Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,898
Picha kushoto
Umati wa wanaCHADEMA wakiwa kwenye maandamano yao mwaka jana (hapa ni Iringa)
Picha kulia
Umati mkubwa sana wa wana CCM wakitembea kwa mshikamano juzi wakati wa maadhimisho ya miaka 35 ya kuzaliwa chama chao (hapa ni Iringa)
Mwenyekiti nimeona niombe ufafanuzi wa mambo haya kwani naona kuna matumizi ya maneno tofauti kwa jambo lilelile kutokana na muhusika. Inapokuwa CCM wanatembea pamoja wanasema ni matembezi ya mshikamano, bali wanapotembea CHADEMA huitwa maandamano. Sasa ni nini tofauti kati ya matembezi ya mshikamano na maandamano na kwa nini maandamano hupigwa marufuku wakati matembezi ya mshikamano hayazuiwi wala kukemewa kama maandamano? Naamini uchambuzi na tafsiri zako mwenyekiti na nadhani utanipa tafsiri sahihi juu ya hili. Asante
Mchokonoaji ni mdau wa Mjengwa Blog
Mpanduji Mpanduji