Lady Whistledown
JF-Expert Member
- Aug 2, 2021
- 1,024
- 1,618
Misungwi. Wakati mamlaka nchini Kenya kutambua makaburi waliozikwa waumini wa Mchungaji, Paul Mackenzie, Mkuu wa Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza, Paulo Chacha ameibaini kuwepo kwa kanisa linaloendesha ibada tata.
Chacha amebaini kuwepo kanisa hilo juzi Juni 8,2023 katika Kijiji cha Nyamayinza Kata ya Gulumungu wilayani humo ambapo alisema kanisa hilo linamilikiwa na William Masuma na mkewe, Kabula Lushika.
Alisema wamebaini kuwepo wagonjwa zaidi ya 200 waliolazwa na kupatiwa matibabu katika mazingira duni huku akiagiza Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi ili kubaini iwapo kuna wagonjwa waliofariki na kuzikwa eneo hilo kinyemela.
Hata hivyo akizungumza chini ya ulinzi wa Polisi, William Masuma alisema pamoja na kuwa na kibali cha kutoa huduma ya Tiba Asili, katika eneo hilo anatoa huduma ya maombezi kwa wagonjwa pekee.
Chacha amebaini kuwepo kanisa hilo juzi Juni 8,2023 katika Kijiji cha Nyamayinza Kata ya Gulumungu wilayani humo ambapo alisema kanisa hilo linamilikiwa na William Masuma na mkewe, Kabula Lushika.
Alisema wamebaini kuwepo wagonjwa zaidi ya 200 waliolazwa na kupatiwa matibabu katika mazingira duni huku akiagiza Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi ili kubaini iwapo kuna wagonjwa waliofariki na kuzikwa eneo hilo kinyemela.
Hata hivyo akizungumza chini ya ulinzi wa Polisi, William Masuma alisema pamoja na kuwa na kibali cha kutoa huduma ya Tiba Asili, katika eneo hilo anatoa huduma ya maombezi kwa wagonjwa pekee.