Mjue omba omba Tajiri kuliko wote Duniani

Mjue omba omba Tajiri kuliko wote Duniani

Miguel255

Member
Joined
May 13, 2020
Posts
35
Reaction score
111
Ama kweli tembea uone tulia usimuliwe, hii dunia haiishiwi mambo. Kuna msemo waswahili husema kuna watu na viatu sasa leo nataka nikusilumie story ya kiatu kimoja hivi.

Katika jiji la Mumbai nchini India kuna jamaa mmoja anaitwa Bharat Jain. Huyu jamaa ni omba omba maarufu jijini na shughuli zake hufanyia kwenye jua katikati ya jiji, yaani jua lake mvua yake.

Huonekana mtaani akiwa amechoka, mavazi machafu sura haina nuru lakini cha kushangaza Bharat ni mmoja kati ya omba omba matajiri zaidi duniani. Pengine hata ndio omba omba mwenye pesa ndefu kuliko wote pale Dodoma.

Jamaa anamiliki maghorofa mawili hapo hapo Mumbai. ana maduka ya nguo na viatu, ana sheli moja pembezoni mwa jiji ana frame kapangishia watu kama uchafu. Unaambiwa utajiri anaomiliki huyu matonya ni zaidi ya dolla milioni 1 za kimarekani. Yaani kwa pesa za bongo ni kama bilioni 2 hivi na upuku upuku.

Familia yake ilimuomba sana aachane na maisha ya kuomba omba kwani walihisi kudharirishwa lakini Bharat aliwaambia hizi pesa ninazomiliki, hizi pesa zilizofanya nyie familia yangu kuwa moja ya familia tajiri hapa India nimezitoa kwenye hii kazi. Chezea mshahara usichezee kazi, siwezi kuacha kuomba labda mmoja wetu atoweke kwenye uso wa dunia yaani yeye afe au kazi ya kuomba omba isiwepo kabisa duniani🤣🤣

Unaambiwa jamaa hanaga utani awapo kazini, ukikutana nae hata uwe na roho ngumu vipi utampa tu hela. Yeye mwenyewe anadai kuomba omba ni sehemu ya nafsi yake. Yqani mapigo yake ya moyo tu hayalii "tum tum tum" yanalia "omba omba omba" Kwahiyo aache kuomba bora afe🤣🤣

Unajua mnaweza kudhani natunga ila hii ni ukweli mtupu kama una mwenyeji wa India hasa mumbai muulize atakwambia kwasababu hakuna kiumbe kisichomjua Bharat. Unaambiwa kila kati ya watu kumi basi kuna mtu mmoja alishawahi kumpa hela mwamba.

images (1).jpeg


Kwenye moja kati ya mahojiano yake alisikika akisema kwa alipofikia sasa yeye haombi kwaajili ya njaa. Anaomba kwasababu kwanza ana enjoy kufanya hivyo pili anafurahia kuona sura mpya mpya mbazo asingeweza kuziona kama angebaki kwenye jumba lake la kifahari.

Huyo ndo Bharat omba omba tajiri kuliko wote Duniani

images.jpeg
 
Umenifanya kucheka kiboya sana
kuna mmoja nimemuwezesha mda si mrefu

ila kutoa ni moyo jamani ombaomba wa kariakoo wana maisha mazuri sana
sema mazingira yao wanapigwa na jua kutwa!
 
Unajimaliza kumbe mwenzako yupo vyema


Aaaah wapi kuna jamaa mmoja anaombaga watu hela kweli kweli na sio kwamba ni mlemavu halafu nakuja kumuona hela hizo anaenda kuvutia sigara na anakula chakula kizuri kunizidi

Yaani soup asubuhi na mapema ili hali mimi nakula gimbi😅😅😅😅😅
 
Hard work bring luc
Ama kweli tembea uone tulia usimuliwe, hii dunia haiishiwi mambo. Kuna msemo waswahili husema kuna watu na viatu sasa leo nataka nikusilumie story ya kiatu kimoja hivi.

Katika jiji la Mumbai nchini India kuna jamaa mmoja anaitwa Bharat Jain. Huyu jamaa ni omba omba maarufu jijini na shughuli zake hufanyia kwenye jua katikati ya jiji, yaani jua lake mvua yake.

Huonekana mtaani akiwa amechoka, mavazi machafu sura haina nuru lakini cha kushangaza Bharat ni mmoja kati ya omba omba matajiri zaidi duniani. Pengine hata ndio omba omba mwenye pesa ndefu kuliko wote pale Dodoma.

Jamaa anamiliki maghorofa mawili hapo hapo Mumbai. ana maduka ya nguo na viatu, ana sheli moja pembezoni mwa jiji ana frame kapangishia watu kama uchafu. Unaambiwa utajiri anaomiliki huyu matonya ni zaidi ya dolla milioni 1 za kimarekani. Yaani kwa pesa za bongo ni kama bilioni 2 hivi na upuku upuku.

Familia yake ilimuomba sana aachane na maisha ya kuomba omba kwani walihisi kudharirishwa lakini Bharat aliwaambia hizi pesa ninazomiliki, hizi pesa zilizofanya nyie familia yangu kuwa moja ya familia tajiri hapa India nimezitoa kwenye hii kazi. Chezea mshahara usichezee kazi, siwezi kuacha kuomba labda mmoja wetu atoweke kwenye uso wa dunia yaani yeye afe au kazi ya kuomba omba isiwepo kabisa duniani🤣🤣

Unaambiwa jamaa hanaga utani awapo kazini, ukikutana nae hata uwe na roho ngumu vipi utampa tu hela. Yeye mwenyewe anadai kuomba omba ni sehemu ya nafsi yake. Yqani mapigo yake ya moyo tu hayalii "tum tum tum" yanalia "omba omba omba" Kwahiyo aache kuomba bora afe🤣🤣

Unajua mnaweza kudhani natunga ila hii ni ukweli mtupu kama una mwenyeji wa India hasa mumbai muulize atakwambia kwasababu hakuna kiumbe kisichomjua Bharat. Unaambiwa kila kati ya watu kumi basi kuna mtu mmoja alishawahi kumpa hela mwamba.

View attachment 3514321

Kwenye moja kati ya mahojiano yake alisikika akisema kwa alipofikia sasa yeye haombi kwaajili ya njaa. Anaomba kwasababu kwanza ana enjoy kufanya hivyo pili anafurahia kuona sura mpya mpya mbazo asingeweza kuziona kama angebaki kwenye jumba lake la kifahari.

Huyo ndo Bharat omba omba tajiri kuliko wote Duniani

View attachment 3514322
Hardwork bring luckoest charm
 
Pale Dodoma square, Kuna jamaa mweupe ana mwili MKUBWA, huyo jamaaa Huwa ana omba shilingi mia TU, na ukimuangalia ni msafi kawaida tu
 
Kuna omba omba mmoja huku usukamani umenikumbusha alivyo kosa aibu anipiga simu si unajua wasukuma kwa kelele akiongea kilugha kwa kiswahili kuwaelekeza wafanyakazi waliopo porini kama mteja wa ng'ombe kafika bei shingapi.
 
Mambo ya rohoni yana siri nyingi sana, kuomba mpaka kufikia utajiri huo Inahitaji maelezo ya kina sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom