Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,870
- Thread starter
- #161
SEHEMU YA 26
Hakuchukua dakika nyingi akafika katika Hoteli ya Bavaria, akateremka kutoka kwenye teksi na kisha kumlipa dereva na kuanza kuelekea ndani. Mavazi yake, kwa kumwangalia ingekuwa vigumu kugundua kama alikuwa mwanaume, alijiremba na kujiremba, hata kutembea kwake alitembea kwa mikogo huku akijitingisha kwa nyuma.
“Nimekuja kumuona Bwana Saed,” alisema Fareed kwa sauti ya kike. “Sawa. Nenda chumba namba 18,” alisema msichana wa mapokezi huku akimpa ufunguo wa chumba hicho.
Akaupokea na kuanza kuelekea huko. Moyo wake ulikuwa kwenye furaha tele, aliamini kwamba kama siku hiyo angepewa kiasi cha dolaa elfu tano kingekuwa kiasi kikubwa sana ambacho angefanya mambo mengi sana katika maisha yake.
Alipofika ndani ya chumba hicho, akajilaza kitandani na kuanza kumsubiri mwanaume huyo kwa hamu kubwa. Hakutulia pale chumbani, wakati mwingine alikuwa akisimama na kuanza kutembeatembea huku na kule, wakati mwingine alikwenda bafuni na kisha kuanza kujiangalia kwenye kioo.
Aliibinua midomo yake, alijiweka vilivyo, akajiosha, akaona hiyo haitoshi, akaoga kabisa na kujipulizia manukato ya Zenji kama kawaida yake.
Aliporudi chumbani, akachukua simu yake na kumtumia ujumbe mfupi Bwana Saed kwa kumwambia kuwa alikuwa tayari na ni yeye tu ndiye aliyekuwa akimsubiri.
“Nipo tayari! Nakusubiri wewe mume wangu! Mbona unakawia! Jamani utaniua kwa presha!” aliandika ujumbe huo na kumtumia.
Bwana Saed aliupata ujumbe huo, pale alipokuwa kwenye kikao, akaachia tabasamu pana. Moyo wake ukajisikia raha kupita kawaida, akawaangalia wenzake walikuwa kwenye kile kikaona na kuona kama walikuwa wakimpotezea muda.
Kwenye kikao hicho pia alikuwepo Godfrey. Macho yake yalikuwa yakimwangalia Bwana Saed, hakujua ni kitu gani alikiona kwenye simu yake mpaka kuonekana kuwa na furaha kiasi hicho, hakutaka kumfuatilia sana, akajua mambo yake, akafuatilia kikao kile mpaka kilipokwisha.
Bwana Saed hakutaka kubaki mahali hapo, haraka sana akaondoka kwa kuwaaga wachache, alihisi kama angeendelea kubaki mahali hapo basi Fareed angekasirika na kuondoka zake.
Hakuchukua dakika nyingi akafika katika Hoteli ya Bavaria, akateremka kutoka kwenye teksi na kisha kumlipa dereva na kuanza kuelekea ndani. Mavazi yake, kwa kumwangalia ingekuwa vigumu kugundua kama alikuwa mwanaume, alijiremba na kujiremba, hata kutembea kwake alitembea kwa mikogo huku akijitingisha kwa nyuma.
“Nimekuja kumuona Bwana Saed,” alisema Fareed kwa sauti ya kike. “Sawa. Nenda chumba namba 18,” alisema msichana wa mapokezi huku akimpa ufunguo wa chumba hicho.
Akaupokea na kuanza kuelekea huko. Moyo wake ulikuwa kwenye furaha tele, aliamini kwamba kama siku hiyo angepewa kiasi cha dolaa elfu tano kingekuwa kiasi kikubwa sana ambacho angefanya mambo mengi sana katika maisha yake.
Alipofika ndani ya chumba hicho, akajilaza kitandani na kuanza kumsubiri mwanaume huyo kwa hamu kubwa. Hakutulia pale chumbani, wakati mwingine alikuwa akisimama na kuanza kutembeatembea huku na kule, wakati mwingine alikwenda bafuni na kisha kuanza kujiangalia kwenye kioo.
Aliibinua midomo yake, alijiweka vilivyo, akajiosha, akaona hiyo haitoshi, akaoga kabisa na kujipulizia manukato ya Zenji kama kawaida yake.
Aliporudi chumbani, akachukua simu yake na kumtumia ujumbe mfupi Bwana Saed kwa kumwambia kuwa alikuwa tayari na ni yeye tu ndiye aliyekuwa akimsubiri.
“Nipo tayari! Nakusubiri wewe mume wangu! Mbona unakawia! Jamani utaniua kwa presha!” aliandika ujumbe huo na kumtumia.
Bwana Saed aliupata ujumbe huo, pale alipokuwa kwenye kikao, akaachia tabasamu pana. Moyo wake ukajisikia raha kupita kawaida, akawaangalia wenzake walikuwa kwenye kile kikaona na kuona kama walikuwa wakimpotezea muda.
Kwenye kikao hicho pia alikuwepo Godfrey. Macho yake yalikuwa yakimwangalia Bwana Saed, hakujua ni kitu gani alikiona kwenye simu yake mpaka kuonekana kuwa na furaha kiasi hicho, hakutaka kumfuatilia sana, akajua mambo yake, akafuatilia kikao kile mpaka kilipokwisha.
Bwana Saed hakutaka kubaki mahali hapo, haraka sana akaondoka kwa kuwaaga wachache, alihisi kama angeendelea kubaki mahali hapo basi Fareed angekasirika na kuondoka zake.
