Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,341
- 51,907
MIUNGU YETU ILISHINDWA, MIZIMU YETU IKAPIGWA, SASA TUMEKUWA JAMII ILIYOANGUKA NA HATUNA TUMAINI TENA LA KUSIMAMA.
Anàandika, Robert Heriel
Mtibeli.
Mila zetu, Desturi zetu, tamaduni zetu, utambulisho wetu na kila kilichokuwa chetu kiliitwa Potofu baada ya kushindwa.
Upotofu upo kwa walioshindwa. Kama tungeshinda katika vita Ile wala istilahi "POTOFU” Isingesikika.
Ni potofu kwa sababu tulishindwa.
Miungu ya Mababu zetu ilishindwa vibaya katika vita ya miungu "god's War" sijajua nini kilipelekea kushindwa kwao. Bado najiuliza.
Je Haikuwa na nguvu ya kutosha kukabiliana na Miungu ya kigeni?
Je Haikuwa na akili na mbinu kabambe za kuwashinda maadui?
Nini kilitokea mpaka Anguko kuu la kutisha lilipotokea ambalo limedumu mpaka leo na hatujui litaendelea mpaka Lini.
Miungu ikishapigwa waumini hawana ujanja tena.
Wakati Ukristo na uislamu unaingia Afrika Wazee na Babu zetu walipambana vilivyo kuukataa kwa nguvu zote lakini ninawasiwasi Miungu yao haikuwapa sapoti ya kutosha kukabiliana na ugeni Ule mbaya.
Au miungu ile ilitoa sapoti lakini haikuwa na nguvu kushinda Maadui waliokuja.
Hatuwezi kusema Waafrika walisaliti miungu yao. Ila ninachokiona ni kuwa miungu ya kiafrika ilizidiwa na haikuwa na nguvu ya kutosha kukabiliana na miungu ya kigeni.
Nakumbuka mpaka nazaliwa zilikuwepo jitihada mbalimbali za wazee wetu wakijitahidi kufurukuta kujaribu kupambana na ujio wa wageni na miungu yao lakini walikuwa wanapambana wakiwa wameshashindwa kwani miungu yao ilikuwa aidha imekimbia au imetekwa au pengine hata kuuawa na miungu ya kigeni.
Miungu ndio imebeba mila, desturi, tamaduni na utambulisho wa jamii husika. Sasa kitendo cha miungu hiyo kupigwa Katiak vita na kufukuzwa au kuangamizwa kabisa kunaiathiri na kuua kabisa desturi , mila na tamaduni ya jamii zao.
Ni mila potofu kwa sababu miungu hiyo imeshindwa.
Ni mila potofu kwa sababu miungu hiyo haina nguvu na haina vigezo na uhalali wa kuitwa miungu.
Ni mila potofu kwa sababu miungu hiyo imeshindwa kutetea Watu wake.
Ni mila potofu kwa sababu miungu hiyo imeshindwa kulinda rasilimali za himaya zao mpaka zinaibiwa na wageni.
Ni mila potofu kwa sababu, miungu hiyo imeshindwa kuwapa Watu wake Akili na kutatua kero na changamoto za jamii yao ikiwemo Umaskini na ujinga.
Miungu na mizimu yako inaposhindwa hauna chochote utakachofanya zaidi ya kujisalimisha kwa miungu ya kigeni.
Ni pigo takatifu ambalo kunyanyuka haiwezekaniki.
Vita ya Miungu, waafrika walipoteza na hatujui miungu yetu ilikimbia, au ipo mateka au iliuawa.
Nyota ya matumaini ya Ukombozi haipo kwa sababu huwezi kukomboa jamii au taifa pasipo Miungu ya kwenu.
Acha Nipumzike sasa.
Nawatakia maandalizi mema ya Sabato.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Anàandika, Robert Heriel
Mtibeli.
Mila zetu, Desturi zetu, tamaduni zetu, utambulisho wetu na kila kilichokuwa chetu kiliitwa Potofu baada ya kushindwa.
Upotofu upo kwa walioshindwa. Kama tungeshinda katika vita Ile wala istilahi "POTOFU” Isingesikika.
Ni potofu kwa sababu tulishindwa.
Miungu ya Mababu zetu ilishindwa vibaya katika vita ya miungu "god's War" sijajua nini kilipelekea kushindwa kwao. Bado najiuliza.
Je Haikuwa na nguvu ya kutosha kukabiliana na Miungu ya kigeni?
Je Haikuwa na akili na mbinu kabambe za kuwashinda maadui?
Nini kilitokea mpaka Anguko kuu la kutisha lilipotokea ambalo limedumu mpaka leo na hatujui litaendelea mpaka Lini.
Miungu ikishapigwa waumini hawana ujanja tena.
Wakati Ukristo na uislamu unaingia Afrika Wazee na Babu zetu walipambana vilivyo kuukataa kwa nguvu zote lakini ninawasiwasi Miungu yao haikuwapa sapoti ya kutosha kukabiliana na ugeni Ule mbaya.
Au miungu ile ilitoa sapoti lakini haikuwa na nguvu kushinda Maadui waliokuja.
Hatuwezi kusema Waafrika walisaliti miungu yao. Ila ninachokiona ni kuwa miungu ya kiafrika ilizidiwa na haikuwa na nguvu ya kutosha kukabiliana na miungu ya kigeni.
Nakumbuka mpaka nazaliwa zilikuwepo jitihada mbalimbali za wazee wetu wakijitahidi kufurukuta kujaribu kupambana na ujio wa wageni na miungu yao lakini walikuwa wanapambana wakiwa wameshashindwa kwani miungu yao ilikuwa aidha imekimbia au imetekwa au pengine hata kuuawa na miungu ya kigeni.
Miungu ndio imebeba mila, desturi, tamaduni na utambulisho wa jamii husika. Sasa kitendo cha miungu hiyo kupigwa Katiak vita na kufukuzwa au kuangamizwa kabisa kunaiathiri na kuua kabisa desturi , mila na tamaduni ya jamii zao.
Ni mila potofu kwa sababu miungu hiyo imeshindwa.
Ni mila potofu kwa sababu miungu hiyo haina nguvu na haina vigezo na uhalali wa kuitwa miungu.
Ni mila potofu kwa sababu miungu hiyo imeshindwa kutetea Watu wake.
Ni mila potofu kwa sababu miungu hiyo imeshindwa kulinda rasilimali za himaya zao mpaka zinaibiwa na wageni.
Ni mila potofu kwa sababu, miungu hiyo imeshindwa kuwapa Watu wake Akili na kutatua kero na changamoto za jamii yao ikiwemo Umaskini na ujinga.
Miungu na mizimu yako inaposhindwa hauna chochote utakachofanya zaidi ya kujisalimisha kwa miungu ya kigeni.
Ni pigo takatifu ambalo kunyanyuka haiwezekaniki.
Vita ya Miungu, waafrika walipoteza na hatujui miungu yetu ilikimbia, au ipo mateka au iliuawa.
Nyota ya matumaini ya Ukombozi haipo kwa sababu huwezi kukomboa jamii au taifa pasipo Miungu ya kwenu.
Acha Nipumzike sasa.
Nawatakia maandalizi mema ya Sabato.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam