SODIUM CYANIDE
JF-Expert Member
- Jun 5, 2013
- 691
- 1,166
Maisha hayafanani habadani. Wao hata kiinua mgongo ni kikubwa na wanapewa kwa wakati tofauti na mfanyakazi wa umma anayesota miaka nenda rudi na mafao kidogo tena yakusotea.
Seriously!?Mimi naona ipunguzwe ya Walimu sababu hawana akili
Hoja yako ni nzuri, ila tatizo ni sheria aliyoitunga Mkapa Mwaka 1999.Kwanza niseme mimi sina kadi ya chama chochote cha siasa. Ila ni mkereketwa wa bendera ya Tanzania.
Hakuna kitu kinanikera kama tabia ya wabunge kusimamia ya vyama vyao na kusahau ya taifa. Kuna wabunge wazuri sana wa kupinga ufisadi. Lakini hutawasikia wakimzogoa fisadi kama yuko kwenye chama chao.
Kwenye hili la mishahara ni kama wote kwa mpigo bila ya kujali vyama vyao wameamua kulikalia kimya. Katika nchi ambayo polisi mwenye shahada ya sheria analipwa laki sita kwa mwezi hesabu ya kuwalipa wabunge zaidi ya milioni nane kwa mwezi imetoka wapi?
Kuna watumishi wa serikali wako kazini zaidi ya miaka thelathini mishahara yao haijafifikia milioni. Na mafao yao wakistaafu yanaweza yasifikie huo mshahara wa mwaka wa mbunge mmoja.
Wengi wa watanzania wanateseka kwa kukosa bima. Nimeshuhudia waliorudi nyumbani kusubiri kufa kwa kukosa bima. Wabunge wao wana utaratibu wa kutibiwa nje kwa fedha za wavuja jasho.
Hivi kweli utaweza kuwakilisha wenye shida iwapo wewe hujui shida?
Wako wapi wale wabunge wasemaji wazuri hawaoni kuwa mishahara yao imekaa kifisadi? Na bado wanapewa posho za vikao. Hii haijatulia ni ya kukemewa vikali na wakereketwa wa bendera ya Tanzania.
Mungu ibariki Tanzania![]()
Point tupuHoja yako ni nzuri, ila tatizo ni sheria aliyoitunga Mkapa Mwaka 1999.
'Political Service Retirement Benefits Act, 1999'; inayohusu pensheni za viongozi wa kisiasa: Rais, Makamu wa Rais, Spika na Naibu wake, Waziri Mkuu.
Chini ya sheria hii mambo yafuatayo yalilifunga Bunge:
1. Ni lazima Bunge lipitie upya viwango vya Pensheni za wakubwa hao kila baada ya miaka mitano kwa lengo la KUZIONGEZA.
2. Kiwango cha pensheni ya Rais mstaafu ni 80% ya mshahara wa Rais aliyepo madarakani.
3. Ili kukidhi matakwa ya 1. hapa juu lazima Bunge liongeze mshahara wa Rais aliyepo madarakani.
4. Kwa mujibu wa Katiba ya JMT 1977; Rais ni sehemu ya Bunge. Hivyo mshahara wake ukiongezwa; chini ya Sheria na 2. ya 1999 mishahara ya wengine waliotajwa hapo juu; pamoja na wabunge, ITAPANDISHWA.
Katika mazingira ya kikatiba na kisheria kama hayo hapo juu; mabadiliko kwenye maeneo kama haya haiwezekani bila kubadili Katiba.
Typical mswahili.Kwanini usishinikize mishahara ya watumishi ipande ili ifanane na ya wabunge?
Hoja yako ni nzuri, ila tatizo ni sheria aliyoitunga Mkapa Mwaka 1999.
'Political Service Retirement Benefits Act, 1999'; inayohusu pensheni za viongozi wa kisiasa: Rais, Makamu wa Rais, Spika na Naibu wake, Waziri Mkuu.
Chini ya sheria hii mambo yafuatayo yalilifunga Bunge:
1. Ni lazima Bunge lipitie upya viwango vya Pensheni za wakubwa hao kila baada ya miaka mitano kwa lengo la KUZIONGEZA.
2. Kiwango cha pensheni ya Rais mstaafu ni 80% ya mshahara wa Rais aliyepo madarakani.
3. Ili kukidhi matakwa ya 1. hapa juu lazima Bunge liongeze mshahara wa Rais aliyepo madarakani.
4. Kwa mujibu wa Katiba ya JMT 1977; Rais ni sehemu ya Bunge. Hivyo mshahara wake ukiongezwa; chini ya Sheria na 2. ya 1999 mishahara ya wengine waliotajwa hapo juu; pamoja na wabunge, ITAPANDISHWA.
Katika mazingira ya kikatiba na kisheria kama hayo hapo juu; mabadiliko kwenye maeneo kama haya haiwezekani bila kubadili Katiba.
Watz kwa rohombaya hawajambo, yaani unataka aliye nacho apunguziwe
Au kama vipi wabunge pia walipwe kulingana na elimu zao. Maana kama Msukuma na Majimarefu anapokea mara tatu ya mtumishi aliye na PhD ya medicine, umuhimu wa elimu hapa haupo.Wanahangaika kupunguza wage bills kwa kudhulumu wanyonge, ati ni darasa la saba hana sifa za kuajiri. Huu ni ubaguzi wa dhahiri mfagizi wa ofisi na fomu 4 inasaidiaje utendaji kazi wake. Msukule Msukuma na Mchawi Majimarefu wana zaidi ya daktari mwenye digrii ya Phd, huu ni ufisadi wa kiasi gani?. Tunapumua kwa kutukana maana uvumilivu umefika mwisho!
Wewe uko tayari kukatwa mashahara wako kwa nusu?Tuchukulie wabunge 265 kila mmoja akilipwa milioni nane kwa mwezi. Kwa hesabu za haraka haraka serikali inatumia milioni 2120 kila mwezi kuwalipa wabunge. Kwa mwaka serikali inatumia shilingi 25, 440, 000,000. Na bado wanapata posho.
Si bora wakatwe nusu yake itumike kuwaongezea mishahara watumishi wa serikali.
Wewe uko tayari kukatwa mashahara wako kwa nusu?