Mimi ni Polisi: Kisa cha mke wa Waziri

Mimi ni Polisi: Kisa cha mke wa Waziri

kuwepo wanapaswa kuwepo maana ndo sehem ya ajira wanapaswa wawe na ajira,sijawazuia,,,,,,na sina mamlaka hayo ya kuwazuia na wengi wanaingia kwakua wamefeli au wamekosa fursa nyingine za maana,naona unatoa mishipa kuwatetea afande Daniel

hahaha kijana wangu, nashukuru kwa kunipa tittle ya uafande japo moshi sijafika, sijawatetea ila nimejaribu kuonsesha umuhim wao kwangu na nchi kwa ujumla, matatizo yako binafsi hayatuzuii wengine tusijivunie jeshi letu lenye kulinda mali.zetu na sisi wenyewe
 
hongera kwa kuwa na kazi ya kuwapachika watu makabila,,,zama hizi bado unawaza ishu za ukabila mi si muha mi ni mtanzania tu,,,sasa wewe unadhan jeshi litafanya kaz kwa ufanisi ikiwa halina vitendea kazi,,,haina logic unaenda kutoa maelezo polisi anaandika insha,RB unapewa kipande cha karatas kama cha kufungia bhangi,,,,,makaz yao wanalala kwenye nyumba za mabati,huo ufanis utatoka wapi???

endelea kusoma hadithi ya mentor, hapa hatuzungumzii changamoto za polisi
 
Nasisitiza una matatizo yako binafsi. Ulitaka awe wapi? Tinailalamikia kila siku kuharibu kwenye chaguzi na sababu tunazotoa hawakusoma. Leo unatajiwa mwenye phd unasema anafanya nini huko? Huoni kama wewe ni tatizo? Haya ulitaka wawepo watu gani?

Na je changamoto za uhalifu wa sasa watazitatua kwa kuwa na watu gani? Na siyo pekee, kuna mmoja ni mhimu sana kwenye shule ya sheria udsm bado ni police.

Kwa taarifa tu, Dr. Enos Robert Lukyaa-Phd, yupo Israel for a study tour. Tutarajie maendeleo ya jeshi la polisi kupitia yeye. Wala usimkatishe tamaa

kama unadhan watu unaowahesabu kuwa watatatua changamoto za Polisi unakosea,mfumo wenyewe wa kuwapeleka vijana CCP si salama,now wanapeleka form mashuleni kwa ajili ya form IV na VI wakajiunge na jeshi,,,,,why wasingekuwa wanachukua degree holders ndo wakaanzie ccp,,,,mpaka ukute polisi mwenye maono ndo anaamua akasome,na mostly huwa wanakataliwa na wakubwa zao kwa sababu ya kutetea nafas zao,,,,maana hawakusoma,zaid ya kozi za kipolisi,,,kwa zama hizi za wizi wa mtandao jeshi uanona limejiandaa kwa dhat kupambana na wizi huo???hapo dsm ni central tu ndo wana unit ya cyber crime,,,nenda Oysterbay ingia vyumba wanavyochukulia maelezo hata panya hawez kuishi,,,,,,,me siongei kwa kubahatisha nachokiandika ndo kipo,na pia kwanin ongezeko la hao polisi wezi,majambaz limekua kubwa?????,,ni kwa sababu wanaona hata wajuu yao hawana maadili,ndo mchezo walioukuta,,,,kusindikiza magendo,kubeba bangi,kubadili vidhibit vya cocaine kuwa sembe la mahindi,,,,,
 
hahaha kijana wangu, nashukuru kwa kunipa tittle ya uafande japo moshi sijafika, sijawatetea ila nimejaribu kuonsesha umuhim wao kwangu na nchi kwa ujumla, matatizo yako binafsi hayatuzuii wengine tusijivunie jeshi letu lenye kulinda mali.zetu na sisi wenyewe

wangekua wanalinda malie wasingekua wanafungwa kwa ujambaz,,,,,,,,unajivunia polisi ambao wananjaa,hata sare wanashindwa kushona,wawezeshe
 
hahaha kijana wangu, nashukuru kwa kunipa tittle ya uafande japo moshi sijafika, sijawatetea ila nimejaribu kuonsesha umuhim wao kwangu na nchi kwa ujumla, matatizo yako binafsi hayatuzuii wengine tusijivunie jeshi letu lenye kulinda mali.zetu na sisi wenyewe

wangekua wanalinda malie wasingekua wanafungwa kwa ujambaz,,,,,,,,unajivunia polisi ambao wananjaa,hata sare wanashindwa kushona,wawezeshe,huenda unakula kwa mgongo wa polisi,wakifanya vizur watasifiwa,,,
 
Ndo maana nasema wewe una matatizo yako binafsi. Na huna taarifa sahihi. Kuna baadhi ya mikoa ambapo wako connected na wireless internet. Ni wewe kuwa na pasword unapata huduma ya mtandao kabisa.

Kama mkoani uliko hawajaunganishwa, usiseme ni mikoa yote. Nenda polisi mwanza pale hata smart phone itakupa alert za wireless internet

so kama una-access internet mwanza ndo una-conclude polisi wako smart????hamishia kwako haya matatizo mdau
 
Mentor mbona waturusha roho hivi jamaniii,tupe full storyy
 
Last edited by a moderator:
Tusubirie tena??? Dah, kweli mtaka cha uvunguni sharti apinde mgongo!
 
"Ukikataa kwenda shule utakuja kuwa kama Yule pale."

hahahahahahaha Mentor kweli kuna watu wana madharau duniani.

".....Amdharauye mwenzake atenda dhambi"
 
Maisha yaliendelea hadi siku hii ya 07/08/2001. Nilipangwa lindo kwa Waziri mmoja ambaye kwa minajili ya maadili ningeomba nisimtaje jina wala wadhifa.

Kupangwa lindo kwa viongozi kulikuwa na faida na hasara zake. Kulikuwa na viongozi waliokuwa na utu sana. Kama mmepangwa jioni mtaandaliwa maji ya kuoga, chakula cha jioni na mnakuta chumba chenu cha ulinzi (centry box) kimepulizwa dawa ya mbu na kufanyiwa usafi na asubuhi mnapewa chai kabla hamjaondoka.

Sitaongelea kwa waziri mmoja hivi ambaye ukifika kwake hata salamu haji kuwapa, hakuna huduma yeyote ila sasa uchelewe kufika dakika moja tu kesi yake utaisimulia.

07/08/2001…Jumanne

Siku hii nilipangwa lindo kwa mheshimiwa waziri huyu. Ilikuwa lindo la asubuhi. Kama kawaida na sheria, inatubidi tufike eneo la lindo robo saa kabla ya muda wa lindo. Na kawaida yangu nilikuwa napenda sana kutunza muda. Hata askari wenzangu walikuwa wakijua na wengi walikuwa wakifurahi ukipangwa lindo ambalo Mentor ndiyo anakuja kuku-leave unafurahi kwani una uhakika wa kuondoka kazini kwa muda.

Tulifika nyumbani kwa waziri saa 05:45 asubuhi na kukabidhiana lindo na kisha kuanza kuzunguka kuhakikisha kote ni salama.

Ni hadi ilipofika saa kumi na mbili na nusu asubuhi niliposikia kelele za mtoto akilia. Alikuwa ni mtoto Tina. Tina alikuwa darasa la sita na asubuhi hiyo kama asubuhi nyingi ambazo nimewahi kuwa lindo kwa waziri huyo alikuwa akilia kwa kutokutaka kwenda shule. Mama yake alisikika akimkaripia kuwa avae haraka asijeachwa na basi la shule.

Kalikuwa na akili lakini kalidekezwa sana. Ni wale watoto waliorushwa madarasa kwani pamoja na kuwa darasa la sita alikuwa ameruka darasa la kwanza na la tatu hivyo kihalisia alikuwa mdogo.

