisha uso wake kufikiria sana lakini mwisho alishusha pumzi za ndani kwa ndani huku akimtupia jicho Pamela. Muda wote Pamela alikuwa anamwangalia kwa makini kwa macho ya kumsisitiza aingie ndani ndani.
Baada ya kuonekana akijishauri kwa kitambo kifupi hatimaye Mama Bigirimana alikubali kuingia chumbani japo kwa shingo upande, akaingia akiwa na wasiwasi na kupita haraka akaelekea moja kwa moja kwenye balcony.
Pamela alimtazama kwa makini kisha akamfuata na kumkaribisha kwenye kiti cha kupumzikia kilichokuwepo pale kwenye balcony. Mama Bigirimana aliketi kwenye kile kiti kando ya ua kubwa zuri lililokuwa kwenye chungu cha udongo. Pamela naye akaketi jirani huku akimtazama kwa makini.
Mama Bigirimana alimtazama Pamela kwa muda akiwa na shaka kidogo, alionekana kutafuta maneno ya kuongea kisha akatingisha kichwa chake kwa huzuni.
“Binti yangu, najua mateso unayoyapata lakini kama mke hebu jaribu kuvumilia, haya yana mwisho. Hivi unadhani mimi nisingekuwa mvumilivu ningekuwa na baba yenu hadi leo?”
Pamela alimtazama yule mama kwa makini na kutingisha kichwa chake taratibu kwa huzuni huku akibetua mabega yake juu na kuyashusha.
“Mama, kumbuka kuwa hakuna kitabu chochote duniani kinachoamuru mimi kama mwanamke niishi maisha kama haya, eti kwa kuwa nimeolewa!”
“Nafahamu, hata mimi inaniumiza sana tangu uliponielezea hali halisi iliyopo hapa nyumbani, lakini elewa kuwa sisi mama zako pia tumetokea huko huko na tuliweza kuyavumilia yote.”
“Natambua lakini wakati ule ulimwengu wa mwanamke ulikuwa umegubikwa na giza la unyonge. Hivi mama, unadhani mambo haya yatavumiliwa hadi lini?”
Mama Bigirimana alikunja sura yake na kuwaza kidogo kisha akavuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu huku akionekana kukata tamaa. Alimtazama Pamela kwa wasiwasi kidogo.
“Sasa unataka tufanyeje mama, maana hivi sasa baba yako amemweka chini mumeo ili amrekebishe.”
“Mama, mwanao amekuwa sugu na sidhani kama anaweza kubadilika, ninachotaka mimi ni kimoja tu ili nami nipumue kwa kweli.”
Mama Bigirimana alimkazia macho Pamela kwa wasiwasi, alitaka kusema neno lakini akasita, maana alikuwa hapendi kabisa kusikia kuhusu suala la Ibrahim na Pamela kuachana kwa namna yoyote ile. Alimpenda sana mkwe wake kwa kuwa alikuwa mwanamke mvumilivu, msomi, aliyejituma na mlezi mzuri kwa watoto.
“Ni nini tufanye basi, labda roho yako itaridhika?” hatimaye yule mama alimuuliza Pamela huku akimkazia macho kwa wasiwasi.
“Hakuna kingine mama, naomba mmwambie anipe talaka yangu tu,” Pamela alisema huku akiyakwepa macho ya Mama Bigirimana na kutazama kando, alikuwa akiyazuia machozi yaliyokuwa yanamlenga.
Mama Bigirimana alishtuka sana kusikia maneno yale kutoka kwa mkwewe, alimkazia macho akiwa haamini alichokisikia. Kwa nukta kadhaa akili ya Mama Bigirimana iligoma kabisa kukubali kuwa alichokisikia ni kile kilichokuwa kimetamkwa na Pamela, au labda alisikia vibaya, badala ya neno “muafaka” yeye kasikia neno talaka! Kwa kifupi, Mama Bigirimana alidhani kuwa huenda alisikia vibaya.
“Unasemaje, mama?” Mama Bigirimana alimuuliza Pamela kwa wasiwasi ili kuhakikisha kama alichokuwa amekisikia kutoka kwenye kinywa cha Pamela kilikuwa sahihi na siyo hisia zake.
“Nasubiri talaka yangu tu, mama yangu… lakini si kama mimi napenda talaka ila ndicho kitu alichokusudia mwanao!” Pamela alisema kwa sauti tulivu huku akimtazama mkwewe kwa makini.
Mama Bigirimana alinyanyua mikono yake na kushika kichwa chake kwa huzuni, akataka kusema neno lakini akashindwaa na kubaki akimtumbulia macho Pamela huku akiwa ameduwaa kwa mshangao mkubwa kana kwamba alikuwa ameona kitu cha kushangaza sana. Kwa nukta kadhaa akili ya yule mama iligoma kabisa kukubali. Hata hivyo, lile neno ‘nasubiri talaka yang utu…’ liliendelea kujirudia akilini mwake na kutengeneza mwangwi uliomkera sana.
Mama Bigirimana anaitoa mikono yake kichwani na kuziba masikio yake huku akikunja uso wake kana kwamba eneo hilo kuna kelele zinazomkera, machozi yanaanza kumtoka.
* * * * *
Kwenye ile baraza kubwa ya mbele ya ile nyumba, Mzee Bigirimana alikuwa akiongea na Ibrahim huku wakiwa wameketi kwenye makochi ya sofa. Mzee Bigirimana alimtazama Ibrahim kwa makini na kukunja sura yake kwa hasira, akasonya kwa huzuni huku akitingisha kichwa chake.

ITAENDELEA...
 
HADI LINI! 18

Na Bishop Hiluka


“Sikiliza bwana mdogo, mkeo hakutuita hapa sisi na wazazi wake kuja kuwatembelea… nadhani hilo unalifahamu vyema.”
Ibrahim alishusha pumzi za ndani kwa ndani huku akilazimisha tabasamu ingawa uso wake ulionesha kinyume chake, akanyanyua mabega yake juu huku akibetua midomo yake.
“Nafahamu baba, lakini sijui kama unafahamu kuwa mkweo siku hizi amekuwa kituo cha uzushi!”
“Kituo cha uzushi ki vipi wakati mengi ya wazi yanaonekana?”
“Najua kuwa tayari mmekwisha jazwa mengi ya kuzushwa…” Ibrahim alisema kwa namna ya kujitetea huku akimkazia macho baba yake.
Mzee Bigirimana alitingisha kichwa chake kwa hasira huku akipumua kwa nguvu kama mtu aliyekuwa amemaliza mbio ndefu za marathoni, akamnyooshea kidole Ibrahim kwa hasira.
“Bwana mdogo, elewa kuwa mimi siyo mtoto mdogo, na uendako wewe ndiko mimi nilikotokea.”
Ibrahim alitaka kusema neno lakini baba yake hakutaka kumpa nafasi ya kuongea, alikunja uso wake uliotengeneza matuta madogo usoni.
“Sikiliza… wewe ni mwanamume na una uhuru wa kufanya utakalo, wala hakuna anayeweza kukupangia. Kama unaweza basi oa mwanamke mwingine wawe wawili, maana hata dini yako inakuruhusu, ila kama huwezi basi mwache mtoto wa watu aende kwao na siyo kumnyanyasa kama hivi!”
“Nadhani hilo la pili ndiyo linaleta maana zaidi, kwani nimeshachoka kwa kweli!” Ibrahim alisema kwa kujiamini zaidi huku akibetua kichwa chake. Tabasamu lilionekana kuupamba uso wake.
“Umesemaje!” Mzee Bigirimana alimuuliza Ibrahim akiwa haamini alichokisikia, mshituko ulijitokeza waziwazi kwenye uso wake.
“Nataka kumuacha ili nioe mke mwingine,” Ibrahim alimwambia baba yake kwa sauti tulivu na kwa msisitizo huku akiyaelekeza macho yake kutazama mbele kwenye kibanda cha mlinzi. Mlinzi alikuwa ameketi kwenye kiti chake kwa utulivu akiwatazama Ibrahim na Mzee Bigirimana kwa mashaka.
Mzee Bigirimana alivuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu huku akiwa hajui aseme nini, aliinamisha kichwa chake na kufikiria kidogo kisha akainua uso wake na kumtazama Ibrahim, akataka kuongea neno lakini maneno hayakutoka kinywani mwake. Akatingisha kichwa chake kwa huzuni huku akiendelea kumtazama Ibrahim.
Ibrahim aliinuka na kufungua mlango mkubwa wa barazani, akaingia ndani akimwacha baba yake pale akiwa bado ameduwaa. Alipoingia ndani alipita pale sebuleni na kuelekea moja kwa moja kwenye ngazi huku akiwapita wakwe zake wakiwa bado wameketi kwenye sofa wakiendelea kujadili mambo kwa sauti ya chini.
Walipomuona akipita waligeuza shingo zao kumtazama kwa mshangao, kisha wakaangaliana wasijue kilichokuwa kikiendelea ndani ya ile nyumba.
Ibrahim alizifikia ngazi za kuelekea juu na kupishana na mama yake aliyekuwa anashuka mngazi akitokea ghorofani huku akiwa analia kwa uchungu mkubwa, mikono yake yote miwili alikuwa kaiweka kichwani. Ibrahim alisimama huku akimtazama mama yake kwa mshangao, akajaribu kumsimamisha.
“Mama, kuna nini tena huko juu?” alimuuliza mama yake huku akimkazia macho kwa wasiwasi.
Mama Bigirimana alionesha ishara ya kutaka aachwe, akampita Ibrahim bila hata kumwangalia usoni wala kumjali na kupita pale sebuleni akiwapita Mzee Tugiramahoro na Mama Ninziza Bernice ambao walikuwa wameketi wakiwa bado wanashangaa, akaelekea moja kwa moja kule nje ya nyumba alikokuwa ameketi Mzee Bigirimana.
Ibrahim akiwa bado amesimama pale kwenye ngazi akimsindikiza mama yake kwa macho yenye mshangao, alijaribu kuwaza akijaribu kubashiri ni jambo gani huenda lilikuwa limetokea kule juu? “Au pengine mama na Pamela wamepishana kauli? Na kama wamepishana, kwa nini?” Ibrahim aliwaza na kukosa jibu.
Alishusha pumzi za ndani kwa ndani huku akibetua mabega yake na kuanza kupanda ngazi haraka akielekea kule juu kisha akaongoza moja kwa moja chumbani kwake. Alifika mlangoni na kuupiga kumbo ule mlango, mlango ukafunguka. Ibrahim akajitoma mle ndani huku akiwa amefura kwa hasira.
Alimkuta Pamela akiwa amesimama katikati ya kile chumba akiwa anatazama nje kupitia ukuta msafi wa kioo cha dirisha ambalo pazia lake lilikuwa limefunuliwa kidogo na kumruhusu mtu aliyekuwa mle ndani kuweza kuona nje. Inrahim alisimama akamtazama Pamela kwa hasira.
Hasira zilikuwa zinamchemka ndani kwa ndani, akamsogelea huku akizidi kuhisi donge la hasira likizidi kumkaba kooni kiasi cha kushindwa hata kupumua.
“We mwanamke, umemfanyia ufedhuli gani mama yangu?” Ibrahim alimwuliza Pamela huku akipumua kwa nguvu, alipoona kimya akamshika mabegani kisha akamgeuza kwa hasira. Wakabaki wanatazamana, Pamela alimwangalia Ibrahim kwa makini huku akijitahidi kuwa mtulivu zaidi, japokuwa alikuwa amebanwa na donge la hasira kooni.
“Nakuuliza umemfanyia ufedhuli gani mama yangu?”
“Nimfanyie kitu gani mama wa watu?” Pamela alijibu kwa sauti yenye utulivu pasipo kuonesha hasira wala dharau yoyote kwa Ibrahim.
“Na kwa nini atoke humu chumbani akiwa analia?” Ibrahim aliuliza huku akiendelea kumkazia macho Pamela.
“Nikuulize wewe, pengine analia kwa vile nimemweleza msimamo wangu,” Pamela alijibu kwa kujiamini huku akimtulizia macho Ibrahim moja kwa moja machoni pasipo kukwepesha macho yake.
“Msimamo gani uliomweleza?” Ibrahim aliuliza kwa pupa huku naye akimtulizia macho Pamela.
“Swali hilo ingependeza zaidi kama ungemuuliza mama mwenyewe,” Pamela alijibu na kugeuka kutazama nje akionekana kumpuuza mumewe.
Ibrahim alimtazama Pamela kwa makini na kushusha pumzi, akauma midomo yake akionekana kuzuia hasira zake, kisha alianza kuranda randa mle chumbani huku akiwa kainamisha kichwa chake, mikono yake akiwa kaiweka nyuma na akionekana kuwaza mbali sana.
Pamela aliendelea kusimama pale pale akiendelea kutazama nje, naye alikuwa akiwaza mbali sana. Ibrahim alikuwa anageuka mara kwa mara kumwangalia Pamela kwa jicho la hasira, na baada ya kuranda randa kwa kitambo kifupi alimfuata huku akimkazia macho. Akasimama hatua moja mbele yake na kumtulizia macho kwa hasira huku akimnyooshea kidole chake.
“Hakika mwalimu wako wa somo la kiburi na jeuri anafanya kazi yake vizuri sana.”
“Ni kweli, hasa baada ya mwalimu wa somo la upendo, nidhamu na uvumilivu kushindwa kazi yake!”
“Sasa, kama ameshindwa kazi ni bora angekushauri uondoke nyumbani kwangu na siyo kunifanyia ufedhuli kiasi hiki!”
“Nilichukuliwa kwa wazazi wangu kwa taratibu zote, japokuwa naweza kuondoka kisheria lakini ninawajibika kuwapa wazazi wangu na wa kwako heshima inayostahili!” Pamela alisema kwa utulivu huku akiendelea kumtulizia macho Ibrahim pasipo kupepesa.

ITAENDELEA...
 
HADI LINI! 19

Na Bishop Hiluka


“Heshima inayostahili ni kumwacha mwanamke aliyenizaa atoke humu ndani akiwa analia?” Ibrahim alimwuliza Pamela akiwa amekerwa sana.
“Nadhani analizwa na yale unayopaswa kuyatenda ambayo hata mimi nayasubiri kwa hamu.”
“Kwani unataka nini hasa kutoka kwangu?”
“Hujui au unapenda kusika wakati natamka? Haipendezi kuuliza jambo ambalo unalifahamu vizuri!”
Ibrahim alimtazama kwa hasira, akataka kusema neno lakini akasita na kushusha pumzi kwa uchungu, donge la hasira lilionekana kumkaba kooni kwake. Alitamani amshike Pamela na kumtupa kutoka kule ghorofani hadi chini ili afe. Alimeza mate kutowesha koo lake lililoonekana kukauka kisha akashusha pumzi ndefu huku akionekana kuizuia hasira zake.
“Okay, ni jambo gani unalotaka toka kwangu, talaka?”
“Nadhani hilo ni la kwanza,” Pamela alimjibu ibrahim kwa kujiamini huku akiendelea kumtulizia macho yake.
Ibrahim aliachia tabasamu la dharau na kubetua kichwa chake kukubali, alijionesha kuwa alikuwa hajali chochote na alikuwa tayari kwa lolote, isitoshe suala la talaka kilikuwa kitu ambacho alikitamani muda mrefu, na sasa ilikuwa jambo rahisi kuliko alivyokuwa ametarajia.
“Naona umeitafuta na utaipata sasa hivi, nipe dakika moja tu,” Ibrahim alisema kwa kujiamini huku akiendelea kutabasamu kwa dharau.
“Naisubiri kwa hamu kubwa, wala usijaribu kabisa kunitisha,” Pamela aliongea kwa sauti iliyobeba dharau huku akionekana kushindwa kuficha hasira zake, donge la hasira lilizidi kumkaba kooni.
Ibrahim aliivua pete ya ndoa kutoka kwenye kidole chake na kumpa Pamela huku akimtazama kwa chuki, “Nilijua tu toka siku ile kwa mkuu wa wilaya kuwa ungeidai siku moja.”
Pamela aliipokea ile pete bila kusita wala kujiuliza huku uso wake ukipambwa na tabasamu, kisha naye akaivua pete yake ya ndoa kutoka kwenye kidole chake na kunyoosha mkono kumpa Ibrahim, “Kama ndivyo ulivyotarajia sawa, na wewe chukua pete yako uliyonivalisha kinafiki.”
Ibrahim aliachia tabasamu pana la dharau usoni kwake huku akiipokea ile pete, akaiweka kwenye mfuko wa suruali yake huku akionesha kutokujali kabisa. Muda ule alikuwa anajihisi mwepesi mno baada ya kuutua mzigo mzito uliokuwa umemwelemea kwa muda mrefu.
Okay, sasa nasubiri kuondoka kwako haraka humu ndani ili nipate kupumua,” Ibrahim alimwambia Pamela na kumfanya aangue kicheko cha dharau huku akimtazama Ibrahim kwa dharau kuanzia unyayoni hadi kichwani.
“Naona wewe ungetangulia kuondoka humu ndani ndiyo ingekuwa vizuri zaidi wakati mimi nikisubiri iwapo wakili wangu atamaliza shauri letu mapema.”
Ibrahim alishtushwa sana na kauli ile, akamkazia macho Pamela huku hasira ikijionesha waziwazi kwenye macho yake, “Umesema nani atamaliza shauri letu?”
“Utamuona panapostahili akisaidiana na wanaostahili kufanya yote yanayostahili kwetu,” Pamela alijibu kwa kujiamini huku akishika kiuno chake na kumtazama Ibrahim kwa dharau.
Ibrahim aliondoka kutoka eneo lile kwa hasira huku akionekana kuchanganyikiwa na kwenda kusimama kule nje kwenye balcony, Pamela aliendelea kusimama pale pale. Ibrahim alisimama pale nje akiangalia chini ya lile jengo kwa muda, akamuona yule mlinzi akiwa ameketi juu ya kiti chake pale kwenye kibanda cha ulinzi huku akitazama kule juu kwenye balcony kwa wasiwasi.
* * * * *
Baada ya Ibrahim na mama yake kupishan kwenye ngazi na Mama Bigirimana kupita akiwa analia, Mzee Tugiramahoro na Mama Ninziza Bernice walikuwa bado wameketi pale pale wakijadiliana kuhusu hatma ya binti yao. Mara wakashtushwa sana kumuona Mama Bigirimana akiingia tena pale sebuleni kutokea kule nje alikouwa na mumewe akiwa analia kwa uchungu huku akifuatwa nyuma na mumewe aliyejaribu kumfariji.
Mama Bigirimana aliketi kwenye sofa huku akiendelea kulia kwa huzuni kilio cha kwikwi, alijiinamia kwa huzuni huku akijitahidi kuzuia machozi yaliyokuwa yakimtoka lakini hakuweza kufanikiwa. Mzee Tugiramahoro alimtazama yule mama jinsi alivyokuwa akilia na kuinuka huku akishika kiuno chake, akageuza shingo yake kumtazama mkewe na kumpa ishara ya kumtaka watoke nje wakazungumze faragha mambo yanayowahusu.
Mama Ninziza Bernice alimtazama mumewe kwa wasiwasi, akataka kukataa lakini hakuwa na namna nyingine yoyote ya kufanya, hasa alipokumbuka kuwa walikuwa wameitwa pale kuja kujaribu kutafuta muafaka na kunusuru ndoa ya binti yao, hivyo akajikuta akiwa hana njia nyingine isipokuwa kuinuka na kutoka nje kumfuata mumewe huku akimtupia jicho Mama Bigirimana aliyekuwa analia.
Mama Ninziza Bernice alimkuta mumewe akiwa kasimama kwenye ile baraza ya nyumba akiwa anamsubiri huku mikono yake akiwa kaiweka nyuma. Mama Ninziza Bernice alisimama huku akimwangalia mumewe kwa wasiwasi mkubwa.
“Unajua hadi sasa sielewi… hivi hapa tumeitwa tuje kufanya nini! Maana muda wote naona uchuro tu wa watu kulia ovyo kama vile kuna msiba!” Mzee Tugiramahoro alimwambia mkewe huku akimtazama kwa makini.
“Ni kweli hata mimi sielewi, lakini ni wajibu wako wewe kumuuliza mzee mwanzako!” Mama Ninziza Bernice alimjibu mumewe kwa utulivu lakini akiwa na uso uliotawaliwa na wasiwasi.
“Kama unyumba wa binti yangu hakuna ni heri watuambie tujue moja, lakini nasema kabisa umtafutie pa kumpeleka maana mimi sikai na watoto walioachika.”
“Lakini hukumuoza mtoto akiwa hana kwao, na siyo wote wanaoachika hawafai… sasa katika mazingira kama haya ndiyo umwache tu aendelee kuteseka eti kwa vile ulimuoza?” Mama Ninziza Bernice alisema kwa mshangao huku akionekana kukerwa sana na yale maneno ya mumewe, donge la hasira lilimkaba kooni.
“Nasema hivi, kama unamuunga mkono basi wewe na yeye mtakwenda kutafuta kiota chenu cha watalikiwa… tena safari yenu muianzie hapa hapa na siyo kwangu.”
Mama Ninziza Bernice alitaka kusema neno lakini akashindwa, donge la hasira lilizidi kumkaba kooni na kumfanya aanze kulia kwa uchungu. Mumewe alimtazama kwa hasira.
“Nasisitiza, akiachika mtu hapa asirudi nyumbani kwangu!” Mzee Tugiramahoro alisema kwa msisitizo na kuondoka akimwacha mke wake pale nje, akaingia sebuleni na kumkuta Mzee Bigirimana akiendelea kumtuliza mke wake ambaye alikuwa bado analia kwa uchungu kilio cha kwikwi. Mzee Tugiramahoro alifika na kusimama huku akiwatazama kwa makini.
“Niwie radhi mzee mwenzangu, naomba tutoke nje tukatete kidogo kama wanaume,” Mzee Tugiramahoro alisema huku akimkazia macho Mzee Bigirimana.
Mzee Bigirimana aliinua shingo yake kumtazama Mzee Tugiramahoro kwa wasiwasi kidogo, akashusha pumzi na kuinuka huku akimwacha mke wake bado analia kilio cha kwikwi. Walitoka nje ambako walimkuta Mama Ninziza Bernice akiendelea kulia kwa uchungu.
“Ingia ndani bibie, tuna mazungumzo ya kiume hapa,” Mzee Tugiramahoro alimwambia mkewe huku akishusha pumzi.

ITAENDELEA...
 
HADI LINI! 20

Na Bishop Hiluka


Mama Ninziza Bernice aliwatazam wale wanaume kwa mashaka kidogo huku akiinuka na kuingia ndani huku akisindikizwa na macho ya wale wazee wawili, alipoingia ndani wakaketi pale kwenye sofa. Mzee Tugiramahoro alitoa paketi ya sigara kali, akatoa humo sigara mbili huku moja akiiwasha na kuanza kuvuta na sigara nyingine akanyoosha mkono wake kumpa Mzee Bigirimana. Mzee Bigirimana alikataa kwa kutingisha kichwa.
Mzee Tugiramahoro alipiga mkupuo mkubwa wa sigara na kuutoa moshi taratibu huku akiutazama kwa makini jinsi ulivyokuwa ukipanda juu na kupotelea hewani. Akapiga mkupuo mwingine na kutoa moshi mwingi, kisha akageuza shingo yake kumtazama Mzee Bigirimana.
Mzee Bigirimana alikuwa ameketi kimya kabisa akimwangalia mzee mwenziye kwa makini. Akashusha pumzi na kusimama kisha akaanza kuzunguka zunguka pale barazani huku akitazama juu, mikono yake akiwa ameiweka nyuma akionekana kuwaza mbali sana.
“Siku hizi tunazaa kenge na siyo watoto kabisa!” Mzee Bigirimana alisema kwa huzuni.
“Inategemea, maana si watoto wote ambao ni kenge, wapo wanaofaa kabisa,” Mzee Tugiramahoro alisema katika hali ya utulivu huku akiendeleaa kuvuta sigara yake taratibu.
“Wapo kweli wala sikatai, lakini si mimi na bwana mwenye mji huu,” Mzee Bigirimana alisema huku akimtupia jicho mzee mwenzake.
“Kwa nini unasema hivyo?” Mzee Tugiramahoro alimtazama kwa makini na kuuliza huku akipiga mkupuo mwingine na kutoa moshi mwingi.
“Kinachomliza mama yake ndicho ambacho yeye kadhamiria kukifanya!”
“Ni kipi hicho cha ajabu?” Mzee Tugiramahoro aliuliza kwa shauku huku akimkazia macho Mzee Bigirimana.
“Eti anataka kumtaliki mkewe na pengine aoe mwanamke mwingine!” Mzee Bigirimana alisema kwa huzuni.
“Kama akili yake ndivyo inavyomtuma basi amtaliki, lakini mimi sirejeshi mahari na wala binti yangu hatarudi nyumbani kwangu,” Mzee Tugiramahoro alisema kwa hamaki huku donge la hasira likimkaba kooni. Muda ule alianza kuiona ile sigara chungu.
“Hapana, tusikose hekima, mzee mwenzangu, wacha tuwaite wote wawili na kisha tuwahoji maana ndilo tuliloitiwa na mkwe wangu!”
Mzee Tugiramahoro alimtazama Mzee Bigirimana kwa kitambo kirefu pasipo kusema neno kisha alipiga mkupuo mwingine mkubwa wa moshi na kuutoa na kukitupa chini kipande cha sigara kilichobakia na kukisigina kwa mguu wake.
“Bahati ya binti yangu ni mbaya sana, walikuja vijana wengi tu wa maana waliotaka kumuoa nikakataa, kumbe sikujua kama namtumbukiza kwenye pango la mbwa mwitu,” Mzee Tugiramahoro alisema kwa huzuni maneno yaliyoonekana kumchoma na kumkera sana mzee mwenziye.
Mzee Bigirimana alimkazia macho mzee mwenziye huku hasira zikianza kumpanda, “Nadhani sasa tusianze kutukanana kirejareja, mimi si mjinga na wewe unafahamu hilo… cha msingi ni kuzungumza na watoto wetu ili tuwaweke sawa.”
“Tuwawekeje sawa wakati tayari mwanao anamuona binti yangu kama chawa!” Mzee Tugiramahoro alimuuliza mzee mwenziye huku hasira zikianza kumtambaa mwilini mwake na kuyafanya maungo yake kuzizima.
Mzee Bigirimana alitaka kusema neno lakini akasita na kushusha pumzi. Kisha wale wazee walibaki wakitazamana pasipo kusema neno kwa kitambo kirefu. Mzee Tugiramahoro alitoa sigara nyingine na kuiwasha kisha akapiga mkupuo mkubwa na kutoa moshi mwingi huku akihema kwa nguvu.
* * * * *
Akiwa pale kwenye balcony Ibrahim aliendelea kutazama kule chini kisha kama aliyekumbuka kitu akaondoka na kurudi chumbani, akaanza kuranda randa mle ndani huku akiwa kainamisha uso wake, alionekana kuwa katika dimbwi la mawazo.
Muda ule Pamela alikuwa amepiga magoti akipanga vizuri nguo zake ndani ya kabati kubwa la nguo la ukutani. Ibrahim alikuwa anageuka mara kwa mara kumtazama Pamela huku akiwa na donge la hasira.
“Kabla sijasahau, naomba ukitaka kuondoka hakikisha kwanza umenitayarishia kabisa orodha ya mali yangu humu ndani.”
“Kila kinachostahili kufanywa tayari kipo kwa wakili wangu, wewe tengeneza listi yako ukampe wakili wako,” Pamela alimjibu Ibrahim huku akiendelea kupanga nguo zake ndani ya lile kabati.
“To hell with your lover boy,” Ibrahim alifoka kwa hasira na kumkwida Pamela kwa ghadhabu. Pamela hakuogopa bali alionekana kumshangaa sana Ibrahim.
“Mimi tena? Siyo wewe na mlolongo wa malaya wako wa ushirika?” Pamela alimuuliza Ibrahim huku akimtazama kwa mshangao.
Ibrahim alionekana kuhamaki sana, akamnyanyua Pamela na kumsukuma kwa ghadhabu, Pamela akaanguka pale sakafuni na kuinuka haraka huku akimtazama Ibrahim kwa tabasamu, kisha akatingisha kichwa chake kwa dharau.
Akiwa bado anatingisha kichwa kwa dharau alishtuliwa na kibao kikali cha ghafla ambacho hakukitegemea kilichotua kwenye shavu lake la kushoto, akaanguka sakafuni huku lile tabasamu likiyeyuka na badala yake hofu ikachukua nafasi yake.
Pamela alijishika shavu lake huku akimtazama Ibrahim kwa hofu kubwa akiwa haamini kilichotokea, mdomo wake wa chini ulikuwa umechanika kidogo na damu zilianza kumtoka kwenye mdomo wake. Alifuta damu huku donge la hasira likizid kumkaba kooni.
“Unanipiga!” Pamela alimwuliza Ibrahim kwa mshangao huku akiinuka kutoka pale sakafuni, akasimama huku akimkazia macho, ni wazi hasira zilikuwa zinachemka ndani kwa ndani. Ibrahim hakumkawiza, akampiga teke lililotua kwenye tumbo lake na kumdondosha chini huku akilishika, akaanza kulia kwa uchungu sauti kubwa.
Sauti ya kilio chake ilipenya na kusambaa kila mahali, kuanzia pale sebuleni walipokuwa wameketi wale kina mama, barazani walipokuwa wamekaa wale wazee wakiongea hadi kule chumbani walikokuwa wamelala watoto wao Nduwimana na Samantha.
Mama Ninziza Bernice na Mama Bigirimana walinyanyuka kutoka kwenye sofa walipokuwa wamekaa huku wakitazamana kwa wasiwasi, walionekana kujaribu kusikiliza kwa makini ili kubaini sauti hiyo ilikuwa ya nani na ilitokea wapi. Mama Ninziza Bernice akamshika mkono Mama Bigirimana na kuanza kulia kwa uchungu.
“Mwanao anataka kuniulia binti yangu,” Mama Ninziza Bernice alisema kwa huzuni huku akitokwa na machozi.
Mama Bigirimana alimtazama Mama Ninziza Bernice kwa wasiwasi na bila kusubiri alianza kukimbilia kule nje huku akiita kwa sauti kubwa yenye hofu, “Baba Ibrahim, mwanao anamuua mtoto wa watu!”
Wakati Mama Bigirimana akiwa anakimbilia kule nje, Mzee Bigirimana naye alikuwa anaingia ndani mbio huku akiwa na wasiwasi mkubwa, wakakumbana mlangoni na kupiga mweleka sakafuni kwa mshindo mkubwa uliowaacha wakigaragara.
Mama Bigirimana alitoa ukelele wa maumivu huku akishika tumbo lake, Mzee Bigirimana alijizoazoa na kuinuka kutoka pale sakafuni huku akikunja uso wake akionekana kusikilizia maumivu, akahema kwa nguvu huku akimtazama mke wake pale sakafuni kwa makini.

ITAENDELEA...
 
HADI LINI! 20

Na Bishop Hiluka


Mama Ninziza Bernice aliwatazam wale wanaume kwa mashaka kidogo huku akiinuka na kuingia ndani huku akisindikizwa na macho ya wale wazee wawili, alipoingia ndani wakaketi pale kwenye sofa. Mzee Tugiramahoro alitoa paketi ya sigara kali, akatoa humo sigara mbili huku moja akiiwasha na kuanza kuvuta na sigara nyingine akanyoosha mkono wake kumpa Mzee Bigirimana. Mzee Bigirimana alikataa kwa kutingisha kichwa.
Mzee Tugiramahoro alipiga mkupuo mkubwa wa sigara na kuutoa moshi taratibu huku akiutazama kwa makini jinsi ulivyokuwa ukipanda juu na kupotelea hewani. Akapiga mkupuo mwingine na kutoa moshi mwingi, kisha akageuza shingo yake kumtazama Mzee Bigirimana.
Mzee Bigirimana alikuwa ameketi kimya kabisa akimwangalia mzee mwenziye kwa makini. Akashusha pumzi na kusimama kisha akaanza kuzunguka zunguka pale barazani huku akitazama juu, mikono yake akiwa ameiweka nyuma akionekana kuwaza mbali sana.
“Siku hizi tunazaa kenge na siyo watoto kabisa!” Mzee Bigirimana alisema kwa huzuni.
“Inategemea, maana si watoto wote ambao ni kenge, wapo wanaofaa kabisa,” Mzee Tugiramahoro alisema katika hali ya utulivu huku akiendeleaa kuvuta sigara yake taratibu.
“Wapo kweli wala sikatai, lakini si mimi na bwana mwenye mji huu,” Mzee Bigirimana alisema huku akimtupia jicho mzee mwenzake.
“Kwa nini unasema hivyo?” Mzee Tugiramahoro alimtazama kwa makini na kuuliza huku akipiga mkupuo mwingine na kutoa moshi mwingi.
“Kinachomliza mama yake ndicho ambacho yeye kadhamiria kukifanya!”
“Ni kipi hicho cha ajabu?” Mzee Tugiramahoro aliuliza kwa shauku huku akimkazia macho Mzee Bigirimana.
“Eti anataka kumtaliki mkewe na pengine aoe mwanamke mwingine!” Mzee Bigirimana alisema kwa huzuni.
“Kama akili yake ndivyo inavyomtuma basi amtaliki, lakini mimi sirejeshi mahari na wala binti yangu hatarudi nyumbani kwangu,” Mzee Tugiramahoro alisema kwa hamaki huku donge la hasira likimkaba kooni. Muda ule alianza kuiona ile sigara chungu.
“Hapana, tusikose hekima, mzee mwenzangu, wacha tuwaite wote wawili na kisha tuwahoji maana ndilo tuliloitiwa na mkwe wangu!”
Mzee Tugiramahoro alimtazama Mzee Bigirimana kwa kitambo kirefu pasipo kusema neno kisha alipiga mkupuo mwingine mkubwa wa moshi na kuutoa na kukitupa chini kipande cha sigara kilichobakia na kukisigina kwa mguu wake.
“Bahati ya binti yangu ni mbaya sana, walikuja vijana wengi tu wa maana waliotaka kumuoa nikakataa, kumbe sikujua kama namtumbukiza kwenye pango la mbwa mwitu,” Mzee Tugiramahoro alisema kwa huzuni maneno yaliyoonekana kumchoma na kumkera sana mzee mwenziye.
Mzee Bigirimana alimkazia macho mzee mwenziye huku hasira zikianza kumpanda, “Nadhani sasa tusianze kutukanana kirejareja, mimi si mjinga na wewe unafahamu hilo… cha msingi ni kuzungumza na watoto wetu ili tuwaweke sawa.”
“Tuwawekeje sawa wakati tayari mwanao anamuona binti yangu kama chawa!” Mzee Tugiramahoro alimuuliza mzee mwenziye huku hasira zikianza kumtambaa mwilini mwake na kuyafanya maungo yake kuzizima.
Mzee Bigirimana alitaka kusema neno lakini akasita na kushusha pumzi. Kisha wale wazee walibaki wakitazamana pasipo kusema neno kwa kitambo kirefu. Mzee Tugiramahoro alitoa sigara nyingine na kuiwasha kisha akapiga mkupuo mkubwa na kutoa moshi mwingi huku akihema kwa nguvu.
* * * * *
Akiwa pale kwenye balcony Ibrahim aliendelea kutazama kule chini kisha kama aliyekumbuka kitu akaondoka na kurudi chumbani, akaanza kuranda randa mle ndani huku akiwa kainamisha uso wake, alionekana kuwa katika dimbwi la mawazo.
Muda ule Pamela alikuwa amepiga magoti akipanga vizuri nguo zake ndani ya kabati kubwa la nguo la ukutani. Ibrahim alikuwa anageuka mara kwa mara kumtazama Pamela huku akiwa na donge la hasira.
“Kabla sijasahau, naomba ukitaka kuondoka hakikisha kwanza umenitayarishia kabisa orodha ya mali yangu humu ndani.”
“Kila kinachostahili kufanywa tayari kipo kwa wakili wangu, wewe tengeneza listi yako ukampe wakili wako,” Pamela alimjibu Ibrahim huku akiendelea kupanga nguo zake ndani ya lile kabati.
“To hell with your lover boy,” Ibrahim alifoka kwa hasira na kumkwida Pamela kwa ghadhabu. Pamela hakuogopa bali alionekana kumshangaa sana Ibrahim.
“Mimi tena? Siyo wewe na mlolongo wa malaya wako wa ushirika?” Pamela alimuuliza Ibrahim huku akimtazama kwa mshangao.
Ibrahim alionekana kuhamaki sana, akamnyanyua Pamela na kumsukuma kwa ghadhabu, Pamela akaanguka pale sakafuni na kuinuka haraka huku akimtazama Ibrahim kwa tabasamu, kisha akatingisha kichwa chake kwa dharau.
Akiwa bado anatingisha kichwa kwa dharau alishtuliwa na kibao kikali cha ghafla ambacho hakukitegemea kilichotua kwenye shavu lake la kushoto, akaanguka sakafuni huku lile tabasamu likiyeyuka na badala yake hofu ikachukua nafasi yake.
Pamela alijishika shavu lake huku akimtazama Ibrahim kwa hofu kubwa akiwa haamini kilichotokea, mdomo wake wa chini ulikuwa umechanika kidogo na damu zilianza kumtoka kwenye mdomo wake. Alifuta damu huku donge la hasira likizid kumkaba kooni.
“Unanipiga!” Pamela alimwuliza Ibrahim kwa mshangao huku akiinuka kutoka pale sakafuni, akasimama huku akimkazia macho, ni wazi hasira zilikuwa zinachemka ndani kwa ndani. Ibrahim hakumkawiza, akampiga teke lililotua kwenye tumbo lake na kumdondosha chini huku akilishika, akaanza kulia kwa uchungu sauti kubwa.
Sauti ya kilio chake ilipenya na kusambaa kila mahali, kuanzia pale sebuleni walipokuwa wameketi wale kina mama, barazani walipokuwa wamekaa wale wazee wakiongea hadi kule chumbani walikokuwa wamelala watoto wao Nduwimana na Samantha.
Mama Ninziza Bernice na Mama Bigirimana walinyanyuka kutoka kwenye sofa walipokuwa wamekaa huku wakitazamana kwa wasiwasi, walionekana kujaribu kusikiliza kwa makini ili kubaini sauti hiyo ilikuwa ya nani na ilitokea wapi. Mama Ninziza Bernice akamshika mkono Mama Bigirimana na kuanza kulia kwa uchungu.
“Mwanao anataka kuniulia binti yangu,” Mama Ninziza Bernice alisema kwa huzuni huku akitokwa na machozi.
Mama Bigirimana alimtazama Mama Ninziza Bernice kwa wasiwasi na bila kusubiri alianza kukimbilia kule nje huku akiita kwa sauti kubwa yenye hofu, “Baba Ibrahim, mwanao anamuua mtoto wa watu!”
Wakati Mama Bigirimana akiwa anakimbilia kule nje, Mzee Bigirimana naye alikuwa anaingia ndani mbio huku akiwa na wasiwasi mkubwa, wakakumbana mlangoni na kupiga mweleka sakafuni kwa mshindo mkubwa uliowaacha wakigaragara.
Mama Bigirimana alitoa ukelele wa maumivu huku akishika tumbo lake, Mzee Bigirimana alijizoazoa na kuinuka kutoka pale sakafuni huku akikunja uso wake akionekana kusikilizia maumivu, akahema kwa nguvu huku akimtazama mke wake pale sakafuni kwa makini.

ITAENDELEA...
Ila wanaume nyinyi mkishaonjeshwaga uko nje mnabadilika sana na kudharau wake zenu
 
Nimejikuta nashusha pumzi kwa huzuni, hii hadithi imenirudisha mawazo yangu mbali mnooo, Ndoa hizi jamani kama mtu hajapitia haya ashukuru Mungu,nmejikuta chozi la hasira limenitoka, uchepuke halafu bado unaishia kumpiga
 
Salama mkuu nitag kiongozi
HADI LINI!

Na Bishop Hiluka

Yalikuwa yamemfika kooni baada ya kuitafuta haki yake kila mahali na kushindikana, akafikia uamuzi wa kuwaita wazazi wa pande zote mbili ili aweke wazi kuhusu msimamo wake juu ya ndoa yake. Kama noma na iwe noma lakini asingeweza kuendelea kuvumilia, avumilie hadi lini!...


JUMAMOSI, saa kumi na mbili na nusu jioni, kwa saa za Burundi, sauti tamu ya muziki laini wa kubembeleza ilikuwa inasikika kutoka katika spika zilizokuwa kwenye kona za ukumbi mkubwa wa kisasa wa burudani ndani ya Hotel Club du Lac Tanganyika.
Club du Lac Tanganyika ilikuwa hoteli yenye hadhi kubwa iliyokuwa imejengwa kwenye mandhari ya kuvutia ya ufukwe wa Ziwa Tanganyika jijini Bujumbura, Burundi. Ilikuwa hoteli ya kisasa kabisa iliyokuwa imezungukwa na mazingira yenye utulivu mkubwa ufukweni mwa ziwa, ikiwa kando ya barabara ya Chausse d'Uvira iliyokuwa inaelekea katika mji mdogo wa Uvira.
Ikiwa imezungukwa na uzio madhubuti ulioifanya kuwa mahali patulivu zaidi na penye usalama wa uhakika, ilikuwa sehemu tulivu zaidi ya kwenda kujirusha kwa watu wenye ukwasi, ikiwa umbali wa kilomita tatu tu kutoka katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Bujumbura.
Pia ilikuwa sehemu muhimu sana kwa burudani na wageni wengi kutoka nje walipenda kwenda sehemu ile, hasa mwisho wa wiki, kutokana na kuwa na kumbi mbili za kisasa: ukumbi mmoja ulitumika kwa ajili ya mikutano, ukiwa na sifa zote, na wenye viyoyozi na umeme wa uhakika saa 24, jambo linaloufanya kuvutia wageni mbalimbali. Ukumbi mwingine ulitumika zaidi kwa ajili ya burudani na matukio.
Ukumbi wa burudani ulikuwa na kila aina ya starehe, ukiwa na madirisha makubwa ya vioo yaliyofunikwa na mapazia safi marefu, na ulikuwa na kila kionjo cha daraja la kimataifa. Ndani ya ukumbi ule kulikuwa na wahudumu wazuri wa kike, warembo kwelikweli, waliokuwa wakihudumia wateja wachache waliokuwemo ukumbini muda huo wakiwa wameketi kwenye meza nzuri za mbao ya mti wa mninga na viti vifupi vyenye foronya laini.
Muda ule wa saa kumi na mbili na nusu za jioni idadi kubwa ya wateja waliokuwemo ndani ya ukumbi ule walikuwa raia wa kigeni, hasa kutoka katika nchi za Ufaransa na Marekani. Upande wa kulia wa ukumbi ule kulikuwa na mlango na dirisha dogo la jikoni, na humo ndani kulionekana wapishi waliokuwa katika mavazi yao ya kazi, wakiandaa chakula.
Katika ukumbi ule, mmoja wa wateja Waafrika walioonekana aliitwa Ibrahim Bigirimana, alikuwa mwanamume wa Kitanzania aliyekuwa na asili ya kutoka mkoa wa Kigoma, mkoa ambao uko pembezoni mwa nchi ya Tanzania katika mpaka wa Tanzania na Burundi.
Ibrahim Bigirimana alikuwa ameketi peke yake kwenye meza moja akionekana kuzama katika fikra fulani huku akiwa na shauku kubwa ya kusubiri kitu fulani muhimu sana, ambacho, ni yeye tu kati ya watu wote waliokuwemo mle ukumbini ndiye aliyekuwa akikijua.
Ibrahim alishusha pumzi za ndani kwa ndani na kutupa macho yake kuangalia nje kupitia ukuta msafi wa kioo cha dirisha, mkono wake mmoja alikuwa ameshika bilauri ndefu iliyokuwa na mvinyo mwekundu wa Kifaransa aina ya Navette de Marseille, na mkono wake wa kushoto alikuwa kauegemeza juu ya kiti alichokalia. Ibrahim akainua bilauri ya mvinyo na kupiga funda taratibu huku akionekana kuwaza mbali sana.
Alikuwa mwanamume mrefu na maji ya kunde, akiwa na sura bashasha ya kitoto iliyokuwa na muonekano uliomfanya mtu yeyote aliyemuona adhani kuwa hangeweza kuzidi miaka therathini, ingawa alishapita miaka hiyo.
Akiwa na umri wa miaka arobaini na mbili, kimuonekano, Ibrahim alikuwa na umbo kakamavu la kimichezo lililofanana na maumbo ya wachezaji wa ligi ya mpira wa kikapu wa nchini Marekani.
Alikuwa mcheshi sana na mtu wa kupenda kujichanganya na watu wengine bila kujali kipato, alikuwa muongeaji mkubwa mwenye kuzimudu vyema lugha za Kiswahili, Kiingereza, Kifaransa na hata Kirundi, lugha iliyokuwa ikizungumzwa zaidi na wenyeji wa nchi ile ya Burundi, jambo ambalo liliwafanya watu wengi kudhani kuwa labda alikuwa Mrundi mwenzao, hasa kwa kuwa hata jina lake la mwisho la ‘Bigirimana’ ni jina lililokuwa linatumiwa na Warundi.
Ibrahim alikuwa Muha kutoka mkoani Kigoma, kabila lililokuwa na utamaduni ulioshabihiana kwa kiasi kikubwa sana na ule utamaduni wa Warundi.
Ibrahim alikuwa ameishi jijini Bujumbura kwa takriban miaka kumi sasa. Na alikuwa akifanya kazi kama Meneja Mkuu wa CRDB Bank Burundi, benki iliyokuwa na makao yake katika barabara ya Chaussée du Prince Louis Rwagasore, ploti namba 490/A, jijini Bujumbura.
Kwa nafasi hiyo, Ibrahim alikuwa mtu mwenye mafanikio mema, ingawa alikuwa na kasoro moja iliyoonekana wazi, hakuwa na wala hakupenda kuwa na kitambi.
Wengi walidhani labda Ibrahim alikuwa amebebwa hadi kufikia nafasi ile, lakaini ukweli hakufikia nafasi ya ile ya umeneja mkuu wa benki hiyo kwa bahati au kama wasemavyo Waswahili ‘zali la mentali’, bali alikuwa nazo sifa zinazostahili ikiwemo elimu ya juu na uzoefu wa kazi.
Kabla hajakuwa Meneja Mkuu wa CRDB Bank Burundi, ibrahimu alikuwa amefanya kazi kama Manager Corporate Banking na baadaye akawa Senior Relationship Manager Corporate Banking katika Benki ya Biashara ya Burundi (Commercial Bank of Burundi) iliyokuwa na makao yake katika makutano ya barabara za Avenue des USA na Chaussée P.L. Rwagasore, ikiwa mkabala na jengo la CRDB Bank Burundi, jijini Bujumbura.
Ibrahim alikuwa msomi wa Shahada ya Umahili ya Business Administration aliyoipata kutoka Chuo Kikuu cha Oxford, Uingereza, ambacho kilikuwa chuo kikongwe zaidi katika ulimwengu wa nchi zinazozungumza lugha ya Kiingereza, na Shahada ya Kwanza ya Banking and Financial Services aliyohitimu kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Tanzania.
Baada ya kumaliza chuo kikuu na kabla hajaenda kufanya kazi nchini Burundi, Ibrahim alikuwa amefanya kazi kaatika Benki Kuu ya Tanzania kwa miaka miwili kisha akaacha na kwenda kuishi jijini Bujumbura ambako aliajiriwa katika benki ya biashara ya Burundi. Hii ilitokana na yeye kuamua kumfuata mke wake aliyekuwa amerudishwa nchini Burundi baada ya kukumbwa na matatizo ya uraia alipokuwa akiishi nchini Tanzania.
Alipofika Burudni na kuajiriwa Commercial Bank of Burundi Ibrahim alifanya kazi kwa miaka kadhaa, na kutokana na uwezo wake na ufanisi kazini alichukuliwa na CRDB Bank Burundi, kama mwanzilishi na Meneja Mkuu wa benki hiyo jijini humo, nafasi ambayo aliweza kudumu nayo hadi wakati huo.
Huyo ndiyo Ibrahim Bigirimana, ambaye Jumamosi hiyo alikuwa katika ukumbi wa maraha wa Hotel Club Du Lac Tanganyika akiwa mwenye shauku kubwa. Alinyanyua bilauri yake na kunywa funda dogo la mvinyo kisha akaitazama saa yake ya mkononi kwa mara nyingine tena kisha akaonekana kutikisa kichwa chake.
Alishusha pumzi za ndani kwa ndani huku akisonya kwa huzuni, ni wazi alikuwa hapo akisubiria kitu muhimu sana lakini hadi muda ule alionekana kuanza kuishiwa na uvumilivu. Aliitazama tena saa yake na kuminya midomo yake akionekana kuwaza mbali, akabaki akiikodolea macho ile saa kana kwamba ilikuwa mbovu.
Laiti kama ingelikuwa saa ya kawaida labda angeweza kusema kuwa ilikuwa na kasoro, lakini hiyo saa kama ilivyo kwa vitu vyake vingi, haikuwa ya kawaida kabisa!

ITAENDELEA...

Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY

Sent using Jamii Forums mobile app
 
HADI LINI! 21

Na Bishop Hiluka


ILIPOISHIA

Mama Bigirimana alimtazama Mama Ninziza Bernice kwa wasiwasi na bila kusubiri alianza kukimbilia kule nje huku akiita kwa sauti kubwa yenye hofu, “Baba Ibrahim, mwanao anamuua mtoto wa watu!”
Wakati Mama Bigirimana akiwa anakimbilia kule nje, Mzee Bigirimana naye alikuwa anaingia ndani mbio huku akiwa na wasiwasi mkubwa, wakakumbana mlangoni na kupiga mweleka sakafuni kwa mshindo mkubwa uliowaacha wakigaragara.
Mama Bigirimana alitoa ukelele wa maumivu huku akishika tumbo lake, Mzee Bigirimana alijizoazoa na kuinuka kutoka pale sakafuni huku akikunja uso wake akionekana kusikilizia maumivu, akahema kwa nguvu huku akimtazama mke wake pale sakafuni kwa makini.

ENDELEA...

Kule chumbani Pamela aliendelea kulia kwa uchungu mkubwa akiwa bado yupo pale sakafuni kashika tumbo lake. Ibrahim alisimama huku akimtazama kwa hasira, akamnyooshea kidole chake kwa hasira na kumfuata pale sakafuni akitaka kumpa kichapo kingine. Hata hivyo, hakuwahi kwani mlango wa chumbani kwao ulipigwa kumbo na kumfanya Ibrahim ashtuke sana na kugeuka kuangalia kule mlangoni.
Akamuona Nduwimana akiingia mbio ndani ya chumba chao pasipo hata kubisha hodi na kusimama huku akimtazama baba yake kwa chuki. Pamela akiwa bado yupo sakafuni alimuona Nduwimana na kujinyanyua huku akiendelea kulia kwa uchungu.
“Tafadhali niache niwalee wanangu,” Pamela alisema huku akijizoa zoa kutoka pale sakafuni.
“Huyu mama yako ni jeuri na mjinga sana, sasa atakula jeuri yake,” Ibrahim alimwambia Nduwimana huku akisonya. Kisha akataka kumfuata tena Pamela akitaka kumwadhibu lakini Nduwimana aliyekuwa akimtazama baba yake kwa chuki alimshika miguu yake na kumng’ang’ania huku akipiga kelele na kulia kwa sauti kubwa.
“Mwache mama yangu! Mwache mama!” Nduwimana alikuwa anasema huku akilia.
Ibrahim alijaribu kujinasua kutoka kwenye mikono ya Nduwimana lakini Nduwimana aliendelea kumng’ang’ania pasipo kumwachia huku akizidi kupiga kelele na kufanya sauti yake na ile ya mama yake zizidi kupaa na kusambaa hewani hata katika eneo la jirani katika ule usiku tulivu.
Mzee Bigirimana na Mama Bigirimana walipanda ngazi mbio kuelekea kule juu huku wakiwa na wasiwasi mkubwa. Nyuma yao walifuatwa na Mzee Tugiramahoro na mkewe ambao walikuwa wakipanda ngazi huku wakiwa na wasiwasi mkubwa.
Mzee Bigirimana na Mama Bigirimana walipofika kwenye korido wakitaka kuelekea kwenye chumba cha Ibrahim na Pamela wakashtulia na Samantha aliyewapita mbio akielekea kule kwenye chumba cha wazazi wake huku akilia kwa uchungu. Alipoufikia mlango wa chumba cha wazazi wake aliupiga kumbo, akaingia na kuuacha mlango ukiwa wazi.
Mama Bigirimana na Mzee Bigirimana walisimama ghafla na kurudi nyuma wakionesha nidhamu katika kuendeleza mila na desturi za Kiafrika za kutotaka kuona kile kilichokuwa kinaendelea ndani ya chumba cha watoto wao. Muda huo huo Mama Ninziza Bernice na mumewe nao wakafika na kusimama nyuma yao, wote wakiwa na wasiwasi mkubwa. Kisha wakawa wanasikilizia kwa makini sauti za vilio kutoka mle chumbani.
Nduwimana aliendelea kumng’ang’ania baba yake huku akilia, Samantha alipoingia alimkumbatia mama yake ambaye alikuwa bado yupo sakafuni, wote wakawa wanalia kwa uchungu na kufanya kile chumba kigeuke ukumbi wa simanzi na vilio kutoka kwa mama na watoto wake.
Ibrahim alibaki amesimama pasipo kufanya chochote, Pamela akainuka kutoka pale sakafuni na kujikung’uta mavumbi kisha akamkumbatia Samantha kwa uchungu huku akifuta machozi na kwenda kuchungulia kwenye ule mlango uliokuwa wazi. Akawaona wazee wote wanne wakiwa wamesimama pale nje ya mlango huku wakiangalia kwenye ule mlango kwa wasiwasi.
Mama Bigirimana alipomuona tu Pamela akashusha pumzi za ndani kwa ndani huku akionesha mashaka yake. “Mwanangu, uko salama kweli?” alimwuliza Pamela huku akishindwa kufika hofu aliyokuwa nayo.
“Hapana mama, nimo mashakani.”
“Mama, naomba niitie mumeo haraka, mwambie namhitaji huku chini,” Mzee Bigirimana alimwambia Pamela huku akiwa amepandwa hasira.
“Sawa, baba,” Pamela alisema na kuufunga ule mlango nyuma yake akiwaacha wale wazee bado wamesimama pale pale wakiendelea kuutazama ule mlango wa chumbani kwa wasiwasi.
Mzee Tugiramahoro na mke wake wakaangaliana kisha yule mzee akampa ishara mke wake amfuate kule chini huku akigeuka kuondoka na kuzifuata ngazi za kurudi sebuleni, mkewe naye akaondoka, wakaanza kushuka ngazi huku kila mmoja akiwa na hisia nzito.
Wakati wakiwa wanateremka zile ngazi taratibu Mzee Tugiramahoro alikuwa anasonya kwa hasira huku akionekana kukasirishwa sana na kitendo cha Ibrahim kumpiga Pamela.
“Yaani jitihada zangu zote za kumkuza mtoto wa kike leo hii navuna ufedhuli huu!” Mzee Tugiramahoro alisema kwa huzuni huku akigeuza shingo yake kumtazama mkewe.
“Binti yangu si fedhuli na sikumlea kifedhuli, hivyo hastahili kutendewa anayofanyiwa hapa, na laiti angelikuwa na baba mwenye kumpenda basi leo angesimama kidete kumtetea,” Mama Ninziza Bernice alisema kwa masikitiko.
“Kwa hiyo, unamaanisha kuwa mimi simuonei uchungu binti yangu, siyo?”
“Kama una uchungu basi fanya kile kinachostahili ili kumnusuru mwanao katika uonevu huu anaofanyiwa… tupo kwenye nchi yetu kwa nini tunyanyasike utadhani ni wakimbizi?”
Mzee Tugiramahoro alionekana kuguswa sana na yale maneno ya mkewe, akamwangalia kwa makini na kushusha pumzi za ndani kwa ndani huku akilamba midomo yake iliyoanza kukauka, kisha hakuongea tena, akawa anashuka ngazi kimya kimya huku akionekana kuzama kabisa kwenye lindi la mawazo.
Walipofika pale sebuleni, Mama Ninziza Bernice aliketi kwenye sofa huku akiwa bado ana wasiwasi, mumewe alikataa kuketi na kubaki akiwa amesimama huku amejishika kiuno. Sasa donge la hasira lilizidi kumkaba kooni na kumfanya apumue kwa shinda. Alisonya kwa hasira na kuanza kukunja mikono ya shati lake kisha akakwida suruali yake tayari kwa lolote.
“Nawasubiri waje! Leo watanitambua!” Mzee Tugiramahoro alisema kwa hasira huku akitazama kule kwenye ngazi. Muda huo huo Mzee Bigirimana na mkewe walionekana wakiziendea zile ngazi kisha wakaanza kushuka taratibu huku wakiongea kwa sauti ya chini. Mzee Bigirimana alikuwa akimuangalia mke wake kwa masikitiko.
“Hivi fedheha gani hii anafanya mwanao! Kama ni kuacha mke amwache basi na aoe mwingine, kwani ana shida gani, mali anayo ni mwanamke gani atamkataa?” Mzee Bigirimana alimwambia mkewe na kumfanya yule mama agune.
“Kuoa ovyo kuna athari zake, hivi unafikiri ni nani mlezi mzuri wa watoto zaidi ya mama?”Mama Bigirimana alisema huku akionekana kutoafikiana kabisa na maneno ya mume wake, alitingisha kichwa chake taratibu kukataa kata kata.
Mzee Bigirimana aligeuza shingo yake kumwangalia mke wake kwa makini, akaonekana kuguswa na yale maneno, alishusha pumzi huku akibaki kimya. Muda ule walikuwa wamefika pale sebuleni na kuwakuta wazee wenzao wakiwa wanawasubiri. Mzee Tugiramahoro alipowaona akawapokea kwa maneno makali huku akianza kutamba pale sebuleni.
“Nasema hivi, nangojea maiti ya binti yangu lakini na mimi leo nitaacha maiti ya mtu mwingine ndani ya nyumba hii,” Mzee Tugiramahoro alisema kwa hasira huku akiranda randa kwa ghadhabu.
“Mzee mwenzangu, najua uchungu ulio nao lakini jaribu kutuliza jazba kidogo… kumbuka kuwa hata jina lako la Tugiramahoro lina maana ya ‘tuwe na amani’,” Mzee Bigirimana alijaribu kumsihi mzee mwenziye.
“Jina ndiyo kitu gani! Yaani nivumilie mwanangu anaumizwa eti kwa kuwa jina langu linamaanisha amani! Na kama kijana wako ameweza kumpiga binti yangu mbele yangu, vipi pale wanapokuwa wenyewe tu?” Mzee Tugiramahoro alisema kwa hasira na kurusha mikono yake juu kudhihirisha hasira aliyokuwa nayo juu ya Ibrahim.

ITAENDELEA...

Cc Shunie the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY ADK Roram
 
HADI LINI! 22

Na Bishop Hiluka


Mzee Bigirimana anamtazama Mzee Tugiramahoro kwa wasiwasi. Anataka kusema lakini anasita na kushusha pumzi.
* * * * *
Alipoufunga ule mlango na kuwaacha wale wazee nje, Pamela alisimama akamtazama Ibrahim kwa makini na kushusha pumzi za ndani kwa ndani. Muda ule Ibrahim alikuwa amesimama huku amewashika watoto wake, mmoja mkono wake wa kulia na mwingine mkono wake wa kushoto. Pamela aliwasogelea wale watoto na kuwashika mikono kwa upole.
“Nendeni mkalale wanangu, hivi sasa ni saa nane usiku,” Pamela alisema kwa sauti tulivu akijaribu nkuwashawishi wale watoto.
Nduwimana na Samantha walimtazama mama yao kwa wasiwasi kisha wakageuza shingo zao kumtazama baba yao kwa hofu na kuondoka bila ubishi, lakini wakiwa na wasiwasi. Pamela aliwatazama wale watoto kwa upole huku akiachia tabasamu. Walitoka na kuufunga ule mlango nyuma yao.
Pamela akaufungua ule mlango na kuwachungulia ili kuhakikisha wameondoka na kuelekea kwenye vyumba vyao kisha akaufunga tena mlango nyuma yake na kumkabili Ibrahim.
“Unaitwa na baba yako huko chini,” Pamela alimwambia Ibrahim huku akimtazama kwa makini.
Ibrahim alimtazama Pamela kwa kitambo kifupi na kushusha pumzi kisha akageuka kuutazama mlango. “Nakwenda kuwaeleza wazee kwamba hunifai na ninakutwanga talaka.”
“Kwangu itakuwa ni bonge la barafu jangwani,” Pamela alisema huku akiachia tabasamu lililokuwa limebeba chuki.
Ibrahim aliinua mkono wake kutaka kumpiga kibao Pamela lakini akasita, kisha akageuka na kuanza kuondoka lakini kabla hajatoka kabisa aligeuka kumtazama Pamela kwa chuki.
“Utajuta nikikuacha,” Ibrahim alisema huku chuki ikijionesha wazi wazi usoni kwake.
“Kama wewe ndiye mfalme wa upendo na faraja n’tajuta,” Pamela alisema huku naye chuki ikijionesha wazi wazi usoni kwake. Wakatazama kwa sekunde kadhaa bila kusema. Kisha Ibrahim akasonya na kuondoka huku akiubamiza ule mlango kwa hasira. Pamela alishusha pumzi huku akitingisha kichwa chake kwa huzuni.
Ibrahim alianza kushuka ngazi taratibu akiwa na wasiwasi kidogo, alipokaribia kufika sebuleni akasimama na kuchungulia pale sebuleni na kumuona baba yake akiwa kasimama huku amejishika kiuno akitazama kule kwenye ngazi kwa hasira, Ibrahim akaonekana kusita sana. Alisimama pale kwa sekunde chache akionekana kujishauri kama ashuke au akaidi agizo la wazee na kurudi chumbani kwake.
Mzee Tugiramahoro pia alikuwa amesimama akiwa kajiandaa kwa lolote, alikuwa anaranda randa pale sebuleni huku akigeuka mara kwa mara kumwangalia Mzee Bigirimana. Mama Ninziza Bernice na Mama Bigirimana wao walikuwa wameketi kwenye sofa kwa utulivu lakini wakiwa na huzuni iliyochanganyika na wasiwasi.
Ibrahim alijipa ujasiri na kuanza kuzishuka zile ngazi taratibu, aliamini kuwa ndiye mwenye uamuzi wa kumuacha mwanamke yule na kuoa mwanamke mwingine na hakuna yeyote wa kumpangia aishi vipi kwenye nyumba yake. alishuka na kufika pale sebuleni, akasimama huku akiwatazama wale wazee akijitahidi kuzuia hofu iliyokuwa inataka kuutawala moyo wake.
Mzee Bigirimana alimkazia macho Ibrahim yaliyoashiria hasira alizokuwa nazo, na wakati huo huo Mzee Tugiramahoro alikuwa anamwangalia Ibrahim kwa hasira huku akiwa ameuma midomo yake.
Mama Bigirimana na Mama Ninziza Bernice walikuwa wanamwangalia Ibrahim kwa wasiwasi. Ibrahim akasimama karibu na baba yake huku akijaribu kuachia tabasamu pana usoni kwake. Bahati mbaya hakujua nini kilichokuwa akilini kwa baba yake wakati huo.
“Bwana mkubwa, hatukuitwa hapa na mkeo kuja kuoneshwa jinsi ulivyo hodari wa kupiga mke, kama ni huo umwamba sisi hatukuona faida yake enzi zetu,” Mzee Bigirimana alimwambia Ibrahim huku akimtazama kwa makini, hata hivyo Ibrahim aliendelea kutabasamu huku akionesha kujiamini.
“Lakini, baba…” Ibrahim alianza kusema lakini akakatizwa na kibao kikali cha ghafla kilichotua kwenye shavu lake kutoka kwa baba yake na kumwangusha pale sakafuni. Ibrahim alitahayari sana na kujishika shavu lake akiwa haamini kilimchotokea, alimkodolea macho baba yake kwa wasiwasi.
Mzee Bigirimana alimtazama kwa hasira huku akikaa sawa, alikuwa amekunja ngumi tayari kwa mpambano endapo Ibrahim angetaka kuleta matata, akafoka kwa ghadhabu, “Simama sasa unipige mimi kama unavyompiga mtoto wa watu.”
Ibrahim alitaka kusema neno lakini maneno yakawa hayatoki mdomoni, akajizoa zoa kutoka pale sakafuni na kusimama akiwa katahayari sana huku akiendelea kujikuna kwenye lile shavu. Mzee Tugiramahoro aliwatazama Mzee Bigirimana na mwanawe kwa zamu na kutingisha kichwa chake kwa masikitiko.
“Wala haitasaidia kumpiga huyu bwana mdogo, naomba tu umweleze kuwa nashukuru sana kwa yote aliyomfanyia binti yangu, hivi sasa nasubiri ampe talaka usiku huu ili alfajiri niondoke naye.”
Mzee Bigirimana alimwangalia Ibrahim kwa hasira. “Haya baba nadhani umemsikia mkweo, kamtwange talaka mkeo na mimi nikuachie radhi yangu niondoke usiku huu huu, wala sina haja ya kusubiri kukuche.”
Ibrahim aliwatazama wale wazee kwa unyonge sana, akashusha pumzi za ndani kwa ndani. “Mimi niseme nini sasa wakati binti yenu tayari kishaamua kuupeleka unyumba wetu kwa wakili ili akaachwe na mahakama.”
Mzee Tugiramahoro akashituka sana na kumkodolea macho Ibrahim, alionekana kushangaa sana na kumkodolea macho kana kwamba alikuwa ameona kitu cha ajabu sana. Kisha akatingisha kichwa chake kwa nguvu zote.
“Sijazaa mtoto wa kwenda kudai talaka mahakamani!” Mzee Tugiramahoro alisema huku akishusha pumzi.
“Lakini hiyo ndiyo hali halisi, sasa mnatarajia nini kutoka kwangu? Kwa kweli mnanionea bure!” Ibrahim alisema kwa unyonge mkubwa.
Mzee Bigirimana akamkodolea macho Ibrahim akiwa haamini kile alichokisikia na kutingisha kichwa chake taratibu kukataa. “Haiwezekani! Yaani mwanamke adai talaka hivi hivi tu!”
Ibrahim aliwatazama kwa makini na kuinamisha kichwa chake chini, akakunja sura yake iliyotengeneza matuta madogo usoni huku donge la hasira ya kupigwa kibao na baba yake likiwa limemkaba kooni. Mzee Tugiramahoro akiwa bado anashangaa, alimsogelea Ibrahim huku akimkazia macho.
“Wewe si ndiye mumewe, tueleze sababu inayomfanya mkeo adai talaka mahakamani, kama ni kweli hayo usemayo!”
“Hakuna kingine ni wivu tu, anadai haki sawa eti kwa vile yeye kasoma na siyo kama mama yangu,” Ibrahim alisema kwa huzuni huku akitingisha kichwa chake kwa huzuni.
Mzee Bigirimana aligeuka kumtazama mkewe kwa makini kisha akayarudisha macho yake kumwangalia Ibrahim. “Usawa wa namna gani anaoudai mkeo?”
“Usawa wa kimaisha ili aweze kwenda baa na kunywa pombe kama mimi, aweze kujiamulia chochote kile mwenyewe bila kupangiwa, na pengine anataka kufuga ndevu kama wanaume walivyo!” Ibrahim alisema kwa kujiamini huku akiinamisha kichwa chake.
Kikazuka kitambo kirefu cha ukimya huku sebule yote ikizizima kwa ukimya ule, kila mmoja alionekana kuzama kwenye tafakari nzito kuhusu kauli ile aliyoitoa Ibrahim.
Mzee Bigirimana alivuta pumzi ndefu kisha akazishusha taratibu huku akionesha kuyaamini yale maneno ya Ibrahim kwa asilimia zote.
“Kama mazingira ndiyo haya, nakushauri mpe talaka haraka na nitahakikisha unapata mke atakayetambua wazi kwamba mwanamke siku zote ni kajakazi tu kwa mwanaume, azae na kulea watoto basi,” Mzee Bigirimana alisema huku akipumkua kwa nguvu.

