Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,445
- 3,403
Baada ya video kusambaa kwenye mitandao ya Kijamii ikiwemo JamiiForums, ikimuonesha Mtumishi wa Afya katika Hospitali ya Kivule Mkoani Dar akisafisha na kuanika juani vifaa ya Afya. Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu ametolea maelezo suala hilo.
Waziri amesema :
“Nimeona clip inayohusu Mtumishi wa Afya akichambua, kusafisha na kuanika vifaa vya Hospitali katika Hospitali ya Kivule Mkoani Dar es Salaam.
Kitendo hiki ni kinyume na taratibu na miongozo ya Kanuni za Udhibiti wa Maambukizi (Infection Prevention and Control). Tayari Viongozi wa Mkoa wa Dar es salaam wanalifanyia kazi suala hili na watatoa Taarifa Rasmi.
Ninamshukuru mwananchi alierekodi na kuisambaza clip hii. Nitoe wito kwa wananchi kutoacha kuibua mambo kama haya yanayotokea katika vituo vyetu vya kutoa huduma za Afya vya umma na binafsi ili kuongeza uwajibikaji katika Utoaji wa Huduma za Afya nchini kwa kuwa Afya zetu ni wajibu wetu.
Aidha, nitoe rai kwa wataalamu wa afya kuzingatia mafunzo na miiko ya kazi zao na kuacha kufanya kazi kwa mazoea. Wizara ya Afya kwa kushirikiana na OR Tamisemi tutaendelea kuchukua hatua ili kuimarisha ubora wa huduma #MtuNiAfya @wizara_afyatz”
Pia, soma
Waziri amesema :
“Nimeona clip inayohusu Mtumishi wa Afya akichambua, kusafisha na kuanika vifaa vya Hospitali katika Hospitali ya Kivule Mkoani Dar es Salaam.
Kitendo hiki ni kinyume na taratibu na miongozo ya Kanuni za Udhibiti wa Maambukizi (Infection Prevention and Control). Tayari Viongozi wa Mkoa wa Dar es salaam wanalifanyia kazi suala hili na watatoa Taarifa Rasmi.
Ninamshukuru mwananchi alierekodi na kuisambaza clip hii. Nitoe wito kwa wananchi kutoacha kuibua mambo kama haya yanayotokea katika vituo vyetu vya kutoa huduma za Afya vya umma na binafsi ili kuongeza uwajibikaji katika Utoaji wa Huduma za Afya nchini kwa kuwa Afya zetu ni wajibu wetu.
Aidha, nitoe rai kwa wataalamu wa afya kuzingatia mafunzo na miiko ya kazi zao na kuacha kufanya kazi kwa mazoea. Wizara ya Afya kwa kushirikiana na OR Tamisemi tutaendelea kuchukua hatua ili kuimarisha ubora wa huduma #MtuNiAfya @wizara_afyatz”
Pia, soma