KWELI Mifugo hufariki wakila maganda ya mihogo mibichi

KWELI Mifugo hufariki wakila maganda ya mihogo mibichi

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Source #1
View Source #1
Katika jamii ya Kitanzania, baadhi ya mifugo kama vile mbuzi na ng’ombe hufariki wanapokula maganda ya mihogo mibichi. Hali hii huwastaajabisha wafugaji wengi, kwa kuwa mihogo hiyo huwa salama na hata tamu kwa matumizi ya binadamu, lakini inapoliwa na baadhi ya mifugo husababisha madhara makubwa, ikiwemo kifo.

ufuatiliaji ambao umefanywa umebainisha kuwa Mihogo ina kemikali zinazoitwa cyanogenic glycosides (hasa linamarin na lotaustralin). Kemikali hizi zikivunjika ndani ya mwili au wakati mihogo inapokatwa/kupondwa, hutengeneza hydrogen cyanide (HCN) ambayo ni sumu kali ndani ya mwili wa mnyama

Utafiti ambao umefanywa Tweyongyere,R. & Katongole (2002)umeeleza kuwa sehemu ya nje ya muhogo mara nyingi ina kiwango kikubwa cha cyanide kuliko sehemu ya ndani.
katika Utafiti umeonyesha kuwa maganda mabichi yanaweza kuwa na 253–1081 mg ya cyanide kwa kilo ya uzito mkavu, kiwango ambacho kinaweza kuwa hatari kwa mifugo

pia katika utafiti mwingine ambao umefanywa na Taabu, H. na wenzake nchini uganda umerejelea kuwa Maganda ya mihogo yana mkusanyiko mkubwa wa linamarin kuliko sehemu ya ndani ya muhogo . Tafiti kadhaa zinaonyesha kuwa kiwango cha cyanide kwenye maganda kinaweza kuwa mara 10 hadi 20 zaidi ya kile kinachopatikana kwenye sehemu ya kuliwa.

tafiti pia zimethibitisha namna mnyama anavyoweza kufariki kwa kupitia hatua zifuatazo ambazo Cyanide ikiingia kwenye damu ya mnayama huzuia matumizi ya oksijen kwenye seli na viungo mhimu kama ubongo pamoja na moyo kushindwa kufanya kazi

Ili kuzuia vifo, wafugaji wanashauriwa kutolisha mifugo maganda ya mihogo mbichi
sambamba na hilo katika kuhakikisha kuwa mifugo haidhuliki na sumu hiyo wataalamu wa masula ya mifugo wanashauri Kukausha maganda kwenye jua ili kupunguza kiwango cha cyanide kwa njia ya kawaida zaidi .
1773295912230.png
 
Tunachokijua
ufuatiliaji ambao umefanywa umebainisha kuwa Mihogo ina kemikali zinazoitwa cyanogenic glycosides (hasa linamarin na lotaustralin). Kemikali hizi zikivunjika ndani ya mwili au wakati mihogo inapokatwa/kupondwa, hutengeneza hydrogen cyanide (HCN) ambayo ni sumu kali ndani ya mwili wa mnyama.

Maganda ya mihogo kwa asili yana kemikali ambazo zinaweza kuwa hatari yakiliwa moja kwa moja bila kuchakatwa. Miongoni mwa kemikali hizo ni pamoja na cyanide, ambayo hupatikana kwa kiwango kikubwa zaidi kwenye mihogo michungu, na pia hupatikana kwenye maganda ya mihogo yote miwili—mihogo mitamu na michungu. Kemikali hizi zinaweza kuwa sumu au hatari kwa afya ikiwa maganda ya mihogo kama haitachakatwa ipasavyo kabla ya kutumiwa.

Utafiti ambao umefanywa Tweyongyere,R. & Katongole "Cyanogenic potential of cassava peels and ther detoxification for utilization as livestock feed" (2002)umeeleza kuwa;

Sehemu ya nje ya muhogo mara nyingi ina kiwango kikubwa cha cyanide kuliko sehemu ya ndani. katika Utafiti umeonyesha kuwa maganda mabichi yanaweza kuwa na 253–1081 mg ya cyanide kwa kilo ya uzito mkavu, kiwango ambacho kinaweza kuwa hatari kwa mifugo

pia katika utafiti mwingine ambao umefanywa na Taabu, H. na wenzake nchini uganda umerejelea kuwa Maganda ya mihogo yana mkusanyiko mkubwa wa linamarin kuliko sehemu ya ndani ya muhogo . Tafiti kadhaa zinaonyesha kuwa kiwango cha cyanide kwenye maganda kinaweza kuwa mara 10 hadi 20 zaidi ya kile kinachopatikana kwenye sehemu ya kuliwa.

Tafiti pia zimethibitisha namna mnyama anavyoweza kufariki kwa kupitia hatua zifuatazo ambazo Cyanide ikiingia kwenye damu ya mnayama huzuia matumizi ya oksijen kwenye seli na viungo muhimu kama ubongo pamoja na moyo kushindwa kufanya kazi

Ili kuzuia vifo, wafugaji wanashauriwa kutolisha mifugo maganda ya mihogo mbichi bil kuichakata

Sambamba na hilo katika kuhakikisha kuwa mifugo hawaathiriwi na sumu hiyo wataalamu wa masula ya mifugo wanashauri Kukausha maganda kwenye jua ili kupunguza kiwango cha cyanide kwa njia ya kawaida zaidi .
Katika jamii ya Kitanzania, baadhi ya mifugo kama vile mbuzi na ng’ombe hufariki wanapokula maganda ya mihogo mibichi. Hali hii huwastaajabisha wafugaji wengi, kwa kuwa mihogo hiyo huwa salama na hata tamu kwa matumizi ya binadamu, lakini inapoliwa na baadhi ya mifugo husababisha madhara makubwa, ikiwemo kifo.

ufuatiliaji ambao umefanywa umebainisha kuwa Mihogo ina kemikali zinazoitwa cyanogenic glycosides (hasa linamarin na lotaustralin). Kemikali hizi zikivunjika ndani ya mwili au wakati mihogo inapokatwa/kupondwa, hutengeneza hydrogen cyanide (HCN) ambayo ni sumu kali ndani ya mwili wa mnyama

Utafiti ambao umefanywa Tweyongyere,R. & Katongole (2002)umeeleza kuwa sehemu ya nje ya muhogo mara nyingi ina kiwango kikubwa cha cyanide kuliko sehemu ya ndani.
katika Utafiti umeonyesha kuwa maganda mabichi yanaweza kuwa na 253–1081 mg ya cyanide kwa kilo ya uzito mkavu, kiwango ambacho kinaweza kuwa hatari kwa mifugo

pia katika utafiti mwingine ambao umefanywa na Taabu, H. na wenzake nchini uganda umerejelea kuwa Maganda ya mihogo yana mkusanyiko mkubwa wa linamarin kuliko sehemu ya ndani ya muhogo . Tafiti kadhaa zinaonyesha kuwa kiwango cha cyanide kwenye maganda kinaweza kuwa mara 10 hadi 20 zaidi ya kile kinachopatikana kwenye sehemu ya kuliwa.

tafiti pia zimethibitisha namna mnyama anavyoweza kufariki kwa kupitia hatua zifuatazo ambazo Cyanide ikiingia kwenye damu ya mnayama huzuia matumizi ya oksijen kwenye seli na viungo mhimu kama ubongo pamoja na moyo kushindwa kufanya kazi

Ili kuzuia vifo, wafugaji wanashauriwa kutolisha mifugo maganda ya mihogo mbichi
sambamba na hilo katika kuhakikisha kuwa mifugo haidhuliki na sumu hiyo wataalamu wa masula ya mifugo wanashauri Kukausha maganda kwenye jua ili kupunguza kiwango cha cyanide kwa njia ya kawaida zaidi .
Hiyo mihogo mibichi ng'ombe wanakula lakini hawajawahi kufa mkuu. Huu utafiti ni wa mchongo.
 
Ni kweli kwa sisi wakulima tunaelewq sana! Ukimpa ngombe miogo mibichi au maganda yake akila kwa wingi anakufa!! Hata binadamu huwezi kula miogo Mibichi achana na hii ya kutafuna, maana Kuna Aina nyingi za miogo nazugumzia Ile miogo ambayo ni michungu ukila mibichi, hata ukiipika bado inakuwa michungu, miogo hii lazima iandaliwe vizuri ukienda ukuriani musoma na Tarime wanaelewa Kuna miogo inaitwa Rumala ni miogo hatari sana ukikosea hata maandalizi yake! Unaitoa shambani lakini mpaka kuliwa kwake lazima hizo process zichukue sio chini ya wiki mbili!! Ukikosea process ya uaandaaji wake ukila ugali wake huwezi kulala!!
 
