Mkapa aipa kolabo Wizara ya Magufuli

Mkapa aipa kolabo Wizara ya Magufuli

Hamna road geometry manual wala upuuzi wowote utakayonishawishi barabara hizi ni salama.

Nimefanya kazi na kusafiri nchi nyingi sana duniani, sijakurupuka.

Najua naongelea nini, ila una haki ya kuamini upendavyo.
Kama hii barabara kwako ni nzuri na ya usalama, hongera sana wasomi wetu.


View attachment 251802

View attachment 251803

watu wanaendesha magari kasi ndo maana wanatumbukia kwenye mitaro.
 
Mkuu,

Hapa tupo kujifunza na kuelimishana.

Kuna wachangiaji wengine hawajafundishwa "debate etiquette" mashuleni.

Wanakurupuka na kutumia lugha ya dharau / kejeli kwa mchangiaji badala ya kujenga hoja za kunipinga.

Ninakusoma na ninajielimisha.

Sure mm binafsi nakereka sana wanaharibu sifa ya jf kabisa haikuwa hivi
 
Kiongozi ajari ni ajri tu hata mwezi juzi waziri mmoja Afrika ya Kusini alifariki kwa ajari, je ni miundombinu ilisababisha? swala la ajari ni la mtambuka, kila mtu anatakiwa kushiriki kudhibiti ajali.

Na amimi kwamba kila ajali inapo tokea, lazima kuna sababu ilio pelekea kutokea kwa ajali hiyo.
Na uchunguzi wa ajali ukifanywa ipaswavyo, lazima utakuta kuna uzembe ulio fanyika sehem hadi kupeekea kutokea kwa ajali
 
Mkuu, Huwezi kuthibiti ajali unapotengeneza barabara zenye mashimo ya mifereji katikati au pembeni mwa barabara bila kuacha nafasi kubwa. Hapo hapo hamna taa za kusaidia kuziepuka usiku.

Huu ndiyo uhandisi uliotumia "safety factors"?

Nina uhakika kuwa ramani za hizi barabara haziwezi kupitishwa katika nchi zinazojali usalama wa wananchi barabarani.

Nina uhakika pia, kama Polisi wa barabarani wanaweka rekodi, utakuta magari mengi yanatumbukia katika mashimo kuliko katika barabara zilizojengwa bila ya hayo mashimo.
mkuu kuna barabara nyingi zinajengwa bila weledi nyingine zinapita vibarazani njoo mabibo external na goba masana road hadi aibu full poor design waenda kwa miguu hawazingatiwi
 
mkuu kuna barabara nyingi zinajengwa bila weledi nyingine zinapita vibarazani njoo mabibo external na goba masana road hadi aibu full poor design waenda kwa miguu hawazingatiwi

Unachosema kinaweza kuwa na ukweli kama DSM ingekuwa imepangwa kikamilifu " Transport and Land use" sasa Dsm ya leo unaanzia wapi kupata eneo la kutosha kuweka pedestrian path? unachokisema kinawezekana kabisa mji ukipangwa kitaalam sisi tumeshindwa kiongozi, sasa tafuta mtu makini wa kuja kurekebisha hayo yote! is you kudecide October 2015
 
Hoja yako hipo zaidi on intention or what was during his era and the ideal beliefs. Mkapa amekuwa champion mkubwa sana wa self development policies tangia aache uraisi which is not a bad thing. Kila mwansiasa kwa sasa anaimba nyimbo hizo hizo it is the popular thing to say and what most Tanzanians wishes for that to happen.

Lakini mkapa huyo ukimuuliza wakati anafanya privatization za mabenki na sector nyingine mbona hakuwapa wazalendo kipaumbele cha kuchukua hisa za mabenki kwanza na sehemu zingine alizofanya privatization.
Hata leo kuna wanasiasa wanalalama sehemu za kigamboni kuachiwa mwekezaji badala ya kupewa wazalendo.

Mimi naangalia katika uhalisia based on the business environment, current political and social issues, national challenges; kwenye uhalali wa hoja zao.

Uwezi kufanya vitu bila ya capital hata yeye mkapa ukimuuliza atakwambia sababu kubwa ya mabenki kununuliwa na wageni ilikuwa hakuna internal buyers, and not much has changed since then very few Tanzania can risk to participate in large industrial activities that need large sums of capital or else kungekuwa na case kubwa sana ya raisi na mawizara kila uchao kusafiri kutafuta capital investment za kuja.

Sasa basi hata hicho kidogo ambacho mtanzania anachoweza ku risk nacho kwenye safe investment za serikari malipo yanachelewa kwa muda mrefu sana ndio maana miradi ya barabara mingine imeishia nusu kati au kwenye hatua za awali kabisa. Hivi unaniambia akija mkenya au mgeni kutokana na mazingira yenyewe na hela ya kumaliza mradi kwa utaratibu wa malipo ya serikari anaweza nyimwa kweli considering watanzania wana demand barabara sehemu zao?

Ndio maana nakwambia wewe unaongea kwa what is ideal mimi nakwambia uhalisia wenyewe wanachosema ni kwa sababu tu wanajua watanzania wanataka kusikia lakini nia hakuna kutokana na facts zenyewe, jinsi serikari inavyodaiwa kwenye investment na namna zake za ulipaji unaotaka mtu kuwa very patient na watanzania wangapi kwa sasa wenye huo moyo wa kusubiri madeni ya miaka au wenye kipato cha kumaliza miradi bila kufidiwa mpaka mwisho. Vinginevyo kusingekuwa na sababu ya miradi kuishia kati sehemu nyingi either kwa sababu ya ubadhirifu au kukosa mapato the situation does not foster large social participation but rather those with enough funds to embark on this risk taking mission.
Mkuu usibadilishe magoli ili uweze kufunga goli ulipendalo.
Katika mada hii unjipeleka nje ya mada kwa minajili ya kumjadili Mkapa badala ya ujumbe alioutoa kwenye kadamnasi ya wajenzi, ikiwa ni wahandisi, wakandarasi na hata wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi.

Mada aliyitoa Mkapa iko consistent toka alipoingia madarakani, wajenzi wa kitanzania kwanza.
Na ndio maana ziliundwa Road FundBoard na hata TANROADS kwa ajili hiyo.

Kwamba alifanya vibaya jatika fani nyingine, mumwite nanyinyi katka fani zenu ili alitolee tamko.
Siyo siri, katika discipline ya matumixi Mkapa alifanya vizuri, hata hivyo ni yale machache aliyoboronga au yaliyoborongwa chini ya utawala wake, yataendelea kumsuta.

Hilo halimkatazi kutamka kuwa katika kazi za majenzi kipaumbele kiwekwe kwa wazalendo kwanza.
 
Mkuu usibadilishe magoli ili uweze kufunga goli ulipendalo.
Katika mada hii unjipeleka nje ya mada kwa minajili ya kumjadili Mkapa badala ya ujumbe alioutoa kwenye kadamnasi ya wajenzi, ikiwa ni wahandisi, wakandarasi na hata wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi.

Mada aliyitoa Mkapa iko consistent toka alipoingia madarakani, wajenzi wa kitanzania kwanza.
Na ndio maana ziliundwa Road FundBoard na hata TANROADS kwa ajili hiyo.

Kwamba alifanya vibaya jatika fani nyingine, mumwite nanyinyi katka fani zenu ili alitolee tamko.
Siyo siri, katika discipline ya matumixi Mkapa alifanya vizuri, hata hivyo ni yale machache aliyoboronga au yaliyoborongwa chini ya utawala wake, yataendelea kumsuta.

Hilo halimkatazi kutamka kuwa katika kazi za majenzi kipaumbele kiwekwe kwa wazalendo kwanza.



Huu ndio uzuri wa 'age of information' alicho kisema Mkapa kila mtu kakisikia na concerns za wakandarasi kila mtu alizisikia tena hapo kwenye stage ni viongozi wao tu wamewekwa: vyombo vingine vilivyo wahoji wakandarasi wengi zaidi ni malalamiko tu ya malipo na jinsi wanavyo athiri sector na biashara zao kwa ucheleweshaji wa malipo.

Sasa basi kwenye dunia ya biashara na siasa ambapo serikari inataka kuonekana inafanya kazi, iwe mushrooming of properties kweye miji au mwongezeko wa kilometa za barabara inataka ao watu wawe na hela in the first place.

Kwa maana hiyo what president Mkapa did during his tenure or said in this instance does not reflect the fact of sound investment kufikia malengo ya uzalendo kwa nyakati za leo. The barrier being capital which is the King in determining the level of local participation since its lacking kwa hivyo wageni watakuwepo tu provided they have the money its just politics and facts in meeting social demands.

Hili sector itawalie na wazalendo kunahitajika mikopo zaidi na pengine yenye unafuu and other investment friendly policies au matajiri zaidi wajiingize vinginevyo maneno yake ni siasa tu kwa mazingira ya sasa kwa sababu hakuna hizo important influences.
 
Last edited by a moderator:


Huu ndio uzuri wa 'age of information' alicho kisema Mkapa kila mtu kakisikia na concerns za wakandarasi kila mtu alizisikia tena hapo kwenye stage ni viongozi wao tu wamewekwa: vyombo vingine vilivyo wahoji wakandarasi wengi zaidi ni malalamiko tu ya malipo na jinsi wanavyo athiri sector na biashara zao kwa ucheleweshaji wa malipo.

Sasa basi kwenye dunia ya biashara na siasa ambapo serikari inataka kuonekana inafanya kazi, iwe mushrooming of properties kweye miji au mwongezeko wa kilometa za barabara inataka ao watu wawe na hela in the first place.

Kwa maana hiyo what president Mkapa did during his tenure or said in this instance does not reflect the fact of sound investment kufikia malengo ya uzalendo kwa nyakati za leo. The barrier being is capital which is the King determining the level of local participation and is lacking kwa hivyo wageni watakuwepo tu; hili sector itawalie na wazalendo kunahitajika mikopo zaidi na pengine yenye unafuu au matajiri zaidi vinginevyo maneno yake ni siasa tu kwa mazingira ya sasa.

I totally dis agree with you on your last note.
Discussion here is serikali itoe kipaumbele kwakazi na madeni ya wakndarasi, na Mkapa laid the foundation ya suala hilo.
Pengine you font see the logic behind.
Kodi kwa ajili ya wajenzi wajandarasi ipo- Road Fund
Vehicle kwa mitaji hiyo ipo-TANROADS, TBA, TEMESA na hata kazi za Halmashauri etc
Sasa kwa kazi hizo kulengwa wazalendo is is too much to ask?

Sasa wewe unaongelea mitaji ya mahoteli na vinginevyo, thats Mars to me, though its not impossible!
Twende na context ya mada
 
Last edited by a moderator:
[/B]I totally dis agree with you on your last note.
Discussion here is serikali itoe kipaumbele kwakazi na madeni ya wakndarasi, na Mkapa laid the foundation ya suala hilo.
Pengine you font see the logic behind.
Kodi kwa ajili ya wajenzi wajandarasi ipo- Road Fund
Vehicle kwa mitaji hiyo ipo-TANROADS, TBA, TEMESA na hata kazi za Halmashauri etc
Sasa kwa kazi hizo kulengwa wazalendo is is too much to ask?

Sasa wewe unaongelea mitaji ya mahoteli na vinginevyo, thats Mars to me, though its not impossible!
Twende na context ya mada
OK turidi kwenye context zako what is the process of tendering on road investment.

Unapewa hela ya kufanya mradi na hizo taasisi au ata serikari za mitaa kabla ya kuanza kazi?

Au unatakiwa uanze na capital yako na serikari itakulipa baadae?
 
OK turidi kwenye context zako what is the process of tendering on road investment.

Unapewa hela ya kufanya mradi na hizo taasisi au ata serikari za mitaa kabla ya kuanza kazi?

Au unatakiwa uanze na capital yako na serikari itakulipa baadae?
Now we are talking!
This industry is very complex na jinsi unavyo weza kuchangaya karata zako za capital investment in construction. Sasa kupewa au kutopewa capital itatokana na uhusiano wako na bankers wako kibisahara.

Kama una collateral , kupata capital si shida.
Songombingo ni pale una kazi, huna mtaji.
 
This industry is very complex na jinsi unavyo weza kuchangaya karata zako za capital investment in construction. Sasa kupewa au kutopewa capital itatokana na uhusiano wako na bankers wako kibisahara.
OK kuna wafanyabiashara wangapi ambao wana mitaji bila ya kutegemea mabenki ili waweze ziba mahitaji ya ujenzi wa barabara kila mwaka? kama awatoshi


Now look at this scenario:

Je pale unapopewa mkopo na benki na ukishindwa kulipa kwa muda wa makubaliano what happens, kama pia una supplier anakudai au labda umekodisha vitendea kazi, au umenunua kwa hire purchase machines, madhara yake yako wapi ukicheleweshewa malipo?

Je mabenki unadhani yataona faida za kuendelea na mikopo ya aina hii kwa muda mrefu kama serikari aitabdili tabia yakuchelewesha malipo ya wakandarasi? Hili tujue kama kweli watanzania wanaweza chukua hizo tender wanazopewa wageni kwa sababu fursa za mitaji pia zipo.

Kama una collateral , kupata capital si shida. Songombingo ni pale una kazi, huna mtaji.

Given the situation kwa mwaka kuna sehemu ngapi ndani ya Tanzania watu wanawapigia kelele wanasiasa wanahitaji barabara na kuna uwiano ya watu wanaopata mitaji kuweza kumudu sehemu zote serikari inazotoa tender wa aina zote mbili za wawekezaji and their sources of capital nilizouliza hapo juu?

Kama hakuna uwiano sahihi wakija wageni wenye hela unadhani serikari itakataa kuwapa kazi kutokana na political pressure na gain kwa wananchi kisa uzalendo?

Ukipata majibu ya maswali yangu utaweza kuona misingi ya hoja zangu na kwanini ni kauli ya kisiasa tu alichosema bwana mkapa kwa mazingira ya sasa.
 
OK ni wangapi ambao wana mitaji bila ya kutegemea mabenki?


Now look at this scenario:

Je pale unapopewa mkopo na benki na ukishindwa kulipa kwa muda wa makubaliano what happens, kama pia una supplier anakudai au labda umekodisha vitendea kazi, au umenunua kwa hire purchase machines, madhara yake yako wapi ukicheleweshewa kulipwa?

Je mabenki unadhani yataona faida za kuendelea na mikopo ya aina hii kwa muda mrefu kama serikari aitabdili tabia yakuchelewesha malipo ya wakandarasi? Hili tujue kama kweli watanzania wanaweza chukua hizo tender wanazopewa wageni.



Given the situation kwa mwaka kuna sehemu ngapi ndani ya Tanzania watu wanawapigia kelele wanasiasa wanahitaji barabara na kuna uwiano ya watu wanaopata mitaji kuweza kumudu sehemu zote serikari inazotoa tender?

Kama hakuna uwiano sahihi wakija wageni wenye hela unadhani serikari itakataa kutokana na political pressure za wananchi kisa uzalendo?

Ukipata majibu ya maswali yangu utaweza kuona misingi ya hoja zangu.
Mkuu now we are in business!
Good to raise the salient issues.
Biashara yoyote inahitaji capital, wengine wanaipata kwa wizi(escrow), wengine waadilifu kwa kufanya kazi kwa bidii na kutumia hizi financial institutions zetu.

Lazima tusisahau kuwa hakuna free capital. Yaani uende benki na usiwe na uhakika wa kurudisha mkopo huo ambao ni mtaji wako, na hapo ndipo panapowashinda watanzania wengi.

Lakini wakati huo huo haitakuwa salama kwa nchi yetu kuruhudu wageni wenye mitaji yao kutawala nchi hii kibiashara , hususan sekta ya ujenzi.
Kisiasa susla hilo si endelevu and potentially explosive.
 
Mkuu now we are in business!
Good to raise the salient issues.
Biashara yoyote inahitaji capital, wengine wanaipata kwa wizi(escrow), wengine waadilifu kwa kufanya kazi kwa bidii na kutumia hizi financial institutions zetu.

Lazima tusisahau kuwa hakuna free capital. Yaani uende benki na usiwe na uhakika wa kurudisha mkopo huo ambao ni mtaji wako, na hapo ndipo panapowashinda watanzania wengi.

Lakini wakati huo huo haitakuwa salama kwa nchi yetu kuruhudu wageni wenye mitaji yao kutawala nchi hii kibiashara , hususan sekta ya ujenzi na watakuza sector nyingine zenye uhusi.
Kisiasa susla hilo si endelevu and potentially explosive.
Nilianza na kusema hoja yako ni ideal na kila Mtanzania would love too see that lakini aikizi mazingira yenyewe ya kuweza kufanikisha.

Serikari inatakiwa irudi kwenye drawing board kama inataka kuakikisha hela inabaki ndani simple ifanye yenyewe through direct investment sehemu kubwa ya miradi ya barabara kutokana na size of the TASK (kwanza wataokoa hela kwa kipindi cha muda mrefu) kama watamiliki vitendea kazi na watakuza sector nyingine zenye uhusiano na ujenzi.

Pili ifanye tathmini ya watanzania wanaoweza chukua size ya tender ndogo ndogo na kupanga mikakati ya sera endelevu kuwasaidia wafanya biashara kupata mikopo that is the only way hela itabaki Tanzania au hata wageni wanapopewa kazi iwe on condition they have settled in Tanzani na kampuni imeajiri watanzania, inalipa kodi Tanzania, imekopa Tanzania, etc to make it a fair game.

Lakini kwa utaratibu wa market forces kwenye hiyo sector na mazingira yalivyo hilo tamko alina uhalisia wa kimazingira (sisemi tuwe wajamaa sehemu zote au serikari ifanye hivyo sehemu zote).

By the way that is my opinion; mtu mwengine anaweza pia akawa na mtazamo tofauti kwa kupima speed ya serikari ikisema ifanye yenyewe na mwendo wa sasa; maana barabara pia zikikamilika kuna faida zingine za kipato kwa serikari.
 
Nimependa exchange kati ya Jidu la Mabambasi na Eric Cartman,

Naomba pia kuwajuza kwa sasa kuna Wazalendo wameweza kupata mradi wa Ujenzi wa barabara na walipata guarantee kupitia benki zetu za hapa hapa changamoto kubwa ni miradi ya serikali GOT kutolipa kwa wakati - erratic cash flow, wanayumba sana ofcourse they are in horrible situation.

Nini cha kufanya ni kurekebisha sheria za manunuzi ziwe nzuri ili kuwawezesha local contractors wapate kazi na waacces benki kirahisi na pia serikali iwe na budget principles - you have cash float tender you don't, better do other business. Ndo dunia ya leo inavyokwenda bla bla hazina nafasi leo.
 
Nimependa exchange kati ya Jidu la Mabambasi na Eric Cartman,

Naomba pia kuwajuza kwa sasa kuna Wazalendo wameweza kupata mradi wa Ujenzi wa barabara na walipata guarantee kupitia benki zetu za hapa hapa changamoto kubwa ni miradi ya serikali GOT kutolipa kwa wakati - erratic cash flow, wanayumba sana ofcourse they are in horrible situation.

Nini cha kufanya ni kurekebisha sheria za manunuzi ziwe nzuri ili kuwawezesha local contractors wapate kazi na waacces benki kirahisi na pia serikali iwe na budget principles - you have cash float tender you don't, better do other business. Ndo dunia ya leo inavyokwenda bla bla hazina nafasi leo.

Swala jepesi lipa wakandarasi kwa wakati sector itakuwa na italeta ushawashi watu kujiunga maana mabenki yapo tayari kutoa mikopo kwa miradi ya serikari.

Kwa hilo lirekebishike serikari lazima sio tu kila mwaka ipange budget halafu hakuna monitoring procedures au vipaumbele vyao. Wewe uwezi kutumia makadirio kufanya miradi wakati auna uhakika na sources of your other income (hizo hela za donors).

Budget aiwezi kuwa aina vipaumbele vya serikari na kujua tukifikia kiasi fulani ni alert sio mpaka serikari ikose hela kabisa kama mwaka jana raisi alivyodai walikuwa wamefilisika bahati nzuri capital gain tax ya $250 baada ya wazungu kubadilishana vitalu ndio iliyo okoa shughuli za serikari vitu vya ajabu hivyo.

Lazima ujue which are reliable sources of income and non guarantee source zako (kwa nchi ambayo short falls are difficult to be covered), weka vipaumbele vyako kikubwa ni shughuli za uendeshaji wa serikari labda mishahara, dawa na mambo ya lazima lengea source ambazo una uhakika nazo huko, vitu ambavyo unaona vinaweza subiri wekea unreable source of income usitoe tender mpaka unapata hela zake, kata marupu marupu ya posho ukifikia kwenye alert etc to do with budgeting monitoring ni vitu vya ajabu sana serikari kukosa hela za mishahara ya walimu, kazi zake including tender inazotoa za chakula cha wanafunzi.

Ni wazi kuna uzembe mkubwa kwa nchi zingine this is unacceptable sio kwamba na wao serikari uwa azipati shortfall kutokana na mambo mengi ambayo awakuyatarajia kwenye source zao; ila wanajiandaa na wanaweza raise funds kwenye bonds market kutokana na watu kuziamini sera zao za maendeleo.

Sio kila mwaka wewe ufikii budget yako na bado unaongeza makadirio kila mwaka, una madeni luluki, una budget deficit na unategemea msaada wa watu wale wale waliokunyima mwaka jana, budget ambayo aina impact ya uchumi mkubwa (kuwafikia watanzania wengi).

I tell you jamaa wa wizara ya fedha na sehemu za uchumi si lolote si chochote ndani ya Tanzania tu-mamskini kwa sababu pia mipango yetu ni mibovu na kuna ombwe la taaluma ya uchumi na finances huo ndio uhalisia ninao uona.
 
Mkuu usibadilishe magoli ili uweze kufunga goli ulipendalo.
Katika mada hii unjipeleka nje ya mada kwa minajili ya kumjadili Mkapa badala ya ujumbe alioutoa kwenye kadamnasi ya wajenzi, ikiwa ni wahandisi, wakandarasi na hata wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi.

Mada aliyitoa Mkapa iko consistent toka alipoingia madarakani, wajenzi wa kitanzania kwanza.
Na ndio maana ziliundwa Road FundBoard na hata TANROADS kwa ajili hiyo.

Kwamba alifanya vibaya jatika fani nyingine, mumwite nanyinyi katka fani zenu ili alitolee tamko.
Siyo siri, katika discipline ya matumixi Mkapa alifanya vizuri, hata hivyo ni yale machache aliyoboronga au yaliyoborongwa chini ya utawala wake, yataendelea kumsuta.

Hilo halimkatazi kutamka kuwa katika kazi za majenzi kipaumbele kiwekwe kwa wazalendo kwanza.

Eti displine ya matumizi.. Pyuuuuu!!! Wew jamaa kipenda roho! !!! Hivi unajua ni 50% ngapi zilipigwa na akina chenge ,mramba ,lyumba wa biot kuhusu ujenzi wa jengo la biot.Mkapa kama ni mwezi atakuwaje na nidham ya matumizi . Ama kwa vile watu walifungwa midomo wanakuja kuyafaham hayo mauzauza baadae.
 
Eti displine ya matumizi.. Pyuuuuu!!! Wew jamaa kipenda roho! !!! Hivi unajua ni 50% ngapi zilipigwa na akina chenge ,mramba ,lyumba wa biot kuhusu ujenzi wa jengo la biot.Mkapa kama ni mwezi atakuwaje na nidham ya matumizi . Ama kwa vile watu walifungwa midomo wanakuja kuyafaham hayo mauzauza baadae.
Una pwaya, tafuta mifano zaidi kujenga hoja yako.
 
Back
Top Bottom