Tokea kufanyika kile kilichoitwa uchaguzi wa marudio mwezi Machi, 2016, sasa ni takribani miaka miwili na miezi miwili ya uongozi wa DR Shein kule Zanzibar. Muda unaenda kwa kasi sana.
Kuna masuali mengi ya kujiuliza hapa.
IPI HATMA YA CUF ?
Kwanza ipi hatma ya CUF ambayo baada ya kumaliza uchaguzi ule waliousisia waliwaaminisha wazanzibari kwamba haki yao ya uchaguzi wa 2015 uliofutwa na Jecha itapatikana na wenyewe walielekeza nguvu zao kupitia jumuiya ya kimataifa hasa kwa kujiweka karibu na taasisi za kimarekani na Uengereza. Jee kwa kile kinachoendelea kuna uwezekano wa kutokea mabadiliko yoyote ya kurejheshwa haki hiyo ? na jee ikiwa hilo halikufanikiwa na mazingira ya uchaguzi ya 2020 yakafanyika bila kutokea mabadiliko ya kimfumo kwenye ZEC na Serikali nini itakuwa hatma ya CUF ?
JEE JUMUIYA YA KIMATAIFA IMEITUPA MKONO ZANZIBAR NA CUF ?
Hili ni suali muhimu, wadau wa uchaguzi wa kimataifa ni UN, kupitia taasisi yake ya UNDP, mataifa makubwa na mashirika yao ya kutetea demokrasia na haki, nchi moja moja na washirika wa maendeleo na marafiki. Zanzibar imekumbwa na tufani ya kisiasa kwa muda mrefu na hakujawa na usawa wa mazingira ya ushindani ya uchaguzi huru na haki kwa wadau , kiasi kwamba kumetokezea mitafaruku na hata mauaji na uvunjifu wa haki za binadamu.
Tuliona jitihada za awali za jumuiya ya Madola baada ya uchaguzi wa 1995 kupitia msuluhishi Chief Ameka Anyauku, ikifuatiwa na miafaka iliyofeli ya 1995, 2000 n.k. Miafaka hii bila shaka ilitiliwa nguvu na Jumuiya za kimataifa mbali mbali.
Hata hivyo, wadau wa demokrasia walidhani SULUHU ya kuingiza maridhiano Kwenye KATIBA YA ZANZIBAR, kupitia mabadiliko ya katiba ya mwaka 2009 chini ya Utawala wa Dr Karume itakuwa Muarubaini wa Matatizo ya Zanzibar kwa washindani kushirikiana kuongoza nchi kwa ulingano wa kuchaguliwa jambo ambalo lilifanya kazi kwa miaka mitano tu 2010 - 2015.
Kinachoshuhudiwa ni kurudi kwa migogoro kama awali huku kukiwa na malalamiko ya chama Dola (CCM ) kutokubali kufuata misingi ya umoja wa kitaifa kwenye Chaguzi na hatimae migogoro kuendelea licha ya JITIHADA KUBWA ZA NDANI NA KIMATAIFA.
Kwa sasa ni zaidi ya miaka miwili ya uongozi wa Dr Shein, Hatusikii masindikizo wala hatuoni jitihada za wazi za jumuiya ya kimataifa kuhusu hali ya Zanzibar. Muda umekwenda kuna ukimya . Jee kwa muhtasari huo tunaweza kusema Jumuiya ya Kimataifa imeshindwa na kuamua kuitupa mkono Zanzibar ?
Tunahitaji wataalamu na wajuzi wa siasa na diplomasia watusaidie maana ikiwa hali itakuwa hivi ilivyo nini itakuwa hatma ya Zanzibar huko mbele ?
Kishada.
Kuna masuali mengi ya kujiuliza hapa.
IPI HATMA YA CUF ?
Kwanza ipi hatma ya CUF ambayo baada ya kumaliza uchaguzi ule waliousisia waliwaaminisha wazanzibari kwamba haki yao ya uchaguzi wa 2015 uliofutwa na Jecha itapatikana na wenyewe walielekeza nguvu zao kupitia jumuiya ya kimataifa hasa kwa kujiweka karibu na taasisi za kimarekani na Uengereza. Jee kwa kile kinachoendelea kuna uwezekano wa kutokea mabadiliko yoyote ya kurejheshwa haki hiyo ? na jee ikiwa hilo halikufanikiwa na mazingira ya uchaguzi ya 2020 yakafanyika bila kutokea mabadiliko ya kimfumo kwenye ZEC na Serikali nini itakuwa hatma ya CUF ?
JEE JUMUIYA YA KIMATAIFA IMEITUPA MKONO ZANZIBAR NA CUF ?
Hili ni suali muhimu, wadau wa uchaguzi wa kimataifa ni UN, kupitia taasisi yake ya UNDP, mataifa makubwa na mashirika yao ya kutetea demokrasia na haki, nchi moja moja na washirika wa maendeleo na marafiki. Zanzibar imekumbwa na tufani ya kisiasa kwa muda mrefu na hakujawa na usawa wa mazingira ya ushindani ya uchaguzi huru na haki kwa wadau , kiasi kwamba kumetokezea mitafaruku na hata mauaji na uvunjifu wa haki za binadamu.
Tuliona jitihada za awali za jumuiya ya Madola baada ya uchaguzi wa 1995 kupitia msuluhishi Chief Ameka Anyauku, ikifuatiwa na miafaka iliyofeli ya 1995, 2000 n.k. Miafaka hii bila shaka ilitiliwa nguvu na Jumuiya za kimataifa mbali mbali.
Hata hivyo, wadau wa demokrasia walidhani SULUHU ya kuingiza maridhiano Kwenye KATIBA YA ZANZIBAR, kupitia mabadiliko ya katiba ya mwaka 2009 chini ya Utawala wa Dr Karume itakuwa Muarubaini wa Matatizo ya Zanzibar kwa washindani kushirikiana kuongoza nchi kwa ulingano wa kuchaguliwa jambo ambalo lilifanya kazi kwa miaka mitano tu 2010 - 2015.
Kinachoshuhudiwa ni kurudi kwa migogoro kama awali huku kukiwa na malalamiko ya chama Dola (CCM ) kutokubali kufuata misingi ya umoja wa kitaifa kwenye Chaguzi na hatimae migogoro kuendelea licha ya JITIHADA KUBWA ZA NDANI NA KIMATAIFA.
Kwa sasa ni zaidi ya miaka miwili ya uongozi wa Dr Shein, Hatusikii masindikizo wala hatuoni jitihada za wazi za jumuiya ya kimataifa kuhusu hali ya Zanzibar. Muda umekwenda kuna ukimya . Jee kwa muhtasari huo tunaweza kusema Jumuiya ya Kimataifa imeshindwa na kuamua kuitupa mkono Zanzibar ?
Tunahitaji wataalamu na wajuzi wa siasa na diplomasia watusaidie maana ikiwa hali itakuwa hivi ilivyo nini itakuwa hatma ya Zanzibar huko mbele ?
Kishada.