Sexer
JF-Expert Member
- Oct 22, 2014
- 8,505
- 8,256
Katika hali ya kusikitisha polisi wilayani Missungwi wamempiga hadi kufa kijana mmoja mtoto wa aliyekuwa mwenyekiti wa CHADEMA wilaya hiyo kamanda Dickson, kosa la kijana huyo ni kwenda kituo cha polisi kutoa taarifa za ugomvi uliokuwa umetokea kwenye guest house moja hapo Missungwi, cha kusikitisha na kushangaza polisi badala ya kupokea taarifa na kuzifanyia kazi walianza kumpiga kijana huyo na baadae kumpeleka hospitali ambapo ilibainika tayari keshafariki.
BABA WA MAREHEMU AKATAA KUZIKA MAITI
Katika hali nyingine baba wa marehemu bwana Dickson pamoja na ndugu wengine na Nzengo pia wamegoma kuichukua maiti hospitali na kwenda kuizika hatua ambayo ilisababisha RC Magesa Mulongo kwenda kushughulikia suala hilo kwa kuongea na ndugu pamoja na Nzengo hatua ambayo iligonga mwamba.
MTOTO MDOGO APATA ULEMAVU WA MAISHA
Katika hali nyingine ambayo mimi binafsi imenisikitisha zaidi, mtoto mmoja mwanafunzi wa shule ya msingi amesababishiwa ulemavu wa maisha na polisi hao wa Tanzania, baada ya Nzengo kujua kijana kafariki kwa kupigwa na polisi, Nzengo ilichachamaa na kuandamana kuelekea kituoni ndipo askari hao wakaitana na wenzao kutoka Mwanza Mjini na kuja kupiga mabomu hovyo hovyo kana kwamba hawana taaluma yoyote ya mambo hayo hapo ndipo kiliruka kitu kutoka kwenye mabomu hayo na kumpata mtoto huyo jichoni na kusababisha jicho la mtoto huyo kutoka, inasikitisha kwa kweli.
Hivi sasa mtoto huyo wa darasa la pili tena binti ndio tayari kawa na kilema cha kudumu maisha yake yote kisa polisi wapuuzi, huruma.
BABA WA MAREHEMU AKATAA KUZIKA MAITI
Katika hali nyingine baba wa marehemu bwana Dickson pamoja na ndugu wengine na Nzengo pia wamegoma kuichukua maiti hospitali na kwenda kuizika hatua ambayo ilisababisha RC Magesa Mulongo kwenda kushughulikia suala hilo kwa kuongea na ndugu pamoja na Nzengo hatua ambayo iligonga mwamba.
MTOTO MDOGO APATA ULEMAVU WA MAISHA
Katika hali nyingine ambayo mimi binafsi imenisikitisha zaidi, mtoto mmoja mwanafunzi wa shule ya msingi amesababishiwa ulemavu wa maisha na polisi hao wa Tanzania, baada ya Nzengo kujua kijana kafariki kwa kupigwa na polisi, Nzengo ilichachamaa na kuandamana kuelekea kituoni ndipo askari hao wakaitana na wenzao kutoka Mwanza Mjini na kuja kupiga mabomu hovyo hovyo kana kwamba hawana taaluma yoyote ya mambo hayo hapo ndipo kiliruka kitu kutoka kwenye mabomu hayo na kumpata mtoto huyo jichoni na kusababisha jicho la mtoto huyo kutoka, inasikitisha kwa kweli.
Hivi sasa mtoto huyo wa darasa la pili tena binti ndio tayari kawa na kilema cha kudumu maisha yake yote kisa polisi wapuuzi, huruma.