Miaka 30 Bila Ramani: Hujafa, Lakini Umechoka

Miaka 30 Bila Ramani: Hujafa, Lakini Umechoka

Rorscharch

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2013
Posts
1,431
Reaction score
3,071
Miaka 18, umemaliza kidato cha sita. Umebeba ndoto zako zote mgongoni kama mzigo mwepesi, macho yako yanang’aa kwa matumaini. Unajiambia, “Nikimaliza chuo nitayabadilisha maisha ya familia yangu.” Miaka 22, degree mkononi, lakini huna pa kwenda.

Dunia haijakukaribisha kama ulivyotarajia. Umebahatika kupata internship—huna mkataba, hulindwi na sheria, hulipwi vizuri. Laki mbili kwa mwezi, elfu sita kwa siku. Na bado unapaswa kula, kuvaa, kutuma pesa nyumbani, kutabasamu japo moyo umejaa huzuni.

Miaka miwili inapita kimya kimya. Unatumika, unajitoa, unajitahidi—kama kuna mtu anayeona. Lakini hakuna. Unapigwa chini bila huruma, nafasi yako inachukuliwa na kijana mwingine aliyejaa matumaini yale yale uliyokuwa nayo. Naye atatumiwa, atachoka, atatupwa. Mfumo unajirudia, kama mdundo wa nyimbo ya huzuni isiyo na mwisho.

Miaka 24, hujui tena unakoelekea. Kila siku ni kivuli cha ile nyingine. Hakuna kazi, hakuna kipato, hakuna matumaini. Na kama hiyo haitoshi—unaachwa na uliyempenda. Si kwamba hukumpenda vya kutosha, bali huna uwezo wa kumnunulia hata chakula cha mchana. Anaenda kwa mtu mwenye umri wa baba yako—aliye na pesa, gari, na uwezo. Unabaki na machungu. Mapenzi yanageuka kuwa kiwewe cha nafsi. Unaanza kuumia ndani kwa ndani. Kila picha ya harusi, kila post ya "baecation", kila story ya mafanikio Instagram inakukata moyo kama kisu. Unaanza kuamini hujatosha. Unaanza kujichukia.

Miaka 27. Sura yako imechoka. Macho yako hayang’ari tena. Unatembea kama kivuli cha mtu uliyokuwa. Hakuna shughuli. Hakuna ndoto. Hakuna hamasa. Njaa imekuwa rafiki. Hali yoyote inakufaa, bora tu ije. Unakubali kazi ya mshahara wa laki tatu—unaishi chumba cha laki moja, kilichojaa joto na mbu. Unakula chakula cha bei rahisi, unaandamana na marafiki wa hovyo, unafanya mazungumzo yasiyo na tija. Huna tena misimamo. Huna tena hofu. Maadamu siku inaisha, basi inatosha.

Na sasa, pombe ni faraja yako. Bangi ni kimbilio. Sigara ni rafiki. Udaku ni starehe. Dopamine ya bei rahisi imekuwa chakula cha akili yako. Unawaangalia waliopiga hatua kama maadui. Unawachukia, si kwa sababu wamekosea—bali kwa sababu wewe umeachwa nyuma. Unagonga miaka 30, huna ndoa, huna mtoto, huna hata mtu wa kuzungumza naye kwa kweli. Upo tu—mtu mzima aliyejaa utupu ndani ya nafsi yake.

Lakini yote haya hayakuanza jana. Yalianza miaka 22, pale ulipomaliza chuo na maisha yalikunyamazisha bila huruma. Ndoto zako zilianza kufa polepole, bila hata kelele.

USHAURI WA MWISHO KWA KIJANA WA MIAKA 20

Kijana, tafadhali usidanganyike. Usitamani maisha ya watu wa Instagram, usitamani mishahara ya laki nne yenye maumivu ya rohoni. Wengi wao ni waathirika wa mfumo. Wanavaa tai lakini ndani wamevunjika. Wanacheka ofisini lakini wanalia chooni. Wanapokea mishahara isiyotosha kulipa hata matumaini yao. Wanaishi maisha ya kujificha—hawana furaha, hawana upendo, hawana amani.

Kama una miaka 20, jifunze. Tafuta ujuzi. Kuwa bora kwenye jambo moja. Jenga mitandao ya watu wema. Linda heshima yako. Usiongozwe na njaa. Jenga msingi wa maisha imara. Tenga akili yako na kelele za mitandao. Siyo kila anayepiga picha nzuri ana maisha mazuri. Wengine wanapiga picha ili kusahau huzuni zao.

Na juu ya yote—chunga akili yako. Ipe nguvu, ilinde, ifunze. Kwa sababu, ikiwa itavunjika, hakuna mtu atakayekutengeneza.

–Makala hii ni kilio cha wengi waliovaa tabasamu la bandia. Kwa kijana wa Kitanzania. Kwa kijana wa Kiafrika. Kwa yule ambaye hajawahi kusikilizwa.
 
Maisha hayana formula mkuu, mim wakat najitafuta huko mererani kwa marehemu Erasto kuna watu walikuwa wanamiliki mabilioni, ila sasa hawana kitu na kuna watu wazima kwenye 50s ndio wamejipata saivi. Umri ni namba tu unaeza fanikiwa ukiwa mdogo, kijana, mtu mzima au hata uzeeni. Chamsingi nikuendelea kupambana.
N.B JAY Z AMEPATA MTOTO WA KWANZA AKIWA NA 40 same to J Lo na Mariah Carey.
 
Kingine cha kuongezea.

Kijana wa 20's inabidi uongee na wanaokuzidi umri wa miaka 10+, wakupe ushauri wa Maisha.
Ndoa, biashara, kazi , familia,

Tena sio mmoja, kama ni binti tafuta wadada na kama ni mvulana tafuta Wanaume . Ni muhimu.

Ukijidai una akili sana, unaweza kufeli huko mbele.
Role model muhimu.
 
Maisha hayana formula mkuu, mim wakat najitafuta huko mererani kwa marehemu Erasto kuna watu walikuwa wanamiliki mabilioni, ila sasa hawana kitu na kuna watu wazima kwenye 50s ndio wamejipata saivi. Umri ni namba tu unaeza fanikiwa ukiwa mdogo, kijana, mtu mzima au hata uzeeni. Chamsingi nikuendelea kupambana.
N.B JAY Z AMEPATA MTOTO WA KWANZA AKIWA NA 40 same to J Lo na Mariah Carey.
Yeah sure
 
Maisha yalivyo kwakweli, ni Mungu tu ndiye anaweza kusaidia.

Funny enough, due to hustles, the distance from 30 to 40 is too short na unafika patupu.

But Katika yote, Mungu ni mwaminifu tusichoke kutumia Kila fursa kwa ukamilifu kwasababu Kila mtu ana fungu lake, kibaya ni kupishana na gari la mshahara kwamba wakati umepata kidogo ukakitumia vibaya ukiamini kikubwa kitakuja.

Mithali 3:5-7
5 Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe;

6 Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.

7 Usiwe mwenye hekima machoni pako; Mche Bwana, ukajiepushe na uovu.
 
Miaka 18, umemaliza kidato cha sita. Umebeba ndoto zako zote mgongoni kama mzigo mwepesi, macho yako yanang’aa kwa matumaini. Unajiambia, “Nikimaliza chuo nitayabadilisha maisha ya familia yangu.” Miaka 22, degree mkononi, lakini huna pa kwenda. Dunia haijakukaribisha kama ulivyotarajia. Umebahatika kupata internship—huna mkataba, hulindwi na sheria, hulipwi vizuri. Laki mbili kwa mwezi, elfu sita kwa siku. Na bado unapaswa kula, kuvaa, kutuma pesa nyumbani, kutabasamu japo moyo umejaa huzuni.

Miaka miwili inapita kimya kimya. Unatumika, unajitoa, unajitahidi—kama kuna mtu anayeona. Lakini hakuna. Unapigwa chini bila huruma, nafasi yako inachukuliwa na kijana mwingine aliyejaa matumaini yale yale uliyokuwa nayo. Naye atatumiwa, atachoka, atatupwa. Mfumo unajirudia, kama mdundo wa nyimbo ya huzuni isiyo na mwisho.

Miaka 24, hujui tena unakoelekea. Kila siku ni kivuli cha ile nyingine. Hakuna kazi, hakuna kipato, hakuna matumaini. Na kama hiyo haitoshi—unaachwa na uliyempenda. Si kwamba hukumpenda vya kutosha, bali huna uwezo wa kumnunulia hata chakula cha mchana. Anaenda kwa mtu mwenye umri wa baba yako—aliye na pesa, gari, na uwezo. Unabaki na machungu. Mapenzi yanageuka kuwa kiwewe cha nafsi. Unaanza kuumia ndani kwa ndani. Kila picha ya harusi, kila post ya "baecation", kila story ya mafanikio Instagram inakukata moyo kama kisu. Unaanza kuamini hujatosha. Unaanza kujichukia.

Miaka 27. Sura yako imechoka. Macho yako hayang’ari tena. Unatembea kama kivuli cha mtu uliyokuwa. Hakuna shughuli. Hakuna ndoto. Hakuna hamasa. Njaa imekuwa rafiki. Hali yoyote inakufaa, bora tu ije. Unakubali kazi ya mshahara wa laki tatu—unaishi chumba cha laki moja, kilichojaa joto na mbu. Unakula chakula cha bei rahisi, unaandamana na marafiki wa hovyo, unafanya mazungumzo yasiyo na tija. Huna tena misimamo. Huna tena hofu. Maadamu siku inaisha, basi inatosha.

Na sasa, pombe ni faraja yako. Bangi ni kimbilio. Sigara ni rafiki. Udaku ni starehe. Dopamine ya bei rahisi imekuwa chakula cha akili yako. Unawaangalia waliopiga hatua kama maadui. Unawachukia, si kwa sababu wamekosea—bali kwa sababu wewe umeachwa nyuma. Unagonga miaka 30, huna ndoa, huna mtoto, huna hata mtu wa kuzungumza naye kwa kweli. Upo tu—mtu mzima aliyejaa utupu ndani ya nafsi yake.

Lakini yote haya hayakuanza jana. Yalianza miaka 22, pale ulipomaliza chuo na maisha yalikunyamazisha bila huruma. Ndoto zako zilianza kufa polepole, bila hata kelele.

USHAURI WA MWISHO KWA KIJANA WA MIAKA 20

Kijana, tafadhali usidanganyike. Usitamani maisha ya watu wa Instagram, usitamani mishahara ya laki nne yenye maumivu ya rohoni. Wengi wao ni waathirika wa mfumo. Wanavaa tai lakini ndani wamevunjika. Wanacheka ofisini lakini wanalia chooni. Wanapokea mishahara isiyotosha kulipa hata matumaini yao. Wanaishi maisha ya kujificha—hawana furaha, hawana upendo, hawana amani.

Kama una miaka 20, jifunze. Tafuta ujuzi. Kuwa bora kwenye jambo moja. Jenga mitandao ya watu wema. Linda heshima yako. Usiongozwe na njaa. Jenga msingi wa maisha imara. Tenga akili yako na kelele za mitandao. Siyo kila anayepiga picha nzuri ana maisha mazuri. Wengine wanapiga picha ili kusahau huzuni zao.

Na juu ya yote—chunga akili yako. Ipe nguvu, ilinde, ifunze. Kwa sababu, ikiwa itavunjika, hakuna mtu atakayekutengeneza.

–Makala hii ni kilio cha wengi waliovaa tabasamu la bandia. Kwa kijana wa Kitanzania. Kwa kijana wa Kiafrika. Kwa yule ambaye hajawahi kusikilizwa.
Yote maisha tu.
 
Tena sio mmoja, kama ni binti tafuta wadada na kama ni mvulana tafuta Wanaume . Ni muhimu.
Mhhh ..... Kwenye hili nashauri mabinti ya miaka 20 wasitafute wadada wa miaka 30+ tu bali waangalie pia mitazamo ya wanaume wasio na nia nao kimapenzi; nasema hivi kwasababu unfortunately kuna wanawake ambao hata wafike 40 bado very delusional, unakuta mtu ndani au nje ya ndoa anaishi kwa mentality ya kudanga na kuhudumiwa kama default, lazima akuingize chaka,
Unakuta mwingine anaonekana kujipata kimaisha ana gari na kibiashara kumbe nyuma ya pazia bila kulipiwa kodi na danga au mme hiyo biashara ingekuwa ishafungwa, gari hajui hata certificates za umiliki ziko wapi na hajui hata kama inahitaji kubadilishwa oil
 
Wkt nchi inapata uhuru,nchi likua na uhaba wa wafanyakazi na hasa serikalini,waliokua wakifika form 4/6 na hata chuo walikua wanachukuliwa moja kwa moja makazini,hii hali haikubadilika kutokana na kuongeongezeka watu,plus watu kutostaafu mapema au nafasi kujaa,hii hali haijabadilika hata leo hii.
Ndio maana wasomi wengi Kazi hakuna.
Mchina alipoona ongezeko la watu yeye aliwapa ujizi waufundi ndio maana mchina hata akija panga kwako lazima anakiwanda ndani
 
Age is just a number you can beat the odds at any time you don't need to count ur age .


Hata Kama Una miaka 30 unaweza kwenda chuo ukapata degree

Hata Kama Una miaka 40 unaweza kuoa ukapata Mtoto.

Don't pressurized the youths .

Kwakuwa tomorrow is Riddle
 
Back
Top Bottom