Mikanganyiko katika Biblia ni kigezo kinachowapa watu uhalali wa kusema hakuna Mungu

passion_amo1

JF-Expert Member
Dec 3, 2023
1,578
3,148
Wakuu habari zenu?binafsi nimekuwa nikifuatilia mijadala mingi sana kuhusu mikanganyiko(contradiction) katika vitabu vya dini.

Nimekuwa nikifatilia nyuzi nyingi za kiranga kuhusu kupinga uwepo wa mungu, tukitoa mihemko tukajenga hoja kwa mantiki (logical) character ya mungu mwenye nguvu zote, mwenye upendo wote na ajuaye yote hayupo na haiwezi kufit kwenye mizani ya mantiki.

Nimekuwa nikisoma Biblia na imekuwa ikijikanganya yenyewe na bado ikidai kwamba mungu huwa hakosei. Leo nitaonyesha baadhi ya mikanganyiko hiyo ambayo hata kiranga amekuwa akiiweka.hizi ni baadhi ya verse zenye mikanganyo👇

Mwanzo 1:3-5 BHN
Mungu akasema, “Mwanga uwe.” Mwanga ukawa. Mungu akauona mwanga kuwa ni mwema. Kisha Mungu akautenganisha mwanga na giza, mwanga akauita “Mchana” na giza akaliita “Usiku.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya kwanza.

Mwanzo 1:14 BHN
Mungu akasema, “Mianga na iweko angani, itenge mchana na usiku, ioneshe nyakati, majira, siku na miaka

Mwanzo 1:11-13 BHN
Kisha Mungu akasema, “Nchi na ioteshe mimea. Mimea izaayo mbegu, na miti izaayo matunda yenye mbegu.” Ikawa hivyo. Basi, nchi ikaotesha mimea izaayo mbegu kwa jinsi yake, na miti izaayo matunda yenye mbegu kwa jinsi yake. Mungu akaona kuwa ni vyema. Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya tatu.

Mwanzo 2:4-9 BHN
Hivyo ndivyo mbingu na dunia zilivyoumbwa. Siku ile Mwenyezi-Mungu alipoziumba mbingu na dunia, Hapakuwa na mimea juu ya nchi wala miti haikuwa imechipua kwani Mwenyezi-Mungu hakuwa ameinyeshea nchi mvua, wala hapakuwa na mtu wa kuilima. Hata hivyo, maji yalitoka ardhini yakainywesha ardhi yote. Basi, Mwenyezi-Mungu akamfanya mwanamume kwa mavumbi ya udongo, akampulizia puani pumzi ya uhai, na huyo mwanamume akawa kiumbe hai. Kisha Mwenyezi-Mungu akapanda bustani huko Edeni,

Mwanzo 1:26-27 BHN
Kisha Mungu akasema, “Tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; atawale samaki wa baharini, ndege wa angani, wanyama wa kufugwa, dunia yote na viumbe vyote vitambaavyo.” Basi, Mungu akaumba mtu kwa mfano wake; naam, kwa mfano wake Mungu alimuumba. Aliwaumba mwanamume na mwanamke. Hapa mungu aliumba mwanamume na mwamke.

Mwanzo 2:7 BHN
Basi, Mwenyezi-Mungu akamfanya mwanamume kwa mavumbi ya udongo, akampulizia puani pumzi ya uhai, na huyo mwanamume akawa kiumbe hai.

(Mbele kidogo mungu anaumba mwanaume)utaona jinsi gani anavyosahau kurekodi matukio katika mtiririko ulio sahihi.

Mwanzo 2:7 BHN
Basi, Mwenyezi-Mungu akamfanya mwanamume kwa mavumbi ya udongo, akampulizia puani pumzi ya uhai, na huyo mwanamume akawa kiumbe hai.

Mwanzo 6:6 BHN
Mwenyezi-Mungu alisikitika sana kwa kumuumba binadamu duniani. Mwenyezi-Mungu alihuzunika sana moyoni mwake

Hesabu 23:19 BHN
Mungu si mtu, aseme uongo, wala si binadamu, abadili nia yake! Je, ataahidi kitu na asikifanye, au kusema kitu asikitimize?

