Michirizi ya Damu

Michirizi ya Damu

SEHEMU YA 26

Hakuchukua dakika nyingi akafika katika Hoteli ya Bavaria, akateremka kutoka kwenye teksi na kisha kumlipa dereva na kuanza kuelekea ndani. Mavazi yake, kwa kumwangalia ingekuwa vigumu kugundua kama alikuwa mwanaume, alijiremba na kujiremba, hata kutembea kwake alitembea kwa mikogo huku akijitingisha kwa nyuma.

“Nimekuja kumuona Bwana Saed,” alisema Fareed kwa sauti ya kike. “Sawa. Nenda chumba namba 18,” alisema msichana wa mapokezi huku akimpa ufunguo wa chumba hicho.

Akaupokea na kuanza kuelekea huko. Moyo wake ulikuwa kwenye furaha tele, aliamini kwamba kama siku hiyo angepewa kiasi cha dolaa elfu tano kingekuwa kiasi kikubwa sana ambacho angefanya mambo mengi sana katika maisha yake.

Alipofika ndani ya chumba hicho, akajilaza kitandani na kuanza kumsubiri mwanaume huyo kwa hamu kubwa. Hakutulia pale chumbani, wakati mwingine alikuwa akisimama na kuanza kutembeatembea huku na kule, wakati mwingine alikwenda bafuni na kisha kuanza kujiangalia kwenye kioo.

Aliibinua midomo yake, alijiweka vilivyo, akajiosha, akaona hiyo haitoshi, akaoga kabisa na kujipulizia manukato ya Zenji kama kawaida yake.
Aliporudi chumbani, akachukua simu yake na kumtumia ujumbe mfupi Bwana Saed kwa kumwambia kuwa alikuwa tayari na ni yeye tu ndiye aliyekuwa akimsubiri.

“Nipo tayari! Nakusubiri wewe mume wangu! Mbona unakawia! Jamani utaniua kwa presha!” aliandika ujumbe huo na kumtumia.
Bwana Saed aliupata ujumbe huo, pale alipokuwa kwenye kikao, akaachia tabasamu pana. Moyo wake ukajisikia raha kupita kawaida, akawaangalia wenzake walikuwa kwenye kile kikaona na kuona kama walikuwa wakimpotezea muda.

Kwenye kikao hicho pia alikuwepo Godfrey. Macho yake yalikuwa yakimwangalia Bwana Saed, hakujua ni kitu gani alikiona kwenye simu yake mpaka kuonekana kuwa na furaha kiasi hicho, hakutaka kumfuatilia sana, akajua mambo yake, akafuatilia kikao kile mpaka kilipokwisha.

Bwana Saed hakutaka kubaki mahali hapo, haraka sana akaondoka kwa kuwaaga wachache, alihisi kama angeendelea kubaki mahali hapo basi Fareed angekasirika na kuondoka zake.
 
SEHEMU YA 26

Hakuchukua dakika nyingi akafika katika Hoteli ya Bavaria, akateremka kutoka kwenye teksi na kisha kumlipa dereva na kuanza kuelekea ndani. Mavazi yake, kwa kumwangalia ingekuwa vigumu kugundua kama alikuwa mwanaume, alijiremba na kujiremba, hata kutembea kwake alitembea kwa mikogo huku akijitingisha kwa nyuma.

“Nimekuja kumuona Bwana Saed,” alisema Fareed kwa sauti ya kike. “Sawa. Nenda chumba namba 18,” alisema msichana wa mapokezi huku akimpa ufunguo wa chumba hicho.
Akaupokea na kuanza kuelekea huko. Moyo wake ulikuwa kwenye furaha tele, aliamini kwamba kama siku hiyo angepewa kiasi cha dolaa elfu tano kingekuwa kiasi kikubwa sana ambacho angefanya mambo mengi sana katika maisha yake.

Alipofika ndani ya chumba hicho, akajilaza kitandani na kuanza kumsubiri mwanaume huyo kwa hamu kubwa. Hakutulia pale chumbani, wakati mwingine alikuwa akisimama na kuanza kutembeatembea huku na kule, wakati mwingine alikwenda bafuni na kisha kuanza kujiangalia kwenye kioo.
Aliibinua midomo yake, alijiweka vilivyo, akajiosha, akaona hiyo haitoshi, akaoga kabisa na kujipulizia manukato ya Zenji kama kawaida yake.

Aliporudi chumbani, akachukua simu yake na kumtumia ujumbe mfupi Bwana Saed kwa kumwambia kuwa alikuwa tayari na ni yeye tu ndiye aliyekuwa akimsubiri.
“Nipo tayari! Nakusubiri wewe mume wangu! Mbona unakawia! Jamani utaniua kwa presha!” aliandika ujumbe huo na kumtumia.
Bwana Saed aliupata ujumbe huo, pale alipokuwa kwenye kikao, akaachia tabasamu pana. Moyo wake ukajisikia raha kupita kawaida, akawaangalia wenzake walikuwa kwenye kile kikaona na kuona kama walikuwa wakimpotezea muda.

Kwenye kikao hicho pia alikuwepo Godfrey. Macho yake yalikuwa yakimwangalia Bwana Saed, hakujua ni kitu gani alikiona kwenye simu yake mpaka kuonekana kuwa na furaha kiasi hicho, hakutaka kumfuatilia sana, akajua mambo yake, akafuatilia kikao kile mpaka kilipokwisha.

Bwana Saed hakutaka kubaki mahali hapo, haraka sana akaondoka kwa kuwaaga wachache, alihisi kama angeendelea kubaki mahali hapo basi Fareed angekasirika na kuondoka zake.
 
SEHEMU YA 27

Alipofika nje, akamwambia dereva wake kwamba alitakiwa kuendesha gari kwa mwendo wa kasi kuelekea katika Hoteli ya Bavaria. Safari hiyo iliwachukue dakika tano tu, walipofika, akaelekea huko chumbani na kumkuta Fareed akiwa kitandani.

“Nimekuja harakaharaka kama nimepaa,” alisema Bwana Saed huku akivua koti lake na kumfuata Fareed pale alipokaa.
**** Akili ya Godfrey ilikuwa ikimfikiria Fareed tu, kila alipokaa, kichwa chake kilikuwa kwa mwanaume huyo tata. Kikaoni hakuwa na furaha, kila alipokaa alikuwa akimfikiria kiasi kwamba wakati mwingine alijiona kama mgonjwa kwa jinsi aliyokuwa amechanganyikiwa kwa penzi lake.

Siku hiyo hali ilionekana kuwa tofauti kabisa, kila alipokuwa, mara kwa mara alikuwa akisumbuliwa na Fareed kwa kutumiwa meseji na hata wakati mwingine video lakini siku hiyo, alikaa mwanzo wa kikao mpaka mwisho hakukuwa na meseji yoyote aliyokuwa ametumiwa.

Akahisi kwamba kuna tatizo, akahisi kwamba Fareed alikuwa na mwanaume mwingine, moyo wake uliumia, ukamchoma kupita kawaida, hakutaka kukubali, akaanza kumpigia simu, cha ajabu simu ilikuwa ikiita bila kupokelewa.
“Mbona hapokei simu? Kuna nini? Au yupo na mwanaume mwingine? Au kuna mwenzangu kamuona akirandaranda akamteka, hapana! Ni lazima niwahi kurudi,” alisema Fareed huku akionekana kuchanganyikiwa hasa.

Hakukuwa na raha kikaoni hapo, muda wote kichwa chake kilivurugika, kwa kile kilichokuwa kimetokea cha kutokutumiwa meseji kiliuchanganya moyo wake, hivyo alipotoka kikaoni, moja kwa moja akaingia ndani ya gari alilolikodi kulitumia na kurudi hotelini.

Hakuchukua muda mrefu, akafika na moja kwa moja kuteremka na kuanza kuelekea humo. Alikimbia kama mtu aliyekuwa na haraka fulani, alipoingia ndani ya chumba hicho, hakumuona Fareed, akaelekea bafuni, napo hakuwepo na kila alipompigia simu, iliita bila kupokelewa, uso wake ukavimba kwa hasira.

“Huyu malaya atakuwa ananisaliti! Atakuwa amelala na mwanaume mwingine,” alijisemea huku akionekana kuwa na hasira kali mno.

Aliendelea kumpigia simu, haikuwa ikipokelewa na mwisho wa siku kutokupatikana kabisa, alichanganyikiwa na moyo wake kujawa na hasira kali.
 
Back
Top Bottom