Mishahara ya viongozi wa Tanzania

Mishahara ya viongozi wa Tanzania


Kwa upande wangu sina la kuongeza kwenye huu mjadala. mwenye kuelewa na aelewe.

Una assume kwamba kila mtu yuko hapa kwa kutaka kueleweshana.

Mtu kadai "leteni sheria tukate mzizi wa fitina." Sheria inakuja anasema "...hai make sense...ime expire...bla bla bla..." kwa vile tu haifanani na vile alivyodhania yeye.

Ukiangalia hiyo "sense" anayoidai yeye inasema Rais mstaafu akisafiri awe na walinzi wawili, "mmoja lazima akalinde chumba...mmoja aende kwenye gari la mizigo..."

Sasa hapo utasema nime exaggerate kusema madai ya huyu mleta data ni outlandish and bizarre ? Huoni kwamba ni kichekesho hicho?
 
1.
Nitajaribu tena kukuelimisha. Hii mada inazungumzia stahili za wastaafu na sivyo wanavyotumia. Wewe ulileta hoja yako kana vile ile ndiyo stahili yao. Na ulipofahamishwa kuwa sheria inasema tofauti na unachokisema ukasema wewe haujali sheria inasema nini, unajua unachokiona. Si unachoambiwa, si unachosikia, unachokiona. Kwa kuweka na kukazania kuwa unayoyaona ndiyo stahili ndiyo nikakuita muongo.

1. Na mimi pia sitanchoka kukuelimisha, kuwa viongozi wote wastaafu wana maisha sawa, isipokuwa wachache tu ambao hawapendi makuu na ndicho kinachonifanya ninamini kuwa hiyo sheria yako haipo au imekufa siku nyingi, kwa sababu ninachokiona kwa wastaafu, hakifanani na sheria zako.

2. Again ninayaona ndiyo wanayafanya ndiyo the style kwa sababu hata Lowassa, aliyetoka juzi tu anye ameshaanza kuishi kwa the same style, sasa hiyo sheria yako ipo wapi? Mimi sikuiti muongo, ila ninakuita hujui unachosema na nimesema toka mwanzo kuwa hujui unachokisema, kwa sababu huwezi kulilia sheria ambayo haifanyi kazi kuwa ndiyo sheria.


2.
Mbona ulipokuja kwa gia nyingine juu ya dataz ulizodai ulizipata kutoka kwa makongora kwenye ulabu, hakuna aliyekuita muongo. ukawekewa sheria, ukakiri kuwa pengine mheshimiwa alikudanganya.

Nilisema nimewahi kumsikia Makongoro, akisema kwenye pombe, na nikaweka wazi kuwa sina uhakika na maneno yake, ni kwa sababu ninamfahamu sana kwa kamba, na niliweka wazi kuwa sina uhakika na maneno yake, lakini haya ya staili za watsaafu na maisha yao hilio sijasema kutokuwa na uhakika, nimesema ninajua for a fact kuwa maisha yao sio kabisa sawa sheria zako,

Huwezi kuniiita muongo wakati hujathibitisha uongo wangu, ninasema hivi marais wastaafu husafiri na watu wengi sana as opposed na sheria yako inayosema wasaidizi wawili, Mwalimu alikuwa akifuatana na watu zaidi ya wawili, kina Mosha, Mwakyusa, Balozi Ngaiza, hawa walikuwa ni baadhi tu wasaidizi waliokuwa wakifuatana na Mwalimu always licha ya wengine lukuki, leo Mkapa na Mwinyi nao ni hivyo hivyo, sasa unasema kuna sheria ingekuwepo basi Mwalimu ambaye ndiye aliyekwua wa kwanza na aliyekwua hapendi mchezo asingekubali kufuatana na watu wengi against sheria,
kwa hiyo labda hiyo sheria haipo, imekufa, au batili.


3.
Mtu yeyote aliyefanya kazi serikalini anajua kuwa viongozi wa juu wana kawaida ya kukiuka sheria na taratibu. Hii haimaanishi kuwa sheria hizo ni batili au zime'expire'. Mfano wa wakristu ulikuwa ni kukuonyesha kuwa haupimi sheria kwa kuangalia vitendo vya wanaotakiwa kuongozwa nazo. lakini kama kawaida yako, unataka ku'misinterpret'.

Haiwezekani kuwa kuanzia Mwalimu, mpaka leo viongozi wetu wastaafu wamekua wakikiuka sheria za kustaafu, hilo ninalikataa kabisa kuwa ni out, kiongozi aliye-retire atavunja vipi sheria za mafao, wakati mafao yao ni part ya bajeti ya taifa inayopitishwa bungeni? Kiongozi aliye-retire hawezi kuwatisha idara ya utumishi, wakampa anything nje ya sheria never! Sasa kwa kweli ninaamini kuwa hiyo sheria mliyonayo sio yote, au ilibadilishwa bila ya nyinyi kuelewa

4.
Kosa lako ni kudai kuwa hayo unayodai unayoyaona ndiyo stahili ya viongozi. mimi sikujui, nitakuitaje muongo kwa kusema kuwa ulimuona Mkapa anaongozana na watu lukuki? Kudai kuwa Mkapa stahili yake ni kuongozana na mpishi kila akisafiri nje, nikakuita muongo.Kwa upande wangu sina la kuongeza kwenye huu mjadala. mwenye kuelewa na aelewe.

Exactly, ninavyosema kuwa ni staili yao kwa sababu wote wanafanya yale yale, sasa kama ninawaona karibu wote wakifanya hivyo ullitaka niseme nini?
Wewe ni kukubali tu kuwa wastaafu wana maisha flani, ambayo yanakubaliwa na sheria, ambayo wewe huna au hujui kama ipo, otherwise hiyo sheria imekufa, au haipo kabisaa.

No matter how huwezi kubadili ninachokisema, kuwa Mkapa anaposaifri huwa anafutana na wasaidizi wengi zaidi ya 10, ndani yake kuna walinzi, kuna mpishi na kuna mpaka watu kutoka foreign, lakini sheria yako inasema wanatakwia kusafiri wawili tu, sasa ndipo hapo unaposhindwa kunielemisha, na sina tatizo kuendelea kusoma hili darasa kwa sababu, ninaamini 100% kuwa wastaafu wanatakiwa kupata yote ninayoyaona tena kisheria kwa sababu inakuwaje wote wanakuwa na maisha sawa baada ya kutoka kwenye power? yaani huduma za serikali haiwezekani zikawa sawa wakati sheria haisemi hivyo, au?
 
Una assume kwamba kila mtu yuko hapa kwa kutaka kueleweshana.

Mtu kadai "leteni sheria tukate mzizi wa fitina." Sheria inakuja anasema "...hai make sense...ime expire...bla bla bla..." kwa vile tu haifanani na vile alivyodhania yeye.

Ukiangalia hiyo "sense" anayoidai yeye inasema Rais mstaafu akisafiri awe na walinzi wawili, "mmoja lazima akalinde chumba...mmoja aende kwenye gari la mizigo..." Sasa hapo utasema nime exaggerate kusema madai ya huyu mleta data ni outlandish and bizarre ? Huoni kwamba ni kichekesho hicho?

Yale yale maneno yako ya chooni ambayo huwa hayana elimu, bali ni kutaka kujionyesha kuwa unajua sana wakati hujui kitu, sheria yenu ni batili na mufilisi, au haipo kabisaa,

Mliyoileta haina ukweli wa ninayoyaona, na sio kudhania, hiyo nimekusaidia kuwa ni kwa nini anasafiri na watu wnegi zaidi ya sheria yako inavyosema, kwamba hawezi kusaifiri na wasaidizi wawili tu!

Outlandish na bizzare, sidhani kama kuna tatizo hapa JF kuhusu nani hasa mwenye hiyo tabia ya kuleta uzushi, wewe ni masikini ya Mungu, confused na hata huelewi unachosema, ninaamini wananchi wengi hapa JF walishakusamehe maana wanajua how unaweza kuleta outlandish na bizzare ukiamua, hoja zimewashinda sasa unajaribu kuleta viroja, ninakuonea huruma sana mkuu maana sijawahi kuona an idiot mfano wako!

Siku utakapo leta ushahidi uliouahidi kuhusu Dr. Masau, nitaamini kila kitu unachosema, na siku utakapo fungua lawsuit uliyoahidi against Dr. Masau then nitaamini kila neno unalosema hapa kuwa ni kweli, otherwise ni maajabu na kweli kwamba wewe unaweza kudai kuwa kuna member hapa analeta outlandish na bizzare, eti kuna anayekuzidi wewe kwa idiotic behavior hapa JF?
 


...sheria yenu ni batili na mufilisi, au haipo kabisaa,

Mliyoileta haina ukweli wa ninayoyaona, na sio kudhania, hiyo nimekusaidia kuwa ni kwa nini anasafiri na watu wnegi zaidi ya sheria yako inavyosema, kwamba hawezi kusaifiri na wasaidizi wawili tu!

Sasa kama sheria huikubali kwa nini ulisema tulete sheria ikate mizizi ya fitina?

Ulitaka sheria inayothibitisha unachokiona ?
 
Sasa kama sheria huikubali kwa nini ulisema tulete sheria ikate mizizi ya fitina?
Ulitaka sheria inayothibitisha unachokiona ?

Mbona unauliza majibu, nilitaka kuona sheria inasema nini ili iwakate mzizi wa fitina kwa sababu mliyokuwa mnayasema hayamo kwenye ninayoyaona, mliyoileta siamini kuwa ni yenyewe na sababu ni moja tu kwamba haiwezekani wastaafu wote wakawa na the same life style,

Na ninachokiona kwa wastaafu ni kile kile, sasa ulitaka niseme nini kuwa sheria yenu ni sawa? Siwezi kwa sababu ninaamini kuwa hela za kuwafaa zinaombwa kwenye bajeti, sasa huwezi kuomba bajeti bila ya kuwa na sheria ya bunge lile lile, kwa hiyo ndio maana ninasema kuwa something is wrong, either na sheria, au haipo, au mliyoileta sio yenyewe!
 
