Mjadala: Je biashara ya uchangudoa ihalalishwe?

Mjadala: Je biashara ya uchangudoa ihalalishwe?

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
372,737
Reaction score
863,623
Hili ni jambo la kijamii la kimaadili zaidi kuliko kimtazamo... Uhalisia wake ukijikita kwenye mikanganyiko ya jinsia, imani, maadili, heshima, hekima, ustawi wa familia nknk
Ni jambo lenye ukakasi wa aina yake kiasi kwamba ukitoa rai lihalalishwe unaweza kuonekana kituko katika jamii na mtu usiye na maadili... Lakini lazima tubadilike na nyakati, hatuwezi kubaki palepale dunia inabadilika na kila kitu kinabadilika
Hili jambo halina madhara kama kutumia vilevi na madawa ama wizi nk... Ni jambo tu la kimaadili zaidi... Na hata tukilikataa na kulipinga leo bado watu wataendelea kufanya
Biashara ya kuuza ngono... Sio kuuza mwili, sio tafsiri sahihi, kinachouzwa mtu anaondoka nacho, akikitumia na kukiacha hapo hapo, huyo kakikodisha... Hii ni mojawapo ya biashara kongwe zaidi duniani inayowaingia watu kipato kikubwa na kuwapa maisha...
Ngono ni hitaji muhimu na la lazima la kiasili, ngono huleta furaha, afya na nafuu ya msongo wa mawazo... Afya ya akili hujengwa pia ufanyaji wa ngono.... Lakini si kila mmoja anaweza kupata hitaji hili kwa uhuru, kwa uwezo na kwa utashi
Kuna ambao hawawezi kutongoza
Kuna ambao hawana muda wa kutongoza
Kuna ambao hawana hisia kabisa za mapenzi (sio ngono)
Kuna ambao ni wa binafsi na hawawezi kuhudumia mwanamke kila siku
Kuna makundi katika jamii ambayo mazingira yao, muonekano, kipato na utashi huwanyima fursa ya kuwa na wapenzi
Wote hawa katika ujumla wao kimbilio lao ni kwa wale wanaofanya biashara ya ngono maarufu kama machangudoa ama madadapoa... Huko hakuna longolongo ni biashara tu
Lakini vilevile kuhalalisha biashara hii kunaweza kuwa na tija kubwa kwa jamii... Kama vile
. Kuwa na maeneo rasmi yanayotambulika
. Kuwa na vibali na leseni
. Kuwa na wahudumu... Ajira tayari
. Serikali kukusanya mapato
. Kuwa na ulinzi kwa watumiaji na watumiwaji
. Kupimwa afya na kufuata taratibu zote za kiafya...
Nknk
Kuendelea kuiharamisha hii biashara bila kuwa na sheria rasmi ni kuendelea kuinyanyasa jamii, kuikosesha uhuru, kuleta unyanyasaji na kufaidisha kundi fulani la watu kwa mapato haramu
Machangu wanapokamatwa huishia kushtakiwa kwa kosa la uzururaji.. Huwekwa mahabusu na kutakiwa kutoa pesa ili waachiwe... Wengine hutoa eneo la tukio, wengine hutoa wakifikishwa polisi, wengine hutoa baada ya kulala lupango na wale vigego hawatoi mpaka waachiwe huru
Tukiamua kwa dhati tunaweza sasa kuamua kuwa na mjadala huru kuhusu kuhalalisha hii biashara kongwe yenye wateja wengi wa kaliba zote
 
 
Walipe kodi hii biashara ni kongwe toka enzi za manabii wa Afrika na Asia..Chamsingi changudoa apimwe awe na afya nzuri pia afuate taratibu za afya anapoingia kwenye gegedo..Wapewe mashine za kodi vile vile wawe na sehemu maalum za kuuzia papuchi cha ziada wawe na bei elekezi ili mapato yajulikane..
 
Hii biashara kongwe duniani

Ova
Walipe kodi hii biashara ni kongwe toka enzi za manabii wa Afrika na Asia..Chamsingi changudoa apimwe awe na afya nzuri pia afuate taratibu za afya anapoingia kwenye gegedo..Wapewe mashine za kodi vile vile wawe na sehemu maalum za kuuzia papuchi cha ziada wawe na bei elekezi ili mapato yajulikane..
Na haina madhara kwa wengine tofauti na madawa ya kulevya[emoji144][emoji144][emoji144]
 
Mshana Jr hiyo sio biashara bali ni huduma.
Ni huduma inayopendwa na wote (wapewa huduma na watoa huduma)
Kilele cha furaha yao huambatana na bakhshishi (tip)
Sasa kuitoza kodi bakhshishi ni kinyume na kanuni za kodi.

Watu waachwe wajivinjari.
Nimekupata vema jogi lakini siku hizi huduma pia zinauzwa... Si unaona kule kwa manabii
Wanauza maji ya baraka
Wanauza mafuta ya upako
Wanauza leso za kukukinga nknk...
 
Hao wakina mama wanahudimia mbaka maboss wa serikali. Umefika muda iwe halali na wawe na eneo lao rasmi maana hii ni biashara kongwe kuliko siasa.
 
Nimekupata vema jogi lakini siku hizi huduma pia zinauzwa... Si unaona kule kwa manabii
Wanauza maji ya baraka
Wanauza mafuta ya upako
Wanauza leso za kukukinga nknk...
Kuitoza kodi bakhshishi ni kinyume na kanuni za kodi.

Huduma hii haiko na mfumo wa kulipishwa kodi, wanachokipata watoa huduma ni "marupurupu" kwa ajili ya kujikimu.
Faida waipatayo wapewa huduma ni kuondolewa msongo wa mawazo hivyo kuwa na utimamu kwenye kutekeleza majukumu yao ya kila siku.
 
Inaitwa biashara ila kihulasia sio biashara ni maisha binafsi ya watu ambayo serikali yenye mambo mengi ya msingi na muhimu haipaswi kujiuhusisha nayo kwani ni upotezaji wa muda na rasimali.
Akizungumza na waandishi wa habari Aprili 30 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es salaam, Lazaro Mambosasa amesema oparesheni hiyo jumla ya watuhumiwa 161 wanaojihusisha na biashara ya ukahaba walikamatwa, ambapo wanawake 118 wanaouza miili yao walikamatwa pia wamiliki wa madanguro 33 na wanunuzi wa biashara hiyo ambao ni wanaume 11 nao walikamatwa.

''Jeshi la Polisi linatoa onyo kali kwa wamiliki wote wa madanguro na machangudoa kuacha biashara hiyo maramoja kwani oparesheni hii ni endelevu na watakaokamatwa watachukuliwa hatua za kisheria'' aliongeza Kamanda Mambosasa

Serikali imewapa mwanya askari wake walinda raia kupata mapato haramu [emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116]
Walikamatwa wengi sana wengine waliachiwa jana asubuhi baada ya kutoa rushwa ya ngono na wengine walitoa elfu 20 kila mmoja...
Wale ambao walikua hawana hata mia halafu hawaridhishi kingono ndio hao 118 waliobakia...
Jamani nchi yangu hii mnaipeleka wapi?
[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
Nimekupata vema jogi lakini siku hizi huduma pia zinauzwa... Si unaona kule kwa manabii
Wanauza maji ya baraka
Wanauza mafuta ya upako
Wanauza leso za kukukinga nknk...
Kuna wanaodai ile hali ya kufanyika kwa kujificha ficha na kila aina ya usiri na makandokando kibao ni moja ya burudani zake. Wanasema kama ikiwa wazi bila mizunguko zunguko itapooza! Ni kama washabiki wengine wa kandanda wanavyodai mechi bila kutokea mijadala kuhusu e.g. makosa ya maamuzi ya refa na makandokando mengine inapooza!
 
Kuitoza kodi bakhshishi ni kinyume na kanuni za kodi.

Huduma hii haiko na mfumo wa kulipishwa kodi, wanachokipata watoa huduma ni "marupurupu" kwa ajili ya kujikimu.
Faida waipatayo wapewa huduma ni kuondolewa msongo wa mawazo hivyo kuwa na utimamu kwenye kutekeleza majukumu yao ya kila siku.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji120][emoji120][emoji123][emoji123][emoji123][emoji123][emoji123]
CC : Jeshi la polisi Tanganyika na Zenjibari
 
Back
Top Bottom