Leo naomba tuambiane visa mbalimbali ambazo tumekutana nayo kwenye nyumba za kulala wageni (guest houses) ambazo kimsingi umeshindwa kuelewa kilichotokea kwa macho ya kawaida.
Binafsi nitaelezea visa viwili ambavyo sijawahi kuelewa kilichonitokea.
Kisa cha kwanza kilinikuta Jijini Arusha mwaka 2014. Baada ya kupatiwa chumba na kuanza kulala ghafla nikahisi kama watu wako chumbani kwangu wanatembea na wamefungua mpaka mlango wa choo.
Nilikuwa sijalala usingizi ikabidi niwashe taa ila sikuona kitu. Hilo jambo likajirudia kama mara tatu kila nikizima taa. Nikaamua kusali kwa imani yangu ndipo nilipopata usingizi na sikusikia kitu tena.
Kisa cha pili kilinikuta Dodoma mwaka 2018. Siku hiyo niliamua kuchukua kipoozeo nikapita nako lakini nikakiondoa room maana kulala na vipozeo unaweza jikuta huna hata bukta ikawa noma asubuhi.
Baada ya kumwondoa bi mdada nikaanza kulala. Majira ya saa 8 hivi nikashtuka damu zinanitoka puani hatari mpaka shuka limeanza kuloa damu. Ikabidi nikurupuke kwenda kunawa huku nikizuia damu kwa kitambaa. Jambo hilo lilidumu kwa takriban dakika 3 damu ikakata.
Wewe umwahi kukutana na kisa gani huko gesti house ukabaki unajiuliza, heee nini hii?
Binafsi nitaelezea visa viwili ambavyo sijawahi kuelewa kilichonitokea.
Kisa cha kwanza kilinikuta Jijini Arusha mwaka 2014. Baada ya kupatiwa chumba na kuanza kulala ghafla nikahisi kama watu wako chumbani kwangu wanatembea na wamefungua mpaka mlango wa choo.
Nilikuwa sijalala usingizi ikabidi niwashe taa ila sikuona kitu. Hilo jambo likajirudia kama mara tatu kila nikizima taa. Nikaamua kusali kwa imani yangu ndipo nilipopata usingizi na sikusikia kitu tena.
Kisa cha pili kilinikuta Dodoma mwaka 2018. Siku hiyo niliamua kuchukua kipoozeo nikapita nako lakini nikakiondoa room maana kulala na vipozeo unaweza jikuta huna hata bukta ikawa noma asubuhi.
Baada ya kumwondoa bi mdada nikaanza kulala. Majira ya saa 8 hivi nikashtuka damu zinanitoka puani hatari mpaka shuka limeanza kuloa damu. Ikabidi nikurupuke kwenda kunawa huku nikizuia damu kwa kitambaa. Jambo hilo lilidumu kwa takriban dakika 3 damu ikakata.
Wewe umwahi kukutana na kisa gani huko gesti house ukabaki unajiuliza, heee nini hii?