Miaka 97 ya Mzee Mwinyi na amani ya moyoni pasipo nongwa na visasi

1960 alikuwa Mkuu wa Chuo cha Ualimu Znz cha Lumumba tangu hapo akaanza kuwa na mshahara mkubwa

1966 Balozi, kaja kuwa Waziri wa Jamhuri tangu 1972

kaja kuwa Rais wa Znz

kaja kuwa Rais wa Muungano

binti yake mmoja kaolewa na mtoto wa Mfalme wa Abudhabi

Mtoto wake Rais wa Znz

mtoto wake mwingine Mbunge wa Bunge la Jamhuri

Ma binti zake ni Wafanyabiashara wakubwa wanaoshiriki kwny kandarasi kubwa kubwa za nje na ndani ya nchi

Vijana wake wa kiume ni ma Tycoon kwny biashara ta Utalii Afrika mashariki

wengine ni Wafanyakazi wa Taasisi kubwa kubwa za kimataifa

sasa hapo akiwa na Ukwasi ni jambo la kushangaa kweli ?

mwenzangu na mie kamshara ka TGSD hata shangazi akidondoka kwny bodaboda kijijini lazima utafutwe utume elf 5 ya kumbeba kwny bodaboda utachomokaje kwny lindi la umskini?
Some people are really blessed
 
Rais Mstaafu wa awamu ya pili leo anatimiza miaka 97, ni mingi kwa kuiandika na kuihisi kichwani ukifanya tafakari ya kina. Ni miongo tisa na miaka saba. Amekula magunia kwa magunia ya chumvi. Ni umri mkubwa sana kuendelea kuwepo hai, akiwaona wajukuu na watoto zao. Mzee Mwinyi kwa sisi tuliokuwepo duniani wakati anaingia na kuondoka ikulu ni heshima na baraka kumuona akiwa hai miaka 27 baada ya kuondoka Ikulu.

Wengi watajiuliza ameweza vipi kuishi miaka mingi namna hii. Wapo watakaosema hana makuu kwa maana ya kutoweka visasi moyoni, wapo watakaosema hanywi pombe akiwa ni muumini mzuri wa dini ya kiislam. Na wapo watakaokwenda mbali zaidi kwa kusema amekuwa akijitunza na siku zote akishiriki matembezi ya hiari na yeye mwenyewe kupenda kutembea. Na anayependa kutembea mazoezi ya asubuhi au kukimbia taratibu (jogging) anakwepa maradhi mengi yakiwepo yale ya moyo yenye kuua haraka na pasipo kutarajiwa.

Mzee Mwinyi ameendelea kuwepo wakati wazee wenzake karibu wote wa miaka ile ya awamu ya kwanza na ya pili wakiwa tayari wameshazikwa. Siku ya msiba wa hayati John Magufuli akasoma pasipo miwani!, na akatembea kwenda na kurudi kwenye kiti chake pasipo msaada wa kushikiliwa na mtu yoyote.

Ni kweli wote tunapita juu ya uso wa dunia, lakini kupita kwa baadhi yetu ni kule kwenye baraka. Unaweza kujiuliza inakuwaje Mzee huyu anazidi kusherehekea siku za kuzaliwa kila mwaka wakati wanasiasa vijana tu wakiaga dunia. Vijana waliozaliwa akiwa tayari ni mwanasiasa wanakufa na kumuacha yeye akiendelea kuishi kwa upole bila ya makuu pale kwake mbele kidogo ya Msasani kwa Mwalimu Nyerere.

Hakuwa na makuu, hakutunza hasira wala visasi. Hakutaka kuibadili dunia (To change the world), hakuamini kuwa kila tatizo anaweza yeye kama yeye akalitatua na hivyo kuumiza walio wengi katika mchakato wa utatuzi wa hilo tatizo. Hata baada ya kukejeliwa na Mwalimu Nyerere pale Kilimanjaro Hotel Simba Grill mwezi March mwaka 1995 aliendelea kuwa mkimya mpaka ilipofika siku akaamua kujibu mapigo.

Na baada ya hapo hakutaka kujikweza au kupandisha mabega, ni kama alisamehe na kuendelea kuwa huru moyoni. Hiyo ni sifa anayotakiwa kuwa nayo kiongozi mkuu wa Taifa. Uwezo wa kunyenyekea kwa kuyaona ni madogo tu baadhi ya mambo yanakukwaza na kukukera ukiwa ofisini. Ni mtihani mgumu sana kwa viongozi wenye madaraka makubwa kwa mujibu wa katiba yetu kuweza kujishusha huku wakiwa na vyombo vyote wanavyoweza kuvitumia katika kumuangamiza mtu anayewakera.

Miaka 27 ya kuishi kama mstaafu ni mingi, wengi wakijitahidi sana wataishi miaka mitano au kumi na kuaga dunia. Amewaona wasaidizi wake watatu wakiingia ikulu na kuondoka akiendelea kula raha pale nyumbani kwake. Huyu ni mwanasiasa ambaye maisha yake ni zaidi ya kitabu alichokizindua mwaka jana. Kwamba ukiwa hai huhitaji kujijazia makorokoro mengi kichwani kwako, yataishia kukuumiza na kukumaliza siku usiyoitarajia.

Pia ni somo la ucha Mungu. Kwamba ukimtegemea Mungu siku zote hataweza kukuacha ukatetereka na kuteseka kiafya. Miaka 97 ni zaidi ya ile miaka 70 ya kwenye Biblia kwa miaka 27. Siku zote jione wa kawaida na jione hufai kitu ukiwa umepiga magoti kanisani au msikitini. Ukiwa mdogo utajifunza kujiona sehemu ya wakosaji hata kama bajeti yako ya ulinzi ni mabilioni ya shilingi kwa siku, hata kama unalindwa na mitambo imara na wanajeshi wanaotumia zana za kisasa.

Na ni hapa marais wastaafu waislam wanapokuwa ni waalimu wa uungwana unaoambatana na maisha marefu. Hawaoni sababu ya kumuonea mtu au watu. Hawaoni sababu ya kuwafanya watu wakajiona ni kwanini wamekuja duniani kupata mateso yote haya!. Wanaweza kuitwa dhaifu kwa kuwa ni watu walio 'too liberal', wakiachia uhuru mwingi wa kuongea na kuandika, lakini hiyo ni sehemu muhimu wa utoaji wa haki ambao umeandikwa katika vitabu vitakatifu. Hivyo kuona marais wastaafu wa kiislam wanaendelea kuzeeka huku nyuso zao zikiwa na tabasamu la kirafiki ni bahati inayokwenda pamoja na kuwa sababu ya tulio wengi kujifunza mambo fulani ya kimaisha.

Kheri ya kuzaliwa Mzee Ali Hassan Mwinyi.
Umeandika vizuri sana lakini mwishoni kabisa usingemalizia vile ingewaachia watu watafakari wenyewe.
Hata hivyo staili ya mwinyi kimaisha ni nzuri sana watu wema wanaweza kuiga hiyo staili
 
Ukiishi ukiwa unafikiria kuumiza wengine mchana kweupe maana yake na wewe uliumizwa sana utotoni. Kule kuumizwa hakuishi kuwa ni tukio la kivitendo tu, bali kunaingia ndani kabisa ya ubongo wako.
Sidhani malezi ya utotobi yatakuwa ndio factor kuu. Kuna hulka na maumbile pia

Mfano akina Mandela mbona wamekulia kwenye msoto lakini wakasamehe

Kuna watoto wa marais na wanasiasa wakubwa huko nchi za DRC Burkina Faso n k sijui walikuwa nao marais na wakawa makatili tu
 
Mkuu Asante kwa andiko!
LAKINI
Ili uwe hivyo ulivyo andika inategemea malezi na makuzi uliyokulia!
Vijana wengi kama kina JPM walikulia shida na suluba za utotoni wakiwa wakubwa ile Hali haiwaachi salama kabisa kiakili na kisaikolojia na jpm anawakilisha kundi kubwa la watoto na vijana wengi wa kisasa hapa NCHINI makuzi na malezi DUNI full stress KILA kukicha mtu Huyo akipewa madaraka tu utaziona nyufa nyingi Sana!!malezi ya Mwinyi junior na Ridhiwan na baadh yao wanaweza kuyaishi hayo lakini sio kwa WENGINE kama Bashite na wengi Sana!
Ni kweli 100% kuhusu family history, shida na suluba za utotoni na hata za makuzi zinavyoathiri mwelekeo wa fikra za mtu na jinsi atakavyotenda ukubwani akitapata madaraka. Mifano ipo mingi, lakini mfano wa wazi kabisa na unaodhihirisha vyema hali hii ni wa Adolf Hitler. Soma historia yake kodogo tu utayaona yote hayo.
 
Sidhani malezi ya utotobi yatakuwa ndio factor kuu. Kuna hulka na maumbile pia

Mfano akina Mandela mbona wamekulia kwenye msoto lakini wakasamehe

Kuna watoto wa marais na wanasiasa wakubwa huko nchi za DRC Burkina Faso n k sijui walikuwa nao marais na wakawa makatili tu
Mandela hakukulia kwenye msoto. Mandela alikuwa wa ukoo wa kichifu, na hadi anaingia gerezani 1963 alikuwa tayari na degree ya chuo kikuu, fursa adimu sana kwa watoto weusi miaka hiyo. Mandela alifungwa akiwa na umri wa miaka 45, kwahiyo kama ni msoto hasa ulianza akiwa na umri huo, kabla ya hapo alikuwa kiongozi mwenye kuungwa mkono na umma na hata mataifa mengine, alipambana lakini hakusota, alianzia msoto gerezani at 45.
Historia inaonesha kuwa watu wenye disturbed childhood wanaishia kuwa watu wa visasi vya kudumu dhidi ya watu ambao hata hawahusiki na kilichowasotesha. Soma habari za Adolf Hitler, ni mfano halisi.
 
