YATC
Duuih!! Pole sana ndugu, kikubwa usikate tamaa ila nikushauri jambo kwa kukupa mfano.
Nina shem wangu nae alikaa kitaa sana akizunguka huku na kule kutafuta kazi. Nilimpa mbinu mbili moja ni kusoma post graduate diploma au kujitolea kufanya kazi.
Aliamua kujitolea, nilimuelekeza mashirika makubwa ya kujitolea ili kuupata mfumo wa juu kabisa ili uweze kupata kazi katika mashirika ya chini. Mfano ukijitolea Ewura ni rahisi kwako kupata kazi Tanesco na idara za maji zote za mikoa yote pia mashirika ya gesi! Sababu kubwa ni kwamba yapo chini ya Ewura na ule mfumo wote utakuwa umeujua, upo ndugu. Hapo nafasi ni kubwa kwako kupata ajira kwa mashirika mbali mbali sababu kubwa ile inferiority itakuwa imekutoka.
Itakuwa ngumu kwako kutoka Dawasco au Moruwasa kupata kazi kwenye mashirika ya kitaifa.
Believe it yule shem baada ya miezi saba ya kazi amekula shavu nono mpaka inatia hasira! Pata picha alikaa mtaani zaidi ya miaka miwili na kajitolea miezi saba akala shavu, kwa nini wewe??
Kikubwa angalia na shirika la kujitole coz kuna mashirika hata ufanye nini cha ajabu ukaweka kwenye CV hupati kazi!! Kila la heri ndugu