Kwanza niseme mimi sina kadi ya chama chochote cha siasa. Ila ni mkereketwa wa bendera ya Tanzania.
Hakuna kitu kinanikera kama tabia ya wabunge kusimamia ya vyama vyao na kusahau ya taifa. Kuna wabunge wazuri sana wa kupinga ufisadi. Lakini hutawasikia wakimzogoa fisadi kama yuko kwenye chama chao.
Kwenye hili la mishahara ni kama wote kwa mpigo bila ya kujali vyama vyao wameamua kulikalia kimya. Katika nchi ambayo polisi mwenye shahada ya sheria analipwa laki sita kwa mwezi hesabu ya kuwalipa wabunge zaidi ya milioni nane kwa mwezi imetoka wapi?
Kuna watumishi wa serikali wako kazini zaidi ya miaka thelathini mishahara yao haijafifikia milioni. Na mafao yao wakistaafu yanaweza yasifikie huo mshahara wa mwaka wa mbunge mmoja.
Wengi wa watanzania wanateseka kwa kukosa bima. Nimeshuhudia waliorudi nyumbani kusubiri kufa kwa kukosa bima. Wabunge wao wana utaratibu wa kutibiwa nje kwa fedha za wavuja jasho.
Hivi kweli utaweza kuwakilisha wenye shida iwapo wewe hujui shida?
Wako wapi wale wabunge wasemaji wazuri hawaoni kuwa mishahara yao imekaa kifisadi? Na bado wanapewa posho za vikao. Hii haijatulia ni ya kukemewa vikali na wakereketwa wa bendera ya Tanzania.
Mungu ibariki Tanzania
Tanzania hatuna na hatujawahi kuwa na mishahara mikubwa. Tatizo lililopo ni uzalishaji mdogo. Tuna raslimali nyingi sana ambazo tukizitumia angalau kwa ailimia moja,twaweza kuwa sehemu nzuri sana. Mfano, 1.Tanzanite iliyopo kwetu, ikitumika kwa asilimia moja kwa ukanda wake kuanzia mpakani mwa kenya(Arusha) hadi Tunduma,angalau kwa asilimia moja,kipato cha wahusika kitapanda sana.
2.Ukanda wa Emerald,Tsavolite,Ruby,Alexandrite na garnets wa (Mara,Arusha) hadi Songea ukitumika vizuri hata kwa asilimia moja,kutakuwa na kipato kizuri
3.Ukanda wa Almasi wa (Mwanza na Mara ) hadi (Mbeya na Songea ) ukitumika vizuri hata kwa asilimia moja ,kutakuwa na kipato kizuri.
3. Ukanda wa Emerals na chrome tourmaline wa Kagera hadi Rukwa na katavi ,ukitumika vizuri hata kwa asilimia moja tu,kipato kitakuwa kizuri.
4. Ukanda wa dhahabu wa (Kagera na kigoma) hadi (Mara,Arusha,Moshi na Tanga) ukitumiwa vizuri hata asilimia moja,kipato kitakuwa kizuri.
5.Ukanda wa dhahabu wa (Rukwa na Mbeya ) (hadi Pwani na Dar es Salaam ) ukitumika vizuri hata kwa asilimia moja,kipato kitakuwa kizuri.
6.Ukanda wa Dhahabu wa Songea hadi mtwala ukitumika vizuri angalau kwa asilimia moja,kipato kitakuwa kizuri.
Vipato kwa watu vikiwa vizuri,serikali itakusanya kodi ya kutosha na mishahara itapanda.
Kwa mtazamo wangu,tatizo letu kuu ni elimu ya jinsi gani rasilimali hizi zivunwe na kuuzwa. Taifa likiamua kuwekeza katika elimu kwa madini na vitu vingine,kwa wananchi,naamini tutafanikiwa.