Mikopo ya bank imekaaje? hii riba ni sawa?

Mikopo ya bank imekaaje? hii riba ni sawa?

john_thesmart

Member
Joined
Jan 20, 2022
Posts
95
Reaction score
304
Ndugu yangu ameomba mkopo bank moja hapa nchi, kwakuwa ni mfanyakazi mshahara unapita bank hiyo na ni kwa muda wa miezi 72. Mkopo anaopewa ni mil 35 na atakatwa zaidi ya laki 7 na nusu kwa mwezi, ukipiga hesabu kwa haraka haraka hadi amalize mkopo atakuwa amelipa zaidi ya milion 54. Je, hii imekaa sawa? riba wanasema ni 16.5%
Kwa maana nyingine ni kama anapewa zaidi ya laki 4 kwa mwezi na analipa zaidi ya laki saba kwa mwezi.
 
ni sawa ajue juu ya time value of money.

anayetaka kutumia pesa ambayo hana lazima damu itoke, either masikioni au kwenye tunduu

haya maisha ni kuchagua upande, uwe mkopaji au mkopeshaji.. ajifunze delay gratification.. la sivyo Bank wana silinda butu itapenya kwenye tundu.
Ila hii ni kutumia advantage shida za watu, inakuwa kama kukomoana
 
Kama mshahara unaruhusu mwambie achukue huo mkopo kwa miaka 3 na miezi 9 (miezi 45). Kila mwezi awe analipa 1M.

Ataokoa karibu 9M kwenye interest. Akichukua miezi 72 (miaka 6) kwa hiyo riba ya 16.5% atalipa 19.8M.

Think about that.
 
ni sawa ajue juu ya time value of money.

anayetaka kutumia pesa ambayo hana lazima damu itoke, either masikioni au kwenye tunduu

haya maisha ni kuchagua upande, uwe mkopaji au mkopeshaji.. ajifunze delay gratification.. la sivyo Bank wana silinda butu itapenya kwenye tundu.
Mtu akiyaelewa haya huwezi kumkuta anakopa hovyo tena kwa hiyo riba ama huo muda.
Kwa bahati mbaya utakuta huyo mkopaji anakopa ili ajenge nyumba ama kununua gari, maamuzi ya kipuuzi kabisa.
 
Ndugu yangu ameomba mkopo bank moja hapa nchi, kwakuwa ni mfanyakazi mshahara unapita bank hiyo na ni kwa muda wa miezi 72. Mkopo anaopewa ni mil 35 na atakatwa zaidi ya laki 7 na nusu kwa mwezi, ukipiga hesabu kwa haraka haraka hadi amalize mkopo atakuwa amelipa zaidi ya milion 54. Je, hii imekaa sawa? riba wanasema ni 16.5%
Kwa maana nyingine ni kama anapewa zaidi ya laki 4 kwa mwezi na analipa zaidi ya laki saba kwa mwezi.
Ni vizuri kama anaenda kufanyia biashara ili azalishe hela ya ziada kuweza kuinua uchumi wake,wengi na hasa watumishi atakimbilia kununua gari au kujengea nyumba ambayo hata haitaisha,na atakaa miaka yote sita akisubiri marejesho yaishe ili akope tena...
 
Haina tofauti na mikopo ya simu, simu ya laki mbili marejesho ni laki 700000 kwa mwaka.
 
Back
Top Bottom