TUTASHINDA TENA
Senior Member
- Aug 12, 2014
- 141
- 78
Huu ni wakati wa upinzani kuendeleza Rombo,
Naomba kifupi cha wasifa wa hawa vijana, je wameshaongoza nini katika chama au vyuoni/makazini, ubunge sio sehemu ya kufanyia majaribio ni sehemu ya kufanya kazi, nauliza sababu siwafahamu.
Rombo ni wilaya kubwa na yenye fursa nyingi sana, ila inasikitisha sana kuona uzembe katika mambo mengi ikiweko kutokuwa na ghala la chakula, watu wanauza mahindi mpaka wanakuja kudhurika na njaa na mambo mengine kama huduma za afya, Huruma Hospital ingeweza kuendelezwa, baadhi ya watu wasingekuwa wanatoka wilayani kutafuta matibabu sehemu nyingine. Kingine ni utamaduni wa kirombo unaopotea siku kwa siku, tunahitaji mbunge atakayefungua ofisi ya wilaya ya utamaduni na historia ya Rombo na kuwa wazee wale wenye kujua nyimbo na ngoma za kirombo wanaopata support ya mbunge. Mtu ukiwa mkoani una harusi unaweza kuwakodi wakaja. Makabila mengine wanadumisha sana utamaduni wao na mila zao na wameweza kuleta hadi Mijini.
Mwisho wa wote ninaomba sifa za Ben na Frate je wanafamilia, je wameshawahi kuongoza nini? cc Mromboo
FRATE MASIKA
-Ni msomi wa ngazi ya Stashahada na alikua anasoma shahada nafikiri
-Ni mtu mwenye Biashara zake Arusha na Useri Rombo
-Ana mke na watoto
-Mama yake ni Diwani wa Viti Maalumu CCM
-Ameshawahi kuongoza taasisi na hata NGO
-Ana miaka takribani 40
-Anatokea Tarakea
-Ni mzoefu wa mikakati kwa kuwa ana uzoefu wa hizi siasa kutoka kwenye familia ingawa wazazi wake wako itikadi tofauti na itikadi yake
BEN SAANANE:
-Ni Msomi wa digrii ya biashara (BBA) na (Masters) ya Uchumi na Masters ya Uhusiano wa kimataifa na Diplomasia kwa mujibu wa CV yake aliyoweka hadharani alipogombea Uenyekiti wa vijana Taifa kabla ya jina lake kuondolewa
-Ni Mkuu wa Idara ya sera na utafiti ya Chadema makao makuu
-Alifanya kazi kwenye kampuni ya Alpha kama meneja masoko
-Ni mjasiriamali pia
-Anatokea Tarafa ya Mashati
-Hajaoa bado ana miaka taribani 30
-Ni mzoefu pia wa mikakati kama huyo mwingine kwa kuwa tayari yupo kwenye siasa za kitaifa na ndani ya jimbo
Last edited by a moderator: