Mishahara ya wabunge itathminiwe upya

Mishahara ya wabunge itathminiwe upya

Kwani mbunge ni mwanasiasa au ni mfanyakazi?!!

Tangu lini Kiongozi akawa sawa kimaslahi na mtu wa kawaida?!!

Kama ulisoma boarding miaka hiyo hukumbuki kuwa viranja wa shule ndio waliokuwa wanakula vipande vingi vya nyama kuliko wanafunzi ambao sio viongozi?
Wewe ni mbunge wa jimbo gani?
 
Wanahangaika kupunguza wage bills kwa kudhulumu wanyonge, ati ni darasa la saba hana sifa za kuajiri. Huu ni ubaguzi wa dhahiri mfagizi wa ofisi na fomu 4 inasaidiaje utendaji kazi wake. Msukule Msukuma na Mchawi Majimarefu wana zaidi ya daktari mwenye digrii ya Phd, huu ni ufisadi wa kiasi gani?. Tunapumua kwa kutukana maana uvumilivu umefika mwisho!
You've made my day...a very sensitive comment.
 
hapo ndo mi hukumbuka msemo mmoja nlioupata sehemu ukisema "democracy is hypocracy".yaan demokrasia imejaa full unafki.ila ndo hivyo huenda tukaja kuwa na serikali inayowajali wananchi wake kwa hali ya juu.
 
Hoja yako ni nzuri, ila tatizo ni sheria aliyoitunga Mkapa Mwaka 1999.

'Political Service Retirement Benefits Act, 1999'; inayohusu pensheni za viongozi wa kisiasa: Rais, Makamu wa Rais, Spika na Naibu wake, Waziri Mkuu.

Chini ya sheria hii mambo yafuatayo yalilifunga Bunge:

1. Ni lazima Bunge lipitie upya viwango vya Pensheni za wakubwa hao kila baada ya miaka mitano kwa lengo la KUZIONGEZA.

2. Kiwango cha pensheni ya Rais mstaafu ni 80% ya mshahara wa Rais aliyepo madarakani.

3. Ili kukidhi matakwa ya 1. hapa juu lazima Bunge liongeze mshahara wa Rais aliyepo madarakani.

4. Kwa mujibu wa Katiba ya JMT 1977; Rais ni sehemu ya Bunge. Hivyo mshahara wake ukiongezwa; chini ya Sheria na 2. ya 1999 mishahara ya wengine waliotajwa hapo juu; pamoja na wabunge, ITAPANDISHWA.

Katika mazingira ya kikatiba na kisheria kama hayo hapo juu; mabadiliko kwenye maeneo kama haya haiwezekani bila kubadili Katiba.
Sense.
Bado nafasi tunayo,tatizo tunaowaongelea ndiyo wenye rungu la kuyafanya hayo kwa mujibu wa katiba ya JMT 1977.
Kwa hiyo, ni ngumu kwa wabunge/mbunge kupeleka hoja binafsi ya kutaka punguzo la mishahara yao au sitting allowance zao.
 
Kwani hili bunge la Tanzania haliwezi kutunga sheria bila ya kubadili katiba? Trump kapangua mfumo mzima wa kodi wa Marekani juzi kwa kutumia kura za wabunge, sisi tunashindwa vipi.
Hatuna wabunge wa namna hiyo. May be over our dead bodies.
 
Million nane ingekuwa inalipwa kwa wabunge wenye akili timamu, wala hapana tatizo.

Kodi za wananchi zinatafunwa na hawa goigoi ngumbaru wasiolewa hata dhima yao ya kuwa ndani ya lile jengo.

Bunge thabiti linahitaji watu thabiti, sio hawa akili nyepesi.

Huyo msukuma hata ukimwambia maana ya subsidiary legislation anaelewa kitu gani pale?

Yupo tu pale kupiga soga na kucheka cheka hovyo!
 
Mimi siku zote huwa nasema wanasiasa ni kikundi cha watu wajanja wajanja waliojikusanya sehemu moja kwa kutumia mbinu tofauti tofauti ili kutafuna kodi za wananchi!

Ukitaka kuthibitisha hilo hebu ajitokeze mtu mmojo aguse haya maslahi yao mapana uone jinsi watakavyoungana kumraruararua na kumchanachana bila kujali itikadi za vyama vyao!

Kwenye hili la mishahara mikubwa na maposho manene, hautowajua CCM ni wapi, CHADEMA, CUF, wala NCCR ni wapi.. Wataungana na kumchachafya kwelikweli yule mwenye kujaribu kugusa maslahi yao ya kifedha!

Uadilifu wa wanasiasa wetu, hasa wabunge una mashaka makubwa mno. Mnamkumbuka yule kiongozi aliyejaribu kutajataja wanaohusika na biashara haramu ya uuzaji wa madawa ya kulevya? Mliona tofauti yoyote kati ya wabunge wa CCM na wale wa upinzani?
Wanasiasa wetu ni tofauti sana na wanavyojiaminisha mbele ya umma.
Kwa hili la mishahara na marupurupu yao ni untouchable. Na hayatakaa yaguswe.Nafikiri hata Mh Rais akithubutu kutumia mamlaka yake katika hili,ajiandae kujiongezea maadui na wengi wao kutoka chama chake.
Nafikiri kuna haja ya kuwa na mjadala wa kitaifa kuhusu mabadiliko ya katiba.Bado tunaihitaji katiba ya Warioba.Vinginevyo, tumekwisha na hatuna pa kutokea.
MP's are selfish...hawatokwi povu kwa maslahi ya umma, bali kwa maslahi yao tu.
 
Hii Nchi Pengo kati ya mwenyenacho na asiyenacho ni kubwaa mno, na kwa Muono wangu pengo hilo linazidi kukuwa siku hadi siku, kama suala hilo litaachwa bila mkakati wowote wa kupunguza pengo hilo basi Taifa kwa ujumla hatutakuwa salama. Bwana Jean-Jacques Rousseau aliwahi kusema, Nanukuu " When the poor shall have Nothing more to Eat, they will eat the Rich" Mwisho wa kunukuu.
 
Kwanza niseme mimi sina kadi ya chama chochote cha siasa. Ila ni mkereketwa wa bendera ya Tanzania.

Hakuna kitu kinanikera kama tabia ya wabunge kusimamia ya vyama vyao na kusahau ya taifa. Kuna wabunge wazuri sana wa kupinga ufisadi. Lakini hutawasikia wakimzogoa fisadi kama yuko kwenye chama chao.

Kwenye hili la mishahara ni kama wote kwa mpigo bila ya kujali vyama vyao wameamua kulikalia kimya. Katika nchi ambayo polisi mwenye shahada ya sheria analipwa laki sita kwa mwezi hesabu ya kuwalipa wabunge zaidi ya milioni nane kwa mwezi imetoka wapi?

Kuna watumishi wa serikali wako kazini zaidi ya miaka thelathini mishahara yao haijafifikia milioni. Na mafao yao wakistaafu yanaweza yasifikie huo mshahara wa mwaka wa mbunge mmoja.

Wengi wa watanzania wanateseka kwa kukosa bima. Nimeshuhudia waliorudi nyumbani kusubiri kufa kwa kukosa bima. Wabunge wao wana utaratibu wa kutibiwa nje kwa fedha za wavuja jasho.

Hivi kweli utaweza kuwakilisha wenye shida iwapo wewe hujui shida?

Wako wapi wale wabunge wasemaji wazuri hawaoni kuwa mishahara yao imekaa kifisadi? Na bado wanapewa posho za vikao. Hii haijatulia ni ya kukemewa vikali na wakereketwa wa bendera ya Tanzania.

Mungu ibariki Tanzania
Inshallah....Rais wetu msikivu ataifanyia kazi hoja hii.
 
Kwanza niseme mimi sina kadi ya chama chochote cha siasa. Ila ni mkereketwa wa bendera ya Tanzania.

Hakuna kitu kinanikera kama tabia ya wabunge kusimamia ya vyama vyao na kusahau ya taifa. Kuna wabunge wazuri sana wa kupinga ufisadi. Lakini hutawasikia wakimzogoa fisadi kama yuko kwenye chama chao.

Kwenye hili la mishahara ni kama wote kwa mpigo bila ya kujali vyama vyao wameamua kulikalia kimya. Katika nchi ambayo polisi mwenye shahada ya sheria analipwa laki sita kwa mwezi hesabu ya kuwalipa wabunge zaidi ya milioni nane kwa mwezi imetoka wapi?

Kuna watumishi wa serikali wako kazini zaidi ya miaka thelathini mishahara yao haijafifikia milioni. Na mafao yao wakistaafu yanaweza yasifikie huo mshahara wa mwaka wa mbunge mmoja.

Wengi wa watanzania wanateseka kwa kukosa bima. Nimeshuhudia waliorudi nyumbani kusubiri kufa kwa kukosa bima. Wabunge wao wana utaratibu wa kutibiwa nje kwa fedha za wavuja jasho.

Hivi kweli utaweza kuwakilisha wenye shida iwapo wewe hujui shida?

Wako wapi wale wabunge wasemaji wazuri hawaoni kuwa mishahara yao imekaa kifisadi? Na bado wanapewa posho za vikao. Hii haijatulia ni ya kukemewa vikali na wakereketwa wa bendera ya Tanzania.

Mungu ibariki Tanzania
Katika mambo haya ya msingi wana mshikamano wa kutisha. Hutamsikia kubenea wala maji marefu.
 
... " When the poor shall have Nothing more to Eat, they will eat the Rich" Mwisho wa kunukuu.
Capt John Komba alipata matatizo na gari lake manzese akashangaa vijana wa pale badala ya kumsaidia, walipora baadhi ya vitu. Wengine tukasema ingeshangaza kama asingeporwa. Ni hali isiyoepukika.
 
Capt John Komba alipata matatizo na gari lake manzese akashangaa vijana wa pale badala ya kumsaidia, walipora baadhi ya vitu. Wengine tukasema ingeshangaza kama asingeporwa. Ni hali isiyoepukika.


Ukiangalia kiuhalisia Makabwela tuko wengi kuliko mabwenyenye, kwaiyo mambo kama hayo hayawezi kuepukika
 
Ubunge iwe ni kazi ya kujitolea,ila wapewe posho stahiki wakati wa vikao vya bunge
Sifa ya mbunge iwe Mtanzania mwenye uwezo wa kujitegemea sio wasaka malupulupu kupitia ubunge.
Kama ilivyo kwa madiwani!
 
Back
Top Bottom