Bishop Hiluka
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 7,148
- 14,716
Na Bishop Hiluka
Yalikuwa yamemfika kooni baada ya kuitafuta haki yake kila mahali na kushindikana, akafikia uamuzi wa kuwaita wazazi wa pande zote mbili ili aweke wazi kuhusu msimamo wake juu ya ndoa yake. Kama noma na iwe noma lakini asingeweza kuendelea kuvumilia, avumilie hadi lini? ...
JUMAMOSI, saa kumi na mbili na nusu jioni, kwa saa za Burundi, sauti tamu ya muziki laini wa kubembeleza ilikuwa inasikika kutoka katika spika zilizokuwa kwenye kona za ukumbi mkubwa wa kisasa wa burudani, ndani ya Hotel Club du Lac Tanganyika.
Club du Lac Tanganyika ilikuwa hoteli yenye hadhi kubwa iliyokuwa imejengwa kwenye mandhari ya kuvutia ya ufukwe wa Ziwa Tanganyika jijini Bujumbura, Burundi. Ilikuwa hoteli ya kisasa kabisa iliyokuwa imezungukwa na mazingira yenye utulivu mkubwa ufukweni mwa ziwa, ikiwa kando ya barabara ya Chausse d'Uvira iliyokuwa inaelekea katika mji mdogo wa Uvira.
Ikiwa imezungukwa na uzio madhubuti ulioifanya kuwa mahali patulivu zaidi na penye usalama wa uhakika, ilikuwa sehemu tulivu zaidi ya kwenda kujirusha kwa watu wenye ukwasi, ikiwa umbali wa kilomita tatu tu kutoka katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Bujumbura.
Pia ilikuwa sehemu muhimu sana kwa burudani na wageni wengi kutoka nje walipenda kwenda sehemu ile, hasa mwisho wa wiki, kutokana na kuwa na kumbi mbili za kisasa. Ukumbi mmoja ulitumika kwa ajili ya mikutano, ukiwa na sifa zote, na wenye viyoyozi na umeme wa uhakika saa 24, jambo linaloufanya kuvutia wageni mbalimbali. Ukumbi mwingine ulitumika zaidi kwa ajili ya burudani na matukio.
Ukumbi wa burudani ulikuwa na kila aina ya starehe, ukiwa na madirisha makubwa ya vioo yaliyofunikwa na mapazia safi marefu, na ulikuwa na kila kionjo cha daraja la kimataifa. Ndani ya ukumbi ule kulikuwa na wahudumu wazuri wa kike, warembo kwelikweli, waliokuwa wakihudumia wateja wachache waliokuwemo ukumbini muda huo wakiwa wameketi kwenye meza nzuri za mbao ya mti wa mninga na viti vifupi vyenye foronya laini.
Muda ule wa saa kumi na mbili na nusu za jioni idadi kubwa ya wateja waliokuwemo ndani ya ukumbi ule walikuwa raia wa kigeni, hasa kutoka katika nchi za Ufaransa na Marekani. Upande wa kulia wa ukumbi ule kulikuwa na mlango na dirisha dogo la jikoni, na humo ndani kulionekana wapishi waliokuwa katika mavazi yao ya kazi, wakiandaa chakula.
Katika ukumbi ule, mmoja wa wateja Waafrika walioonekana aliitwa Ibrahim Bigirimana, alikuwa mwanamume wa Kitanzania aliyekuwa na asili ya kutoka mkoa wa Kigoma, mkoa ambao uko pembezoni mwa nchi ya Tanzania katika mpaka wa Tanzania na Burundi.
Ibrahim Bigirimana alikuwa ameketi peke yake kwenye meza moja akionekana kuzama katika fikra fulani huku akiwa na shauku kubwa ya kusubiri kitu fulani muhimu sana, ambacho, ni yeye tu kati ya watu wote waliokuwemo mle ukumbini ndiye aliyekuwa akikijua.
Ibrahim alishusha pumzi za ndani kwa ndani na kutupa macho yake kuangalia nje kupitia ukuta msafi wa kioo cha dirisha, mkono wake mmoja alikuwa ameshika bilauri ndefu iliyokuwa na mvinyo mwekundu wa Kifaransa aina ya Navette de Marseille, na mkono wake wa kushoto alikuwa kauegemeza juu ya kiti alichokalia. Ibrahim akainua bilauri ya mvinyo na kupiga funda taratibu huku akionekana kuwaza mbali sana.
Alikuwa mwanamume mrefu na maji ya kunde, akiwa na sura bashasha ya kitoto iliyokuwa na muonekano uliomfanya mtu yeyote aliyemuona adhani kuwa hangeweza kuzidi miaka therathini, ingawa alishapita miaka hiyo. Akiwa na umri wa miaka arobaini na mbili, kimuonekano, Ibrahim alikuwa na umbo kakamavu la kimichezo lililofanana na maumbo ya wachezaji wa ligi ya mpira wa kikapu wa nchini Marekani.
Alikuwa mcheshi sana na mtu wa kupenda kujichanganya na watu wengine bila kujali kipato, alikuwa muongeaji mkubwa mwenye kuzimudu vyema lugha za Kiswahili, Kiingereza, Kifaransa na hata Kirundi, lugha iliyokuwa ikizungumzwa zaidi na wenyeji wa nchi ile ya Burundi, jambo ambalo liliwafanya watu wengi kudhani kuwa labda alikuwa Mrundi mwenzao, hasa kwa kuwa hata jina lake la mwisho la ‘Bigirimana’ ni jina lililokuwa linatumiwa na Warundi.
Ibrahim alikuwa Muha kutoka mkoani Kigoma, kabila lililokuwa na utamaduni ulioshabihiana kwa kiasi kikubwa sana na ule utamaduni wa Warundi. Ibrahim alikuwa ameishi jijini Bujumbura kwa takriban miaka kumi sasa. Na alikuwa akifanya kazi kama Meneja Mkuu wa CRDB Bank Burundi, benki iliyokuwa na makao yake katika barabara ya Chaussée du Prince Louis Rwagasore, ploti namba 490/A, jijini Bujumbura.
Kwa nafasi hiyo, Ibrahim alikuwa mtu mwenye mafanikio mema, ingawa alikuwa na kasoro moja iliyoonekana wazi, hakuwa na wala hakupenda kuwa na kitambi. Wengi walidhani labda Ibrahim alikuwa amebebwa hadi kufikia nafasi ile, lakaini ukweli hakufikia nafasi ya ile ya umeneja mkuu wa benki hiyo kwa bahati au kama wasemavyo Waswahili ‘zali la mentali’, bali alikuwa nazo sifa zinazostahili ikiwemo elimu ya juu na uzoefu wa kazi.
Kabla hajakuwa Meneja Mkuu wa CRDB Bank Burundi, ibrahimu alikuwa amefanya kazi kama Manager Corporate Banking na baadaye akawa Senior Relationship Manager Corporate Banking katika Benki ya Biashara ya Burundi (Commercial Bank of Burundi) iliyokuwa na makao yake katika makutano ya barabara za Avenue des USA na Chaussée P.L. Rwagasore, ikiwa mkabala na jengo la CRDB Bank Burundi, jijini Bujumbura.
Ibrahim alikuwa msomi wa Shahada ya Umahili ya Business Administration aliyoipata kutoka Chuo Kikuu cha Oxford, Uingereza, ambacho kilikuwa chuo kikongwe zaidi katika ulimwengu wa nchi zinazozungumza lugha ya Kiingereza, na Shahada ya Kwanza ya Banking and Financial Services aliyohitimu kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Tanzania.
Baada ya kumaliza chuo kikuu na kabla hajaenda kufanya kazi nchini Burundi, Ibrahim alikuwa amefanya kazi kaatika Benki Kuu ya Tanzania kwa miaka miwili kisha akaacha na kwenda kuishi jijini Bujumbura ambako aliajiriwa katika benki ya biashara ya Burundi. Hii ilitokana na yeye kuamua kumfuata mke wake aliyekuwa amerudishwa nchini Burundi baada ya kukumbwa na matatizo ya uraia alipokuwa akiishi nchini Tanzania.
Alipofika Burudni na kuajiriwa Commercial Bank of Burundi Ibrahim alifanya kazi kwa miaka kadhaa, na kutokana na uwezo wake na ufanisi kazini alichukuliwa na CRDB Bank Burundi, kama mwanzilishi na Meneja Mkuu wa benki hiyo jijini humo, nafasi ambayo aliweza kudumu nayo hadi wakati huo.
Huyo ndiyo Ibrahim Bigirimana, ambaye Jumamosi hiyo alikuwa katika ukumbi wa maraha wa Hotel Club Du Lac Tanganyika akiwa mwenye shauku kubwa. Alinyanyua bilauri yake na kunywa funda dogo la mvinyo kisha akaitazama saa yake ya mkononi kwa mara nyingine tena kisha akaonekana kutikisa kichwa chake.
Alishusha pumzi za ndani kwa ndani huku akisonya kwa huzuni, ni wazi alikuwa hapo akisubiria kitu muhimu sana lakini hadi muda ule alionekana kuanza kuishiwa na uvumilivu. Aliitazama tena saa yake na kuminya midomo yake akionekana kuwaza mbali, akabaki akiikodolea macho ile saa kana kwamba ilikuwa mbovu.
Laiti kama ingelikuwa saa ya kawaida labda angeweza kusema kuwa ilikuwa na kasoro, lakini hiyo saa kama ilivyo kwa vitu vyake vingi, haikuwa ya kawaida kabisa!
ITAENDELEA...
Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY
Yalikuwa yamemfika kooni baada ya kuitafuta haki yake kila mahali na kushindikana, akafikia uamuzi wa kuwaita wazazi wa pande zote mbili ili aweke wazi kuhusu msimamo wake juu ya ndoa yake. Kama noma na iwe noma lakini asingeweza kuendelea kuvumilia, avumilie hadi lini? ...
JUMAMOSI, saa kumi na mbili na nusu jioni, kwa saa za Burundi, sauti tamu ya muziki laini wa kubembeleza ilikuwa inasikika kutoka katika spika zilizokuwa kwenye kona za ukumbi mkubwa wa kisasa wa burudani, ndani ya Hotel Club du Lac Tanganyika.
Club du Lac Tanganyika ilikuwa hoteli yenye hadhi kubwa iliyokuwa imejengwa kwenye mandhari ya kuvutia ya ufukwe wa Ziwa Tanganyika jijini Bujumbura, Burundi. Ilikuwa hoteli ya kisasa kabisa iliyokuwa imezungukwa na mazingira yenye utulivu mkubwa ufukweni mwa ziwa, ikiwa kando ya barabara ya Chausse d'Uvira iliyokuwa inaelekea katika mji mdogo wa Uvira.
Ikiwa imezungukwa na uzio madhubuti ulioifanya kuwa mahali patulivu zaidi na penye usalama wa uhakika, ilikuwa sehemu tulivu zaidi ya kwenda kujirusha kwa watu wenye ukwasi, ikiwa umbali wa kilomita tatu tu kutoka katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Bujumbura.
Pia ilikuwa sehemu muhimu sana kwa burudani na wageni wengi kutoka nje walipenda kwenda sehemu ile, hasa mwisho wa wiki, kutokana na kuwa na kumbi mbili za kisasa. Ukumbi mmoja ulitumika kwa ajili ya mikutano, ukiwa na sifa zote, na wenye viyoyozi na umeme wa uhakika saa 24, jambo linaloufanya kuvutia wageni mbalimbali. Ukumbi mwingine ulitumika zaidi kwa ajili ya burudani na matukio.
Ukumbi wa burudani ulikuwa na kila aina ya starehe, ukiwa na madirisha makubwa ya vioo yaliyofunikwa na mapazia safi marefu, na ulikuwa na kila kionjo cha daraja la kimataifa. Ndani ya ukumbi ule kulikuwa na wahudumu wazuri wa kike, warembo kwelikweli, waliokuwa wakihudumia wateja wachache waliokuwemo ukumbini muda huo wakiwa wameketi kwenye meza nzuri za mbao ya mti wa mninga na viti vifupi vyenye foronya laini.
Muda ule wa saa kumi na mbili na nusu za jioni idadi kubwa ya wateja waliokuwemo ndani ya ukumbi ule walikuwa raia wa kigeni, hasa kutoka katika nchi za Ufaransa na Marekani. Upande wa kulia wa ukumbi ule kulikuwa na mlango na dirisha dogo la jikoni, na humo ndani kulionekana wapishi waliokuwa katika mavazi yao ya kazi, wakiandaa chakula.
Katika ukumbi ule, mmoja wa wateja Waafrika walioonekana aliitwa Ibrahim Bigirimana, alikuwa mwanamume wa Kitanzania aliyekuwa na asili ya kutoka mkoa wa Kigoma, mkoa ambao uko pembezoni mwa nchi ya Tanzania katika mpaka wa Tanzania na Burundi.
Ibrahim Bigirimana alikuwa ameketi peke yake kwenye meza moja akionekana kuzama katika fikra fulani huku akiwa na shauku kubwa ya kusubiri kitu fulani muhimu sana, ambacho, ni yeye tu kati ya watu wote waliokuwemo mle ukumbini ndiye aliyekuwa akikijua.
Ibrahim alishusha pumzi za ndani kwa ndani na kutupa macho yake kuangalia nje kupitia ukuta msafi wa kioo cha dirisha, mkono wake mmoja alikuwa ameshika bilauri ndefu iliyokuwa na mvinyo mwekundu wa Kifaransa aina ya Navette de Marseille, na mkono wake wa kushoto alikuwa kauegemeza juu ya kiti alichokalia. Ibrahim akainua bilauri ya mvinyo na kupiga funda taratibu huku akionekana kuwaza mbali sana.
Alikuwa mwanamume mrefu na maji ya kunde, akiwa na sura bashasha ya kitoto iliyokuwa na muonekano uliomfanya mtu yeyote aliyemuona adhani kuwa hangeweza kuzidi miaka therathini, ingawa alishapita miaka hiyo. Akiwa na umri wa miaka arobaini na mbili, kimuonekano, Ibrahim alikuwa na umbo kakamavu la kimichezo lililofanana na maumbo ya wachezaji wa ligi ya mpira wa kikapu wa nchini Marekani.
Alikuwa mcheshi sana na mtu wa kupenda kujichanganya na watu wengine bila kujali kipato, alikuwa muongeaji mkubwa mwenye kuzimudu vyema lugha za Kiswahili, Kiingereza, Kifaransa na hata Kirundi, lugha iliyokuwa ikizungumzwa zaidi na wenyeji wa nchi ile ya Burundi, jambo ambalo liliwafanya watu wengi kudhani kuwa labda alikuwa Mrundi mwenzao, hasa kwa kuwa hata jina lake la mwisho la ‘Bigirimana’ ni jina lililokuwa linatumiwa na Warundi.
Ibrahim alikuwa Muha kutoka mkoani Kigoma, kabila lililokuwa na utamaduni ulioshabihiana kwa kiasi kikubwa sana na ule utamaduni wa Warundi. Ibrahim alikuwa ameishi jijini Bujumbura kwa takriban miaka kumi sasa. Na alikuwa akifanya kazi kama Meneja Mkuu wa CRDB Bank Burundi, benki iliyokuwa na makao yake katika barabara ya Chaussée du Prince Louis Rwagasore, ploti namba 490/A, jijini Bujumbura.
Kwa nafasi hiyo, Ibrahim alikuwa mtu mwenye mafanikio mema, ingawa alikuwa na kasoro moja iliyoonekana wazi, hakuwa na wala hakupenda kuwa na kitambi. Wengi walidhani labda Ibrahim alikuwa amebebwa hadi kufikia nafasi ile, lakaini ukweli hakufikia nafasi ya ile ya umeneja mkuu wa benki hiyo kwa bahati au kama wasemavyo Waswahili ‘zali la mentali’, bali alikuwa nazo sifa zinazostahili ikiwemo elimu ya juu na uzoefu wa kazi.
Kabla hajakuwa Meneja Mkuu wa CRDB Bank Burundi, ibrahimu alikuwa amefanya kazi kama Manager Corporate Banking na baadaye akawa Senior Relationship Manager Corporate Banking katika Benki ya Biashara ya Burundi (Commercial Bank of Burundi) iliyokuwa na makao yake katika makutano ya barabara za Avenue des USA na Chaussée P.L. Rwagasore, ikiwa mkabala na jengo la CRDB Bank Burundi, jijini Bujumbura.
Ibrahim alikuwa msomi wa Shahada ya Umahili ya Business Administration aliyoipata kutoka Chuo Kikuu cha Oxford, Uingereza, ambacho kilikuwa chuo kikongwe zaidi katika ulimwengu wa nchi zinazozungumza lugha ya Kiingereza, na Shahada ya Kwanza ya Banking and Financial Services aliyohitimu kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Tanzania.
Baada ya kumaliza chuo kikuu na kabla hajaenda kufanya kazi nchini Burundi, Ibrahim alikuwa amefanya kazi kaatika Benki Kuu ya Tanzania kwa miaka miwili kisha akaacha na kwenda kuishi jijini Bujumbura ambako aliajiriwa katika benki ya biashara ya Burundi. Hii ilitokana na yeye kuamua kumfuata mke wake aliyekuwa amerudishwa nchini Burundi baada ya kukumbwa na matatizo ya uraia alipokuwa akiishi nchini Tanzania.
Alipofika Burudni na kuajiriwa Commercial Bank of Burundi Ibrahim alifanya kazi kwa miaka kadhaa, na kutokana na uwezo wake na ufanisi kazini alichukuliwa na CRDB Bank Burundi, kama mwanzilishi na Meneja Mkuu wa benki hiyo jijini humo, nafasi ambayo aliweza kudumu nayo hadi wakati huo.
Huyo ndiyo Ibrahim Bigirimana, ambaye Jumamosi hiyo alikuwa katika ukumbi wa maraha wa Hotel Club Du Lac Tanganyika akiwa mwenye shauku kubwa. Alinyanyua bilauri yake na kunywa funda dogo la mvinyo kisha akaitazama saa yake ya mkononi kwa mara nyingine tena kisha akaonekana kutikisa kichwa chake.
Alishusha pumzi za ndani kwa ndani huku akisonya kwa huzuni, ni wazi alikuwa hapo akisubiria kitu muhimu sana lakini hadi muda ule alionekana kuanza kuishiwa na uvumilivu. Aliitazama tena saa yake na kuminya midomo yake akionekana kuwaza mbali, akabaki akiikodolea macho ile saa kana kwamba ilikuwa mbovu.
Laiti kama ingelikuwa saa ya kawaida labda angeweza kusema kuwa ilikuwa na kasoro, lakini hiyo saa kama ilivyo kwa vitu vyake vingi, haikuwa ya kawaida kabisa!
ITAENDELEA...
Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY
