Mkapa, Vincent na Madaraka: What Else?

Mh! Hapa umetuingiza chaka, hili tukio halijapata kutokea katika historia ya Mwalimu. Kansa yake iligunduliwa 1998, mwaka mmoja baada ya ile birthday yake maarufu ya 75 (mwaka 1997) ambako katika hotuba alikuwa amesema "....nitapiga makumi mawili manne, NINA HAKIKA! Nitamwona rais wetu wa nne, NINA HAKIKA" akimaanisha alikuwa na uhakika wa kuishi miaka zaidi ya themanini na kuchagua hadi rais wetu wa nne.

Na hiyo kansa alidumu nayo mwaka mmoja tu na kufariki akiwa na miaka 77, maskini hakuifikia ile 80 aliyokuwa amesema ana uhakika "angepiga"! Na wala hakuwahi kufanyiwa operesheni, haiko kwenye rekodi za maisha yake. Kama unazungumzia bone marrow biopsy hiyo ni diagnostic procedure, na wala siyo huo mwaka wa 1989, ni 1998 alipogunduliwa na Chronic Lymphocytic Leukemia.

Hakuna taarifa kuwa Mwalimu aliwahi kufanyiwa bone marrow transplant ambayo ni mojawapo ya tiba za uhakika za CLL, na hii ingefanana na operation, na ingemwezesha kuishi miaka isiyopungua 10 bila leukemia. Lingine ni kuwa prognosis ya CLL siyo mbaya kama ilivyotokea kwa Mwalimu Nyerere ambaye alidumu nayo kwa mwaka mmoja tu.
 
Duh mkuu wangu umerukia treni kwa mbele...Haya cheza James Bond chini kwa chini urudi nyuma utalipata jibu..

mkuu wengine wavivu kusoma mwanzo na kufuatilia page zote !
 
Mkuu Mzee Mwanakijiji naiamini sana Hard Disk yako huwa inatupatia vitu adim sana hapa jukwaani. Nadhani ukiiscan inaweza kutupa japo fununu kuhusu kuhusika kwa Mkapa kwenye kifo cha mwalimu.
hebu tusaidie kutegua kitendawili hiki
 
CCM waliamini Mkapa atakua silaha kubwa ya maangamizi dhidi ya CDM ila Jinamizi la Mwalimu Nyerere limemvaa Mkapa na kugeuza kibao ambapo matokeo yake Mkapa kageuka kuwa silaha ya maangamizi dhidi ya chama chake CCM.
Damu ya Mwalimu iwaangamize wote walioshiriki kumzimisha mzee huyu.
 

kwa watu wote wa cccm waliobaki hakuna msafi-
eti kwao 'mkapa anaonekana msafi"-ndo maana wanampeleka yeye-maana hao wengine waliobaki wana madudu sana kiasi kwamba watachafua hali ya hewa kwenye kampeni kama hizi
 
kweli kumbe viongozi wetu wengi i.e. mkapa, ni mcharuko, lol.
 

Mkandara,

..nakubaliana na wewe 100% kwamba Mkapa alikuwa na lake jambo.

..Mkapa alilenga kumdhalilisha Vicent Nyerere. tatizo ni kwamba hawa ndugu zetu wa kutoka Mara dharau ni kitu ambacho hawa-entertain hata siku moja.

..nikupe kisa kimoja kilichonitokea mimi binafsi.

..yupo rafiki yangu mmoja tumeshibana sana toka shuleni. huyu bwana alihudhuria mkutano mmoja wa hadhara wilayani kwetu akakumbana na mtu ana jina kama langu. Yaani jina la kwanza na la ukoo!!!

..alichofanya huyu rafiki yangu ni kumtafuta yule jamaa mwenye jina kamili kama langu na kumdadisi kidogo undani wake. matokeo yake alikuja kufahamu kwamba yule alikuwa mtoto wa baba yangu mdogo!!!

..baadaye huyu jamaa yangu akanipigia simu na kunieleza kisa chote, na jinsi alivyopata mshituko kusikia mtu anajitambulisha kwa majina yangu. na mimi nikamhakikishia kwamba huyo aliyekutana naye ni ndugu yangu.

..alichotakiwa kufanya Mkapa ni kumdadisi Vicent Nyerere directly, kwa uungwana, au kuwatafuta kina Makongoro,Madaraka,Magige, na kuwauliza habari za Vicent.

NB:

..haiyumkiniki Mkapa akawa hamfahamu Josephat Kiboko Nyerere, baba mzazi wa Vicent Nyerere.
 
.... pamoja na yote yanayojulikana leo hii kuhusu UFISADI wa kutisha ambao umefanyika baada ya tukio la October 14, 1999 HAIPANDI akilini kwamba UFISADI HUO hauonewi aibu na wahusika. They remain as cocky albeit shameless as statesmen. Very strange!
 

Mkuu JokaKuu,

Kuna mwana familia mmoja wa Nyerere amesema kwamba, Marehemu Mzee Josephat Kiboko Nyerere (RIP) alipofariki, Mkapa alienda kuhudhuria mazishi. Kwa hiyo hisia kwamba Mkapa alikuwa hamfahamu Mzee Josephat Kiboko Nyerere haiko sahihi.

Bottom line ni kwamba Mkapa hakuwa na hoja/sera za kuwapa wana Arumeru Mashariki na ndipo alipoingiza sera mufilisi za madharau na kejeri akijua kwamba labda Vincent Nyerere angekaa kimya kwa kumheshimu.
 

FMES,
Wewe ukienda safari Uingereza, ukapewa honorary citizenship haina maana kwamba wewe sasa ni raia wa Uingereza.
Kama Mkapa angekuwa real member wa family ya Nyerere angejua Vincent ni nani. Full stop.
 
Ufamilia wa Mkapa ni wa kutunukiwa tu, kama ilivyo kwa udokta wa kutunukiwa nk.

Dokta wa ukweli ni tofauti na dokta wa kutunukiwa, vivyo hivyo kwa ndugu, yani ndugu wa ukweli ni tofauti na yule wa kutunukiwa regardless of the customs.

Status ya undugu itakuwa enforced kutokana na customs za kabila husika, lakini kiukweli there is lots of differences btn the two.
 
asanteni chadema kwakumchagua vincent nyerere kuwa meneja kampeni mana angekuwa muheshimiwa mwingine haya yote tusingeyajua..
 
Siku ya nyani kuuawa miti yote huteleza..
bado, tutafahamu maovu mengi ya hawa m.a.f.i.a wa kibongo
 
Wasiwasi wa Mkapa ni Kwamba now hana Uhakika Familia ya Nyerere inasemaje juu ya Kifo Cha Mwalimu. Yawezekana kabisa Kilichosemwa na Vicent ni Manung'uniko katika Familia ya Mwalimu ya Kifo cha Mwalimu. Kwamba Vicent amezungumza Hadharani kile kinachozungumzwa kwa Kificho huko Butiama.

Kwa Kifupi Mkapa Atakuwa amegundua kwamba HAAMINI ndani ya Familia ya Nyerere
 
Ahaaaa kumbee
Ndo maana ufisadi wote uliofanyika kipindi cha Mkapa ni baada ya kumuua Nyerere

ANNBEN kuanziswa ikulu, kuuza dhahabu yetu bure kwa manufaa binafsi, kuuza mashirika ya umma , kujikwapulia majengo na viwanja vya TTCL kupitia mwanae aliyekuwa MD SIMUE2000 waliopewa dhamana ya real estate za TTCL

Na ushenzi mwingine wa mkapa ni baada ya kummaliza aliyekuwa kikwazo , JKN
 

kwa hiyo wameamua kuweka siri za mwanafamilia hadharani sio? wanamkumbatia mwanafamilia muuaji sio?
 
wanajf,hakuna jipya wanarudia rudia tu,mod maliza mjadala kama ile ya ubadhilifu ya cdm,mod be fair
 
wanajf,hakuna jipya wanarudia rudia tu,mod maliza mjadala kama ile ya ubadhilifu ya cdm,mod be fair
Lakini mkuu wangu sii aliyefungua mjadala ni Mkapa mwenyewe..sasa tatizo liko wapi kumjadili mwanafamilia ambaye sisi hatukujua?..
 
Duh yaani leo narushiwa virus kwenye Pc hadi mwenyewe nashika adabu...Jamani nazungumza kipi hadi mnaniwekea cookie ya ku trace na worms na kadhalika..tujadili tu wakubwa hakuna sababu ya kuharibiana Pc..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…