mi mi la kusema sina.wana jf semeni wenyewe

wifi kaumia sana alivotemwa sasa analipa kisasi kwa mdogo mtu khaa!.....ila nibora alivoaamua kulipa kisasi kwa mtindo huo kuliko angejiua.........mana angemnufaisha kaka mtu na dada mtu kwa vyeti kua officially vyake
 
Aende mahakamani akale kiapo abadilishe jina liw jina la kwenye cheti.
You Got It.... Apige QT apate cheti cha sekondari kwa jina lake...... aende amahakamani aape kuwa jina lake alotumia chuoni lifute na litambuke jina lake halisi na ikiwezekana afanye taratibu na vyeti vyake vibadilishwe baada ya kiapo(cjui kama inawezekana hapa)...v ikifanikiwa akamshukuru yule dada alomfanizia na maisha yasonge.... ajifunze kutokana na makosa..!!! wazo tu..
 
Pole sana, anza upya hiyo fraud haitakusaidia kabisa sana sana sasa hivi utaenda jela. Hili ni funzo kwa makanjanja wengine waache huo mchezo maana wenye sifa wapo wengi hawapati kazi nyie na ma Godfather wenu pamoja nakukosa vigezo mnakula kiulaini.
 
Nakushauri usifakamie Vyeti, tafuta elimu.. Hicho Kiswakinge ulivyokiandika unaonekana muhuni .. Eleweka Na lugha unayotumia sio unachanganyachangaya wewe umekuwa Waziri mkulu.. Pinda!
 
Huyo x wifi yako ni dhahiri hata ukimtafuta ukafanya nae dialogue hapatakua na suluhu ! Coz kuna kila vimelea vya kuonesha kesharipoti kunakohusika kuhusu cheti chake.
Hilo limeshavunda, hebu jaribu kugeuza hewa uangalie kufanya shughuli ambazo hazitohitaji uwepo wa vyeti.
Sikushauri urudi shule, timeframe ina matter ktk life. Maisha hayalazimishi yaende kwa kazi zinazohitaji vyeti peke yake.
Kaa na familia yako wa'consult wakufanyie mikakati ujikite ktk ajira binafsi.
 
Nadhani unachotakiwa kufanya ni kuangali mambo kama biashara,au mengine. Kwenda mahakani kwa mtazamo wangu itakuletea shida,maana yule wifi bado anakufuatilia kulingana na maelezo yako. Pia jua wazi maisha hayana kanuni zaidi ya kujituma,lakini matatizo yote kayaleta kaka. Yaliyokupata ni makubwa nakupa pole ila ulisema wazi ulikuwa mdogo hukujua kifuatacho baadaye. Jaribu hata vibarua vya muda kama vinapatikana,napenda pia ujue yameshatokea huna budi.
 
muue huyo mwenye jina then uendelee na maisha. anamwaga mboga unamwaga ugali. yeye si aligawa cheti bana?
 
Nakushauri usifakamie Vyeti, tafuta elimu.. Hicho Kiswakinge ulivyokiandika unaonekana muhuni .. Eleweka Na lugha unayotumia sio unachanganyachangaya wewe umekuwa Waziri mkulu.. Pinda!

Member wewe ! Hayo maelezo mbona alivyojieleza ni mtiririko mzuri tu? Wapi ulipopaona kuna elements za kihuni ?
Au muhuni utakua wewe ?
Sometimes wakosoaji aina yako mnatu'bore ? Hamuishi "hila"!
Huna cha kuchangia si fanya mengineyo.
 
Mimi napenda nikushauri hivi, ukisema urudi shule kweli muda utakua umeenda sana, afadhali ungelifanya hayo ukiwa na umri wa miaka 20 ungeweza kurudi shule, wanasemaga "elimu haina mwisho" lakini jaribu kuipotezea, lakini si vibaya kwa sababu umesoma ila vyeti ndio tatizo. Cha msingi tafuta fani yoyote uisomee, ni mwaka mmoja tu, chukua hata masuala ya hotel management. Usikae tu nyumbani maisha hayamsubiri mtu.
 
Nenda kwa huyo dada, mwumbe msamaha,mwambie wewe huna kosa kama ni kosa la kakayako akuonee huruma japo kakako hakumwonea huruma.
 
Duh waanze pia kupekua na vyeti vya viongozi wetu kama halijazuka scandal.. Pole kwa huyo dada kwa kweli.. Ajaribu kutafuta mkopo ajiajiri..
 
Kusoma hakunaga mwisho wala umri, ajisacrifice aue tena miaka apige shule, I remember when I was at university nlikuwa napiga kitabu na wababu kabisa ukiwauliza mbona mnajitesa they just replied kusoma hakuna mwisho na they wanted mshahara na marupurupu mengi..
Inaddition nkiwa 3rd year ticha wangu wa primary akawa 1st year na nikawa nampiga muongozo.
KUSOMA HAKUNA AIBU
 

sio mimi smile
Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 25,
nilimaliza form four miaka kadhaa iliyopita kwa bahati mbaya sikuweza kufaulu kuendelea na kidato cha 5,
nilipata division four ya mwisho
i have to admit uwezo wangu ulikuwa mdogo darasani,
nikakaa one year home bila issue yoyote
baadaye kaka yangu ambaye alikuwa chuo mwaka wa 2 akaniambia amenitafutia cheti cha mtu niingie chuo,
kweli akanitafutia nafasi CBE nikaanza kusoma certificate ya accounts kwa kutumia cheti cha huyo dada ambaye nilikuwa simjui later nilikuja kufahamu kumbe alikuwa girlfriend wake,

