Midege ya jeshi inayozunguka angani

Midege ya jeshi inayozunguka angani

kwa hiyo ukiwa na pistol yako nyumbani si lazima uwe unaitoa kuisafisha safisha ama?ama itakaa kama pambo ndani tu
 
Hayo ni mazoezi ya kijeshi, yana tija na ni muhimu kwa usalama wetu. Hakuna nchi isofanya vitu hivyo. Hata nchi zilizoendelea bajeti zao za mambo ya ulinzi ni kubwa sana.
Na pia kama kuogopa gharama basi hata wanajeshi waende likizo hadi tunapojiandaa kwa vita ndio waitwe
 
mmh jamani...umeanza vizuri hoja mwishoni utumbooo. hivi nyie watanzania mtu huwezi kuongelea jambo muhimu bila kunyunyizia na umbea? yaani uwezi kabisa?

upikie ndizi huo utumbo huwaga ni mzuri sana.
 
Hivi wewe unadhani Jamii Forum ni ukurasa wa wapumbavu. Una elimu gani kuhusu taratibu za urukaji wa ndege za jeshi? Kuona ndege za jeshi zinaruka unakurupuka eti mafuta kodi ya wananchi inatumika vibaya. Unajua hiyo ndege imenunuliwa na kodi hiyohiyo ya wananchi au kwa upeo wako mdogo ukajua jeshi limenunua ndege ili lichezee mafuta ya wananchi? Haya mambo sio ya kukurupuka kwenye mitandao kama hii unajiandikia tu. Kumbuka hii nchi inalindwa na wanajeshi mpaka wewe unapata jeuri ya kuongea madudu yako humu. Ndege za jeahi la wananchi katika anga hili la watanzania zitaruka mahala popote pale na wakati wowote ule na hii no katoka kutekeleza majukumu yake kipindi cha amani ili kurahisisha mapambano kipindi cha Vita.

ni vizuri umemwambia maana kanichefua sana
 
Labda tuanze na maoni ya mleta uzi. Yeye anafikiri nini? Kwani anahisi lolote baya? Na kwa nini?
 
mleta mada ni kilaza anastress za maisha hasa mambo ya siasa,uccm na uchadema,anadhan kila kitu n siasa.amezoa kualalamika.anadhan jeshini kuna mwenyekiti na mtendaji ama katibu,ama kula za maoni hahahhaa,
 
Ivi tulishanunua ndege mpya? Au bado tuna rusha zile mig79 za kirusi tangu wakati wa nduli.
 
Wazirushe tu maana siona kama hiyo ni bahati mbaya kwa hizo ndege kuwa angani. Yote unayoyaona yaliandaliwa katika budget ya mwaka wa fedha. 😛
 
Heshima kwenu waungwana,
kwa mliopo dar wengi wenu mtakua mmeshuhudia ndege tatu za jeshi zikiwa zinarushwa kwa kufuatana kwa kasi sana angani, mimi swali langu ni je gharama zake zina faida au tija kwa taifa? Je mafuta yanayotumika sio kodi ya jasho la watanzania? Hebu tupia maoni yako hapa

Vilaza kama wewe hawataisha Tanzania kamwe
 
Ukisha kuwa maskini hata mawazo yako yanakuwa ya kimaskini unadhani ndege huwekwa hanga kungojea vita bila mazoezi?
 
hayo ni mazoezi kwaajili ya kumpigia salut baba riz pale taifa katika sherehe za uhuru 9 desemba, na hela zake zimepangwa kutoka kwenye bajeti na wala sio ufujaj ea kodi
 
Sio kila jambo linalofanywa na Serikali basi lazima upinge. Mbona hukuuliza kwanini zimenunuliwa kwa Kodi zetu???
Embu ulizia Nchi zilizoendelea harafu watakwambia wao ndege wanarusha lini hadi lini, mimi ninavyojua wenzetu kila siku wanafanya haya mazoezi tofauti na sisi mpaka sikukuu.
Kumbuka hili ni Jeshi la Ulinzi la Watanzania ambao wamekufanya wewe uwe huru muda huu kwenye Simu/PC yako unaandika vitu kama hivi.

Safi sana maana wapumbavu kama mleta mada wapo wengi sana na kuna siku mtawahoji hata wazazi wenu kwanini walikuzaa.
 
Heshima kwenu waungwana,
kwa mliopo dar wengi wenu mtakua mmeshuhudia ndege tatu za jeshi zikiwa zinarushwa kwa kufuatana kwa kasi sana angani, mimi swali langu ni je gharama zake zina faida au tija kwa taifa? Je mafuta yanayotumika sio kodi ya jasho la watanzania? Hebu tupia maoni yako hapa

Mkuu ni mazoezi kwa ajili ya maonyesho ya sherehe za uhuru. Pia ni moja ya ishara kuonyesha kuwa tunaweza kutumia ndege zetu za kivita. zikikaa tu bila kutumika unadhani ndo itanufaisha watanzania? bora hivi zinavyoruka na wakati mwingine vijana wetu huwa wanafanya mazoezi ili wawe fiti. Tusiwe watu wa lawama. Zingekuwa hazitumiki na likaja tatizo najua pia utakuwa wa kwanza kusema
MAVITU YANAOZA HAYATUMIKI HALAFU TUMEVAMIWA KWA JAMBO AMBALO TUNGEWEZA KUFUNDISHA WATU NA WAKAZITUMIA KUJILINDA.
Samahani lakini mkuu. ila tusiwe watu wa lawama kwa mambo ambayo hata kwa kufikiri unaona maana yake
 
tatizo unatumia ------ kufikiri,unadhan kila jambo linalofanyika lazima uone faida zake moja kwamoja,kaa na uzezeta wako,ivoivo

jeshi lina faida sana tu kwa raia,kwani hukuona kule mtwara?we upo dunia ipi???
 
jamani tulikuwa tunafanya ontest sasa kama mmechukia mtusamehe watanzania aah nchi ngumu hii
 
Jwtz wakifanya vizuri Congo,Darfur tunawasifia. Unadhani jeshi bila mafunzo/mazoezi wanaweza kushinda vita?
vita gain ya kupigana namadege sasa hivi? Adui was taifa la Tz ni ujinga ,umaskini,rushwa iliyokithiri na viongozi kusaini mikataba yenye kufilisi nchi yetu . kurusha ndege ni kupotosha malengo kama ni mazoezi waende porini . kama wanavyofanya US mazoezi wanafanyia kwenye jangwa la Nevada.
 
Back
Top Bottom