Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,703
- 218,248
Taarifa ikufikie popote ulipo kwamba Mwenyekiti wa Chadema , ambaye pia ni mwamba wa siasa za Tanzania , na muasisi wa siasa za kisasa kwenye ukanda wa Maziwa Makuu , Freeman Mbowe leo 30//7/2023 ameshiriki katika kumtukuza Mungu kwenye ibada ya Jumapili iliyofanyika kanisa la KKKT , Usharika wa Kayanga , Karagwe , Mkoani Kagera , ambako alipewa nafasi ya kusalimia waumini wenzake .
Pamoja na salamu kwa waumini wenzake , Lakini Mbowe hakuwaacha mikono mitupu waumini hao , ameahidi kununua sare kwa ajili ya kwaya za kanisa hilo (Zipo kwaya 4) kwa gharama ya tsh mil 2.8 na ameahidi kuchangia tsh 10mil kwa ajili ya Ujenzi wa Kanisa hilo , Binafsi namshukuru Mbowe kwa moyo wake wa kumtolea Mungu , na kwa kweli namuomba Mungu amzidishie , Amina .
Ikumbukwe kwamba Mbowe na viongozi wenzake wa Chadema wako Mkoani Kagera kwenye Oparesheni kabambe ya 255 KATIBA MPYA , OKOA BANDARI ZETU , ambayo leo inatimua vumbi Karagwe .
Pamoja na salamu kwa waumini wenzake , Lakini Mbowe hakuwaacha mikono mitupu waumini hao , ameahidi kununua sare kwa ajili ya kwaya za kanisa hilo (Zipo kwaya 4) kwa gharama ya tsh mil 2.8 na ameahidi kuchangia tsh 10mil kwa ajili ya Ujenzi wa Kanisa hilo , Binafsi namshukuru Mbowe kwa moyo wake wa kumtolea Mungu , na kwa kweli namuomba Mungu amzidishie , Amina .
Ikumbukwe kwamba Mbowe na viongozi wenzake wa Chadema wako Mkoani Kagera kwenye Oparesheni kabambe ya 255 KATIBA MPYA , OKOA BANDARI ZETU , ambayo leo inatimua vumbi Karagwe .