Ni kweli kwa sisi wakulima tunaelewq sana! Ukimpa ngombe miogo mibichi au maganda yake akila kwa wingi anakufa!! Hata binadamu huwezi kula miogo Mibichi achana na hii ya kutafuna, maana Kuna Aina nyingi za miogo nazugumzia Ile miogo ambayo ni michungu ukila mibichi, hata ukiipika bado inakuwa michungu, miogo hii lazima iandaliwe vizuri ukienda ukuriani musoma na Tarime wanaelewa Kuna miogo inaitwa Rumala ni miogo hatari sana ukikosea hata maandalizi yake! Unaitoa shambani lakini mpaka kuliwa kwake lazima hizo process zichukue sio chini ya wiki mbili!! Ukikosea process ya uaandaaji wake ukila ugali wake huwezi kulala!!
Nafikiri kuna namna ya udongo fulani mihogo inaweza kutengeneza sumu ya aina fulani kiasili tu🤔
 
Dah bora iwe kweli kesho niwategeshee mbuzi sumbufu wa jirani
 
Hapana Usifanye Hivyo ..Utakuwa hujatenda Sawa Kabisa
Kwani hao mbuzi na mwenye mbuzi wananitendea sawa mimi?yaani niangaikie bustani yangu halafu mbuzi aje kula kesho watakula maganda ya mihogo nakwambia...mida huo mi nakula futari mwenye mbuzi atakuwa anachinja vibudu
 
Kwani hao mbuzi na mwenye mbuzi wananitendea sawa mimi?yaani niangaikie bustani yangu halafu mbuzi aje kula kesho watakula maganda ya mihogo nakwambia...mida huo mi nakula futuristic mwenye mbuzi atakuwa anachinja vibudu
Hakuna haja ya kuchukua maganda ya mihogo. Utaratibu unaofaa ni kumkamata mbuzi huyo kisha kumtafuta mwenye mifugo wake ili muzungumze na kufikia muafaka kwa kina. Endapo hamtaelewana, mtafikisha suala hilo katika ngazi ya mtaa kwa ajili ya kujadili kilichotokea na kumaliza mgogoro huo kwa njia ya kidiplomasia zaidi.
 
Hakuna haja ya kuchukua maganda ya mihogo. Utaratibu unaofaa ni kumkamata mbuzi huyo kisha kumtafuta mwenye mifugo wake ili muzungumze na kufikia muafaka kwa kina. Endapo hamtaelewana, mtafikisha suala hilo katika ngazi ya mtaa kwa ajili ya kujadili kilichotokea na kumaliza mgogoro huo kwa njia ya kidiplomasia zaidi.
Unadhani hata wa kumtafuta ni mchaga mmoja nyuma ya nyumba yangu mbuzi zake zinaleta fujo tu kesho stereo mapemaa kuchukua mihogo....mkuu we mfugaji nini mbona unawahurumia hao wanyawa mapepe?
 
Unadhani hata wa kumtafuta ni mchaga mmoja nyuma ya nyumba yangu mbuzi zake zinaleta fujo tu kesho stereo mapemaa kuchukua mihogo....mkuu we mfugaji nini mbona unawahurumia hao wanyawa mapepe?
“Hapana mkuu, huo ndio utaratibu ulio bora zaidi kuliko kuchochea sintofahamu baina yenu. Inafaa kuchukua hatua ambazo hazitaleta madhara kati yenu, huku mkizingatia kuwa bado ninyi ni majirani na ni vyema kudumisha mahusiano mema ya ujirani.”
 
Unadhani hata wa kumtafuta ni mchaga mmoja nyuma ya nyumba yangu mbuzi zake zinaleta fujo tu kesho stereo mapemaa kuchukua mihogo....mkuu we mfugaji nini mbona unawahurumia hao wanyawa mapepe?
“Hapana mkuu, huo ndio utaratibu ulio bora zaidi kuliko kuchochea sintofahamu baina yenu. Inafaa kuchukua hatua ambazo hazitaleta madhara kati yenu, huku mkizingatia kuwa bado ninyi ni majirani na ni vyema kudumisha mahusiano mema ya ujirani.”
 
Mihogo mibichi hata binadamu inaua

 
“Hapana mkuu, huo ndio utaratibu ulio bora zaidi kuliko kuchochea sintofahamu baina yenu. Inafaa kuchukua hatua ambazo hazitaleta madhara kati yenu, huku mkizingatia kuwa bado ninyi ni majirani na ni vyema kudumisha mahusiano mema ya ujirani.”
Ni kama yeye na mbuzi wake wanavyoniletea taharuki.
 
Mihogo mibichi hata binadamu inaua

sahihi kabisa
 
Mmmmhhh mbona tunalisha sana wanyama wetu haya majani na hawafi?
Nadhani kuna mazingira yakiwekwa au yakichanganywa na majani fulani ndiyo huleta maafa.

Ninakotokea majani ya mihogo (siyo maganda) majani mbuzi wanaweza kuyatumia kama chakula toka kunakucha mpaka saa tano asubuhi jua likianza kuwa kali wakala basi inageuka kuwa hasara kubwa.
 
Back
Top Bottom