Mikataba ya Madini na Serikali ya Tanzania

Mikataba ya Madini na Serikali ya Tanzania

sio wote, mbona wewe na mimi hatupigi makofi
 
Cheyo alia na madini

na Mwandishi Wetu

WAKATI serikali ipo kwenye mjadala na wawekezaji wakubwa wa madini nchini, Kamati ya Hesabu za Serikali ya Bunge, imeanza kuhoji matumizi ya fedha zinazopatikana kupitia sekta hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ofisi za Bunge Dar es Salaam, jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha, John Cheyo, alisema kamati yake inahitaji kufahamu kiasi cha mrahaba kinachopatikana kutoka kwenye madini na matumizi yake.

Kwa mujibu wa takwimu zilizopo, sekta ya madini huchangia kiasi cha asilimia 40 ya pato la taifa litokanalo na fedha za kigeni.

Hoja ya Cheyo, ambaye ni Mbunge wa Bariadi Mashariki (UDP), alijikita katika kutaka kufahamu jinsi serikali inavyotumia asilimia 40 ya fedha za kigeni nchini zinazotoka kwenye sekta ya madini.

Alisema, inashangaza kuona kuwa, wakati mapato kupitia sekta hiyo yamekuwa yakiongezeka, hali za maisha ya wananchi wanaoishi katika maeneo ya migodi, zimeendelea kuwa duni.

Cheyo alisema, ni vyema Bunge likaelezwa kuwa serikali inapata au inakosa nini kutoka kwenye madini, na kwa misingi ipi, ili kupata ufumbuzi wa tatizo hilo.

Cheyo alisema, kamati imedhamiria kumwita Mkaguzi Mkuu wa Serikali ili kutoa ufafanuzi wa kina kuhusu pato halisi la fedha kutoka katika sekta ya madini.

“Tunataka kukutana na wenye migodi tuwape nafasi nao waseme waonavyo na watuambie wana mchango gani kwa serikali juu ya madini.

“Kamati inataka kufahamu kutoka serikalini kuwa, tunapata au kukosa nini katika makusanyo ya fedha zitokanazo na madini, hivyo tumepanga kuzungumza na mkaguzi mkuu wa serikali afafanue, na wenye machimbo nao waseme ili wananchi waelewe.

“Tunaambiwa kuhusu ajira kwa Watanzania, lakini kila kukicha bado walioajiriwa kwenye migodi hiyo wanalia shida, hii inaonyesha kwamba hakuna kitu huko… sasa hoja za uendeshaji wa madini na mrahaba ndio kitu kikubwa ambacho kamati inahitaji kujua,” alisema Cheyo.

Aidha, ameonya mvurugano katika sekta hiyo kwa kuwa ipo hatari ya kukosa wawekezaji, na hata fedha kidogo zinazoingia serikalini zitakwama ikiwa migogoro itaendelea.

“Hakuna haja ya kutajana majina kuwa huyu nani, anafanya nini, wote tunajua kuwa, wachimbaji wa kawaida wapo chini ya Alex Stewart, lakini hakuna haja ya kugombana, tushirikiane ili tuongeze kipato,” alisema.

Kamati hiyo ilikutana na wawakilishi kutoka taasisi mbalimbali zikiwamo Benki Kuu, Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Fedha na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
 
Karibu kila uchao tunahabarishwa tatizo moja au jingine, na hususan kinachojitokeza kama uzembe kwa watendaji wa serikali kushughulikia na kusimamia sheria, taratibu na kanuni katika sekta ya madini na nishati, hasa katika mikataba. Mifano ni lukuki. THISDAY wamekuwa wakiandika kuhusu habari za Mwadui (WDL na akina New Alamasi). Kumekuwa pia kukiripotiwa habari za ukwepaji kodi unaofanywa na makampuni ya uchimbaji wa madini, na pia migogoro na migongano Mererani, Kahama, Tarime, Buhemba, Geita na kote ambako kuna wawekezaji wa kigeni.

Serikali ya JK iliahidi kurekebisha mambo.
Je, wamefikia wapi?

Tuliambiwa kaunda tume ya wataalam wakiwemo wanasheria (bila shaka si wa kutoka Norway!), maofisa wa wizara ya nishati madini, usalama wa taifa nk. Je, tume (au kamati?) imemaliza kazi yake?
 
Hivi uliamini kwamba JK anaweza kweli kufanya ama kutenda aliyo yasema ?
 
Niliposoma haya nikaamini!

Kikwete afumua mikataba madini

  • Migodi kuanza kulipa kodi asilimia 30
  • Wakubwa wahoji Mkapa alishindwaje

Nasra Abdallah na Deodatus Balile (Tanzania Daima 23 Agosti 2006)

KAULI ya Rais wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete, ya kutaka mikataba ya madini ipitiwe na kulipatia taifa faida zaidi, imetekelezwa.

Serikali imetekeleza kauli hiyo kwa kupitia na kurekebisha mikataba ya madini, ambayo chini ya uongozi wa Serikali ya Awamu ya Tatu ilikuwa ikitajwa kuwa haiwezekani kufumuliwa.

Mabadiliko makubwa yameanzia katika Kampuni ya Barrick Gold ya Canada, inayomiliki migodi ya Bulyanhulu, North Mara na Tulawaka, ambayo baada ya majadiliano na Rais Kikwete mwenyewe juzi, imekubali kutoa sh milioni 9,100 au dola milioni 7, kama kodi serikalini kwa mwaka.

Mbali na kiasi hicho, kila halmashauri ya wilaya ilipo migodi hiyo, itapatiwa sh milioni 260 sawa na dola 200,000 kwa mwaka.

“Nia ya serikali, kama ambavyo imekuwa ikielezwa mara kwa mara na Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete, ni kuhakikisha kuwa nchi yetu (a) inanufaika ipasavyo na utajiri mkubwa wa madini, (b) inajenga mazingira endelevu ya uwekezaji, (c) inapata kodi ya 30% (corporate tax), (d) inapata maendeleo katika maeneo yanayochimbwa madini, na (e) inafaidika kwa kupata ajira na huduma mbalimbali zinazotokana na kuwepo kwa uchimbaji wa madini,” alisema Waziri wa Nishati na Madini, Dk. Ibrahim Msabaha.

Dk. Msabaha aliyeambatana na naibu wake, Laurence Marsha, alisema juzi viongozi wa Barrick walikutana na Rais Kikwete na kukubaliana naye mambo saba, ambayo ni:-

Kuondoa katika mikataba kipengele cha nyongeza ya kivutio cha asilimia 15 kwenye salio la gharama za uwekezaji (15% additional capital allowance on unredeemed capital expenditure) na kulipa kodi ya US $200,000 (sawa na sh milioni 260) kila mwaka katika halmashauri za wilaya zenye migodi ya Barrick.

Nyingine ni kulipa US $ milioni 7 (sawa na sh bilioni 9.1) kila mwaka kwa Serikali Kuu hadi kampuni itakapoanza kulipa kodi (corporate tax) na kununua bidhaa za ndani ya nchi kwa kadri zitakavyopatikana; kutumia kampuni za ndani ya nchi na wazalendo katika kutoa huduma mbalimbali katika migodi.

Pia walikubaliana kushirikiana na serikali katika kutatua matatizo ya muda mrefu ya wachimbaji wadogo wadogo na kutafuta njia za kutoa elimu endelevu ya ufundi kwa Watanzania ili waweze kushiriki ipasavyo katika soko la ajira na katika ujenzi wa taifa.

Kuondolewa kwa kivutio cha nyongeza ya asilimia 15 kwenye salio la gharama za uwekezaji, kutaifanya serikali iweze kupata kodi ya asilimia 30 kutoka kwa wachimba madini hao ambayo haijapata kutolewa tangu waanze kuchimba madini hapa nchini mwaka 1997.

Kivutio hiki cha asilimia 15 kimekuwa kikitumiwa na kampuni za kuchimba madini kuonyesha kuwa zinapata hasara muda wote, hali inayozifanya zisilipe kodi kabisa, lakini sasa imefutwa.

Dk. Msabaha alisema pamoja na makubaliano hayo, bado kampuni za kuchimba madini zina jukumu la kuendeleza jamii zinapofanyia kazi ya kuchimba madini (social responsibility), hivyo zitapaswa kuwaletea maendeleo wananchi.

Makubaliano hayo yataiwezesha serikali na Kampuni ya Barrick Gold Mine kufanya marekebisho katika Mikataba ya Uendelezaji wa Madini (Mining Development Agreements - MDA). Huu ni mkataba unaokubalika kimataifa na Afisa mwandamizi wa serikali aliiambia Tanzania Daima baada ya mkutano na Dk. Msabaha, kuwa Rais Kikwete alijua kuwa palihitajika mabadiliko, lakini kuepusha vurugu zisizo za lazima, ilibidi mabadiliko hayo yasipandikizwe bali yawe shirikishi.

Alisema kama serikali isingezishirikisha kampuni za madini na kujadiliana nazo juu ya umuhimu wa kulipa kodi, ingeweza kuzua mtafaruku na migogoro mikubwa ambayo nchi ingeshindwa kuaminika kimataifa.

“Huwezi kubadili peke yako. Nchi haitapata wawekezaji kwa utaratibu huo kwani utajenga migogoro, utapata kesi na nchi itaongezewa riba kubwa katika mikopo ya kimataifa, hii inaitwa sovereign risk. Inaongezeka sana ukibadili mikataba bila utaratibu.

“Rais anastahili kupongezwa kwani mabadiliko haya yaliyofanyika yataliingizia taifa wastani wa sh bilioni 500. Amekuwa rais makini, mwenye kufikiri na kuweka mikakati na kwa kutumia ushawishi wa hali ya juu katika diplomasia ya uchumi, amewezesha mabadiliko kufanyika nao wakashawishika,” alisema afisa huyo.

Alisema katika nchi nyingine, mikataba inapobadilishwa kinakuwa chanzo cha kuvuruga uchumi wa nchi na anafarijika kuwa Tanzania imeweza kubadili mikataba hii bila kuathiri heshima ya nchi, kuitia wasiwasi Jumuiya ya Kimataifa (Sovereign risk), na wawekezaji wataendelea kuamini kuwa ni nchi inayothamini mazungumzo (negotiation) katika kufikia makubaliano badala ya mabavu.

Afisa huyo alisema Rais Kikwete ameonyesha tofauti katika kipindi cha miezi saba tu, ameweza kumpiku Rais aliyemtangulia, Benjamin Mkapa na sasa anafanya waliyodhani hayawezekani. Pia aligusia mpango wa kupeleka vijijini sh bilioni moja kwa ajili ya kukopesha wananchi kuwa ni sehemu ya ubunifu wenye manufaa kwa Watanzania.

Kwa wabunge wa Kanda ya Ziwa, mabadiliko haya yatakuwa ni sherehe kwao kwani kimekuwa kilio chao cha muda mrefu, wakitaka serikali itenge fungu lenye kueleweka litumike kwa ajili ya maendeleo ya maeneo yanapochimbwa madini.

Wabunge hao wamekuwa wakidai malipo hayo kama mrahaba, kwa maelezo kuwa wawekezaji hawawezi kufika mahala wakatoa fedha bila kubanwa na sheria.

Kwa mujibu wa Dk. Msabaha, makubaliano hayo yaliyofikiwa juzi kati ya Kampuni ya Barrick na Serikali ya Tanzania, yatahusisha kampuni nyingine baada ya majadiliano na kampuni moja moja na baadaye yataingizwa katika sheria.
 
Mwanagenzi what is the message hapa maana habari ina mwaka karibia sasa lakini unaileta leo tena .Kuna mahali unapigilia msumari ama kuna kitu unataka kutueleza ?
 
Mwanagenzi

Hii habari ni kiporo, what is going on?
 
Mwanagenzi what is the message hapa maana habari ina mwaka karibia sasa lakini unaileta leo tena .Kuna mahali unapigilia msumari ama kuna kitu unataka kutueleza ?
Mwanagenzi alianza kuamini haya yaliyosemwa na Muungwana Lakini hadi sasa hakuna hata moja lilotekelezwa kati ya hayo aliyoanza kuyamini..............na hajui ni Lini yatatekelezwa hasa hilo mrahaba kwani Mh. Aliikana kauli yake ya asilimia 30% NA KUSEMA DUNIA KOTE WANAPEWA ASILIMIA 3%.
 
Mwanagenzi,
Unahitaji kusoma ile hotuba aliyotoa Kikwete Afrika kusini kwenye kikao cha madini, Indaba 07. hapo utaona ni kwa nini hakutakuwepo mabadiliko yeyote katika suala la madini. Wataendelea kuzoa na nchi itabaki na makorongo tu. Mwalimu alipoyaacha madini mpaka Watanzania wenyewe watakapokuwa na uwezo hawa viongozi wa sasa walimwona amepitwa na wakati. Lakini ukweli ni kwamba Mwalimu aliona mbali. Tutakuja juta siku moja.
 
Jasusi kama una copy ya hotuba ile naomba mwaga hapa ili tuichambue
 
Kuna mtu ana ripoti ya Tume ya Kipokola kuhusu madini? Anaweza akaweka hapa au akani-PM?
 
Nazidi kushangazwa...