Yale yale maneno yako ya chooni ambayo huwa hayana elimu, bali ni kutaka kujionyesha kuwa unajua sana wakati hujui kitu, sheria yenu ni batili na mufilisi, au haipo kabisaa,

Kwa maneno kama haya ndiyo maana tumebaki sisi peke yetu kwenye hii mada. Hauoni, lakini unaonyesha ignorance yako kila unavyoendelea. Word to the wise, achia yaishe! Sisi kupinga dataz zako na kukuona muongo hakukupunguzii umaarufu wako.

Watu wengi zaidi wataendelea kukuamini. Kwa kuendelea kushindana na majuha kama sisi unafanya na wewe uonekana juha kama sisi.
 
Last edited:
Ninarudia tena, Seif alifukuzwa kazi na CCM, na ni CCM katika mazungumzo ya muafaka ndio waliomshaiwshi Seif kuanza kupewa mafao, kwa ujumbe waliomtumia kupitia Katibu mkuu wa CCM then Mang'ula, na akakubali na kuanza kupewa,

Hayo ya nembo ni yako mimi siyajui, ya kuandika barua ya serikali kusainiwa na Mang'ula ni yako pia mimi sikuyasema wala siyajui, ila ninajua as a fact, kwamba viongozi wengi wakuu wa serikali mara nyingi wameondolewa nyazifa zao serikalini na CCM, kwa mfano Aboud Jumbe, Seif Bakari, Maaalim Seif, Prof. Mbilinyi, Idd Simba, hawa ni baadhi tu ya wakuu wa serikali yetu ya jamhuri waliowahi kuondolewa kwenye power na CCM, sasa labda wewe utuelimishe kwa nini CCM na sio sheria za jamhuri kama unavyozidai?

Mang'ula aliweza kumpelekea ujumbe. Aliweza kuishauri serikali ya mapinduzi Zanzibar kumpa mafao lakiniasingeweza kiutendaji kumpa mafao hayo.

Mang'ula au mtu yeyote wa CCM hana uwezo wa kumchukulia hatua mtumishi wa serikali kama yeye si kiongozi wa serikali ( Rais, Waziri Mkuu, Waziri, Mkuu wa Mkoa n.k.). Wakina Jumbe na Seif walifukuzwa wakati wa utawala wa Chama kimoja . Wakati huo utawala wa chama na serikali uliunganishwa. Ndiyo maana hata katika mashirika ya umma kulikuwa na sehemu ya chama. Profesa Mbilinyi, Iddi Simba na hao mawaziri wengine wa serikali walijiuzulu kwa Rais wa serikali ya JMT uwaziri wao na si kwa Mwenyekiti wa CCM!

Kama kuachishwa, waliachishwa na kiongozi wa serikali na si wa chama. CCM hawana mamlaka ya kumuondoa mtendaji wa serikali nje ya kumnyang'anya uanachama na kumfanya akose sifa ya kuwa sehemu hiyo kama ni kiongozi wa kisiasa. Wanaweza kuamua atemwe ( kuamua atoke) lakini mtekelazaji lazima awe ni mtendaji wa serikali. Vile vile mtu hawezi kushitakiwa au kufukuzwa kazi serikalini kwa kupingana na katiba ya CCM.

Anaweza kufukuzwa au kuadhibiwa akionekana amevunja sheria ya nchi (si CCM) au amekiuka taratibu ( standing orders) zinazoongoza watumishi wa serikali. Vile vile mafao ya mstaafu yeyote wa serikali yanaongozwa na sheria na waraka za utendaji wa serikali na si matakwa ya kiongozi wa chama. Chama hakiwezi kumnyang'anya au kumrejeshea mtu mafao yake yanayotokana na utendaji wake serikalini, period.

Chama kinachoweza kufanya hivyo kwa KUPITIA serikali inayoongoza tu. Hatari ya kufanya hivyo nje ya sheria ni kuwa chama kingine kikishika utamu kitakuwa na haki na uwezo wa kuwachukulia hatua wahusika kwa kupindisha sheria. Hii ni serikali inayoongozwa na chama cha CCM lakini chama cha CCM si serikali. Ingawa watendaji wengi wanasahau hiyo lakini ndivyo ilivyo.

Hapa kigumu kipi kuelewa?
 
1
. kusema madai ya huyu mleta data ni outlandish and bizarre ? Huoni kwamba ni kichekesho hicho?

Hayo maneno juu kwako ni hoja, kwangu ni maneno ya chooni period.

2.
Mang'ula aliweza kumpelekea ujumbe. Aliweza kuishauri serikali ya mapinduzi Zanzibar kumpa mafao lakiniasingeweza kiutendaji kumpa mafao hayo. Mang'ula au mtu yeyote wa CCM hana uwezo wa kumchukulia hatua mtumishi wa serikali kama yeye si kiongozi wa serikali ( Rais, Waziri Mkuu, Waziri, Mkuu wa Mkoa n.k.). Wakina Jumbe na Seif walifukuzwa wakati wa utawala wa Chama kimoja . Wakati huo utawala wa chama na serikali uliunganishwa. Ndiyo maana hata katika mashirika ya umma kulikuwa na sehemu ya chama. Profesa Mbilinyi, Iddi Simba na hao mawaziri wengine wa serikali walijiuzulu kwa Rais wa serikali ya JMT uwaziri wao na si kwa Mwenyekiti wa CCM! Kama kuachishwa, waliachishwa na kiongozi wa serikali na si wa chama. CCM hawana mamlaka ya kumuondoa mtendaji wa serikali nje ya kumnyang'anya uanachama na kumfanya akose sifa ya kuwa sehemu hiyo kama ni kiongozi wa kisiasa. Wanaweza kuamua atemwe ( kuamua atoke) lakini mtekelazaji lazima awe ni mtendaji wa serikali. Vile vile mtu hawezi kushitakiwa au kufukuzwa kazi serikalini kwa kupingana na katiba ya CCM. Anaweza kufukuzwa au kuadhibiwa akionekana amevunja sheria ya nchi (si CCM) au amekiuka taratibu ( standing orders) zinazoongoza watumishi wa serikali. Vile vile mafao ya mstaafu yeyote wa serikali yanaongozwa na sheria na waraka za utendaji wa serikali na si matakwa ya kiongozi wa chama. Chama hakiwezi kumnyang'anya au kumrejeshea mtu mafao yake yanayotokana na utendaji wake serikalini, period. Chama kinachoweza kufanya hivyo kwa KUPITIA serikali inayoongoza tu. Hatari ya kufanya hivyo nje ya sheria ni kuwa chama kingine kikishika utamu kitakuwa na haki na uwezo wa kuwachukulia hatua wahusika kwa kupindisha sheria. Hii ni serikali inayoongozwa na chama cha CCM lakini chama cha CCM si serikali. Ingawa watendaji wengi wanasahau hiyo lakini ndivyo ilivyo.

Hapa kigumu kipi kuelewa?

1. Hakuna anything hapo juu kuhusiana na point ya msingi kwamba kwa nini wastaafu karibu wote wana same lifestyle wakati kwenye sheria hakuna back up?

2. Seif, Jumbe, Seif Bakari walifukuzwa kazi serikalini na CCM under cahma kimoja kama unavyosema, Idd Simba na Mbilinyi walifukuzwa kazi kwenye kikao cha CC kama hao wengine, infact ni Kawawa ndiye aliyewalalzimisha kutoka kazi zao huko CC, wewe unasema walijiuzulu, sasa ni nani aliyekuambia kuwa Jumbe hakujiuzulu if that is the case?

Lets stick to the real ishu here, kwa nini sheria ya mafao haifanani na lifestyle za wastaafu?
 
Seif, Jumbe, Seif Bakari walifukuzwa kazi serikalini na CCM under cahma kimoja kama unavyosema, Idd Simba na Mbilinyi walifukuzwa kazi kwenye kikao cha CC kama hao wengine, infact ni Kawawa ndiye aliyewalalzimisha kutoka kazi zao huko CC, wewe unasema walijiuzulu, sasa ni nani aliyekuambia kuwa Jumbe hakujiuzulu if that is the case?

Lets stick to the real ishu here, kwa nini sheria ya mafao haifanani na lifestyle za wastaafu?

CCM inawezekana iliwashinika kujiuzulu. Sasa unataka kutuambia kuwa barua ya kujiuzulu walimwandikia Kawawa? Au Mang'ula?

Ninachokwambia ni kuwa hata kkama walishinikizwa na chama chao (kitu ambacho sikipingi) kujiuzulu kwao kuna effective tu pale kunapokubaliwa na Rais wa nchi na si Mwenyekiti wa CCM hata kama kofia hizo kavaa mtu mmoja.

Sheria ipi ya mafao? Hii unayodai ime-expire?

Sheria ya mafao inahusu kipato chao kutoka serikalini na hakizuii mtu kujiongezea kipato kutoka sehemu nyingine. Kabla ya kuwahukumu kuwa wanaibia serikali kwa kudai wanatumia zaidi ya wanavyopaswa kisheria, ni lazia tujue hao walio ziada ya sheria wanalipiwa na nani? Kosa litafanyika ikiwa kuwa wote wanalipiwa na serikali nje ya utaratibu.

Napenda kukutahadharisha, sheria haimzuii mstaafu kuongozana na msafara wa serikali kama anaenda kikazi. Au hata pengine wanaelekea sehemu moja lakini kila mmoja ni kivyake vyake.

Baada ya kusema yote haya, sitashangaa kama wale waliopewa jukumu la kusimamia hayo mafao wakaamua kupuuza sheria kwa kuwaonea aibu wastaafu. Haitakuwa mara ya kwanza watendaji kuwaonea aibu viongozi wao wa siasa. Hivi karibuni Tanroad wamejenga matuta kwa kufuata maagizo ya kiongozi wao wa kisiasa ( ambaye si mtaalamu wa barabara) bila kuangalia kama yanakubalika kitaaluma!

Wanasheria waliobobea waliangalia tu wakati viongozi wao wakipindisha sheria zinazohusu madini na nishati. Na walipoulizwa walitetea upindaji huo! Sheria kupindwa, kudharauliwa nyumbani haitakuwa mara ya kwanza.

Amandla.
 
FMeS,

Mfano mwepesi mwengine. Mtaani tunasema leseni ya udereva tumeitoa trafik. Lakini wote tunajua trafik hawana mamlaka ya kutoa leseni. Wao wanakupa mtihani na kutoa kibali cha wewe kupata leseni. Leseni unaifuata revenue ambao ndiyo wenye mamlaka ya kutoa leseni. At least, ilikuwa hivyo wakati wangu.