Kutoka 12:13 BHN
Basi, ile damu itakuwa ishara yenu ya kuonesha nyumba mtakamokuwa. Nami nitakapoiona hiyo damu, nitawapita nyinyi, na hamtapatwa na dhara lolote wakati nitakapoipiga nchi ya Misri.

Mithali 15:3 SRUV
Macho ya BWANA yako kila mahali; Yakimchunguza mbaya na mwema.

( kwenye kutoka mungu wa kiyahudi anatoa maagizo wapake damu kwenye vizingiti vya milango ili asije kujichanganya, lakini mungu huyo huyo anajinasibu katika mithali macho yake yapo kila mahali)

Kutoka 20:14 BHN
“Usizini.

HOSEA 1:2
2 Hapo kwanza Bwana aliponena kwa kinywa cha Hosea, Bwana alimwambia Hosea, Enenda ukatwae mke wa uzinzi, na watoto wa uzinzi; kwa maana nchi hii inafanya uzinzi mwingi, kwa kumwacha Bwana.

Karibuni tujadili bila kashfa tujadiliane, hizi ni baadhi ya mikanganyiko iliyopo katika biblia.

Kwanini mungu mkamilifu kitabu chake kiwe na mikanganyiko kiasi hiki?

Mungu anasifa zote za binadamu anasahau, anabadili mawazo yake, ana hasira, Ana wivu, katili, na tabia zingine nyingi za kibinadamu.
 
Sasa kama huyo Mungu muweza na mwenye nguvu tulieaminishwa kuwa ana nguvu kumbe nae anafanya makosa kama ya kibinadamu, yaani Neno lake alilotuaminisha ni takatifu kumbe limejawa uongo na mikanganyiko, tunawezaje kuthibitisha au kuamini hata uwepo wake sio Uongo?

Ni sawa na kulazimisha maji kupanda mlima, ndivyo hivyo kulazimisha Mungu wa biblia/quran kuwepo wakati hawana vithibitisho.

Biblia/quran sio kithibitisho cha uwepo wa huyo Mungu maana hivyo vitabu havina logic wala ushahidi wa stories zake, pia huwezi kumthibitisha Mungu kupitia hizo ngonjera zake za uongo za vitabu vya dini.

Kuna wale wanaosingizia masuala ya Uumbaji, nipende tu kuwaambia ukweli mchungu, Mungu hausiki na uumbaji wa dunia wala kiumbe chochote dunian wala nje ya dunia, maana kiuhalisia Mungu nae ni kiumbe, je inawezekana kiumbe kuumba kiumbe mwingine?

Someni vizuri hizo ngonjera za vitabu vya dini zenu mtagundua kuwa kumbe hata binadamu akiwa na nguvu ktk jamii yake nae ni Mungu, kiumbe cha kiroho chochote ni Mungu, hata huyo Mungu wa Mbinguni nae ni kiumbe maana anaishi ktk ulimwengu, na sifa kuu ya kiumbe ni kuishi au kuwa covered/kupatikana/existence ktk ulimwengu wa Mwili au Roho.

Haiwezekani muumbaji aishi ktk kitu/ulimwengu aliouumba yeye mwenyewe je kabla hajazifanya hizo mbingu alikuwa wapi? Someni vizuri na mzielewe hizo stories zenu za uongo mtayajua madhaifu mengi ya huyo mnaemuita Mungu.

Narudia tena wanaopinga uwepo wa Mungu wako sahihi na wanaolazimisha uwepo wa Mungu wako sahihi pia maana hata sisi binadamu ni waungu kwa baadhi ya viumbe dhaifu hivyo tunavitawala, na wanaopinga uwepo wa Mungu wako sahihi maana huyo Mungu tulieaminishwa hayuko na wala hatowai kuwepo zaidi ya ngonjera za vitisho.
 
Maandiko yote ya kidini ni Hadithi za kutungwa sawa na Hekaya za Abunuwasi au riwaya za Alfu Lela ulela.

Mungu hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.

Dhana ya uwepo wa Mungu mwema, mkamilifu, mwenye kujua yote, muweza wa vyote na mwenye upendo na huruma Kwenye Dunia iliyojaa uovu, ukatili, uasi, mabaya na shida za kila aina ni uthibitisho kwamba Mungu huyo Hayupo.

Mungu mkamilifu, Alishindwaje kuumba Dunia isiyo na uovu?