basi nikamaliza certificate, nikasoma diploma, mpaka advance diploma,
wakati niko Advance diploma mwaka wa mwisho kakangu akaoa
lakini hakumuoa yule girlfriend wake nayemjua mimi na ambaye natumia cheti chake
akamuoa dada mwingine tofauti,
kwakweli mpaka leo sijui kwanini hakumuoa yule dada na siwezi kumuuliza,
basi yule dada alikasirika sana na akaninyang'anya cheti chake
yeye wakati huo alikuwa mwaka wa mwisho Institute of Accountancy Arusha,
kwakweli nilichanganyikiwa ila sikujua kama impact yake itakuja kuwa kubwa hivi
, nilipomaliza chuo nikapata kazi shirika moja Arusha
sasa hapo ndo mchezo ulipobadilika after 6 months wakaniambia nipeleke original certificates zangu,
Duuh nilidata nikampigia kaka simu akaniambia omba likizo njoo Dar tudiscuss nikarudi tukahauriana nikaamua niache kazi maana ntapeleka vyeti gani wakati cheti cha form four sina.
nikakaa home kama one year my cousin sister akanifanyia mpango nikapata cheti cha kuchonga mtaani akanitafutia kazi Bank moja hapa Dar,

nikaanza kufanya kazi sijafikisha hata mwaka last month nikaitwa HR naambiwa nisubmit my original certificates, nikasema ni nini tena hiki, basi nikapeleka kile cheti cha kuchonga na vile vingine original vya chuo but natumia jina la yule dada, after a week nikasimamishwa kazi ili kupisha investigation nikaambiwa nimeforge vyeti na mimi sio mwenye hvyo vyeti,

as am speaking to you am just home sijui la kufanya, naona kama kakangu ameniponza ningejua ningerisit by then imagine vyeti vyangu vyote vya chuo vina jina la huyo dada,

naomba mnielewe wakati huo nilikuwa mdogo sikujua impact ya kutumia cheti cha mtu but i think my brother did so msinihukumu kwa hilo, nimepoteza 6yrs kusoma with all my effrots amd energy na nilijitahidi sana nikapata lower second na sikuwahi kusupp,

i have i feeling huyu dada ananifatilia kila napoenda na kuniharibia,

hivi naanzia wapi jamani, nirudi tena kurisit form four, naona siwezi that means another 7 yrs za kurudi shule by then ntakuwa na 32yrs ntazeekea shule jamani,

yani sijui hata la kufanya nawaza mpaka nafika mwisho, naishia kulia sipati hata usingizi.

ndugu zangu wananishauri nirudi shule nianze moja but nahisi siwezi kusoma tena, naombeni mnishauri labda naweza pata options hapa ambazo hazitahitaji kutumia muda mwingi

Its me a frustrated lady

Sipaswi kukulaumu dada yangu pole sana,mara nyingi mambo yanayotokea katika maisha yasikukatishe tamaa ni moja ya mapito na kama ukiwa jasiri wa kukabiliana na mapito utajikuta unafanikiwa kwa kiasi kikubwa.Kwenda shule haimaanishi ni lazima uajiriwe tunakwenda shule ili tupate maarifa yatakayotusaidia kukabiliana na changamoto zilizoko huku duniani maana aliyekwenda shule anatakiwa kufanya mambo ambayo yataonekana ni tofauti na asiyekwenda shule hata kama ni biashara inatakiwa iwe ya ubunifu tofauti na mtu ambaye hakwenda shule ninachokushauri huna haja ya kupoteza muda na kuanza kurudia mitihani tena muda hausimami unasonga mbele cha kufanya kama huyo kaka yako ana kazi na anaweza kukusaidia angalau mtaji kidogo wa kujiajiri ongea nae ujiajiri maadamu una elimu itakusaidia kufanya kitu tofauti na asiye na elimu,usifikirie kwenye mitaji mikubwa kupita kiasi buni biashara ndogo tu inayoendana na mtaji unaoweza kupata anza kwa upande huo inawezekana Mungu hajakupangia kuajiriwa anataka ufanye kazi zako mwenyewe kule kufukuzwa kazi kusikukatishe tamaa kiasi hicho,jitie moyo usonge mbele maisha yanaendelea hata bila ya kuajiriwa.
 
sometimes tatizo lipo kwenye system yetu.. kama mtu anauwezo wa kufanya kazi vizuri kabisa stil unafatilia vyeti vya kazi gani.!? matokeo yake ndo kupata mafisadi yaliyosoma..
bak to the topic, hamna kurudi nyuma talk na huyo mdada mmalizane vizuri ka ye ndo huwa anakualibia if not huwe unawapoza mabosi wako ata kwa ten percent ya salary, hope hawatakua wanoko tena.!!

Aise hiyo ni ngumu sana.Utaanzaje kumwambia mwajiri kuwa utampa certain percent ya mshahara kisa huna vyeti?Siku ukiharibu kazi itakuwaje?Si ndo utasema mbona huwa unampa vihela kidogo!
 
Nenda kwa huyo dada, mwumbe msamaha,mwambie wewe huna kosa kama ni kosa la kakayako akuonee huruma japo kakako hakumwonea huruma.

Ruv actvist embu jiongoze mwenyewe!Kumbuka cheti kilitolewa katika mazingira fulani yaani mazingira ya mapenzi.Sasa hayo mazingira hayapo tena.Kwa hiyo hicho cheti hakiwezi kutolewa unless yale mazingira yapo.Kumbuka huyu dada alikuwa hafahamiani na mwenye cheti,brother ndo alisuka mipango yote.
 
mpe pole sana muathiririka wa vyeti,hayo yapo humuhumu dunian, na hasa Tanzania wala hayatoki kwa MUNGU wanaoforge ni wengi sana, sema ya kwake imeingia kidudu m2.
 
Back
Top Bottom