Misaada ya EU imerudi kwa masharti yaleyale, japo....

Bavicha mnajitekenya na kucheka wenyewe.
EU waliamua kusitisha misaada,si Rais,Makamu wala waziri yoyote aliefunga safari kwenda kuwalamba miguu.
Zaidi tuliwaona chadema wakiwa kwenye bunge la ulaya,wakishindilia fitna eti tusipewe misaada.
Haiingii akili serikali eti ikubali misaada kwa masharti wakati ilishaamua kufa na tai.
Hapa bavicha mnatakiwa mjadili matunda ya ziara zenu kwenye bunge la EU,na mualiko mliompa balozi wa EU Tanzania pale bungeni zimezaa nini?
 
Bavicha mnajitekenya na kucheka wenyewe.
EU waliamua kusitisha misaada,si Rais,Makamu wala waziri yoyote aliefunga safari kwenda kuwalamba miguu.
Zaidi tuliwaona chadema wakiwa kwenye bunge la ulaya,wakishindilia fitna eti tusipewe misaada.
Haiingii akili serikali eti ikubali misaada kwa masharti wakati ilishaamua kufa na tai.
Hapa bavicha mnatakiwa mjadili matunda ya ziara zenu kwenye bunge la EU,na mualiko mliompa balozi wa EU Tanzania pale bungeni zimezaa nini?
Sio kila anaeandika hapa ni bavicha mkuu.
Nimekuwekea link hapo ya habari kamili si usome? Acha kupotosha watu kama huna facts, muulize waziri Mpango atakuelewesha.
 
Mnyarwanda anaongoza mazungumzo kwa niaba ya serikali ya Tanzania?

Ni kiasi gani wanywaranda sasa wanaingia na kutoka serikalini? Ni nani alimpa kazi hiyo na amelipwa nini? Alitumwa na kukubaliwa na kagame?

Ameweza kupata siri ngapi za nchi na kuzipeleka idara ya usalama ya Rwanda? Hawa watu wanaingia mpaka jikoni kujua tuna akiba ya chakula kiasi gani!! Usalama wa fedha na uchumi ni usalama wa Taifa

Wako maafisa nguli nchi hii tangu enzi ya Mkapa walioongoza majadiliano magumu kabisa mpaka tukasamehewa madeni,hawaaminiki?

Katibu Mkuu Fedha haaminiki? Kwa nini yuko hapo?

Je ni masharti gani hayo?

Haya ya kutaka watu wafanye mikutano ya hadhara ? Haya ya uchaguzi wa Zanzibar? Haya ya sheria za mitandao? Haya ya demokrasia? Nani anazuia na kwa faida ipi kwa taifa? Wangapi wamekufa kwa kukosa madawa hospital I kutokana na kukosa misaada na wangapi wanaishi kwa kuzuia mikutano ya hadhara?

Haya mambo ambayo kagame anaongoza kwa kuyakiuka eti leo inaonekana ana nafuu mpaka anaenda kutubembelezea kwa wahisani?
Hawa wanyarwanda tunaowapandikiza katika nchi hii bila kutazama madhara yake baadaye itakuja kutugharimu kama inavyo wagharimu wakongo ambao waliwapa nafasi hadi jeshini na ndicho kinacho wagharimu mpaka leo na kwa jinsi inavyosemekana hata Joseph kabange ndezira kabila ni mnyarwanda. Watanzania tuweni makini tuache tabia ya kupiga makofi bila tafakuri.
 
Misaada kutoka nchi za Ulaya imerudi kwa gharama. Taarifa za ndani ni kwamba nchi za Ulaya zilikataa kabisa kutoa misaada kwa Tanzania. Tukalazimika kumtumia mtu wa kati, Rais Mstaafu wa Benki ya Afrika Donald Kaberuka, kutuunganisha na nchi za Ulaya.

Misaada inarudi kwa masharti ambayo tumerudhia:
1) Kuheshimu demokrasia, pamoja na kuruhusu vyama vya siasa vifanye kazi bila vipingamizi vya serikali
2) Utatuzi wa mgogoro wa Zanzibar
3) Utawala wa sheria
4) Uhuru wa maoni
5) Uhuru wa vyombo vya habari
Hii ya uhuru wa mitandaoni lazima ni kweli kwani Siku hizi siwaoni TISS wakitugasi uku Facebook. Naona kidogo tunaanza kuheshimiana hasa kiheshimiwa
 
Tanzania ni nchi tajiri. Sisi ndio tunatakiwa kuwapa misaada wao siyo wao kutusaidia sisi - Lorry driver

Duh hii ndo inaitwa nightmare. Wewe unayelia njaa ndo ukawasaidie wazungu. Wewe hata kujisaidia huwezi ndo uwasaidie wengine. Hili sahau over and ever
Nchi za kiafrika zilipewa Uhuru wa bendera,kiuchumi bado jamaa wanatawala na huu ni ushahidi tosha,kimsingi viongozi wa kiafrika ni magavana wa G7, na wazungu waliona ili kupunguza misuguano,ngoja tuwawekee waafrika marais wanaotokana na wao,lakini uchumi tubaki nao,

Miaka michache ijayo Dhahabu iliyoko Geita,Shinyanga, itakuwa imechimbwa yote na kuhifadhiwa kwenye maghala ulaya,na marekani,sisi tutabaki na ardhi tupu tukilima mtama,na baadae tutaanza kununua Dhahabu ulaya kuleta afrika
 
Wewe ndio hamnazo. Hiyo ni vision ya Rais that Tanzania is going to be a Donor Country. Aliyekuambia itakuwa baada ya mwaka mmoja ni nani! Namuelewa Mh. Rais Kuchagua Madoctor na maprofessor ndio wanaomulewa . Sisis kina kapuku huku tujishebedue katika level yetu ya Mtandaoni!

Sio sisi ni kapuku... Washauri wake toka CCM ndo kapuku pia vilaza mpaka anachukua viraka vya ACT ah ah ncheke mieeer
 
Ni raia wa nchi gani?

Kimsingi hana haki za kiraia hata kama ana nia njema kiasi gani,huwezi kutumikia mabwana wawili,Rwanda na Tanzania
You are just a small boy! Hujui haya majambo. Dr kaberuka alikuwa president wa Afdb ambayo ni sawa na world bank ya africa. Kubali kuelimishwa young man. Maswali unayouliza yanaonyesha ulivyo
 
Hawa wanyarwanda tunaowapandikiza katika nchi hii bila kutazama madhara yake baadaye itakuja kutugharimu kama inavyo wagharimu wakongo ambao waliwapa nafasi hadi jeshini na ndicho kinacho wagharimu mpaka leo na kwa jinsi inavyosemekana hata Joseph kabange ndezira kabila ni mnyarwanda. Watanzania tuweni makini tuache tabia ya kupiga makofi bila tafakuri.
Kuna mmoja alikuwa jeshini na cheo kikubwa enzi za
You are just a small boy! Hujui haya majambo. Dr kaberuka alikuwa president wa Afdb ambayo ni sawa na world bank ya africa. Kubali kuelimishwa young man. Maswali unayouliza yanaonyesha ulivyo
"Alikuwa" ni zamani

Umemaliza darasa la saba?
 
Huu ulikuwa mgogoro kati ya wahisani na serikali ya Tanzania. Msuluhishi alihitajika. Kaberuka is not just another Mnyarwanda. Alikuwa rais wa Benki ya Afrika na Tanzania ilifaidika sana wakati wa urais wake. Essentially, an outsider, neutral person with impeccable credentials was required.
 
Hata ukiwa na PhD lazima umalize darasa la saba. You seem to be naive am sorry lazima tuwaelimishe nyie watu.
Wewe ndiye unastahili elimu,mpaka sasa unaona ni sawa Mnyarwanda kuzunguka dunia nzima kwa nauli ya watanzania eti akituombea msamaha kwa wafadhili

Makosa yenyewe ni ya kurekebisha tu sisi wenyewe,kuruhusu mikutano ya hadhara mpaka tushauriwe? Kuruhusu demokrasia mpaka tushauriwe?

Hivi vitu vilikuwepo tangu Nyerere akiwa hai, na yeye kama baba wa taifa aliona havina tatizo,sisi wa miaka hii tunajiona wajuaji,haya sasa,hospitali hazina dawa,na hata hizo hela za wafadhili haziji ghafla,ukitangaza sasa mikutano ya hadhara ruksaaaa,inakuja mia tano,bunge laivu,mia mbili,utaongea na maalim,inakuja milioni moja,unarekebisha sheria ya mitandao,wanakupa milioni mbili, ni piece by piece,hela inatolewa kwa action plan iliyowekwa na mzungu mwenyewe
 
Kuna ule mchanga aliouzuia Bandarini nao utamtokea puani soon
Hapo ndio patamu,mkataba tumesaini wenyewe kuwaruhusu kupeleka mchanga,na wao wakasaini mikataba lukuki na kampuni nyingi zikiwemo za malori ili kusafirisha,meli, na kiwanda cha kuchenjua,yote imevunjwa!!!

Na haya makampuni ya madini ni Multinational,unapo deal nayo fanya au assume unadeal na serikali ya nchi yalikotoka,iwe Canada,Marekani,Uingereza,yanabeba bendera ya nchi yaliyotoka,na yanaweza kulilia protection ya mother countries.

Pia mengi hutumia mikopo ya mabenki makubwa makubwa duniani au taasisi kubwa kubwa duniani ambazo zinaweza kuwa na impact

Ni sawa na Carl Peters alipokuja kutafuta makoloni,alikuwa na kampuni inaitwa Germany East Africa Company,machifu wakasaini mikataba wakijua wanasaini na mzungu mmoja tu,baada ya kusaini ndipo wakajua walikuwa wana deal na nchi ya ujerumani
 
Kwanza nianze kwa kusema, naunga mkono juhudi za Rais wetu kutaka Tanzania ijitegemee. Ni mtazamo wa watanzania wengi tu na hata vyama vya upinzani wameliongelea sana suala hili.

Misaada ambayo Rais wetu amepokea juzi toka kwa umoja wa ulaya imerudi kwa masharti yaleyale, The Citizen linaripoti. Kwa mujibu wa gazeti hilo licha ya msimamo wa Rais kuhusu misaada toka nje, ilikuwa vigumu kwa bajeti ya 2016/2017 kutekelezeka kama mchezo wa paka na panya ungeendelea.

Ukweli ni kwamba watu kutoka serikalini walikuwa wanafanya jitihada nyuma ya pazia kuokoa jahazi kwani ilikuwa bayana kwamba misimamo wa kisiasa wa Rais wetu ulikuwa haumsaidii yeyote.

Wakati Rais Magufuli akiendelea kutuaminisha wananchi masikini kwamba wahisani hawana tena nafasi ya kutupangia masharti, inaelezwa kuwa wawakilishi wa serikali walijadiliana mpango ambao kimsingi utamfanya mkuu wa nchi aendelee kuyaishi masharti yaleyale ambayo alijinasibu huko nyuma kuwa hatoyakubali asilani.


Naishauri serikali na Rais wetu, ukimya nao una busara zake katika kufanya maamuzi na kuweka mambo sawa, "tusitukane mamba kabla hatujavuka mto", tusipende kuongea sana kwa kufurahisha genge, “twende strategically” tutafika. Kwa madhara yaliyotukuta safari hii kwa bajeti yetu ya 16/17 kupumulia mashine hili liwe fundisho kwetu sote.

Ushauri kwa wasomi wetu, acheni kujipendekeza, mwambieni Mh. Rais ukweli, ongeeni ukweli kwa faida ya Taifa letu na vizazi vijavyo. Msiongee kumpendezesha Mh. Rais ili tu muonekane.


Mwisho, shukrani za pekee kwa bosi wa zamani wa Africa Development Bank Ndg. Donald Kaberuka kwa kuongoza mazungumzo yaliyofanikisha misaada tuliyoshuhudia ikirudi wakati Rais wetu alipokutana na Balozi wa Umoja wa ulaya.


Mungu ibariki Tanzania
Nitajie mashrti matano tu tuliyokuwa tumepewa na inabdi tuyatekeleze
 
Sitaki kumsingizia mchawi, Ila tuna shida ya jinsi tunavyo fikiria, hayo uliyo ainisha ni aibu kuhimizwa kuyatekeleza. Yanatakiwa kuwa sehemu ya maisha yetu ya kila siku.
Na yalikuwa sehemu ya maisha yetu kwa karibu miaka thelasini,na hapakuwa na tatizo!!
 
Huu ulikuwa mgogoro kati ya wahisani na serikali ya Tanzania. Msuluhishi alihitajika. Kaberuka is not just another Mnyarwanda. Alikuwa rais wa Benki ya Afrika na Tanzania ilifaidika sana wakati wa urais wake. Essentially, an outsider, neutral person with impeccable credentials was required.
Umeniamsha vizuri na nusu siku yangu.
True, we needed someone with reputation and trustworthiness who would stand for professionalism and ethics without the fear of putting their political or government position in jeopardy.
 
Nitajie mashrti matano tu tuliyokuwa tumepewa na inabdi tuyatekeleze
Kama miaka yote hii hujui tunapokea misaada kwa masharti yepi unanitia mashaka sana kama kweli wewe ni Expert Member, na sina namna ya kukusaidia, you are a thinker, jiongeze.
Hint: mtafute mpango, au hata Zitto Kabwe yuko vizuri, ukikwama kuwapata muone mstaafu Likwelile yeyote kati ya hao atakujuza.
By the way hata kwenye uzi huu thinker wameainisha baadhi, usiwe mvivu kusoma mkuu.
 
Unajua Wazungu wanaifahamu vizuri sana Afrika naweza sema kuliko waafrika tunavyoihamu Afrika. Wana kumbukumbu ya vitabu vinavyoelezea Afrika kwa kina miaka 300-400 iliyopita, lakini pia wamekuwa involved na plan zote za maendeleo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii kwa Bara la Afrika hata baada ya kuondoka.

Wao wanachoamini ni kwamba viongozi wa kiafrika wanapatikana 'by chance". Lakini pia wanakuwa hawana uelewa wa kutosha wa changamoto kiasi gani walizonazo watu wao na nchi yao na hivyo kukosa dira ya maana ya kuziondoa. Mara nyingi wanawachukulia poa tu kwani wanajua wakiendelea kuishi kwa fikra za viongozi hao, watawaathiri wananchi zaidi. Kwahiyo hata huyu walimchukulia poa tu. Walijua akishajua ugumu wa urais na changamoto halisi za nchi yake ataanza kufikiri sawasawa.

Hakuna asiyejua usmart wa Nyerere au Mkapa. Lakini walikuwa makini sana katika kukosoa mataifa makubwa. Wengine tuliposikia yale, tukacheka tu kwani tukajua ni harakati pasipo mkakati.
Nami niweke neno kidogo. Awam ya tano iliingia ikiwa focused na kujitegemea,ni jambo jema sana. Lakini kila jambo lina hatua.Matamko ya kisiasa yalikua ni mengi bila ya kufanyika utafiti. Kwa mfano trend yetu ya makusanyo yalifahamika kwa miez mitatu ya kwanza kuwa ni Tsh 1.12 hadi1.3+Tn/- kwa mwezi. Hii trend tayari kwa mtu makini angejua tu hatuna hela za kutosha kuendesha nchi kwa 100%.Hivyo ilitakiwa kuchunga maneno ya kuongea. Kwa maana hiyo makusanyo kwa mwaka unaona kabiasa isingeweza kufika Tsh 15.5tn/- kwa mwaka. Sasa unapopitisha bajeti ya 29tn/- huku uwezo wako wa kukusanya ni nusu tu ya bajeti yako,basi jua bado utalazimika kuwa mtumwa wa IMF,WB,ADB na misaada ya Nchi za Magharibi ambao wao kamwe hawawez kutoa misaada ukienda nje ya matakwa yao. Hili ni somo kubwa la kujifunza.
 
Back
Top Bottom