Mungu muweza wa vyote, Alishindwaje kuumba Binadamu wema tu wasio na uwezo wa kutenda dhambi, ukatili na ubaya?

Mungu mwenye kujua yote, Hakujua kwamba uovu, ukatili na mabaya yatakuja kuwepo duniani ayadhibiti mapema?

If God wanted us in Heaven Why he created us on Earth?

Mungu huyo, Alishindwaje kutuumba tukiwa mbinguni directly kama alitaka tuwe Mbinguni?

God is a fictional character invented by religion to scam people.

Religion convinced people that there's an invisible man beyond the sky who watches everything.

Human beings created God through assumptions Based on things beyond their imaginations.

God doesn't EXIST.

Kila mtu huzaliwa Atheist hata wewe ulizaliwa Atheist mpaka pale ulipo aminishwa kwamba kuna invisible creature beyond the sky anaitwa Mungu.

Hizi ni fiction stories za kurithishwa.
 
Maandiko yote ya kidini ikiwemo hiyo Quran yenu ni Hadithi za kutungwa, Fairytales, myths.

Allah( Mungu) hajawahi kuwepo, hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.
ALLAH anawauliza wale wanaodai kuwa hakuna Mola

At-Tur 52:35

أَمْ خُلِقُوا۟ مِنْ غَيْرِ شَىْءٍ أَمْ هُمُ ٱلْخَٰلِقُونَ


Or were they created by nothing, or were they the creators [of themselves]?

Swahili

"Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?"
 
Allah huyo, Anashushaje Quran kwa lugha moja tu ya kiarabu?

Allah huyo, Hakujua kwamba Duniani kuna watu wa lugha mbalimbali?

Allah huyo, Alishindwaje kushusha Quran hiyo kwa watu wote duniani wa lugha zote akaeleweka na watu wote kwa wakati mmoja?
Ash-Shura 42:7

وَكَذَٰلِكَ أَوْحَيْنَآ إِلَيْكَ قُرْءَانًا عَرَبِيًّا لِّتُنذِرَ أُمَّ ٱلْقُرَىٰ وَمَنْ حَوْلَهَا وَتُنذِرَ يَوْمَ ٱلْجَمْعِ لَا رَيْبَ فِيهِۚ فَرِيقٌ فِى ٱلْجَنَّةِ وَفَرِيقٌ فِى ٱلسَّعِيرِ

English -

And thus We have revealed to you an Arabic Qur’ān that you may warn the Mother of Cities [i.e., Makkah] and those around it[1] and warn of the Day of Assembly, about which there is no doubt. A party will be in Paradise and a party in the Blaze.

Swahili

Na namna hivi tumekufunulia Qur'ani kwa Kiarabu ili uwaonye watu wa Mama wa Miji na walio pembezoni mwake. Na uhadharishe na Siku ya Mkutano, haina shaka hiyo. Kundi moja litakuwa Peponi, na kundi jengine Motoni.
 
Quran. Yusuf 12:2

إِنَّآ أَنزَلْنَٰهُ قُرْءَٰنًا عَرَبِيًّا لَّعَلَّكُمْ تَعْقِلُونَ

English - Sahih International

Indeed, We have sent it down as an Arabic Qur’ān[1] that you might understand.

Swahili - Ali Muhsin Al-Barwani

Hakika Sisi tumeiteremsha Qur'ani kwa Kiarabu ili mpate kuzingatia.
 
Ar-Ra'd 13:37

وَكَذَٰلِكَ أَنزَلْنَٰهُ حُكْمًا عَرَبِيًّاۚ وَلَئِنِ ٱتَّبَعْتَ أَهْوَآءَهُم بَعْدَمَا جَآءَكَ مِنَ ٱلْعِلْمِ مَا لَكَ مِنَ ٱللَّهِ مِن وَلِىٍّ وَلَا وَاقٍ

English

And thus We have revealed it as an Arabic legislation.[1] And if you should follow their inclinations after what has come to you of knowledge, you would not have against Allāh any ally or any protector.

Swahili

Na ndio kama hivi tumeiteremsha Qur'ani kuwa ni hukumu kwa lugha ya Kiarabu. Na ukifuata matamanio yao baada ya kukujia ilimu hii, hutakuwa na rafiki wala mlinzi mbele ya Mwenyezi Mungu.
 
ALLAH anawauliza wale wanaodai kuwa hakuna Mola
Allah huyo anauliza, kwani yeye hajui?
At-Tur 52:35

أَمْ خُلِقُوا۟ مِنْ غَيْرِ شَىْءٍ أَمْ هُمُ ٱلْخَٰلِقُونَ


Or were they created by nothing, or were they the creators [of themselves]?

Swahili

"Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?"
 
Quran. Yusuf 12:2

إِنَّآ أَنزَلْنَٰهُ قُرْءَٰنًا عَرَبِيًّا لَّعَلَّكُمْ تَعْقِلُونَ

English - Sahih International

Indeed, We have sent it down as an Arabic Qur’ān[1] that you might understand.

Swahili - Ali Muhsin Al-Barwani

Hakika Sisi tumeiteremsha Qur'ani kwa Kiarabu ili mpate kuzingatia.
Naku uliza hivi 👇

Allah huyo Hakujua kwamba duniani kuna watu wa lugha mbalimbali ashushe Quran hiyo kwa watu wote duniani wa lugha zote?

Kwani Duniani lugha ni kiarabu tu?

Allah huyo, Hakujua kwamba kuna wajerumani, waingereza, waswahili, wafaransa, wafilipino, wahindi n.k

Yani Allah huyo Aumbe watu wa lugha tofauti tofauti kisha ashushe neno lake kwa lugha moja tu?

Hivi huyo Allah ana jielewa kweli?
 
Naku uliza hivi 👇

Allah huyo Hakujua kwamba duniani kuna watu wa lugha mbalimbali ashushe Quran hiyo kwa watu wote duniani wa lugha zote?

Kwani Duniani lugha ni kiarabu tu?

Allah huyo, Hakujua kwamba kuna wajerumani, waingereza, waswahili, wafaransa, wafilipino, wahindi n.k

Yani Allah huyo Aumbe watu wa lugha tofauti tofauti kisha ashushe neno lake kwa lugha moja tu?

Hivi huyo Allah ana jielewa kweli?
Quran imejibu kila hoja zenu

ALLAH anawauliza tena wale wasioamini.

Fussilat 41:44

وَلَوْ جَعَلْنَٰهُ قُرْءَانًا أَعْجَمِيًّا لَّقَالُوا۟ لَوْلَا فُصِّلَتْ ءَايَٰتُهُۥٓۖ ءَا۬عْجَمِىٌّ وَعَرَبِىٌّۗ قُلْ هُوَ لِلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ هُدًى وَشِفَآءٌۖ وَٱلَّذِينَ لَا يُؤْمِنُونَ فِىٓ ءَاذَانِهِمْ وَقْرٌ وَهُوَ عَلَيْهِمْ عَمًىۚ أُو۟لَٰٓئِكَ يُنَادَوْنَ مِن مَّكَانٍۭ بَعِيدٍ

English

And if We had made it a foreign [i.e., non-Arabic] Qur’ān, they would have said, "Why are its verses not explained in detail [in our language]? Is it a foreign [recitation] and an Arab [messenger]?" Say, "It is, for those who believe, a guidance and cure." And those who do not believe - in their ears is deafness, and it is upon them blindness. Those are being called from a distant place.[1]

Swahili -

Na lau tungeli ifanya Qur'ani kwa lugha ya kigeni wangeli sema: Kwanini Aya zake haziku pambanuliwa? Yawaje lugha ya kigeni na Mtume Mwaarabu? Sema: Hii Qur'ani ni uwongofu na poza kwa wenye kuamini. Na wasio amini umo uziwi katika masikio yao, nayo kwao imezibwa hawaioni. Hao wanaitwa nao wako pahala mbali.
 
Rhetorical questions! Ni maswali yasiyohitaji majibu
Hakuna maswali yasiyo hitaji majibu.
ila yanamfanya msikilizaji afikiri zaidi. Mungu kuwauliza wapagani sio kwamba hajui majibu yake ila anawauliza ili wapate kutafakari zaidi.
Allah huyo, Alishindwaje kuumba binadamu watakao mtii na kufuata neno lake siku zote?

Yeye si muweza wa yote?

Sasa kwa nini, Ashindwe kuumba Binadamu wenye kujua neno lake?
 
Back
Top Bottom