......Mkaidi hafaidi mpaka siku ya Eid

......Mkaidi hafaidi mpaka siku ya Eid

Shantel

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2011
Posts
2,018
Reaction score
1,132
Nachukua nafasi hii kuwapongeza wenzetu wote waliokuwa wamefunga kwenye
huu mwezi Mtukufu, marafiki zangu wa karibu sana pia nawapongeza sana
na ninawatakia sikukuu njema ya Eid

Mfurahie sikukuu huku mkitafakari kwa undani kabisa uzito wa mwezi huu na
mlipoweza kufunga, yale mema yote mliyokuwa mnayafanya mwezi mzima
muendelee kuyafanya,isiwe kwamba mlikuwa mnasubiria kwa hamu siku ifike
ili mrudie yale mabaya pia

Nawaombea Mungu awatie nguvu na kuwabariki kwa mema yote mliyoyafanya
Nawatakia sikukuu njema na msherekee kwa amani na upendo

Mwisho kabisa...title nimeandika tu ila sijui huo msemo unamaanisha nini
na nini chanzo chake....naomba kuchukua fursa hii kuomba kujibiwa kwa
anayefahamu
 
Thanks Shantel its very kind of you,wishing you Eid Mubarak.
 
Mwisho kabisa...title nimeandika tu ila sijui huo msemo unamaanisha nini<br />
na nini chanzo chake....naomba kuchukua fursa hii kuomba kujibiwa kwa <br />
anayefahamu
<br />
<br />

Siku hiyo watu wote husheherekea pamoja kwa kula na kunywa ikiwezekana na mavazi plus miyuzik na mambo mengine ya sherehe hivyo basi hata yule ambae alitengwa kutokana na kubishia jambo fulani, basi siku hiyo usamehewa nae akaburudika na wenzake! (tafsiri isiyo rasmi; source-hadithi za Babu)
 
Mwisho kabisa...title nimeandika tu ila sijui huo msemo unamaanisha nini
na nini chanzo chake....naomba kuchukua fursa hii kuomba kujibiwa kwa
anayefahamu

Msemo wenyewe ni mwana mkaidi hafaidi hadi siku ya Idd...............................una maanisha ya kuwa siku ya Idd wazazi huwavalisha watoto wao lakini pia ni nafasi kwao kutowazawadia watoto wao ambao wanawaona ni wakaidi.............kwahiyo mtoto mkaidi hafaidi hadi siku ya Idd anapozoa matunda ya ukaidi wake kwa kunyimwa mapochopocho ya wazazi wake................
 
Hiyo inamaanisha kuwa, cku ya Eid wazaz wanajitahd cku hyo kuandaa either chakula cha pekee kwa familia ili kushirik pamoja cku hyo ndio nafasi pia kwa mkaidi kufaidi, kwa sababu kutakuwa na wagen kwa hyo itakuwa ngumu kwa mzaz kusema lolote mbele yawagen.
 
Hiyo inamaanisha kuwa, cku ya Eid wazaz wanajitahd cku hyo kuandaa either chakula cha pekee kwa familia ili kushirik pamoja cku hyo ndio nafasi pia kwa mkaidi kufaidi, kwa sababu kutakuwa na wagen kwa hyo itakuwa ngumu kwa mzaz kusema lolote mbele yawagen.
<br />
<br />

Hahahaha....hii ya kwako imekaa vyedi!

.
 
kweli mkaidi hafaidi mpaka siku ya eid, kwa hiyo siku hiyo hadi wakaidi wanapata kislope au mkono wa eid
na kwa nini kila mtu akiombwa mkono wa eid anasema minailfaidhina? kama huwa ni siku ya kugawa kwa nini
huwa hawagawi basi
 
kweli mkaidi hafaidi mpaka siku ya eid, kwa hiyo siku hiyo hadi wakaidi wanapata kislope au mkono wa eid
na kwa nini kila mtu akiombwa mkono wa eid anasema minailfaidhina? kama huwa ni siku ya kugawa kwa nini
huwa hawagawi basi


ha ha ha... Shantel bana! Nini hasa are you getting at??
 
kweli mkaidi hafaidi mpaka siku ya eid, kwa hiyo siku hiyo hadi wakaidi wanapata kislope au mkono wa eid
na kwa nini kila mtu akiombwa mkono wa eid anasema minailfaidhina? kama huwa ni siku ya kugawa kwa nini
huwa hawagawi bas
i

Shantel; Nafikiri nimefaidi kama wewe ulivyofaidi kujua na kutambua kuwa ... Hata makaidi ... Siku ya Eid ... isnt excluded kwenye sherehe ni kama anapata break anafaidi pia naye... kama nchi nzima ilivyo faidi umeme (Lol) lakini hapo kwenye blue.. Kama sijelewe kidogo ..Mgao gani Shantel?
 
Back
Top Bottom