Tinna alitoka nje huku akilia; hajavaa tai, viatu, hajabeba begi wala kuchukua ‘lunch box’ yake. Nilimuangalia anavyolazimishwa kwenda shule nikakumbuka wakati nipo kijijini. Nilimuonea wivu kwa bahati anayoipata ya kuweza kwenda shule kwa starehe vile. Nilitamani bahati ile ingeniangukia mimi. Nilishindwa kuendelea na shule kwa kuwa mama yangu mjane alishindwa kunilipia ada ya chuo baada ya kushindwa kupata daraja la kwanza hivo kuwa vigumu kupata mkopo wa kusoma chuo.

Mama Tinna alimwita Tinna nje na huku amebeba viatu vyake. Tinna alikuwa akikataa kuvaa viatu akisema hataki kwenda shule.

Ndipo mama yake Tinna alipotamka maneno ambayo hadi kesho hayatokaa yafutike akilini mwangu. Mama Tinna alimshika Tinna kwa nguvu na kisha akamwambia (huku akininyoshea kidole), “Ukikataa kwenda shule utakuja kuwa kama Yule pale.”

.
.
.
.


2008, November

Kwa ufupi tu: Nilibahatika kupata ruhusa ya kwenda masomoni mwaka 2006. Nilikuwa nimeomba kwenda kusoma masomo ya Uhasibu na kukubaliwa kujiunga na chuo cha uhasibu cha Arusha (IAA). Niliomba ruhusa kazini na kukubaliwa kuhamia mkoani arusha.

”Hallo mentor” Nilipokea simu kutoka kwa lecturer wangu wa Business Mathematics. Kipindi hiki nilikuwa mwaka wa tatu wa masomo yangu na kwa kuwa nilikuwa na masomo machache muhula huo mwalimu huyu alikuwa akipenda sana kuniomba nimsaidie kusahihisha mitihani/tests za wanafunzi wa mwaka wa kwanza. Kwa kweli nilipenda hesabu na kufundisha hivyo sikuona shida, nikawa namsaidia.

Aliendelea, “Aisee, nimeamka sijisikii vyema kidogo naomba uende darasa langu la first year ukawasaidie kufanya masahihisho ya test ya juzi.”


Itaendelea tena Jumatatu...

Mungu ni mwema; watu wengi wenye uwezo hasa wale wenye mali lakini hawakusoma mali zao hutoweka mara wanapofariki na watoto wao hurudi kwenye kundi la walevi. Wale watoto wa maskini pamoja na kusoma kwa kuunga unga baadaye hujikuta wana mafanikio kimaisha kuliko wale waliokuwa watoto wa matajiri.............Tatizo ni kwamba tukishakuwa na mafanikio tunawalea watoto wetu katika maadili ambayo nao wanakwenda kuwe kwenye kundi la walevi
 
Mimi ni Polisi: Kisa cha Mke wa Waziri


“Yanyukwe....Yakobolewe” (hii iliashiria kupiga makofi)

“Ipo siku moja nitarudi nyumbani, kwa baba na mama nikiwa kamanda… (repeat)”

Weka changer…

“Mama nipokee, nimechoka zangu na safari, nimetoka zangu Msumbiji na bunduki yangu mkononi mama..(rudia kiitikio)”

“Malela! Malela! Malela (Malela)…Malela! Malela wangu namtafuta! Nimesikia Malela yupo Tabata, Malela! Malela! Malela wangu namtafuta”

Badilisha CD hiyo hatujafiwa hapa…

“Isamawela, isamawela..Isamawela Isamawela (isamawelaaa);
Tutamaliza, tutamaliza..tutamaliza, tutamaliza… (huu wimbo una-emotion jamani)”

“Ugonile ndaga (ugonile ndaga fijo) ugonile ndaga (ugonile ndaga fijo)
Ugonile ndaga fijo (ugonile ndaga fijo)

Wanyakyusa wosa (ugonile ndaga fijo)..ugondile ndaga fijo (ugonile ndaga fijo)
NA wapare/wachaga/wakurya/wajita/wasukuma/insert tribe (ugonile ndaga fijo)…ugonile ndaga fijo (ugonile ndaga fijo)”

“Mama Jeniii mamaa (mama Jeni), Mama Jeni (mama Jeni) ouoo (Mama Jeni)…;

Mama Jeni nitarudi (Mama Jeni), Mama Jeni (mama Jeni) ouoo (Mama Jeni)…”


“Mama bonge (eeh), hebu sikia (eeh) mwanao bonge (eeh) anavyolia;
Alizoea (eeh) chipsi mayai (eeh) soda bagia (eeh) na mishikaki;
Akaja depo (eeh) kuamka sa nane (eeh) ugali harage (eeh) bila kuungwa;
Na sasa boongeee..;
Bonge analia bonge (jamani bonge) bonge analia bonge…”


Ilikuwa tarehe 31/12/2011 usiku tukiupokea mwaka mpya wa 2012 tukiwa porini huku kuruta wakiendelea mafunzo yao ya kujiunga na Jeshi la Polisi (recruit course) mimi nikiwa kama Mkufunzi. Ulikuwa ni mkesha bila kupenda. Hapo kuruta walipiga disko kuanzia saa moja jioni hadi mwaka ulipoingia.

Nakumbuka mchana wa siku hiyo kuruta walipikiwa pilau ambayo kila mtu alitamani wangekula tu ugali kwani liligombaniwa na wala hawakushiba. Sisi tu waalimu kuwasimamia ilikuwa kama fatiki, hawazuiliki.

Mida ya kama saa nne niligundua wameanza kuchoka na sauti zinafifia nikawaambia wanyamaze nikawahadithia kisa kilichonikuta miaka ya mwanzo wa ajira yangu.

07[SUP]th[/SUP] August 2001, Dar es salaam

Baada ya kumaliza depo nilipangiwa kufanya kazi mkoa wa Dar es salaam. Nilikuwa kikosi cha FFU na hivyo kazi yangu kubwa ilikuwa malindo na kuzuia fujo, ingawa kwa kipindi kile nikiwa Dar sikupata kushiriki sana kwenye kazi hiyo ya kuzia fujo. Moyoni nilikuwa natamani sana ningebahatika kwenda maana nilikuwa natamani niwapige virungu wale waliokuwa wakituita sisi ‘darasa la saba’.

Mimi nilijiunga na Jeshi la Polisi kwani ndiyo ilikuwa ndoto yangu. Tangu nikiwa mdogo nilikuwa napenda sana sare zao na magwaride yao na kwa kuwa nilikulia maeneo ya Moshi nilihakikisha nahudhuria sherehe zote za kipolisi ambazo zilifanyika pale CCP.

Nilifanikiwa kujiunga na Jeshi hili mara baada ya kumaliza kidato cha Sita. Nilipata daraja la pili katika masomo yangu ya ECA hivyo nikakosa fursa ya kusomeshwa kwa mkopo wa serikali. Kwa bahati mbaya wazazi wangu pia hawakuwa na uwezo wa kunilipia ada ukizingatia nilikuwa nikipenda sana kusoma masomo ya biashara.

Kwa ufupi ilinibidi nijiunge na Jeshi la Polisi ila moyoni sikukata tamaa nikajiambia ipo siku nitakuja kusoma masomo hayo ya biashara.

Maisha yaliendelea hadi siku hii ya tarehe 07/08/2001. Nilipangwa lindo kwa Waziri mmoja ambaye kwa minajili ya maadili ningeomba nisimtaje jina wala wadhifa.




Itaendelea kesho...

JF Mentor kesho haijafika bado? au mi ndio nimepoteza majira?
 
Last edited by a moderator:
Hahaha hiyo changer imenikumbusha JAKATA. Hapo usiku unausogeza kwa changer,doso na morali
 
Kwa maana hiyo Mentor hii uliyotufanyia ndiyo style yako mpya? Why unatuacha kwenye mataa??!! dah!!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom