Mageseunique
Member
- Mar 23, 2011
- 6
- 1
je kwa mtindo wa wanaccm kurumbana,staili hii CHAMA TAWALA hawawezi kujimaliza kisiasa wao kwa wao? habari kwa unyeti huwa nazidabika Unique Entertainment
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya UVCCM Moshi Mjini na mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi, Paul Makonda, amewavua nguo viongozi wa UVCCM Taifa na kuwataka wachuchumae kwa kujiuzulu ndani ya siku saba kwa kuigeuza jumuiya hiyo kuwa kijiwe cha kutukana na kukemea wazee ndani ya CCM kinyume na maadili na malezi ya Kiafrika na Kanuni za UVCCM.
Makonda, kada kinda anayejiamini kisomi, amewaomba radhi wazee wote ndani ya CCM kwa utovu wa nidhamu unaooneshwa na vijana wenzake ndani ya UVCCM ambao wamejenga tabia ya kuwarushia matusi na vitisho wazee kutokana na kulewa madaraka na kutetea ajenda za mafisadi.
Msimamo huo ameutoa leo jioni kwenye mkutano na waandishi wa habari jijini Dar na kuwaomba wazee wanyamaze, vijana waadilifu ndani ya UVCCM wapambane na mamluki hao wa mafisadi.
sija wahi kushuhumdia nchi ikiwa imekosa dira namna hii..kila sehemu matamko...kinachofata ni vitendo
Kinachoumiza ni kuona ishu za msingi kama Katiba mpya,Dowans na nyingine zinafunikwa na matukio ya wanasiasa wapumbavu kama hao wa UVCCM.....nchi haina mwelekeo,kila kukicha ni story za uropokaji tu na fitna......nikiangalia mbele naona giza,manake kampeni zimeanza mapema sana na kwa namna ya kushtua na kushangaza:washing:
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya UVCCM Moshi Mjini na mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi, Paul Makonda, amewavua nguo viongozi wa UVCCM Taifa na kuwataka wachuchumae kwa kujiuzulu ndani ya siku saba kwa kuigeuza jumuiya hiyo kuwa kijiwe cha kutukana na kukemea wazee ndani ya CCM kinyume na maadili na malezi ya Kiafrika na Kanuni za UVCCM.
Makonda, kada kinda anayejiamini kisomi, amewaomba radhi wazee wote ndani ya CCM kwa utovu wa nidhamu unaooneshwa na vijana wenzake ndani ya UVCCM ambao wamejenga tabia ya kuwarushia matusi na vitisho wazee kutokana na kulewa madaraka na kutetea ajenda za mafisadi.
Msimamo huo ameutoa leo jioni kwenye mkutano na waandishi wa habari jijini Dar na kuwaomba wazee wanyamaze, vijana waadilifu ndani ya UVCCM wapambane na mamluki hao wa mafisadi.
HUYO KIJANA NIMEMWONA KIDOGO TU KWENYE ITV. NAMWOMBA MZEE MENGI AMPE KIPINDI MAALUM AWAPASHE SAWASAWA MAMLUKI HAO WA KINGUNGE! Wamemtukana Sumaye kwa kukopa sh. milioni 50 tu, huku wao wanampa mzee wa ufisadi Kingunge ulezi wa UVCCM Taifa huku wakijua kuwa Kingunge alipora miradi ya mabilioni bila kufuata utaratibu: miradi ya Kituo Kikuu cha Mabasi na Uegeshaji Magari jijini Dar. Wanamsema Sumaye wakati mfadhili wao ni fisadi nambari moja nchini, mmiliki wa Dowans (RA) na shoga yake (EL).