Nianze kwa kumshukuru sn
Nyani Ngabu kwa thread hii ya pekee iliyotuibua wengi toka kwenye machimbo.
Kwa mimi binafsi kazi zangu za sasa hazinipi nafasi ya kutosha kuingia huku mtandaoni.
Lakini pia niushukuru uongozi mzima wa JF kwa kazi kubwa ya kutuunganisha wadau mbalimbali kwa kipindi cha miaka 10 sasa.
Nilijiunga JF 2009. Hakika kipindi hicho JF ilikuwa bado ina nguvu ya juu sn, na ilikuwa na watu makini sn kwenye siasa na MMU.
Sitarudia kuwataja waliokwishatajwa, lakini nawa'salute sn wote, maana mmeweka alama za kudumu 'Landmarks' katika nyaja ya mijadala ya mitandao. Lkn ni lazima nimtaje mtu maarufu sn ambaye hajatajwa hapa, ambaye amewasaidia watu wengi sn kwenye nyanja muhimu ya afya, akijulikana kama
MziziMkavu, Salamu sana ndugu.
Mimi binafsi nina mchango wa kutosha ktka hii miaka 10. Enzi hizo ilikuwa ngumu sn kwa members wa JF kuonana kwa kuhofia usalama wao.
Lkn taratibu mimi ni mmoja wa watu walioanza kuhudhuria kwenye social gatherings kama misiba na kuugua kwa members hasa pande za huku Arusha.
Nakumbuka mwaka 2011 nilimtembelea member mkongwe kabisa aliyekuwa mgonjwa anaitwa
Lunyungu, akashangaa sn.
Taratibu baadaye ikaonekana kuwa members wanaweza kuonana na kujadili mambo ya msingi, tofauti na kujificha nyuma ya screen.
Mwaka 2010 nilifiwa na Baba mzazi huko Dar, nilishangaa kuona kundi kubwa la wanaJF, wakanifariji sana na kuniwezesha, chini ya Bwana
Teamo, wakati huo akijiita Geoff
Asprin,
bht na wengineo wengi.
Sisi wa huku kanda ya Kaskazini tukaanzisha kambi iliyoitwa ArushaWing, ikapata nguvu sn kiasi cha kuitikisa Dar, na kuwa mfano na Icon ya JF nzima kwa mshikamano
Nakumbuka tulifanya safari za kutembelea vivutio vya nchi yetu kama Tarangire, Ngoro2 Duluti Amboni Tanga, etc.
Safari ya Tarangire ilivutia hisia kali kiasi cha kuwafanya wanaJf toka Dar kumiminika Arusha jioni hiyo kuungana na sisi kwa blast la hatari na tukakesha.
Kilele kilifikiwa pale Mkuu
Maxence Melo alipoungana na hao members wa Dar na kuwasili Arusha na kutangaza kuwa wazo la kuanzisha JF lilikuwa conceived huku Arusha, yeye akiwa katika hali ya mzozo na dola akiwakimbia Polisi na kuishi maisha ya kujifichaficha.
Siku hiyo tulifahamiana, tulikula na kunywa, tukacheza muziki sana na mengine mengi ambayo siwezi kuyasema.
Baadaye watu wa MMU Dar nao wakajikongoja na kuanza kuonana phyisically kwa organization za akina Babu
Asprin na wengineo. Wakaanza kufanya safari za outing kwa kuogopana sana, na baadaye walikuja kuorganize tukio lililoitwa White Party.
Kwa ufupi ni kwamba tulisaidia sn kubadili mitazamo ya members, na kuwezesha urafiki wa mitandaoni kubadilika kuwa wa wazi, na mengi mengineyo.
Ukiacha mijadala ya siasa, JF imekuwa ni site ya msaada sn na imebadili maisha ya wengi.
Kuna marafiki zetu wengi walipata biashara, kazi, mbinu za ujasiriamali, ujuzi, wengine wamepona magonjwa kupitia JF Doctor, na zaidi sn kuna wadau wengi niwajuao ambao hatimaye walioana na tumecheza sana harusi zao na hadi leo wana watoto na maisha yanaendelea.
ArushaWing ya wakati huo tulipata wageni wengi sana toka nchi nzima. Ilikuwa kila mdau wa Jf akipata Fursa kuja Arusha basi anapata mapokezi ya daraja la kwanza toka kwa members!
Hapa nawakumbuka watu maarufu sn kama
DARKCITY Mwita Maranya, @Woman of Substance
TIMING na watu kibao.
Tuliripoti sn matukio ya siasa za Arusha kwa kupangana ili kupata coverage nzuri. Ilikuwa mmoja anakuwa internet cafe, mwingine eneo la tukio, na wengine wanarusha kwa simu kila bit ya matukio. Hapo ndio utajua kazi ya
Saharavoice na
Crashwise.
Mwisho kabisa nakumbuka JF Dar ilipata kuanzisha kitu kama Saccos, wadau wakawa wanakutana , wakafungua Bank account, sijajua ile kitu inaendeleaje ndani ya hii miaka 10, au kama ilitumbuliwa sina ufahamu. Naomba ajuaye atujuze.
Jf imetupanua ufahamu sn na hizi taarifa za juzi kwamba wanalazimishwa kutaja wanaogenerate habari ni mbinu chafu za wachache kuitoa makali. Kwa taaluma zetu na michango ya hali na mali tupigane kuhakikisha frontliners wanashinda na haki inaibuka Bingwa.
Mungu awabariki sn.
PakaJimmy.