Aramun
JF-Expert Member
- Nov 8, 2023
- 254
- 1,092
Asilimia 90 ya watumishi wa umma Tanzania ni wa daraja la kati, wengi ni walio na diploma. Mishahara ghafi yao ina range laki 6 mpaka laki 8.
Baada ya makato, wanaondoka na kama laki 5. Hapo ni kwa wale ambao hawana mikopo. Ukijumlisha mikopo (ambao wengi wanayo) utakuta mtumishi anaondoka na laki 2, 3. Ukiangalia salary slip ya mtumishi wa umma wa sasa unaweza usiamini hayo makato yaliyomo humo ndani.
Utumishi wa umma wa sasa si kama wa zamani. Zamani watumishi wa umma ndiyo walikuwa wanaonekana wana chochote kitu mtaani. Ila kwa sasa watumishi wa umma ndiyo wamegeuka wasio na chochote mitaani. Wengi wanaishi kwa msaada wa mkopo wa mangi.
Mtumishi wa umma wa sasa anashindwa pesa hadi na boda boda. Kama boda boda anaingiza mkwanja mrefu zaidi kumshinda mtumishi wa umma tunategemea nini kama nchi? Thamani ya utumishi wa umma inabidi ilindwe.
Kama hadhi ya utumishi wa umma haitalindwa, basi tusitegemee watumishi wa umma ku-deliver vile inavyotakiwa, na kwa sababu ya mishahara kiduchu tutegemee hizo ripoti za CAG zikiendelea kuwa chafu kwa ubadhirifu wa pesa za miradi.
Pamoja na mishahara kiduchu ila serikali ikaona iwawekee na kikokotoo kiduchu kwenye kiinua mgongo. Yani ni full mateso.
Kingine kinachotia hasira ni kwamba wanasiasa wao wamejiwekea mishahara minono, na marupurupu lukuki. Na wakistaafu wanachukua viinua mgongo vyao kama vilivyo tena on time.
Baada ya makato, wanaondoka na kama laki 5. Hapo ni kwa wale ambao hawana mikopo. Ukijumlisha mikopo (ambao wengi wanayo) utakuta mtumishi anaondoka na laki 2, 3. Ukiangalia salary slip ya mtumishi wa umma wa sasa unaweza usiamini hayo makato yaliyomo humo ndani.
Utumishi wa umma wa sasa si kama wa zamani. Zamani watumishi wa umma ndiyo walikuwa wanaonekana wana chochote kitu mtaani. Ila kwa sasa watumishi wa umma ndiyo wamegeuka wasio na chochote mitaani. Wengi wanaishi kwa msaada wa mkopo wa mangi.
Mtumishi wa umma wa sasa anashindwa pesa hadi na boda boda. Kama boda boda anaingiza mkwanja mrefu zaidi kumshinda mtumishi wa umma tunategemea nini kama nchi? Thamani ya utumishi wa umma inabidi ilindwe.
Kama hadhi ya utumishi wa umma haitalindwa, basi tusitegemee watumishi wa umma ku-deliver vile inavyotakiwa, na kwa sababu ya mishahara kiduchu tutegemee hizo ripoti za CAG zikiendelea kuwa chafu kwa ubadhirifu wa pesa za miradi.
Pamoja na mishahara kiduchu ila serikali ikaona iwawekee na kikokotoo kiduchu kwenye kiinua mgongo. Yani ni full mateso.
Kingine kinachotia hasira ni kwamba wanasiasa wao wamejiwekea mishahara minono, na marupurupu lukuki. Na wakistaafu wanachukua viinua mgongo vyao kama vilivyo tena on time.