Kwenye hili CCM ni trafik na serikali ni revenue.
 
1.
CCM inawezekana iliwashinika kujiuzulu. Sasa unataka kutuambia kuwa barua ya kujiuzulu walimwandikia Kawawa? Au Mang'ula? Ninachokwambia ni kuwa hata kkama walishinikizwa na chama chao (kitu ambacho sikipingi) kujiuzulu kwao kuna effective tu pale kunapokubaliwa na Rais wa nchi na si Mwenyekiti wa CCM hata kama kofia hizo kavaa mtu mmoja.

Sasa tuko nje ya topic kabisaa, lakini sio tatizo mkuu ndio maana tupo hapa JF ni pamoja na kuitaka serikali yetu ibadili katiba, kwa sababu katiba tuliyonayo imepitwa na wakati, kiongozi wa serikali hawezi kulazimishwa kujiuzulu na chama katika siasa za kisasa za maendeleo,

Halafu haiewezekani sheria iseme mstaafu anatakiwa kusaifiri na wasaidizi wawili, huku tunamuona akisafiri na wasiadizi zaidi ya kumi that is wrong, ndio maana nilisema leteni sheria tukate mzizi wa fitina!


2.
Sheria ipi ya mafao? Hii unayodai ime-expire?

Sheria ya mafao mliyoileta inaonyesha ime-expire siku nyingi sana kama haitumiki kabisa, hiyo ndiyo point yangu, kwa sababu haiwezekani wastaafu wote wawe na the same lifestyle, halafu ukasema eti wanai-abuse sheria no way! Haiwezekani ikawa wote toka enzi za Mwalimu!

3.
Sheria ya mafao inahusu kipato chao kutoka serikalini na hakizuii mtu kujiongezea kipato kutoka sehemu nyingine. Kabla ya kuwahukumu kuwa wanaibia serikali kwa kudai wanatumia zaidi ya wanavyopaswa kisheria, ni lazia tujue hao walio ziada ya sheria wanalipiwa na nani? Kosa litafanyika ikiwa kuwa wote wanalipiwa na serikali nje ya utaratibu. Napenda kukutahadharisha, sheria haimzuii mstaafu kuongozana na msafara wa serikali kama anaenda kikazi. Au hata pengine wanaelekea sehemu moja lakini kila mmoja ni kivyake vyake.

Bwa! ha! ha! ha! haijawahi kutokea eti mstaafu kuwalipia wasaidizi wake nauli na kila kitu kwenda majuu na kurudi? Never! Wote hulipiwa na serikali bro!

3.
Baada ya kusema yote haya, sitashangaa kama wale waliopewa jukumu la kusimamia hayo mafao wakaamua kupuuza sheria kwa kuwaonea aibu wastaafu. Haitakuwa mara ya kwanza watendaji kuwaonea aibu viongozi wao wa siasa. Hivi karibuni Tanroad wamejenga matuta kwa kufuata maagizo ya kiongozi wao wa kisiasa ( ambaye si mtaalamu wa barabara) bila kuangalia kama yanakubalika kitaaluma! Wanasheria waliobobea waliangalia tu wakati viongozi wao wakipindisha sheria zinazohusu madini na nishati. Na walipoulizwa walitetea upindaji huo! Sheria kupindwa, kudharauliwa nyumbani haitakuwa mara ya kwanza.

Amandla.....

Hawawezi kuwa wlaikuwa wanamuonea aibu Mwalimu, maana angewauliza pale pale, otherwise noana finally unakubali argument yangu kuwa sheria na ninachokiona ni tofauti, kabisaaa sasa either haipo, imekufa, au ilisha expire.

Ahsante.
 
Mfano mwepesi mwengine. Mtaani tunasema leseni ya udereva tumeitoa trafik. Lakini wote tunajua trafik hawana mamlaka ya kutoa leseni. Wao wanakupa mtihani na kutoa kibali cha wewe kupata leseni. Leseni unaifuata revenue ambao ndiyo wenye mamlaka ya kutoa leseni. At least, ilikuwa hivyo wakati wangu.

Kwenye hili CCM ni trafik na serikali ni revenue.

Bwa! ha! ha! ha! ha! sijui kama hii hoja ina anything to do na sheria butu ya mafao ya wastaafu!

Thanx!
 
1.

Sasa tuko nje ya topic kabisaa, lakini sio tatizo mkuu ndio maana tupo hapa JF ni pamoja na kuitaka serikali yetu ibadili katiba, kwa sababu katiba tuliyonayo imepitwa na wakati, kiongozi wa serikali hawezi kulazimishwa kujiuzulu na chama katika siasa za kisasa za maendeleo,

Halafu haiewezekani sheria iseme mstaafu anatakiwa kusaifiri na wasaidizi wawili, huku tunamuona akisafiri na wasiadizi zaidi ya kumi that is wrong, ndio maana nilisema leteni sheria tukate mzizi wa fitina!


Haya sasa, na katiba nayo imepitwa na wakati! Chama cha siasa kama chama kingine kina haki zote za kumuadhibu na hata kumlazimisha mwanachama wake ajiuzulu kutoka nafasi yeyote kama amepata nafasi hiyo kupitia mgongo wa chama hicho. Chama cha ANC kimemlazimisha Rais wa Afrika ya Kusini kujiuzulu. Nae amekubali kwa sabau hana support katika chama chake. Lakini barua ya kujiuzulu hakumuandikia Mwenyekiti wa Chama chake (Nzuma) bali Spika wa Bunge. Pamoja na kufanya hivyo, angeweza kukataa kujiuzulu na kuki'dare' chama kimfukuze uanachama kwani chama hakikuwa na mandate ya kumfukuza kwenye urais! Mbona Rais Bingu wa Mutharikai wa Malawialikataa kuwa disciplined na chama chake cha UDF na alijitoa na kuanzisha chama chake bila kujiuzulu urais?

Mpaka hapo utakapoweka ushahidi kuwa kweli hao watu zaidi ya kumi wote ni wasaidizi wake ndipo nitakapokubali hoja yako. Zaidi ya hapo ni speculation maana kuongozana na Mkapa si lazima uwe msaidizi wake![/SIZE][/FONT]

2.

Sheria ya mafao mliyoileta inaonyesha ime-expire siku nyingi sana kama haitumiki kabisa, hiyo ndiyo point yangu, kwa sababu haiwezekani wastaafu wote wawe na the same lifestyle, halafu ukasema eti wanai-abuse sheria no way! Haiwezekani ikawa wote toka enzi za Mwalimu!

Unataka kutuambia hata Nyerere alikuwa anaongozana na wapishi na wasaidizi kibao?

Leo unataka kusema Mkapa na Mwinyi na Jumbe na Mwalimu wana'life style' zinazofanana? Au maana ya lifestyle, siielewi? Unahakika gani wao wanategemea mafao yao kama wastaafu kulipia lifestyle yao? Una hakika gani kuwa wake zao ( wafanyabiashara wakubwa) hawalipii hiyo unayoiita lifastyle kama ilivyo kwa McCain?

Sijasema wana abuse sheria. Si lazima wote waliokatika msafara na mstaafu walipiwe na serikali kama sehemu ya stahili ya mstaafu. Sasa kama Mwinyi anaenda Umoja wa Mataifa kuwakilisha serikali katika kongamano ya ukimwi, ulitegemea aende peke yake? Ni lazima ataongozana na watu kutoka foreign, wizara ya Afya na Ofisi ya Waziri Mkuu (TACAIDS). Hawa si sehemu ya stahili yake inayozungumziwa hapa ingawa ukienda kumpokea mizigi airport utaona wote wako nae!

Mkapa yuko kwenye Foundation kadhaa ambazo zinamfanya asafiri kila wakati. Hizi foundation bila shaka zinamlipia gharama zake. Sasa kama huo mkutano anaoenda kuhudhuria kwa niaba ya Foundation yake una mslahi na Tanzania, basi asiongozane na watumishi wa serikali kwa kuhofia kuwa wako watu kama nyinyi mnaohesabu ukubwa wa ujumbe wake?

Mimi sijasema kuwa wana-abuse sheria. Nitasemaje wakati sikubaliani na wewe kuwa hiyo lifestyle unayodai inalipiwa yote kutokana na mafao yao ya ustaafu? Pamoja na hayo, unashangaa nini kuambia kiongozi ana abuse sheria? Mara hii umesahau Richmond na Buzwagi?


3.

Bwa! ha! ha! ha! haijawahi kutokea eti mstaafu kuwalipia wasaidizi wake nauli na kila kitu kwenda majuu na kurudi? Never! Wote hulipiwa na serikali bro!

Umeona wapi hilo? Wewe si unawaona tu wanapoingia na kutoka airport! Au unakuwa nao wanapoomba madurufu ya safari? Unahakika gani kwamba hawa wote wanalipiwa kutoka katika 'vote' ya wastaafu?Unajua lakini utaratibu wa kusafiri serikalini?

3.

Hawawezi kuwa wlaikuwa wanamuonea aibu Mwalimu, maana angewauliza pale pale, otherwise noana finally unakubali argument yangu kuwa sheria na ninachokiona ni tofauti, kabisaaa sasa either haipo, imekufa, au ilisha expire.


Ahsante.

Kwani watu walikuwa hawamuonei aibu Nyerere? Unadhani ile kasri aliyojengewa Butiama aliiomba au aliitaka? Unaamini kweli kama Nyerere angetaka kitu kuna mtu aliyekuwa na ubavu Tanzania kumwambia kuwa hiyo si stahili yake maana inapingana na sheria? Unadhani kila maamuzi aliyokuwa akiyatoa Nyerere alikuwa kwanza anaulizia sheria inasemaje?

Kutofuatwa kwa sheria au kupingishwa kwa sheria hakuna maana kuwa haipo. Ninatofautiana na wewe unapodai kuwa unachokiona tukiamini kuliko sheria iliyopo. Unapodai kuwa unachoona ( kitu ambacho sikiamini) ndiyo stahili ya mstaafu ndipo unapokosea. Unapoendelea kubisha hata hapo unapowekewa sheria ndipo unapoonekana muongo. Ndiyo maana tukakupinga kuhusu mpishi kuwasehemu ya mafao ya mstaafu.

