Uchaguzi 2020 Mizengwe mizengwe ya nini Uchaguzi Mkuu?

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,854
35,860
Uchaguzi ni mchakato unaoanzia kwenye kutia nia hadi angalau kutangazwa kwa mshindi.

Watia nia na hata wapiga kura wote ni wana wa nchi hii hii. Fitina, ufedhuli, chuki, pepo wachafu wachafu, uchawi uchawi, uonevu nk vya nini wakati sisi sote tu-watanzania?

Kweli haiwezekani kutendeana haki wakati kila siku tuko kwenye nyumba za ibada ati kuomba, kuombeana na hata kuliombea taifa hili kheri?

Hivi ni Mungu yupi huyu wa kupokea hizi sala zetu wakati kimsingi sisi wenyewe tu-majahili na waovu wakubwa tuliotayari kutoana roho bila hata ya simile?

Inakera mno kusikia kuwa ati kuna mgombea yeyote kazuiwa kugombea tena ikiwa hata kwa mzengwe mzengwe tu. Au ati kuwa kawekewa pingamizi la kijinga jinga tu ili asipate fursa ya kufika kwenye sanduku la kura.

Jidanganyeni. Ila Mungu anawaona na ufedhuli wenu wote unaozijaza nyoyo zenu. Kumbukeni yote yana mwisho.

Hofu yote hii ya kuwahofia washindani wenu inatoka wapi kama kweli nyie ndiyo mnaofaa sana kwa (mema yenu) kuwa washindi?

Kwa nini pawe na wagombea waliopita ati tu kwa sababu wengine wote walienguliwa ili kuwawezesha hawa kupita bila kupingwa? Mambo mengine haya mbona ni ya kutia kinyaa kwa kweli?

Atasikilizwa mno mgombea yeyote atakaye kuja na agenda yenye muarobaini wa kuondosha hizi janja janja, ghiliba ghiliba na ufedhuli yaliofanywa kuwa ni sehemu katika michakato ya chaguzi.

Hata kama tumeishi katika chaguzi zenye ufedhuli wa namna hii, angalau basi wajukuu wa wajukuu zetu yasiwakute haya, inshallah.

Kwa nini isiwe kuwa jitihada zote zifanyike ili kuwawezesha wagombea wote kukamilisha nia zao za kugombea kwa halali tu?

Kwa nini kupata nafasi ya kutumia vyombo vya habari kujitangaza ihusishwe na uwezo wa mgombea kifedha?



Uhalali wa kufanya kampeni kupitia vyombo vya habari kuwa ni fursa ya kiuchumi kwa vyombo vya habari inatoka wapi?

Tutakula vipi 'ubwabwa' kwa mipangilio ya kunadi sera kwa pesa ki hivi?

Fursa sawa katika kampeni zinapatikana vipi kama pana vyama vyenye TV, radio, na hata magazeti yao hali habari za wengine zikiminywa waziwazi kama tunavyoona?

Enyi wenye mamlaka kwa hakika mjitafakari.

Mko nayo nafasi ya kurekebisha mambo na historia haitawasahau:

Pongezi Sirro, Mahakama na Tume ya Uchaguzi kazi kwenu
 
Politics is an art of making personal interests to look like public interests.


Why do people fights, kills, abducts, humiliates in politics?

Answer is that politics is only place to accumulate wealth cheaply, si kweli kwamba watu wanapigana wakiwa na uchungu wa kukuletea wewe maendeleo hili halipo na wala halijawahi kuwepo siku zote.

Hata kama kwa macho yako utaona fulani kanunua ndege, kajenga flyover hii its for his own interests hata kama hivyo vitaonekana kuwa vitawanufaisha watu moja kwa moja au isiyo moja kwa moja.


Kuna wabunge wamekaa bungeni tangu mwaka 1980 hadi leo but hata kisima cha futi 1 hawajawahi kuwezesha uchimbaji wake, wao anachosubiri ni msimu wa kampeni wapite mitaani wakinunua pombe ili wananchi walewe akili ziwapotee wamchague tena arudi bungeni.
 
Jitahidi kusoma "novels" kwa wingi ili ka-English kanyooke. Correction: Why people fight, kill, abduct, humiliate others in politics? Haka ndiko ka-English kalikonyooka.
 
Siamini kama hiyo mikakati ya kupita bila kupingwa ni mkakati wa CCM maana Kama hao wa chini wakipita bila kupingwa maana yake majimbo yao hawatakuwa na muda wa kutangaza chama wala mgombea wa Raisi maana watajiona wameshinda kweli anayepanga huo ujinga anakiharibu chama, maana huwezi kupita nyumba kwa nyumba wakati ulishapata wagombea wako ukaeleweka.
 
Siamini kama hiyo mikakati ya kupita bila kupingwa ni mkakati wa CCM maana Kama hao wa chini wakipita bila kupingwa maana yake majimbo yao hawatakuwa na muda wa kutangaza chama wala mgombea wa Raisi maana watajiona wameshinda kweli anayepanga huo ujinga anakiharibu chama, maana huwezi kupita nyumba kwa nyumba wakati ulishapata wagombea wako ukaeleweka.

Mkuu inakuwa taabu kuwatenganisha na ubaradhuli huu hawa jamaa wa hiki chama. Ni wao tu wanaoushadadia, wanaoushangilia na wanaoupigia upatu vilivyo. Hakuna wanapo ukemea wala kuulaani. Hawana tatizo nao.

Kingine ni kuwa chama kinacho nufaika na wagombea wa hivi ni wao tu. Hakuna hata sehemu moja waliko athirika nao hata kidogo.

Inawezekana namna gani?

Mbona hakuna hata mmoja japo wa chauma aliyepita bila kupingwa angalau ili nasi tukaanza kujipanga panga kujilia ubwabwa wetu japo kwa uma?
 
Ndiyo hivyo unapokuwa kwenye madaraka ukweli huuoni ukitoka ndiyo unauona, hata hayati mzee Mkapa aliona tunafaa kuwa na tume huru lkn ndiyo akawa hana tena mamlaka.
 
ndiyo hivyo unapokuwa kwenye madaraka ukweli huuoni ukitoka ndiyo unauona, hata hayati mzee Mkapa aliona tunafaa kuwa na tume huru lkn ndiyo akawa hana tena mamlaka.

Eeh mola wetu ukawajalie hawa walioko madarakani leo hekima ya kutambua kuwa kuwapenda na kuwasikiliza wanaowadhania ni maadui zao haswaa, ndiyo yaliyo maagizo thabiti kutoka kwako.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom