Tarehe 26 Desemba Mkapa alikuwa Karagwe na alisali kanisa la St George mjini Kayanga. Alhamisi kuu hii amesali kanisa hilo hilo. Na mwezi wa saba mwaka jana alikuwa Karagwe ikiaminika kwamba alikwenda kwenye msiba wa rafiki yake Balozi Ruhinda. Kwa ujmla tangu aondoke madarakani ameenda Karagwe mara nyingi sana.
Kuna uvumi ambao haujawahi kukanushwa kwamba wakati wa utawala wake alijibinafisisha kiwanda cha Kagera Sugar na kwamba anamiliki zaidi ya hekta elfu 40 za mashamba ya miwa. Na kwamba alipokuwa rais aliwahi kuchelewa kuhutubia mkutano wa hadhara Karagwe kwamba alikuwa na kikao cha kamati ya ulinzi na usalama kilichofanyika Kagera Sugar, kumbe alikuwa anakagua mashamba yake.
Hivi tunavyoongea yupo Karagwe amelala KDRDP anapopendelea kulala. Hutoka pale kusalimia kwa Balozi Ruhinda na marehemu Balozi Tibandebage. Maswali ni mengi kuliko majibu, Mkapa huwa anatafuta nini Karagwe?
Kuna uvumi ambao haujawahi kukanushwa kwamba wakati wa utawala wake alijibinafisisha kiwanda cha Kagera Sugar na kwamba anamiliki zaidi ya hekta elfu 40 za mashamba ya miwa. Na kwamba alipokuwa rais aliwahi kuchelewa kuhutubia mkutano wa hadhara Karagwe kwamba alikuwa na kikao cha kamati ya ulinzi na usalama kilichofanyika Kagera Sugar, kumbe alikuwa anakagua mashamba yake.
Hivi tunavyoongea yupo Karagwe amelala KDRDP anapopendelea kulala. Hutoka pale kusalimia kwa Balozi Ruhinda na marehemu Balozi Tibandebage. Maswali ni mengi kuliko majibu, Mkapa huwa anatafuta nini Karagwe?