Mikadi Beach Sio Salama Siku Za Sikukuu

Mikadi Beach Sio Salama Siku Za Sikukuu

ibra87

R I P
Joined
Jul 22, 2015
Posts
5,614
Reaction score
5,379
Kabari, uporaji na Kila aina Ya Uhuni unapatikana pale siku Ya Leo.

Dada Zangu mliopanga kwenda pale kuweni makini na Simu Zenu, Mikoba Yenu na Hata nguo Zenu.

Madada mnaokuja na Watoto Wadogo naomba sana tena sana muwe mnaondoka mapema kabla Ya giza kuingia na Hili ni Angalizo kwasababu Ya Usalama wa Watoto mlionao.

Msijiachie kwa Pozi mnapoongea na Simu kwa kuwa kitakachotokea kinaweza kuwapa ukilema iwapo utakuwa mbishi.

Vikundi vya wahundi kutoka Mbagala, tandika, manzese na kigamboni wanaweza kuwarudisha Nyumbani mkiwa hamna hata Nguo Mwilini...

Makaka ambao mtaambatana na Madada wakiwemo na watoto ni jukumu lenu kuwalinda na mkiwaacha na Nyie kukimbia kitakachotokea mtakibeba nyie.

Ukiona wewe ni muoga na mpenzi wako ni muoga Sikushauri Uende mikadi, chadibwa, ng'onda na Hata Beach Comber kwani kitakachotokea unaweza kumchukia mpenzi wako.

Pia unapotoka Mikadi ndani angalia Unapotaka kuvuka barabara kwa kuwa ni Sehemu ambayo ni Hatari sana na ajali huwa zinatokea mara kwa Mara.

MSIPOZINGATIA NILICHOSEMA MTATUFANYA WATU WAKIGAMBONI TUONEKANE HATUFAI....

Tambua thamani Yako na angalia thamani ya watoto wako.. X mass bila beach inawezakana

HERI YA SIKUKUU
 
Ile beach nafikiri ni ya kulipia , anayechukua huo mchango ahakikishe usalama wa wateja wake, otherwise atumbuliwe jipu
 
Ile beach nafikiri ni ya kulipia , anayechukua huo mchango ahakikishe usalama wa wateja wake, otherwise atumbuliwe jipu

Beach ni ya kulipia ndio lakini ndani huko huko ndipo Ujinga mwingi hutokea.. Na kuna wakati Inalazimika wanajeshi wa kambi ya Mizinga kupita kila wakati kuangalia usalama. Lakini Mikadi kama mikadi hawana ulinzi.
 
Mkuu upo karibu na hapo nin??mi npo bar ya hapa nje panaitwa joint!!karibu tule ugimbi!!
 
Mikadi ilikuwa vizuri zamani

Yeah mkuu! Mikadi ilikuwa zamani lakini kwasasa imekuwa kimbilio la vibaka wa Tandika, mbagala na manzese.. Nawahurumia sana wa dada wanaokwenda na Watoto maeneo yale..
 
Mkuu upo karibu na hapo nin??mi npo bar ya hapa nje panaitwa joint!!karibu tule ugimbi!!

nitakuwa hapo mishale ya saa mbili usiku mkuu... Kwasasa nipo mwananyamala.. Kuwa makini hapo kuna wadada wanachuna sana.. Msalimie Erasco
 
bora umewakumbsha mkuu... kwanza sikukuu ni muda wa kutulia ndani na familia!!!
 
Nilipanga kupita hapo siku moja. Hivi kuna nini hasa cha kuvutia muda wa mchana na majira ya usiku? Anaepafaham pls.
 
mikadi siyo kabisa,
nilikwenda pale na marafiki muda wa kutoka ilikua shughuli yaani visu nje nje, nilikimbia kama mwehu.. sitokwenda tena mikadi kamwe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom