Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Uko kwenye mizunguko yako maeneo mbali na nyumbani kwako, mara ghafla anakutokea mwanamke usiyemjua kabisa na anakwambia kwa sauti kiasi cha kuwavuta wapita njia wengine waliokuwa wakipita na shughuli zao kusimama na kusikiliza kinachoendelea.
Mwanamke huyo anakwambia……, "Wee baba we, nakuomba sana umkanye mkeo kutembea na bwana angu, la sivyo nitamfanya kitu ambaccho hatakuja kukisahau maishani mwake…..Mwambie asisahau kama mie ni mzaliwa wa Tanga. Kama humtoshelezi, si akatafute wanaume mwengine huko, kuliko kutembea na mabwana za watu, mpaka anataka kunihatarishia uchumba angu, mwambie akome tena akome kama alivyokoma kunyonya titi la mama yake…………….." mwanamke huyo anaondoka huku akiendelea kubwabwanya na njia kwa maneno yenye kukera.
Hebu niambie kama ni wewe unachukua hatua gani ………..?
Mwanamke huyo anakwambia……, "Wee baba we, nakuomba sana umkanye mkeo kutembea na bwana angu, la sivyo nitamfanya kitu ambaccho hatakuja kukisahau maishani mwake…..Mwambie asisahau kama mie ni mzaliwa wa Tanga. Kama humtoshelezi, si akatafute wanaume mwengine huko, kuliko kutembea na mabwana za watu, mpaka anataka kunihatarishia uchumba angu, mwambie akome tena akome kama alivyokoma kunyonya titi la mama yake…………….." mwanamke huyo anaondoka huku akiendelea kubwabwanya na njia kwa maneno yenye kukera.
Hebu niambie kama ni wewe unachukua hatua gani ………..?