ITAENDELEA...
 
HADI LINI! 23

Na Bishop Hiluka


Mama Bigirimana akamtazama mumewe kwa jicho kali huku akiguna, akatingisha kichwa chake kwa huzuni huku akionekana kutofautiana kabisa na yale maneno ya mumewe. Wakati huo huo Mzee Tugiramahoro alimsogelea mkewe na kuongea naye kwa sauti ya chini.
“Umesikia mambo ya binti yako? Kumbe kibiritingoma ni yeye… tangu lini mwanamke akawa huru akiwa kaolewa, na haki hiyo aipate wapi?”
Mama Ninziza Bernice alionekana kukerwa zaidi na maneno ya mume wake, akamwangalia kwa makini na kushusha pumzi huku akitingisha kichwa chake taratibu.
“Sidhani kama maneno haya yana ukweli wowote, binti yangu namjua vizuri, hajawahi na hana tabia kama hiyo!” Mama Ninziza Bernice alisema kwa kujiamini na kuwafanya watu wote wageuke kumtazama kwa mshangao. Donge la hasira lilikuwa limemkaba kooni na kumfanya aanze kulengwa na machozi, alimtazama Mzee Bigirimana kwa makini.
“Naomba niitieni binti yangu nimsikie mwenyewe mbele yenu, na kama ni kweli haya asemavyo mwanenu basi usiku huu huu nitaondoka naye, maana kibaya chako ni chako, vizuri waachie wenye navyo.”
Mzee Tugiramahoro alimtazama mke wake kwa makini na kuonekana kuafiki maneno yake huku akionesha kutokuwa na msimamo, hakujua asimamie upande upi. Sasa donge la hasira lilikuwa limesimama kwenye koo lake na kumfanya ashindwe kupumua vizuri, akaona kuwa hakuwa na namna nyingine ya kuliondoa isipokuwa kusema kile alichodhani kuwa ni sahihi.
“Bwana mdogo, unaweza kuwadanganya watu wote kwa muda fulani tu lakini siyo muda wote. Sisi si wajinga kama unavyodhani japo hatukusoma kama wewe, ikiwa umepanga kumwacha binti yangu basi mwache kwa usalama ila usitake kutafute sababu zisizoeleweka, lakini nataka nikwambie kabisa sitakubali bali nitapigania haki yake hadi mwisho…” Mzee Tugiramahoro alisema na kuwafanya watu wote wamtazame kwa mshangao uliochanganyika na wasiwasi.
“Na mimi nataka ukamwite binti yangu ili nimsikie mwenyewe mbele yako, kisha nitajua cha kufanya,” Mzee Tugiramahoro aliongeza huku akimkazia macho Ibrahim.
Ibrahim alimtazama Mzee Tugiramahoro kwa wasiwasi, akataka kusema neno lakini akasita sana na kuonekana kutahayari sana. Aliendelea kumkodolea macho yule mzee kwa wasiwasi kwa kitambo fulani kisha akainamisha kichwa chake kutazama chini huku akishusha pumzi ndefu.
“Nadhani umewasikia wakwe zako, nenda kamwite mkeo, mbona bado upo hapa?” Mzee Bigirimana alimwambia Ibrahim kwa sauti iliyojaa hasira huku akimkazia macho.
Ibrahim alishusha pumzi ndefu akionekana kusita sana, akamtupia jicho la wasiwasi Mzee Tugiramahoro.
“Sisi siyo wajinga, hatuwezi kuacha shughuli zetu huko tukaja hapa kuchezeshwa kama vikaragosi! Itashangaza sana mke atuite kuja kusaidia kutafuta ufumbuzi wa ndoa yake halafu eti kumbe huyo huyo ndiye amekwenda kutafuta talaka mahakamani! Huu si upuuzi wa karne!” Mzee Tugiramahoro alisema huku akimkazia macho Ibrahim.
“Ni kweli… mimi sitaki kumtetea mwanangu, ukweli ni bora usemwe kuliko kuficha ficha, maana hatukuja hapa kuwatenganisha wanetu ila kuwaweka sawa ili waishi vizuri na kulea watoto wao…” Mama Bigirimana ambaye muda mwingi alikuwa kimya alisema kwa huzuni.
Mama Ninziza Bernice alitaka kusema neno lakini akashindwa, machozi yakaanza kumtoka na kutiririka kwenye mashavu yake. Mzee Bigirimana alitaka kusema lakini hatia ikamkaba kooni na kubaki kimya akiwatumbulia macho wazee wenzake.
“Kama hali ndiyo imefikia hapa sitakuwa na furaha tena iwapo binti yangu ataendelea kuishi kwenye nyumba hii, ni bora niondoke naye!” Mama Ninziza Bernice alisema kwa huzuni huku akifuta machozi.
Kauli ile ikaonesha kumuogopesha sana Mama Bigirimana ambaye alimtazama Mama Ninziza Bernice kwa wasiwasi kisha akageuka kumtazama Ibrahim.
“Kama akili yako imefikia hatua hiyo ya kutaka kumwacha mkeo ili uoe mwanamke mwingine, nasema huyo mwanamke sitakuwa na radhi naye na wala hataingia humu ndani, na utakapooa tu nakuachia laana, bora nijue kuwa sina mtoto kuliko kunitia aibu kiasi hiki!” Mama Bigirimana alisema kwa hasira na kufunika uso wake kwa viganja vya mikono yake, machozi yalianza kumtoka.
Ibrahim alikuwa amechangayikiwa kabisa, aliwatazama wale wazewe bila kujua afanye nini, kikazuka tena kitambo kirefu cha ukimya pale sebuleni, kila mmoja alionekana kutafakari kwa kina. Ibrahim alikuwa ametahayari sana, akainamisha kichwa chake chini kwa wasiwasi.
Mzee Bigirimana alikuwa akimtazama kwa makini huku naye akionekana kuwaza mbali sana, kisha akakohoa kidogo kurekebisha sauti yake.
“Haya baba, nadhani umewasikia mama zako… wewe ndiye mwenye uamuzi wa mwisho ikiwa kusuka ama kunyoa. Mimi sitii tena neno hapo…” Mzee Bigirimana alisema huku akishusha pumzi.
“Hapa suluhu ni moja tu, akamwite mkewe ili tusikie na upande wa pili, mimi sioni sababu ya kumlazimisha huyu bwana aendelee kuishi na mke ambaye tayari ameshaamua kumwacha,” Mzee Tugiramahoro alisema kwa sauti iliyoashiria kuwa alikuwa na hasira.
“Jamani, kutokana na maelezo tuliyoyapata kutoka kwa mkwe wangu yanadhihirisha kabisa huyu bwana ni muongo, sioni kwa nini tusiamue tu,” Mama Bigirimana alijaribu kushauri.
“Tunaamuaje katika mazingira ya aina hii, kumlazimisha mtu aishi na mtu aliyemchoka ni hatari sana, ni bora tukubaliane na uamuzi wake hata kama hatuupendi ili asije akamuua bure!” Mzee Tugiramahoro alisisitiza huku akionekana wazi kutotaka suluhu.
“Kwa maana hiyo, tusichukue hatua yoyote eti kwa sababu tutaonekana tumemlazimisha! Kwani tulichoitiwa hapa na mkwe wangu ni nini kama si kutafuta suluhu?” Mama Bigirimana alihoji huku naye akianza kukosa uvumilivu.
“Ndiyo maana nataka huyo aliyetuita hapa aitwe ili tutakapoamua tuwe tumepata nafasi ya kuwasikia wote wawili na wao tuwape nafasi, ili tukiamua basi tuamue mbele yao wote wawili,” Mzee Tugiramahoro alisisitiza.
Watu wote wakaonekana kuafikiana na maneno yale bila kipingamizi, kisha macho yote yakamtazama Ibrahim kwa makini huku kikizuka kitambo kingine cha ukimya mzito.
Ibrahim alionekana kugwaya sana, akawatazama wale wazee huku akitamani kulia. Aliinuka na kwenda kuanguka miguuni kwa Mama Bigirimana na Mama Ninziza Bernice, akaishika miguu yao huku akitokwa machozi.
“Mama zangu, naomba mnisamehe. Nimewakosea sana wazazi wangu, na siyo nyinyi tu, nimemkosea pia Pamela mke wangu, watoto wangu na nimeikosea nafsi yangu vile vile…” Ibrahim alisema kwa huzuni.
“Nenda kamuombe msamaha mkeo kwanza, kisha mje wote hapa tuyazungumze,” Mama Bigirimana alisema huku akimkazia macho Ibrahim.
Ibrahim alinyanyua uso wake kumtazama mama yake kwa huzuni, kisha akasimama akiwa mnyonge mno na kuondoka kutoka eneo lile huku akitazamwa na macho ya wale wazee wote kwa makini. Alizipanda ngazi taratibu na kupotelea ghorofani.

ITAENDELEA...
 
HADI LINI! 24

Na Bishop Hiluka


Alifika kwenye mlango wa chumba chake na kusimama, akajifuta machozi na kufungua mlango na kuingia chumbani huku akiufunga mlango nyuma yake, kisha akasimama pale mlangoni akiuegemea ule mlango, akamwangalia Pamela huku akiwa amekunja sura yake na kushusha pumzi.
Pamela alikuwa ameketi kitandani akiwa kajiinamiaakiwa anawaza mbali sana. Alipohisi ujio wa Ibrahim mle ndani aliinua uso wake kumwangalia, macho yake yalikuwa yanadhihirisha chuki aliyokuwa nayo kwa Ibrahim. Alimtazama kwa sekunde chache kisha akageuza shingo yake kuangalia upande mwingine huku akiendelea kuonesha chuki yake kwa mumewe.
“Hivi ni mambo gani haya yasiyoisha?” Ibrahim alimuuliza Pamela huku akimtazama kwa makini. Pamela akamkata jicho Ibrahim bila kusema neno.
“Hata kama ni kudai haki, ni haki ipi inapatikana kwa kumletea nyodo unayetaka akupe hiyo haki?” Ibrahim alisema kwa sauti tulivu lakini kavu.
“Tafadhali naomba uniache. Sitaki kabisa kuendelea kubishana na wewe saa hizi!” Pamela alisema huku donge la hasira likizidi kumkaba kooni.
”Unan'letea jeuri ya kwenu, siyo? Mi naongea na wewe kistaarabu lakini wewe unaleta jeuri! Kwa taarifa yako hata ukinuna mimi ndiye mwanaume humu ndani, wewe utabaki kuwa mwanamke tu wa kulea watoto basi!” Ibrahim alisema huku hasira mpya ikifumuka ndani yake.
Pamela alimtazama Ibrahim kwa makini kuanzia juu na kumshusha hadi chini, akakunja sura yake na kuinuka kisha akaelekea nje kwenye balcony akionekana kutomjali mumewe, kitendo kile kikaonekana kumkera sana Ibrahim.
“Hmm! Najuta sana kukuoa…” Ibrahim alisema kwa huzuni.
“Hata mimi najuta kuolewa na wewe, tena najuta majuto ya Firauni!”
Ibrahim alimtazama Pamela kwa makini kisha akapiga hatua kumfuata kule kwenye balcony na kusimama mbele yake, alimtazama kwa kitambo kirefu na kushusha pumzi ndefu kwa masikitiko.
“Kilichobaki ni kukutwanga talaka tu nikaoe mwanamke wa kwetu Tanzania.”
“Kaoe hata kesho, kwani unadhani nababaika! Ila ujue tu kuwa haki yangu haitapotea na watoto wangu hawawezi kulelewa na mwanamke mwingine kama bado niko hai.”
Ibrahim akaduwaa asijue la kufanya, alimkodolea macho Pamela huku akihisi donge la hasira likianza kumkaba kooni, akaminya midomo yake akionekana kuzuia hasira. Hata hivyo, alionekana kuchanganyikiwa zaidi na kukosa neno la kusema. Akashika kiuno chake kwa mikono yake miwili na kusimama akimtazama Pamela kwa makini.
Mawazo kibao yakaanza kupita kichwani kwake; alijiuliza inamaana Pamela alikuwa amekusudia kweli kuachwa au alikuwa anatingisha kiberiti ili aone kama kimejaa njiti? Na kama ni kweli alikuwa amekusudia kuachwa, ilimaanisha kuwa alikuwa amekwisha pata mwanaume mwingine? Na kama sivyo kulikuwa na nini alichojivunia?
Ibrahim alifikiria sana akakosa majibu, hata hivyo akajipa moyo kuwa hata kama Pamela angeondoka, hakuwa mwanamke peke yake duniani, mbona wapo wengi tu wazuri na wachapakazi, kama Jeanine…
Alipomkumbuka Jeanine akasita sana, ikamjia picha ya fumanizi pale nyumbani kwa Jeanine. Hakuipenda sana ile picha ya kumfumania mwanamke aliyekuwa akimpenda na kumuamini sana akiwa na mwanamume mwingine! Hasira zikamchemka zaidi ndani kwa ndani na hapo akajikuta akisonya kwa hasira.
Pamela aligeuka kumtazama Ibrahim kwa makini akadhani kuwa ni yeye aliyekuwa akimsonya. Ibrahim aligundua akajibaraguza huku akilazimisha tabasamu lililoonekana usoni lakini moyoni akiwa ana roho iliyojaa uchungu. Alionesha wasiwasi mwingi, akamwangalia Pamela kwa makini huku akiendelea kuonesha tabasamu.
Pamela aliketi pale kwenye kiti cha kupumzikia kilichokuwa kwenye balcony huku akimtazama Ibrahim kwa makini, macho yake yalikuwa yanaonesha uchungu. Akatingisha kichwa kwa huzuni.
Ibrahim alimtupia jicho la wizi na kuonekana akijishauri kama aendelee kumsemesha au aondoke zake. Akashusha pumzi na kuuma midomo yake huku akiwaza kidogo, kisha anamsogelea na kupeleka mkono wake wa kulia kwenye uso wa Pamela kwa uangalifu huku akiachia tabasamu, si kwa kulazimisha.
“Usiniguse!” Pamela aliusukuma mkono wa Ibrahim kwa hasira na kumfanya Ibrahim aminye midomo yake huku akimtazama kwa makini, alimtazama kwa kitambo kirefu bila kusema neno. Wakabaki wanaangaliana kama majogoo waliotaka kupigana.
Kisha Ibrahim alikwenda kujiegemeza kwenye ukuta wa ile balcony huku akionekana kufikiria kidogo, kiukweli muda ule alikuwa amechanganyikiwa zaidi na hakujua afanye nini. Alijishika kichwa chake kwa mikono yake miwili na kuinamisha kichwa chini. Pamela akamwangalia kwa makini bila kusema neno.
Baada ya muda wa sekunde kadhaa, Ibrahim alimtazama Pamela, akamsogelea tena na kukaa sakafuni mbele yake huku akiishika miguu ya Pamela na kuanza kutembeza mikono yake kwenye miguu ya Pamela, kuanzia magotini mpaka unyayoni. Pamela hakumzuia bali alibaki kimya akimtazama kwa makini.
“Pamela, naomba unisamehe… ni kweli nilitaka kukuacha lakini nimegundua kuwa wewe ndiye mwanamke wa maisha yangu na chaguo kutoka kwa Mungu… tafadhali usinihini nafasi ya kuwa mimi pekee ninayestahili kuchezea miguu hii,” Ibrahim alimsihi Pamela na kuegemeza kichwa chake juu ya magoti ya Pamela.
Donge la hasira lililizidi kumkaba Pamela kooni, alimwangalia Ibrahim kwa makini huku akiona kama aliyekuwa akimchezea akili yake, machozi yakaanza kumtoka na kumdondokea Ibrahim, ambaye aliinua uso wake kumwangalia Pamela kwa mshangao.
“Usilie, nadhani anayestahili kulia ni mimi, na wala siyo wewe Pamela… kitu gani kinachokuliza?” Ibrahim alimuuliza Pamela huku akimtazama kwa makini.
“Naomba niache tafahdhali… silii kwa sababu nakupenda ila kinachoniliza ni hayo maigizo yako,” Pamela alisema huku akimsukuma kando Ibrahim na kuinuka, akasimama na kujiegemea kwenye ukuta wa balcony, macho yake akayaelekeza kutazama kule chini ya ghorofa huku akionekana kuwaza mbali.
Ibrahim alibaki akiwa amepiga magoti pale pale sakafuni huku akimkodolea macho Pamela huku akionekana kuchanganyikiwa zaidi, alitamani kulia.
“Nimegundua kuwa kumbe muda wote wa ndoa yetu ulikuwa hunipendi, ulikuwa unatafuta sababu ili tugombane uondoke!” Ibrahim alisema kwa huzuni.
Pamela akageuka kumtazama Ibrahim kwa mshangao, alimkazia macho akiwa na maswali mengi kichwani kwake yaliyokosa majibu.
“Imekuwaje huyu mwanaume akabadilisha ghafla msimamo wake wa kutaka kuniacha na kuwa mpole kiasi hiki! Ni nini kimetokea kule sebuleni alikokuwa ameitwa na wazee? Je, amelazimishwa kuja kuniomba radhi au ni kweli amegundua kuwa mimi ndiye mwanamke wa maisha yake kama anavyodai?” Pamela aliwaza na kukosa majibu.
Alimtazama Ibrahim kwa makini huku yale maswali na mengine mengi yakizidi kuzunguka kwenye akili yake na kuonekana kumchanganya zaidi, hata hivyo aliapa kuendelea kukaza kamba ili aone mwisho wa maigizo ya Ibrahim.
“Kama umegundua kuwa nilikuwa sikupendi sijui unasubiri nini sasa, fanya kile ambacho umegundua kuwa nakisubiri kwa hamu,” Pamela alisema huku akimtazama Ibrahim kwa makini.

ITAENDELEA...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom