Tony antony
JF-Expert Member
- Nov 17, 2013
- 4,988
- 3,270
Ndugu yangu bado upo UKAWA ipi wewe maana ulishasema unatoka??Lowasa akija UKAWA mimi natoka , amechafuka , hana na wala hajawahi kuwa na fikra mpya , ndio maana hadi leo anaamini kwamba rushwa itampeleka ikulu .
Hahaaaaa pipooz....Wewe Ulikuwa hujui kuwa Jukumu lako linaishia kwny kukunja ngumi hewani na kusema pipoooz, Chama kina wenyewe na wakiamua kufanya Maamuzi huulizwi chochote !
Uliyeleta mada ni mkereketwa wa ACT.Kwa taarifa yako,Ukawa haiitaji mtu anayeitwa mamvi.Kumkubali mtu mzee huyu ndani ya ukawa ni kama kuchambia mfuko wa Rambo.
UKAWA nako wakimgomea ataenda wapi.?
Hata mimi nilikuwa na mawazo kama haya hapo awali. Lakini baada ya Lowassa kufunguka ukweli wote na kujua hiyo Richmond ni nini na nani hasa muhusika nilibadili msimamo wangu juu yake.
Binadamu huwezi kumchukia mtu kwa vile umeambiwa ni mchawi halafu ukaja ujua ukweli nawe ukaendelea na msimamo wako uleule. Huo utakuwa ujinga mkubwa, ambao watu wa ccm wanataka tuwe hivyo. After 8 years tumeujua ukweli na ule uovu tuliokuwa tunaambiwa ni wa Lowassa bado uko huko huko wanaendelea nao.
Wewe hebu acha fiksi zako.Lowasa akija UKAWA mimi natoka , amechafuka , hana na wala hajawahi kuwa na fikra mpya , ndio maana hadi leo anaamini kwamba rushwa itampeleka ikulu .
Uchu wa fedha unakisambaratisha hiki chama.Mungu hajaumba Mchaga wa Kukataa hela A Mamvi Chadema
Dr Slaa kastaafu siasa?Ndio maana akina Dr Slaa wakaamua kustaafu siasa kama vijana tegemeo kwa ukombozi ndio hawa ....Mbowe alivyobadili gia angani wakala matapishi yao ....
DuhHahahahahahaaaa! Lowassa hana ubavu wa kubaki CCM kama atatoswa kwenye kuwania Urais. Kwa sababu anajua hawezi tena kusubiri miaka kumi ijayo kama alivyokubali kumsubiri Kikwete hadi atakapomaliza ungwe yake. Akitoshwa Urais atatoka tu CCM, na kuna kila dalili kuwa CCM hawatampa nafasi ya kuwania Urais mwakani.
Ova
We nomaJapo ambalo si la siri kwamba kambi zote za wagombea urais CCM zinamuogopa sana Lowassa, hivyo kuna kila aina ya jitihada ya kuhakikisha jina la Lowassa halipitishwi kugombea nafasi ya urais.
Huku wapinzani wakijipanga kukata jina lake lakini Lowassa yeye anaendelea na mikakati yake ikiwa ni pamoja na kugawa fedha kama njugu kwani anaamini yeye ni rais wa Tanzania 2015-2025 "PIGA UA"
Lowassa anatishia kukiua chama (CCM) endapo hata pitishwa kugombea urais.
Wakati huo huo, endapo jina la Lowassa halitapitishwa CCM wanyetishaji wetu wanasema mkakati wa Lowassa kugombea kupitia UKAWA kwakuwa tayari ana mtaji wa wanaCCM wengi hivyo ni rahisi kwake kushinda nafasi ya uraisi.
Inasemekana kuwa tayari Lowassa ameshaanza mazungumzo ya chini chini na viongozi wa UKAWA lakini bado hawajafikia makubaliano rasmi.
Say it again haaaaLowasa akija UKAWA mimi natoka , amechafuka , hana na wala hajawahi kuwa na fikra mpya , ndio maana hadi leo anaamini kwamba rushwa itampeleka ikulu .
Hawa wafukua makaburi hawa!!!Mtu anayeshindwa kuitetea ccm japo Arusha Tu hatumtaki.
Wewe baba upoHata kama atahongo billions viongozi wa ukawa hawawezi kumpendekeza na hawawezi kumkubali by any means. Hauziki huyo
Kaka za sikuukiona mtu anamsifu mtu mchafu kama Lowassa ujue yeye ni mchafu zaidi raisi ajaye chaguo la watanzania ni DR Slaa pekee yake hana skendo za wizi kama ccm
Mkuu bado uko hai?Tena akome anajua jasho la wananchi wanaopigania UKAWA abaki na mazimwi wenzie CCM
ChademaaaaNashangaa watu wanavyomnadi EL huyu hawezi kuwa rais wa Tanzania pamoja na njugu zote anazomwaga, watakula na kuvimbiwa kama JK alivyovimbiwa wizi kwa miaka 10 iliyopita. Hana jipya. wakuu endeleeni kufaidi hizo njugu kutoka Voda phone hazina mwenyewe. Kiini cha kuvuruga shirika la simu Tanzania.