Hukutoa ufafanuzi wa swali uliloulizwa. Uchaguzi na ubinafsishaji wapi na wapi?
Mimi nilitaka ufafanuzi wa para hii
"Mrema alipambana akamshinda kwenye uchaguzi. Nyerere alimuunga mkono Mrema kugombea, kui -challenge CCM."
Fafanua unataka nifafanue nini?

Mrema alikuwa jembe hashwa. Majambazi yote yalikaa nyumbani. Panya Road angewaua wote. Wasingethubutu kujitokeza. Alikuwa kama JPM. Zaidi ya JPM. Chuma.

Watz wengi wanataka amani, usalama, ajira, ,mazingira mazuri ya kufanya biashara. Sio taarabu, ngojera, maneno mengi.

Majaliwa anaweza kutufaa ni mchapakazi, anatatua matatizo ya sisi walalahoi.

Watz wanataka kiongozi imara sio legelege, kurembue macho.
 
Hakuna ushahidi wa kuuza kila kitu ni habari zile zile za kizushi za watanzania. Wakasema mke wake na hayati Hassan Diria walikuwa wauza madawa ya kulevya. Sio habari za kweli.

Ni kama Samia wanavyomhusisha na biashara za maeneo ya mbugani, ni habari za kimbeya zisizo na ukweli.
Huyo Ahmed Hassan Diria, balozi na waziri, usituchefue wengine tuna ndugu waliumia sababu yake. Nyumba ya Upanga jirani na hekalu la wahindu, niseme zaidi? Dogo amesota sana jela kwa kubebeshwa ngada na huyo mzee. Na alimtaja lakini hola.
 
Haupo sawa hapa Mungu ni wetu sote kwa walio wagonjwa na wazima.
Kuishi maisha marefu ni mapenzi ya Mungu ambayo kila binadamu anatamani ayapate,kusema kuwa Marais wa kiislamu wameishi maisha marefu kuzidi wale wakikristo ukimtoa Mzee wetu Mwinyi ni kutudanganya.

Mzee Kikwete ana miaka 71 bado haijui kesho yake.

Rais samia ana miaka 62 Naye bado haijui kesho yake.

Je unajuaje Kama Rais Samia anaweza kufikia miaka aliyoishi Mkapa[81] au Rais Mstaafu Kikwete akafikisha miaka 77 ya baba wa Taifa.Bado ni fumbo.

Maisha ya binadamu kwa yeyote yule ni fumbo Lissu alipigwa risasi zaidi ya kumi yupo hai lakini Magufuli hayupo hayo ni mapenzi ya Mungu sitaki kukufuru.
[Mwalimu aliishi miaka 14 baada ya kustaafu kwake while Mkapa 15 bado ni miaka Mingi tu kwao.
Nami namtakia heri ya kuzaliwa mzee wetu.
Asante. Wakumbushe pia kuwa yule afande wa Mutukula Gen David Musuguri ametimiza miaka 102 mwezi January. Na katika mahojiano yake siku alipotimiza miaka 100 alisema ameishi na ugonjwa wa kisukari tangu alipotimiza miaka 60, yaani amedumu na kisukari for 40 years!
 
Aliachiwa nchi maskini sana na Nyerere. Tulikuwa tumetoka vitani mwaka 1978 madhara yake yakiwa dhahiri kwa kila sekta.

Ndio miaka ya mwanzoni ile, tofauti na hawa kina Samia na hayati JPM waliokuta kuna wasomi wa kila aina.
Ukiwa Nchi maskini haimaanishi uuze kila kitu. Kuna vitu vya msingi vinavyoisaidia jamii, Taifa. Vibaki mikononi ya serikali (Wananchi).
 
Umenikumbusha kifo cha mwandishi wa habari wa gazeti la Mfanyakazi enzi hizo anaitwa Francis Katabalo, alikua anaandika sana habari za Uchunguzi, gazeti la Mfanyakazi those years lilikua gazeti la habari za Kiuchunguzi. RIP Francis Katabalo
Rekebisha jina. Aliitwa Stanslaus Katabaro, kwa kifupi Stan Katabaro.
Tuliokuwepo tulimjua personally.
 
Hivi ukimwondoa mzee wa Msoga, Getrude Mongela, Anna Makinda na Msuya Kuna waziri wa mzee Mwinyi ambaye bado Yuko hai?
 
Back
Top Bottom