Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,720
- 21,779
Na Mussa Mkama
HATIMAYE mtambo mmoja wa kufua megawati 10 za umeme wa kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), umewashwa jana na kuingizwa kwenye gridi ya taifa.
Mtambo huo ni kati ya mitambo kumi ya IPTL inayofanyiwa matengenezo na kampuni kandarsi ya Wartsila kwa ajili ya kutoa jumla ya megawati 100 za umeme.
"Tayari megawati kumi zimeshaingizwa kwenye gridi ya taifa na hii ni kutokana na kuwashwa kwa mtambo mmoja baada ya kukamilika kwa matengenezo," alisema meneja mkuu wa IPTL, Dk Magesvaran Subramaniam.
Kukamilika kwa mtambo huo kunatokana na juhudi za mafundi wa hapa nchini wakishirikiana na wengine kutoka Uhoranzi.
Alisema kuwa mtambo huo uliwashwa jana (juzi) usiku, lakini kwa bahati mbaya ukazima kutokana na hitilafu za kiufundi na sasa umewashwa tena na unaendelea kufanya kazi bila matatizo.
Tathmini ya mafundi na wataalam hao inaonyesha kuwa mitambo hiyo haina ubovu mkubwa hivyo kuna matumaini ya kuwashwa kwa mashine zote kwa awamu baada ya mafanikio ya mtambo huo namba moja.
"Mafundi wanaendelea na juhudi ya kuhakikisha mitambo yote inawashwa kwa kufanyia matengenezo na kukagua mtambo mmoja mmoja kwa umakini ili kuhakikisha kuwa ikikamilika na kuwashwa haisababishi matatizo madogo madogo" alisema Subramaniam.
"Kukamilika kwa mtambo huo ni ishara nzuri ya kuendelea kukamilika kwa mingine tisa iliyobaki."
Kuwashwa kwa mtambo huo ni kielelezo tosha kwa wananchi kuwa maumivu ya mgao ulioanza Septemba kuisha hivi karibuni.
Mtambo huo umewashwa zikiwa zimepita siku 18 tangu Rais Jakaya Kikwete aagize kuwashwa mara moja kwa mitambo ya kampuni hiyo iliyo katika mgogoro na serikali kiasi cha kupelekana mahakamani.
Kikwete aliingilia kati tatizo la umeme Oktoba 20 baada ya makali ya mgawo kuzidi na kusababisha wananchi na wafanyabiashara kumtaka afanye hivyo. Baada ya agizo lake, ilitangazwa kuwa mitambo hiyo ingewashwa Novemba mosi, lakini ilibainika baadaye kuwa serikali haikuwa imeilipa IPTL na hivyo matengenezo ya mitambo kuchelewa.
Mitambo hiyo ilifungwa nchini mwaka 1998, lakini serikali ikaamua kutoitumia kutokana na gharama za uzalishaji na kuagiza kampuni hiyo iangalie uwezekano wa kuibadili ili iendeshwe kwa kutumia nguvu za gesi na hivyo kupunguza makali ya bei.
Hata hivyo, IPTL ilifungua kesi nchini Marekani ikidai kulipwa gharama za uzalishaji, huku utekelezaji wa agizo la kuigeuza mitambo hiyo ili iwe inatumia gesi asilia likionekana kusuasua.
Mgao wa umeme wa safari hii umetokana na kuharibika kwa mtambo wa kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia wa kampuni Songas na mingine miwili ya kuzalisha umeme kwa kutumia nguvu ya maji iliyo kwenye mabwawa ya Kihansi na Pangani.
Sababu nyingine ilielezwa kuwa ni kupungua kwa uzalisha umeme kwenye mabwawa ya Kihansi, Hale na Pangani kulikotokana na kupungua kwa kiwango cha maji.
HATIMAYE mtambo mmoja wa kufua megawati 10 za umeme wa kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), umewashwa jana na kuingizwa kwenye gridi ya taifa.
Mtambo huo ni kati ya mitambo kumi ya IPTL inayofanyiwa matengenezo na kampuni kandarsi ya Wartsila kwa ajili ya kutoa jumla ya megawati 100 za umeme.
"Tayari megawati kumi zimeshaingizwa kwenye gridi ya taifa na hii ni kutokana na kuwashwa kwa mtambo mmoja baada ya kukamilika kwa matengenezo," alisema meneja mkuu wa IPTL, Dk Magesvaran Subramaniam.
Kukamilika kwa mtambo huo kunatokana na juhudi za mafundi wa hapa nchini wakishirikiana na wengine kutoka Uhoranzi.
Alisema kuwa mtambo huo uliwashwa jana (juzi) usiku, lakini kwa bahati mbaya ukazima kutokana na hitilafu za kiufundi na sasa umewashwa tena na unaendelea kufanya kazi bila matatizo.
Tathmini ya mafundi na wataalam hao inaonyesha kuwa mitambo hiyo haina ubovu mkubwa hivyo kuna matumaini ya kuwashwa kwa mashine zote kwa awamu baada ya mafanikio ya mtambo huo namba moja.
"Mafundi wanaendelea na juhudi ya kuhakikisha mitambo yote inawashwa kwa kufanyia matengenezo na kukagua mtambo mmoja mmoja kwa umakini ili kuhakikisha kuwa ikikamilika na kuwashwa haisababishi matatizo madogo madogo" alisema Subramaniam.
"Kukamilika kwa mtambo huo ni ishara nzuri ya kuendelea kukamilika kwa mingine tisa iliyobaki."
Kuwashwa kwa mtambo huo ni kielelezo tosha kwa wananchi kuwa maumivu ya mgao ulioanza Septemba kuisha hivi karibuni.
Mtambo huo umewashwa zikiwa zimepita siku 18 tangu Rais Jakaya Kikwete aagize kuwashwa mara moja kwa mitambo ya kampuni hiyo iliyo katika mgogoro na serikali kiasi cha kupelekana mahakamani.
Kikwete aliingilia kati tatizo la umeme Oktoba 20 baada ya makali ya mgawo kuzidi na kusababisha wananchi na wafanyabiashara kumtaka afanye hivyo. Baada ya agizo lake, ilitangazwa kuwa mitambo hiyo ingewashwa Novemba mosi, lakini ilibainika baadaye kuwa serikali haikuwa imeilipa IPTL na hivyo matengenezo ya mitambo kuchelewa.
Mitambo hiyo ilifungwa nchini mwaka 1998, lakini serikali ikaamua kutoitumia kutokana na gharama za uzalishaji na kuagiza kampuni hiyo iangalie uwezekano wa kuibadili ili iendeshwe kwa kutumia nguvu za gesi na hivyo kupunguza makali ya bei.
Hata hivyo, IPTL ilifungua kesi nchini Marekani ikidai kulipwa gharama za uzalishaji, huku utekelezaji wa agizo la kuigeuza mitambo hiyo ili iwe inatumia gesi asilia likionekana kusuasua.
Mgao wa umeme wa safari hii umetokana na kuharibika kwa mtambo wa kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia wa kampuni Songas na mingine miwili ya kuzalisha umeme kwa kutumia nguvu ya maji iliyo kwenye mabwawa ya Kihansi na Pangani.
Sababu nyingine ilielezwa kuwa ni kupungua kwa uzalisha umeme kwenye mabwawa ya Kihansi, Hale na Pangani kulikotokana na kupungua kwa kiwango cha maji.