Mimi sijasoma kitabu hata kimoja tangu nimalize chuo.

Mimi sijasoma kitabu hata kimoja tangu nimalize chuo.

Mimi nimesoma vitabu elfu moja na majarida elfu nane mwaka uliopita mkuu
 
Hata kusoma hadithi au tamthilia? Vipi masuala ya dini, Biblia au Kuraan?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hadithi sisomi kabisa niliacha zamani sana, biblia na Koroani nimewaachia ma padri, wachungaji, mapastor, manabii na masheikh wafanye kazi yao wao nikienda kwenye ibada watanisimulia. Nikisoma halafu nikienda kusali/kuswali tena wakisoma biblia/koroani naona najipotezea muda bora huo muda nilale kuupumzisha mwili.
 
Yoote kwa yote, account yako ya benki inasoma ngapi, hicho ndio cha msingi.
 
chaajabu nikisoma kurasa 30 napata usingizi wa kutosha.
Hivyo sijawahi kumaliza kitabu 2018.

2019 nitaanza na kiyabu cha alfu lela ulela "sp"
Hahaha endelea hivyo hivyo maana inakusaidia kupata usingizi. Kuna wengine huwa wanaandika humu hawapati usingizi mpaka wanywe pombe, ambayo ni gharama na hatari kwa afya zao. Ikiwa kitabu kinakusaidia kupata usingizi basi usiache kushika shika hicho hicho muda uleule unaotaka kulala.
 
Yoote kwa yote, account yako ya benki inasoma ngapi, hicho ndio cha msingi.
Yani iko safi na natatua matatizo yangu binafsi na kiasi ya familia yaani wazazi na ndugu na jamaa.
Hakuna kitabu kinaongeza salio kwenye account hata wakisoma encyclopedia volume zote.
 
maisha ni yako..
uzuzu ni wako..

usiwaze wala nini mkurugenzi
Hahaha nilidhani kuna kitu napungukiwa, kujistukia tu. Nimeona list za wasomaji zikanitisha.
 
ukikaa na watu unaongea nini??
Maongezi yaliopo huwa nasikiliza na kuchangia inaponidi, na inategemea hasa na mazungumzo yenyewe, siwezi kucomment mambo ya space science, au terrestrial theories siyafahamu zaidi ya kusikia tu.
Ila ni msikilizaji mzuri.
 
Mimi tangu 2001 sijasoma kitabu chochote zaidi ya heading za magazeti vituo vya mabasi. Naona niko sawa tu au ninatatizo nisilolifahamu.
Waungwana msaada.
Kama umemaliza chuo 2001 na bado unapanda dala dala mpaka leo, life yako haiko poa na hilo ndilo tatizo. Umeridhika na dhiki ndo maana unaona life iko poa tu. Ukianza kusoma vitabu mwaka huu 2019, huenda ukaambulia ka Vitz.
 
Kama umemaliza chuo 2001 na bado unapanda dala dala mpaka leo, life yako haiko poa na hilo ndilo tatizo. Umeridhika na dhiki ndo masna ubaona life iko poa tu. Ukianza kusoma vitabu mwaka huu 2019, huenda ukasmbulia ka Vitz.
Hahaha kusoma hakuleti vits, kweli nimeridhika sana.
 
"Ni vyema kujifunza mengi na sio kujua kila kitu"

Mkuu uko fresh tu, kusoma magazeti na Jf inatosha, ongezea na career yako kiaina (sio lazima)
 
Huwezi kuwa sawa na anaesoma vitabu kila siku wakati wewe umesoma mara ya mwisho 2001. Hata kama maisha yanaenda poa ila usiseme eti mko sawa.

Kwangu mimi naamini siwezi kuwa well informed na kujua mambo kama sisomi vitabu, majarida n.k

Ukitaka hata kujenga hoja huwezi kwenda sawa na anaesoma maana mwenzio anajua mambo kibao ambayo wewe hujui hata kama yana exist
Hawa ndio wale wanasema rais wa Kuwait ni Sadam Hussein
 
Back
Top Bottom