tpaul
Platinum Member
- Feb 3, 2008
- 25,956
- 25,345
Kipindi cha michepuko kimewadia! Utafiti unaonyesha kwamba kila michuano mikubwa ya mpira inapoanza kama vile Kombe la Dunia, UEFA Champions League na Kombe la Mataifa ya Afrika, wanaume wengi wakware huwalaghai wake/wapenzi zao kwamba wanaenda kutazama mechi kumbe hutumia mwanya huo kuteleza kwenda kwa nyumba ndogo (Michepuko).
Leo michuano ya Kombe la Dunia inafungua pazia huko Brazil. Tayari kutakuwa na wanaume wakware ambao wameishapanga ‘appointment' za kukutana na michepuko yao kwa kutumia kisingizio feki cha Kombe la Dunia. Nawaasa akina mama muwe makini na ‘Njia Kuu' zenu kwani huu ndio wakati mtakaodanganywa na hatimaye ‘kuibiwa' waume zenu kirahisi kabisa. Jengeni utaratibu wa kuandamana na waume zenu kwenda mpirani ili muweze kuzidhibiti nyendo zao za kilaghai. Siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli. Nimetimiza wajibu wangu wa kuwapa tahadhari. Kama kuna mwanamke atamuachia mumewe aondoke nyumbani hiiivi hivi na hatimaye kuibiwa, shauri yake.
Nawasilisha.
:help:
Leo michuano ya Kombe la Dunia inafungua pazia huko Brazil. Tayari kutakuwa na wanaume wakware ambao wameishapanga ‘appointment' za kukutana na michepuko yao kwa kutumia kisingizio feki cha Kombe la Dunia. Nawaasa akina mama muwe makini na ‘Njia Kuu' zenu kwani huu ndio wakati mtakaodanganywa na hatimaye ‘kuibiwa' waume zenu kirahisi kabisa. Jengeni utaratibu wa kuandamana na waume zenu kwenda mpirani ili muweze kuzidhibiti nyendo zao za kilaghai. Siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli. Nimetimiza wajibu wangu wa kuwapa tahadhari. Kama kuna mwanamke atamuachia mumewe aondoke nyumbani hiiivi hivi na hatimaye kuibiwa, shauri yake.
Nawasilisha.
:help: