Paul Alex
JF-Expert Member
- Jul 14, 2012
- 4,240
- 9,527
- Thread starter
- #141
Nina vitabu viwili vya ROBIN SHARMA
1. THE MONK WHO SOLD HIS FERRARI
2. DISCOVER YOUR DESTINY
Mungu akinipa nafasi nitaviweka kwenye jukwaa hili..
Naamini vitakuwa msaada sana kwa watu wengi...
Kuna mahali anazungumzia;
※ watu wenye mapungufu wasioyajua.
※watu wenye mapungufu wanayoyajua ila wasiojua namna ya kukabiliana nayo.
※watu wenye mapungufu wanayoyajua na wanajitahidi kukabiliana nayoa japo kwa njia zisizo na uhakika sana.
※watu wenye mapungufu na wanayafahamu na wanafahamu kwa hakika ni njia gani wazitumie kuyakabili na wanayakabili kwa umahiri mkubwa.
Nadhani sisi wote tuko kwenye moja ya hizo hatua.. tukipata muongozo mzuri tunaweza kuacha haya mambo ya kulipuka.
Kimsingi mtu anayewalipukia wengine kila wakati ana msongo mkubwa wa mawazo, hafurahii maisha yake kwasababu moja au nyingine... ameipoteza nafsi yake na hajitambui tena..
Ila akipata muongozo na akawa tayari kubadilisha matendo na tabia ili kurudia nafsi yaka safi na yenye amani na furaha aliyozaliwa nayo, basi mtu huyo atayafurahia maisha yake na itakuwa rahisi sana kuziona fursa na kutimiza ndoto za maisha yake.