Mhudumu wa Afya aliyeonekana kwenye video akisafisha vyombo vya hospitali kwa njia isiyofaa asimamishwa kazi

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
5,897
10,358
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu Ummy Mwalimu amepongeza hatua iliyochukuliwa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala kwa kumsimamisha kazi Mtumishi wa Afya katika Kituo cha Afya Kivule, Dar es salaam kufuatia kuonekana kwenye video akiwa akisafisha vyombo vya Hospitalini kwa njia isiyofaa.

Kuhusu clip hiyo, soma

Waziri Ummy amesema hayo leo akiwa Bariadi, Simiyu kwenye ziara yake ya kukagua ubora wa huduma za afya katika vituo vya kutolea huduma za afya ambapo amesema kuwa kitendo alichofanya Mtumishi huyo hakikubaliki hata kidogo.

“Tumeona juzi kule Dar es salaam, Mtumishi anaosha vyombo vya Hospitali kwa maji ya baridi na kuanika juani, sijawahi kuona na nimefurahi kuona kuna hatua imechukuliwa, hivi ni kweli Mtumishi unafundishwa hivyo kuosha vyombo na kuanika juani?“

Kufuatia kusambaa kwa video ya Mtumishi huyo akisafisha vifaa vya Hospitalini kwa njia isiyo rasmi, mnamo Julai 8, 2023 Waziri Ummy alitoa tamko na kusema kuwa Mtumishi huyo alikuwa amefanya kosa kwa kukiuka Miongozo ya Kanuni za Udhibiti wa Maambukizi wa Magonjwa (Infection Prevention and Control).

Waziri Ummy amewasisitiza Watumishi wa Afya kuzingatia weledi katika majukunu yao ya kazi, huku akiwataka Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuwachukulia hatua za kisheria Watumishi wanaokiuka maadili na miiko ya kazi zao.

Millard Ayo
 
Badala ya kuwafuza viongozi wote wa hiyo hospitali mnaenda kumtoa kafara dada wa watu. Katika hili nina hakika kabisa Mungu hatawaacha salama wale wote waliomuonea huyo dada wa watu. Dada wa watu masikini ya Mungu hajui hata madhara ya kushika vile vifaa bila kuwa na gloves na si ajabu pale alipo anaweza hata kuwa amaepata maambukizi mbali mbali kutokana na kusafisha vifaa kwa mikono mitupu halafu wanamuone kwa kumfukuza kazi kuficha uzembe wao.

Lakini si kila siku tunaambiwa mama katoa hela za kutosha vipi hazikufika huko kwenye hiyo hospitali kununulia vitendea kazi muhimu? Au watu wamezilamba?
 
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu Ummy Mwalimu amepongeza hatua iliyochukuliwa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala kwa kumsimamisha kazi Mtumishi wa Afya katika Kituo cha Afya Kivule, Dar es salaam kufuatia kuonekana kwenye video akiwa akisafisha vyombo vya Hospitalini kwa njia isiyofaa.

Kuhusu clip hiyo, soma

Waziri Ummy amesema hayo leo akiwa Bariadi, Simiyu kwenye ziara yake ya kukagua ubora wa huduma za afya katika vituo vya kutolea huduma za afya ambapo amesema kuwa kitendo alichofanya Mtumishi huyo hakikubaliki hata kidogo.

“Tumeona juzi kule Dar es salaam, Mtumishi anaosha vyombo vya Hospitali kwa maji ya baridi na kuanika juani, sijawahi kuona na nimefurahi kuona kuna hatua imechukuliwa, hivi ni kweli Mtumishi unafundishwa hivyo kuosha vyombo na kuanika juani?“

Kufuatia kusambaa kwa video ya Mtumishi huyo akisafisha vifaa vya Hospitalini kwa njia isiyo rasmi, mnamo Julai 8, 2023 Waziri Ummy alitoa tamko na kusema kuwa Mtumishi huyo alikuwa amefanya kosa kwa kukiuka Miongozo ya Kanuni za Udhibiti wa Maambukizi wa Magonjwa (Infection Prevention and Control).

Waziri Ummy amewasisitiza Watumishi wa Afya kuzingatia weledi katika majukunu yao ya kazi, huku akiwataka Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuwachukulia hatua za kisheria Watumishi wanaokiuka maadili na miiko ya kazi zao.

Millard Ayo
Hawa watu wanajua drama.

Kwahyo uongozi wa hospital haukuwa unajuaga hilo?

Ni yeye peke yake hufanya hivyo!?
 
Ukiangalia kwa makini ile video utagundua haya.
1. Yule mtumishi katumwa tu kufanya ile shughuli.
2. Hakuna miundo mbinu mahususi ya kufanya vile.
3. Sio mtaalamu kamili wa ili shughuli.
4. Hana vitendea kazi.
 
Back
Top Bottom