Mizania ya haki; Kile alichopaswa kufanya Makamba jr

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,775
699,200
9238e9bbe945e16083d6298943955f24.jpg
Nimemtaja yeye kama mhusika mkuu kutokana na nyazifa zake kisiasa, nafasi yake katika jamii na historia yake kwenye uwanja wa siasa na maamuzi mengi yaliyotokana na yeye...kwenye hii skendo iliyoko kwenye hatua za tuhuma yeye ndio muathirika mkuu...kwahiyo busara uvumilivu mkubwa akili iliyo sharp na werevu vilihitajika sana kipindi hiki
Hii ni vita yenye pande nyingi na wapambe wengi...mbinu bora zinahitajika ili kuweza kushinda vita
Vyovyote vile iwavyo kuna kufahamiana kwa karibu kati ya watatu hawa January Mwamvita na muitaliano na kwa vyovyote kulikuwa na makubaliano fulani fulani yaliyohusisha pesa nyingi (za rushwa?)ahadi za upendeleo kwenye mambo fulani nk nk
Kwa kulifahamu hili na zile tambo za bibie Kimange...kwamba ana lundo la ushahidi wa kila aina, Makamba hakupaswa kujibu lolote kwasasa...angekaa kimya akinote kila kitu yakiwemo malumbano ya mitandaoni, angesubiri walau kwa siku kadhaa aone kimange anajua kiasi gani
Kuwalipa haraka haraka vijana wa mtandaoni wakanushe kijinga kabisa na yeye kukimbilia kukanusha kumempa kimange credit moja kubwa sana
Kimange anajulikana alivyo mchokonozi na mdaku, hivyo mpaka jana jioni watu walikuwa hawamuamini kivile na hakukuwa na post nyingi...lakini baada tu ya watuhumiwa kuongea na kukiri baadhi ya mambo mjadala ukageuka mwelekeo na post zikaongezeka maradufu....!
Makamba kama kiongozi aliyekuwa msaidizi wa rais (nafasi kubwa sana hii) alipaswa kuwa na subra katika hili ili mihemko kwenye mitandao ipoe apate pa kuanzia
Bahati mbaya sana the guilty are afraid hiyo ni kanuni ya maisha...alipaniki kwa kuguswa pabaya bila maandalizi
Wakati ushahidi na ukweli ndio vitaleta mizania ya haki...lakini mpaka tutakapofika huko Makamba atakuwa sio huyu tena....!
e7f4f4799bac872b7325d9ed1eb562cc.jpg
 
Amesahau, palipo na uchafu, msafi huchafuka zaidi. Anachokifanya ni sawa na kupaka mafuta bila kuoga, mange ni daraja tu, maana data zote analetewa, kuendelea kubishana nae kushinda ni ngumu, coz Makambaz walishapataga kashfa ktk uchaguzi wa 2010 ya bidada kuhongwa hela na watu wa BARICK GOLD ili kakaa akishinda ubunge arahjsishe madili yao maana waliamini atakuwa waziri. Sasa ukijumlisha na hili, hapo kutumia magazijuto ni kutaka kuzunguka tuu, issue iliopo ni kujumlisha na kutoa tuu hakuna hesabu nyngne inayohitajika kwa mwenye akili za tafakari.
 
Hii kitu kabla ya kukimbilia kwenye mitandao na kukanusha kizembe angewatafuta wanasheria na watu wengine wenye uelewa na uzoefu zaidi kumzidi wakae chini watafakari kwa pamoja....awe mkweli kwao wafuatilie mjadala kimya kimya kisha wajipange... lakini J akaona hili analimudu...!hakuna kitu kibaya kwenye maisha kama kudhani unajua kuliko wengine
 
Ukimya ni jibu.tunampa haki anayesema, kama anayesemwa kakaa kimya.
Tuamini kwamba Mange yupo sahihi.
 
Huyu makamba alivotoka na kukiri imewaaminisha watu kuwa ni kweli wamehusika. Kwenye life lazima kujipanga kabla ya kujibu. Mange watu walijua mzusji ila walivojibu ndo basi tena bora sasa wapige kimya kwanza
 
Hivi hii kitu ya Msoga kweli?
Mwanzoni mwa wiki hii aliutukana utawala wa kikwete kuwa ulijaa kulindana, wakati yeye alikuwa sehemu ya utawala huo na maovu yake mengi yanajulikana kwa Kikwete....ni mwendawazimu tu ambaye angemwacha dogo atambe
 
Angewahi haraka mahakamani kabla Mange hajaendelea kuyatoa hayo makombora mengine aliyoyaahidi.
 
Hii kitu kabla ya kukimbilia kwenye mitandao na kukanusha kizembe angewatafuta wanasheria na watu wengine wenye uelewa na uzoefu zaidi kumzidi wakae chini watafakari kwa pamoja....awe mkweli kwao wafuatilie mjadala kimya kimya kisha wajipange... lakini J akaona hili analimudu...!hakuna kitu kibaya kwenye maisha kama kudhani unajua kuliko wengine
Walipanic mno huyo mange watu walishampuuza sasa alivotoka kujibu bila kujipanga yeye na dadake ndo wakachochea moto. Si vtu vyote hutakiwa kukanushwa Mara moja ushauri wa wengine muhimu
 
Hapa ndipo ninapopata shida mimi. Kama JPM aliamini kuwa watu alionao kwenye baraza la mawaziri ndio wazuri na wasafi zaidi ya watu wengine kwenye CCM, sasa hali ikiwa hivi itafika muda atakuja jikuta yuko peke yake maana wasaidizi wake wote watakuja jikuta wana skendo za rushwa na ufisadi. JE TUTAFIKA?
 
Back
Top Bottom