Princemwalejr
JF-Expert Member
- Nov 9, 2017
- 496
- 488
Kwanza niseme mimi sina kadi ya chama chochote cha siasa. Ila ni mkereketwa wa bendera ya Tanzania.
Hakuna kitu kinanikera kama tabia ya wabunge kusimamia ya vyama vyao na kusahau ya taifa. Kuna wabunge wazuri sana wa kupinga ufisadi. Lakini hutawasikia wakimzogoa fisadi kama yuko kwenye chama chao.
Kwenye hili la mishahara ni kama wote kwa mpigo bila ya kujali vyama vyao wameamua kulikalia kimya. Katika nchi ambayo polisi mwenye shahada ya sheria analipwa laki sita kwa mwezi hesabu ya kuwalipa wabunge zaidi ya milioni nane kwa mwezi imetoka wapi?
Kuna watumishi wa serikali wako kazini zaidi ya miaka thelathini mishahara yao haijafifikia milioni. Na mafao yao wakistaafu yanaweza yasifikie huo mshahara wa mwaka wa mbunge mmoja.
Wengi wa watanzania wanateseka kwa kukosa bima. Nimeshuhudia waliorudi nyumbani kusubiri kufa kwa kukosa bima. Wabunge wao wana utaratibu wa kutibiwa nje kwa fedha za wavuja jasho.
Hivi kweli utaweza kuwakilisha wenye shida iwapo wewe hujui shida?
Wako wapi wale wabunge wasemaji wazuri hawaoni kuwa mishahara yao imekaa kifisadi? Na bado wanapewa posho za vikao. Hii haijatulia ni ya kukemewa vikali na wakereketwa wa bendera ya Tanzania.
Mungu ibariki Tanzania
Hakuna kitu kinanikera kama tabia ya wabunge kusimamia ya vyama vyao na kusahau ya taifa. Kuna wabunge wazuri sana wa kupinga ufisadi. Lakini hutawasikia wakimzogoa fisadi kama yuko kwenye chama chao.
Kwenye hili la mishahara ni kama wote kwa mpigo bila ya kujali vyama vyao wameamua kulikalia kimya. Katika nchi ambayo polisi mwenye shahada ya sheria analipwa laki sita kwa mwezi hesabu ya kuwalipa wabunge zaidi ya milioni nane kwa mwezi imetoka wapi?
Kuna watumishi wa serikali wako kazini zaidi ya miaka thelathini mishahara yao haijafifikia milioni. Na mafao yao wakistaafu yanaweza yasifikie huo mshahara wa mwaka wa mbunge mmoja.
Wengi wa watanzania wanateseka kwa kukosa bima. Nimeshuhudia waliorudi nyumbani kusubiri kufa kwa kukosa bima. Wabunge wao wana utaratibu wa kutibiwa nje kwa fedha za wavuja jasho.
Hivi kweli utaweza kuwakilisha wenye shida iwapo wewe hujui shida?
Wako wapi wale wabunge wasemaji wazuri hawaoni kuwa mishahara yao imekaa kifisadi? Na bado wanapewa posho za vikao. Hii haijatulia ni ya kukemewa vikali na wakereketwa wa bendera ya Tanzania.
Mungu ibariki Tanzania