1. Mpaka sasa kuna tume/kamati si chini ya nne zimewahi kuundwa na serikali kuhusu matatizo/kero mbalimbali kwenye sekta ya madini, zikiwemo
Tume ya Jenerali Mboma kuhusu migogoro ya Mererani (wakati wa Majogo), Tume ya Kipokola (nadhani iliundwa na Sumaye) kupitia, pamoja na mambo mengine, mikataba na takwimu za uzalishaji na mapato;
Kamati ya Jen Mang'enya (?) kuhusu migodi na mazingira(?);
Kamati ya Bunge chini ya Mhe Hamad Rashid (MB) iliyofuatilia TANSORT na WDL.
Pia Kamati ya Kudumu Bunge ya Uchumi na Fedha chini ya Mhe John Cheyo

2. Mawaziri wa madini wamekuwa wakitembelea migodi na kuzungumza na wananchi wanaoishi karibu na migodi kusikiliza kero (kutatua bado!):
Msabaha alizunguka
Masha akazunguka
Membe akatembelea
Ngelleja akapitia
Karamagi anakagua
Kamishna wa Madini naye kishazungukia.
Lowassa naye alishaongea Mererani.

Wote wanatoa "maombi" kwa wawekezaji badala ya "amri" na utekelezaji! Serikali toka lini ikabembeleza?

Kiasi kikubwa majibu ya kero na hoja zote ambazo watendaji wa serikali wamekuwa wakiahidi kushughulikia yako wazi na yashafayiwa kazi na hizo tume au kamati.

KWA NINI SERIKALI BADO INAJIVUTA NA KUVUTA MIGUU (kama inayo hiyo miguu!!)
au Ari, na Nguvu na Kasi (ANGUKA) imekwishaanguka??
 
I hope this is not a cheap talk that will end on IPP and Mwananchi. For him to declare this, he needs to present a bill through Magufuli to be passed by the BUnge this April, then he can have ubavu.

I think Tanzanian politicians are still operating on Ujamaa modes, forgeting that Presidential Decree does not translate into law especially in ths era of free market

Amuulize Mkapa ni kwa nini hakutumia rungu na mabavu ya Uraisi kusitisha mikataba kama BAE,IPTL na upup mwingine tuliokaa mezani na kuweka shahada zetu!

JK moves to prevent big land conflict

2007-03-25 10:11:48
By Adam Ihucha, Arusha


President Jakaya Kikwete has announced sweeping reforms, the highlight of which will be the seizure of big tracks of land owned by rich individuals and transfer them to poor, landless people.

The move is aimed at forestalling a land crisis in future.
``One controversial trend that may disrupt our stability is the erratic sale of communal land to rich individuals,`` President Kikwete told Arusha leaders at the end of his tour in the region.

Kikwete said land disputes have the potential to cause chaos. That eventuality has to be avoided, he said.

The president said he won`t hesitate to revoke a land title deed if by so doing, he would be catering for the interests of poor people and broader national stability.

That exercise would put to an end many land disputes and also dissuade rich people from acquiring large chunks of village land to the detriment of the welfare of the majority, he said.

He said that experience shows that well-to-do individuals usually capitalized on the ignorance of common people on land issues, to dispossess them of their ancestral land.

``These people normally follow all legal procedures required to secure land�so procedures are legal, but the deeds are illegal because they actually dispossess poor people of their ancestral land,`` President Kikwete explained.

``It is unfair indeed to have internally displaced people�this dishonest move, if left unaddressed, can disrupt peace in he explained.

He cited Arusha region as one of the areas in the lead in land disputes.
Kikwete was particularly concerned by the schemes of district land officials who turned communal land into commercial commodities.

He directed regional authorities to side with common people, to prevent their ancestral land from being grabbed.

All land in Tanzania is held in trust by the President on behalf of all Tanzanians and is therefore public property.

In order to ensure higher security of land tenure, Tanzania has three laws, namely, the Land Act No. 4 of 1999, Village Land Act No. 5 of 1999 and the Land Disputes Act No. 2 of 2002.

The general purpose of these laws is to make sure that the land policy objectives are achieved.

Analysts say that despite the existence of the Land Policy and Land Laws, some problems still persist.

These include lack of awareness about the existence of the policy and land laws by most land users, particularly farmers and livestock keepers.

This has resulted into intermittent conflicts among the two communities namely farmers and livestock keepers in some areas of the country, claiming many lives.


SOURCE:
Sunday Observer
 
Na hiyo itahusu ardhi inayosemekana kuwa kapewa/kamilikishwa Sinclair?
 
Jasusi ukihoji vya Waziri Mkuu na kumwacha JK mwenyewe ni makosa tunafanya . JK we thought kwamba hata nyumba hakununua kumbe alikuwa nayo kwenye viwanja be sure kwamba anavyo na yeye na wapambe wake . JK anatoa matamshi ya kisiasa kupata umaarufu na kuandikwa kila mara . Kashindwa mikataba, Richmonduli nk
 
another publicity stunt ! am not buying better yet not paying attention to it !!
 
Back
Top Bottom