Hakatazwi kuongozana nae lakini si kama sehemu ya mafao au kama mpishi. Pengine ampe cheo kingine kinachokubalika kiutaratibu! Lakini vile vile wahusika wanaweza kufumbia macho na kumuachia aongozane nae? Viongozi wangapi wameongoza na vidosho wao katika safari zao na kuhakikisha kuwa wanalipiwa kila kitu na chombo anachokiongoza hata kama si stahili yake?

Mara ngapi ma'typist' wamebandikwa cheo kikubwa (kwa ajili ya safari tu) ili waweze kuongozana na boss mshikaji? Yote haya hayaondoi ukweli kuwa vitendo kama hivi haviendani na sheria!

Tumefika mahali unapotaka kulazimisha kuwa nakubaliana na hoja zako zisizo na msingi? Pamoja na kukwepa, kupindisha hoja bado haujani'convince kuwa mpishi, au hayo unayodai unayaona ni stahili ya mstaafu. Lakini naona tunaendelea kuuzunguka mbuyu bila sababu na mimi siko hapa ili nimshinde FMeS.

Umeshinda, Mkuu.
 
Kwani watu walikuwa hawamuonei aibu Nyerere? Unadhani ile kasri aliyojengewa Butiama aliiomba au aliitaka? Unaamini kweli kama Nyerere angetaka kitu kuna mtu aliyekuwa na ubavu Tanzania kumwambia kuwa hiyo si stahili yake maana inapingana na sheria? Unadhani kila maamuzi aliyokuwa akiyatoa Nyerere alikuwa kwanza anaulizia sheria inasemaje?

Kutofuatwa kwa sheria au kupingishwa kwa sheria hakuna maana kuwa haipo. Ninatofautiana na wewe unapodai kuwa unachokiona tukiamini kuliko sheria iliyopo. Unapodai kuwa unachoona ( kitu ambacho sikiamini) ndiyo stahili ya mstaafu ndipo unapokosea. Unapoendelea kubisha hata hapo unapowekewa sheria ndipo unapoonekana muongo. Ndiyo maana tukakupinga kuhusu mpishi kuwasehemu ya mafao ya mstaafu. Hakatazwi kuongozana nae lakini si kama sehemu ya mafao au kama mpishi. Pengine ampe cheo kingine kinachokubalika kiutaratibu! Lakini vile vile wahusika wanaweza kufumbia macho na kumuachia aongozane nae? Viongozi wangapi wameongoza na vidosho wao katika safari zao na kuhakikisha kuwa wanalipiwa kila kitu na chombo anachokiongoza hata kama si stahili yake? Mara ngapi ma'typist' wamebandikwa cheo kikubwa (kwa ajili ya safari tu) ili waweze kuongozana na boss mshikaji? Yote haya hayaondoi ukweli kuwa vitendo kama hivi haviendani na sheria!

Tumefika mahali unapotaka kulazimisha kuwa nakubaliana na hoja zako zisizo na msingi? Pamoja na kukwepa, kupindisha hoja bado haujani'convince kuwa mpishi, au hayo unayodai unayaona ni stahili ya mstaafu. Lakini naona tunaendelea kuuzunguka mbuyu bila sababu na mimi siko hapa ili nimshinde FMeS.

Umeshinda, Mkuu.

Sheria yako inasema kuwa mstaafu anatakiwa kusaifiri na wasaidizi wawili tu, nimekuambia hiyo sheria haipo, batili au imekufa, kwa sababu hawa ni baadhi tu ya watu niliona kw amacho yangu Mwalimu alikuwa akifutana nao always, Mosha, Mwakyusa, Balozi Ngaiza, hawa peke ni watatu pamoja na wasaidizi wawili kama sheria yako basi ni watano,

Sitakutajia wengine tuishie hapo tu, mbona wanazidi wasaidizi wawili as of your sheria? Kama Mwalimu alikuwa na ubavu kuliko sheria basi hiyo sheria haipo au ni dead from the beggining, au?

Bwa! ha! ha! ha! ha! ha! ha!
 
Yale yale maneno yako ya chooni ambayo huwa hayana elimu, bali ni kutaka kujionyesha kuwa unajua sana wakati hujui kitu, sheria yenu ni batili na mufilisi, au haipo kabisaa,

Outlandish na bizzare, sidhani kama kuna tatizo hapa JF kuhusu nani hasa mwenye hiyo tabia ya kuleta uzushi, wewe ni masikini ya Mungu, confused na hata huelewi unachosema, ninaamini wananchi wengi hapa JF walishakusamehe maana wanajua how unaweza kuleta outlandish na bizzare ukiamua, hoja zimewashinda sasa unajaribu kuleta viroja, ninakuonea huruma sana mkuu maana sijawahi kuona an idiot mfano wako!
0749852143.gif
 
MISHAHARA YA VIONGOZI-RAIS ZAIDI YA MIL 1

Nakumbuka kuna wakati gazeti moja (nimesahau jina) limewahi kuandika mishahara ya mawaziri na Rais; kwa mujibu wa gazeti hilo mawaziri wa kawaida walikuwa wakilipwa 750,000, waziri mkuu 900,000 na Rais 1,200,000.

Enzi hizo zilikuwa za Sumari, ooh sorry, Sumaye. Kwa misingi hiyo basi mshahara wa rais ungekuwa zaidi ya Mil1 kwa wakati huo wa mawaziri wake. Sasa basi sasa hivi mshahara wake utakuwa zaidi ya Mil moja.

Au utakuwa umeshuka wazee?.😛
 
Nakumbuka kuna wakati gazeti moja (nimesahau jina) limewahi kuandika mishahara ya mawaziri na Rais; kwa mujibu wa gazeti hilo mawaziri wa kawaida walikuwa wakilipwa 750,000, waziri mkuu 900,000 na Rais 1,200,000. Enzi hizo zilikuwa za Sumari, ooh sorry, Sumaye. Kwa misingi hiyo basi mshahara wa rais ungekuwa zaidi ya Mil1 kwa wakati huo wa mawaziri wake. Sasa basi sasa hivi mshahara wake utakuwa zaidi ya Mil moja. Au utakuwa umeshuka wazee?.


Great contribution, angalau kuna some education in it! Na sio bendera fuata upepo! Bwa! ha! ha! ha! ha!
 
THE POLITICAL SERVICE RETIREMENT BENEFITS ACT, 1999 No. 3
Grant of Benefits to former President, Part III (i) 9 (3)
If the former President is requested by the Government to travel outside the United Republic, the appropriate authority shall meet all First C1ass traveling which expenses shall also cover expenses for the spouse and two Assistants


Talking about nonesense, haiwezi kwenda lower than this! Wakati sheria inasema one thing na viongozi wanafanya another thing, lakini kuna wanoililia kuwa ni sheria, hii sio sheria, lazima kuna nyingine ambayo ni uptodate than this.

Thanx!
 
Talking about nonesense, haiwezi kwenda lower than this! Wakati sheria inasema one thing na viongozi wanafanya another thing, lakini kuna wanoililia kuwa ni sheria, hii sio sheria, lazima kuna nyingine ambayo ni uptodate than this.

Thanx!

Weka basi iliyo up to date! Kwako wewe hao viongozi ni miungu? Kwa hiyo wanachokifanya ni zaidi ya sheria au wote ni watiifu na wanafuata sheria? Sasa kwa nini mnakazania kumkoma nyani whatever kama hakuna kiongozi anayevunja sheria? Au ni wale tu unaowachagua wewe, mzee wa dataz?

Huchoki uongo? Kuna muungwana alisema "uchizi ni kufanya kitu kile kile kila wakati na kutegemea matokeo tofauti"! Vile vile kusema kile kile kila wakati na kutegemea matokeo tofauti! Kwa vile sitaki kuonekana chizi, sitaki kurudia yale yale kila wakati na kutegemea utaelewa! Mtu usiyeelewa tofauti ya katiba na sheria! Unayesema sheria ime'expire'! Unayedai kuna specification ya kazi! Unayeamini unayoyaona zaidi kuliko sheria tawala!

Hapana, FMeS! Ndiyo maana nimesema umeshinda! lakini bado hauridhiki! Unataka uambiwe nini?
 
Weka basi iliyo up to date! Kwako wewe hao viongozi ni miungu? Kwa hiyo wanachokifanya ni zaidi ya sheria au wote ni watiifu na wanafuata sheria? Sasa kwa nini mnakazania kumkoma nyani whatever kama hakuna kiongozi anayevunja sheria? Au ni wale tu unaowachagua wewe, mzee wa dataz?

Huchoki uongo? Kuna muungwana alisema "uchizi ni kufanya kitu kile kile kila wakati na kutegemea matokeo tofauti"! Vile vile kusema kile kile kila wakati na kutegemea matokeo tofauti! Kwa vile sitaki kuonekana chizi, sitaki kurudia yale yale kila wakati na kutegemea utaelewa! Mtu usiyeelewa tofauti ya katiba na sheria! Unayesema sheria ime'expire'! Unayedai kuna specification ya kazi! Unayeamini unayoyaona zaidi kuliko sheria tawala!

Hapana, FMeS! Ndiyo maana nimesema umeshinda! lakini bado hauridhiki! Unataka uambiwe nini?

Mkuu mimi ninakata ishu, I could care less kama upo au haupo, na huwezi kunikataza kutumia haki yangu kuchangia hapa JF kwa sababu sijakukataza sasa kwa nini unataka kuni-limit haki yangu,

Ninasema hivi sheria yako haitumuki, na haiwezekani kuwa ni valid ni lazima kuna nyingine iliyofanyiwa marekebisho kama alivyoshauri mtu mmoja huko nyuma na mimi ninakubaliana na huyo aliyesema hivyo, ninasema hivi this week nimewaona wastaafu wengi wakelekea NY, na ninajua kua sasa wako huko, wamesafiri na makundi makubwa sana ya wasaidizi as opposed na sheria yako, sasa for that you can call me whatever you want lakini siwezi kubadili msimamo wangu kuwa hiyo sheria yako ya wasaidizi wawili is dead au haipo, kama haiku-expeire,

one thing huwezi fanya ni kuninyamazisha, that you can't!
 
Back
Top Bottom