Michirizi ya Damu

Michirizi ya Damu

MICHIRIZI YA DAMU-31

Asteria akakata simu na kisha kufanya kama alivyoambiwa. Hakuamini macho yake baada ya kugundua kwamba alikuwa akiwasiliana na bilionea mkubwa nchini Marekani. Kwanza akaanza kutetemeka, yeye mwenyewe alihofu, hakujiamini kwani miongoni mwa watu waliokuwa mabilionea, Keith alikuwa balaa.
“Umeona sasa?” aliuliza Keith baada ya kumpigia simu.

“Ndiyo! Unahitaji wanawake wangapi?”
“Tuanze na mmoja.”
“Nitakupa aitwaye Penny?”
“Anajua?”
“Usiwe na shaka na watu wangu. Wewe niachie anuani yako!” alisema Asteria na kukata simu.
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kufahamiana na bilionea huyo, mara kwa mara walikuwa wakiwasiliana huku akimwambia kwamba alikuwa akihitaji wanawake zaidi. Alipenda kufanya ngono na wanawake weusi, maishani mwake, japokuwa alikuwa Mzungu lakini hakuwapenda Wazungu.

Wakatengeneza uswahiba mkubwa na kujikuta ndani ya miezi sita wakiwa marafiki wakubwa. Wakati mwingine Asteria alikuwa akisafiri mpaka nchini Marekani ambapo huko alikutana na mwanaume huyo na kuzungumza mambo mengi.

Biashara yake iliendelea kukua. Alizidi kuwasafirisha wanawake kwenda huko kwa ajili ya kufanya nao mapenzi na bilionea huyo.
Baada ya mwaka mmoja kupita huku urafiki wao ukiwa mkubwa ndipo siku moja bilionea huyo akamualika Asteria katika shere yake ya kuzaliwa ambayo angeifanya Jijini Los Angeles, alimuomba sana ahudhurie kwani ilikuwa ni sherehe kubwa ambayo ingekutanisha mastaa wengi kutoka sehemu mbalimbali hapo Marekani.

“Nitakuja!”
“Njoo na marafiki zangu basi!”
“Haina shida. Wangapi?”
“Wawili!” “Sawa.”
Asteria akafurahia, moyo wake ukajua kwamba hiyo ndiyo ilikuwa nafasi ya kutengeneza fedha zaidi. Hakutaka kuiacha nafasi hiyo, alitaka kuhakikisha anaitumia vizuri kuhakikisha kwa mwaka huo anakuwa na kiasi kikubwa cha fedha.

Akawachukua wasichana wawili, Ester na Queen lakini pia akamuongeza na Fareed kwa kuamini kwamba ndani ya sehemu ambayo wangeonana kwa ajili ya sherehe hiyo ingewezekana kabisa kupata mteja mwingine kupitia Fareed.
“Marekani?”
“Ndiyo! Kuna mabwana wa Kizungu, wenye hela zao,” alisema Asteria.
“Basi sawa. Nitakwenda!”
 
SEHEMU YA 32

Fareed alifurahi, kwa kipindi kirefu alitamani kufika nchini Marekani, kitendo cha kuambiwa kwamba alitakiwa kwenda huko, moyo wake ukarukaruka na siku hiyo ilipofika, wakaondoka kuelekea huko.

Baada ya saa zaidi ya ishirini, ndege ikaanza kutuka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa LAX uliokuwa hapohapo Los Angeles. Walipoteremka, tayari kulikuwa na gari lililokuwa likiwasubiria ambapo moja kwa moja wakaingia na kuanza kupelekwa katika hoteli waliyotakiwa kufikia.

Njiani, Fareed alikuwa na furaha tele, hakuamini kama kweli alifika Marekani. Aliangalia nje, jinsi jiji hilo lilivyokuwa limejengeka, lilipendeza machoni mwake na kila alipokuwa akiliangalia, alijiona kama yupo katika pepo ndogo.

Hawakuchukua muda mrefu wakafika hotelini. Wakateremka na kuelekea ndani, huko, wakatulia vyumbani na kuagiza chakula ambapo wakaletewa kwani kila kitu kililipiwa na Bilionea Keith.
“Vipi? Mmekwishafika?” aliuliza bilionea huyo.

“Yeah! Ndiyo tumeingia!”
“Nakuja!”
Wala hazikupita dakika nyingi bilionea huyo akafika hotelini humo na moja kwa moja kuelekea katika chumba hicho. Alipofika katika korido ya iliyokuwa na chumba kile akaingia ndani. Macho yake yakatua kwa watu waliokuwa humo ndani, walikuwa wasichana wazuri, aliwapenda lakini mbali na wasichana hao, alipomwangalia Fareed, akashtuka sana, hakuamini kama kulikuwa na msichana mwingine mzuri namna hiyo.

“Ooh! Ni wasichana wazuri! Naona umeniongezea wa tatu kabisa,” alisema Bilionea Keith huku akitoa tabasamu pana.
Asteria hakujibu, akamvutia pembeni na kuanza kuzungumza naye kuhusu Fareed kwamba hakuwa msichana kama alivyohisi bali alikuwa mwanaume tata maneno yaliyomfanya bilionea huyo kushangaa.
Hakuamini kama kulikuwa na mwanaume aliyekuwa mrembo kama Fareed.

Aliwafahamu wanaume tata waliokuwa nchini Marekani, hawakuwa na uzuri mkubwa lakini kwa Fareed alionekana kuwa tofauti, alikuwa na muonekano wa kike na hata maringo yake, jinsi alivyokuwa akiuweka mwili wake, alionekana kama msichana.

“Ni mwanaume?”
“Ndiyo!”
“Unanitania!”
“Siwezi kukutania!”
“Mbona kama mwanamke mrembo?”
“Ndiyo hivyo! Ni mwanaume huyo.”
 
Mh.!! Jamani Shunie.!! Akina ya nani huyu Fareed huyu.!! Yaani hata cmueleei vile.!! Ssuti ilibadilikaje kutoka la Kidume na kuwa la Kike.!!
 
Back
Top Bottom