Ingekuwa mimi ni UKAWA,ningemkaribisha kwa masharti.
1.Sharti la kwanza,atoke hadharani na kueleza kinagaubaga jinsi alivyohusika na kashfa ya Richmondi,AICC n.k
2.Aseme alimaanisha nini wakati wa kuijuzulu aliposema ameamua kung'atuka ili kuiokoa serikali ilhali yeye ndio alikuwa kiongozi mkuu wa serikali na kujiuzulu kwake maana yake serikali ilianguka.
3.Aeleze fedha zote alizogawa misikitini,makanisani,kwenye saccos mbalimbali alikuwa anazitoa wapi na lengo lake lilikuwa nini maana kabla ya kujiuzulu hakufanya hivyo.
4.Akane kutamani nafasi yeyote kisiasa kupitia UKAWA kinyume na utaratibu ulipo wa UKAWA.
5.Aeleze sababu zinazomfanya ahame ccm ambazo hizo sababu hazipo kwenye hichi chama kwenye UKAWA.
Akijibu haya yoote kiufasaha mbele ya waandishi wa habari,NINGEMPATIA kadi ya uanachama wa chama na ningemtumia kwa kadiri nitakavyomhitaji.