Mjadala: Je, ruzuku ya bilioni 100 kwenye mafuta itapunguza bei ya mafuta kwa kiasi gani? "Jambo letu hatarini"

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Feb 17, 2016
17,506
15,997
Ndugu zangu,

Leo siku ya jumanne tarehe 10.05.2022 Ndugu Januari Makamba, Waziri wa Nishati akiwa bungeni ametangaza uamuzi wa serikali kutoa ruzuku ya takribani bilioni 100 za kitanzania.

Nikirejea uamuzi wa Waziri Makamba miezi michache iliyopita wa kuondoa tozo ya shilingi 100 kwenye mafuta ulisababisha Serikali kukosa mapato zaidi ya bilioni 100 ikabidi Rais Samia abatilishe nafuu hio na kurudisha tozo hiyo.

Kwa hesabu za haraka haraka ni dhahiri ruzuku ya bilioni 100 huenda isiwe na unafuu wenye tija kwa lita ya mafuta ambayo kwa sasa yanauzwa angalau shilingi 3,200 kwa lita moja kwani wakati Makamba akitangaza nafuu hii itakayoanza tarehe 01.06.2022 pia amesema bei ya mafuta itaendelea kupaa.

Je,ruzuku hii ya bilioni 100 itaweza kumeza ongezeko la bei ya mafuta kiasi cha kuleta ahueni kwa mwananchi? Kimahesabu jibu ni hapana.

Bila Serikali kuwa kali na makini katika usimamizi wa "mnyororo" wa biashara ya mafuta ruzuku hii ni kazi bure.Mnyororo wa biashara ya mafuta unaanzia kwenye ununuzi wa mafuta kutoka ng'ambo hadi kumfikia mtumiaji wa mwisho.Hili ndilo jukumu la msingi kwani ruzuku sio "sustainable".

Serikali ikumbuke kuwa Rais kaahidi wafanyakazi nyongeza ya mshahara sasa kupunguza matumizi ya kawaida (recurrent expenditure) na kutumia kama ruzuku itasababisha kutokuwa na bajeti ya nyongeza ya mshahara.

Nawasilisha.
 
Jibu ni inategemea na muda ambao serikali itaSubsidize..

Kumbuka: Subsidy iko fixed yaani Tsh 100 Billioni.

Quantity to be subsidized: Variable

Tanzania inatumia Mafuta jumla lita Million 400 kwa mwezi.

Hivyo basi, kama serikali itasubsidize kwa muda wa mwezi mmoja, bei itapungua kama ifuatavyo:

Punguzo, P1 = Tsh100 Billioni / 400 Million litres

P1 = Tsh 250 per litre for 1 month

Pia, kama serikali itasubsidize kwa muda wa mwaka mmoja, bei itapungua kama ifuatavyo:

Punguzo, P12 = Tsh100 Billioni / 4.8 Billion litres

P12 = Tsh 20.8 per litre for 1 year.

Hitimisho: kiwango cha bei ya mafuta itakayopungua kutokana subsidy iliyoweka serikali itategemea na distribution timeframe, kwa maana kwamba kama muda utakuwa ni kwa mwezi mmoja, bei itapungua Tsh 250 kwa kila lita ya mafuta..ila kama distribution itakuwa kwa mwaka mzima then bei ya mafuta itapungua kwa Tsh 20.8 kwa kila lita..
 
Ni heri gharama za maisha zipungue jambo lisubiri kuliko jambo liwepo na gharama zipande zaidi
 
Ruzuku itaanza Juni 1 mpaka bajeti ijayo itakapoanzwa kutekelezwa(Julai 1). Inamaanisha ruzuku hii itakuwa ya siku 30, chukua bilioni 100 ukigawanya kwa lita zinazotumika nchini kwa mwezi mmoja ndio itakuwa ruzuku kwa lita..
Mafuta kwa mwezi matumizi ni Lita mil 400, ambazo ni sawa na takribani trillion1.2
Bado bil 100 haitasaidia
 
Ni mapema sana kuzungumzia pesa hata ambayo bado hatujaipata(hiyo bilioni 100) kuwa aidha itasaidia au la!
 
Serikali ifanye yafuatayo

Isitishe uendelezaji wa Makao Makuu

Ipunguze posho

Isiajiri

Safari zipunguzwe, ile misafari mirefu iwe mifupi

Miradi isiyo na manufaa ifutwe, maana haitarudisha pesa

Tufunge mikanda haswa
 
Mleta mada umeandika jambo la msingi, hekima na Akili kubwa.

Watanzania hawana shida au habari za hayo matozo kwenye mafuta, kilio chao ni kuona bei ya mafuta inashuka, bei za bidhaa kupungua na kuwa na uhakika wa bei ya Petrol kutokupanda kiholela.

Watanzania wanataka kusikia leo hii bei ya mafuta imeshuka kiasi gani baada ya tamko la waziri
 
Watu wa uchumi hapa wanawezkutupa tathimin
Suala la mfumuko wa bei linahitaji immediate remedial solutions na long term solutions! Sasa hizo 100bill za mafuta zitatusaidia mpaka muda gani?
 
Nilijua tu hakuta kuwa na jipya!!

Washaona watanzania mapopoma hivyo wanacheza na akili zetu tu.
 
Kama Bei ya Mafuta Nchi ni ndogo kuliko ya Marekani kwanini serikali inahangaike hivi si wamekubali tuhangaike watuache wenyewe waendelee kutangaza Royal Tour tu
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom